Mimi simu ilikuwa inazingua touch na nipo mkoa kikazi nasubiri nirudi Dar ndio nibadili, aisee sina hili wala lile simu ipo mfuko wa suruali, kwenye mida ya SAA sita mchana simu yangu Nokia ndogo simu inapigwa kucheki mshkaji wangu wa kitambo na tulikuwa hatujawasiliana almost miezi 6, napokea simu cha kwanza ananiambia wewe ..mse... ingia haraka WhatsApp status kafute kimeo chako akakata simu, naingia status nakuta pilau linapikwa limeivaa hatari nikafuta fasta na ile simu sikuitumia tena.