Mkuu
Bigstone kwanza u bukheri wa afya ?
Turudi kwenye mada ndugu kaka mwalimu kumiliki Vanguard au Ist au Vitz sio kuonekana ana hela au tuseme wanalipwa vizuri mpaka kufanya hivyo .
Ila ni kuwa kwa leo kuna access za mikopo kwahiyo hata hiyo Vanguard uisemayo yawezekana kakopa ndiyo kanunua .
Sasa lengo anuwai sio huo ujinga wa kumiliki gari ya mamimilioni alafu huku unaliendesha siku za kutoka mshahara tu .
Ni imani yetu kuwa maslahi ya mwalimu yakiimarishwa vizuri tegemea mwalimu awe na biashara zake kubwa na maendeleo zaidi ya kumiliki gari la mkopo .
Hivyo wito ni kuwa masilahi yaongezwe ili hata akinunua gari la gharama vipi asiwe na hofu juu ya gharama za kuliendesha hilo gari .
Ila pia niwakumbushe kumiliki gari sio utajiri ni kuwa na kitu ambacho ni mahitaji ya binadamu katika karne ya leo .
Ulimbukeni wa familia nyingi watokazo ndugu walimu walio wengi ndiyo maana ufikiri kumiliki gari ni utajiri ila ni ulimbukeni uliopindukia .
Wito ni kuwa ni lazima masilahi ya walimu yaongezwe .
Teachers wake up the time of your liberation is now.[emoji123]