#COVID19 Tutegemee nini baada ya Rais Samia kusema 'Gwajiboy oyee Tunachanja, hatuchanji' mbele ya Askofu Gwajima?

#COVID19 Tutegemee nini baada ya Rais Samia kusema 'Gwajiboy oyee Tunachanja, hatuchanji' mbele ya Askofu Gwajima?

Unauliza watachanjwa au hawachanjwi kudhibiti korona wakati at the same time unawakusanya watu barabarani ba kuweka msongamano!

Nadhani wameelewa sasa kuwa Watanzania siyo watu wa kupelekwapelekwa!
Watanzania gani unaowazungumzia, hawa hawa ninaowafahamu au wengine!!!!!!!!!!!!
 
Wanapenda kutuvuruga sana! Sasa waliosema achukuliwe hatua na chama chake, sijui chama gani tena maana mwenye chama ndo huyo keshasema Gwajiboy oyeee.

Gwajigirl, ****** wajipange upya
Kumbuka alimpa salaam za pole Mh Mbowe kumbe anamlia timing. Hatabiriki.huyo.
 
Sema hii serikali haieleweki...ikumbukwe Ndugai kasema Aajibishwe endapo haitokua hivo Wazari wa mambo ya Ndani ataitwa Na sijui hadi mda huu ile kamatai ya ndugai nayo inajisikiaje kwa kweli inafikia wakati Mama unamwacha aende anavyoenda tu.
Kama magu tu aliwalinda baadhi ya alio wapenda gwajima ana backup ya mama
 
Wa KUDEMKA hajitambui.

Mapema Leo wakati Rais Samia yupo Tegeta jimbo la Kawe kwa Mchungaji Gwajima akiongea na wananchi na wakazi wa Kawe waliojitokeza kumsikiliza ameongea mengi lakini kati ya hayo ni pale aliposema "Gwajiboy oyeee, tunachanja, hatuchanji? Haya mheshimiwa gwajima endelea"


Kwa kauli hii Spika na Waziri wa Afya wako na hali gani kwa sasa?

Je, tuendelee kutegemea hatua zozote kutoka kwenye chama (CCM) dhidi ya Gwajiboy?
 
Ule ni mchezo tu niliwaandikia hapa kwamba CCM na bunge lao hawana uwezo wa kumfukuza hata mbunge mmoja,yaani afukuzwe mbunge ? aloo wanatafuta mboga kumwagwa walichokitifua kwenye uchaguzi mkuu uliopita ni jambo baya sana sana sana,si raisi si wabunge inabidi walindane tu na kusitiriana.

Mkuu wewe umemchagua Nani. Mana unaongea sana. Jihesabuni njioni. Tutaamia. Instagram. Then tutamalizia Facebook. Mana huko mtaani hakuna kitu.
 
Kwa hiyo huyo Mungu ana uwezo wa kuzuia Corona ukiwa nyumbani kwake tu na mtaani hawezi kuzuia usipatwe na Corona?Kama anaweza kuzuia Corona ukiwa nyumbani kwake anashindwa vipi kuzuia Corona ukiwa mtaani?
Kwa hiyo kwako wewe nyumbani kwa Mungu na mtaani ukakuona kuko sawa? Nyumbani kwa Mungu Kuna madhabahu au altare huko mtaani kwako na nyumbani kwako kuna madhabahu au altare huko mabarabani?
 
Yaani gwajima boy chuma cha reli maana ingekuwa mtu mwingine hata salamu asingetoa angedodoka mwenyewe puuuuu chali mpelele mzena au kairuki kwa kiholo mbele ya amirijeshi mkuu
 
Kwa hiyo kwako wewe nyumbani kwa Mungu na mtaani ukakuona kuko sawa? Nyumbani kwa Mungu Kuna madhabahu au altare huko mtaani kwako na nyumbani kwako kuna madhabahu au altare huko mabarabani?
Kwa hiyo watu wakiwa mitaani huwa hawalindwi na Mungu?
 
Kwa hiyo watu wakiwa mitaani huwa hawalindwi na Mungu?
Mitaani ni kila mtu na imani yake kwa MUngu .Mitaani ukikuta waiovaa barakoa wanaomwamini Mungu YEYE atawalinda wasiomwamini kuwa aweza kuwalinda wanaoamini mibarakoa kazi kwao

Mitaani ni kila mtu na imani yake ndio itaamua Mungu alinde mtu au asilinde

Nyumbani kwake ni tofauti ndipo penye usalama kuliko popote
 
Leo wakati Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akielekea Bagamoyo kurecord filamu ya kutangaza utalii wa Tanzania alisimama kwenye jimbo la Kawe ili kusalimia wananchi.

Rais alimsimamisha Mbunge wa Kawe ili kutoa neno lakini kabla ya kumsimamisha aliwauliza wananchi wa Kawe kama watachanja au la kama video inavyoonyesha hapa chini.Katika hali ya kustaajabisha na ya kushangaza wananchi walimwambia Rais bila ya kupepesa macho kuwa hawatachanja kama video hii inavyoonyesha hapa chini.

Nimejiuliza maswali mengi sana.Kwa nini Rais aulize swali hilo kwenye jimbo ambalo mbunge wake hakubaliani na mambo ya chanjo?Ina maana Rais hajui kwamba kazi kubwa ambayo walifanya katika awamu ya tano ya kupinga chanjo ilifanikiwa sana hasa ukizingatia kuwa kazi hiyo ilifanyika katika Taifa lenye umasikini mkubwa sana wa akili?

My take:
Kwa sasa hivi serikali ya CCM inapata shida sana kula matapishi yake yenyewe ambayo waliyatapika katika awamu ya tano.Ni vyema serikali ikiri mbele ya wananchi kuwa Rais Magufuli hakuwa sahihi na alipotosha sana uma ili wananchi waanze upya kuelimishwa juu ya gonjwa la Corona na chanjo.



Sio sifa kutokuchanja maana yake ni watu wengi kufa.
 
Video nzima hii hapa[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mitaani ni kila mtu na imani yake kwa MUngu .Mitaani ukikuta waiovaa barakoa wanaomwamini Mungu YEYE atawalinda wasiomwamini kuwa aweza kuwalinda wanaoamini mibarakoa kazi kwao

Mitaani ni kila mtu na imani yake ndio itaamua Mungu alinde mtu au asilinde

Nyumbani kwake ni tofauti ndipo penye usalama kuliko popote
No!!Mimi nazungumzia yule ambae ameenda kanisani bila kuvaa barakoa kisha akalindwa na Mungu,je akirudi mtaani na akaendelea kupeta bila kuvaa barakoa si ataendelea kulindwa na Mungu kwa kuwa ni mshika imani tayari?
 
Yaani gwajima boy chuma cha reli maana ingekuwa mtu mwingine hata salamu asingetoa angedodoka mwenyewe puuuuu chali mpelele mzena au kairuki kwa kiholo mbele ya amirijeshi mkuu
Ndugai alisema Gwajima anakichwa kigumu.
 
Back
Top Bottom