Tweets za January Makamba na Zitto kuhusu Hotuba ya Warioba

Tweets za January Makamba na Zitto kuhusu Hotuba ya Warioba

Status
Not open for further replies.
Zitto Kabwe: Watanzania watakapoamka watakuta hili saga la #IPTL limegharimu Taifa takribani dola nusu bilioni. #TegetaEscrow
Huyu jamaa ni mtata na sasa anaumbuka, ni suala la muda tu. Hebu angalia hapa alipoandika baada ya kutoka kwenye kikao alichokuwa mwenyekiti (PAC). Yaani anaandika utafikiri yeye sio Mtanzania na hayo mambo hayamhusu, kwa maana tulitegemea kwa nafasi yake kama mbunge angesaidia kuamsha hisia ili wananchi wa kawaida tuamke kuipinga IPTL.
Kwa hakika ameisaliti cdm iliyomkuza na wengi hawakujua kuwa kwa kufanya hivyo amewasaliti wananchi kama ccm na sasa eti anapimana ubavu na mwandishi wa Katiba ya mwaka 1977 Mzee Warioba kana kwamba yeye anaelewa na ni mzalendo zaidi yake!
Na huyu mtu anafanya PhD!
 
MACCM leo yamevurugwa mno ila mm bado napata mashaka hawa jamaa watachakachua tu maana idadi yao tu inatosha kua na two third.
Warioba leo kanikosha mno
 
kama ni maneno ya huyu msaliti tumeyazoea kumbuka ni tabia ya watu wanaotoka katika maeneo dhaifu wanapenda kujulikana sana. hapo kashapewa mlungula anatapatapa. kwani uso wako hamuuoni? bila chakula huyu si angekuwa tishio kwa watoto jamani
 
Kwa uchangiaji huu napata jibu y wengi hawakumuelewa prof Shivji - majibu yake kwa warioba! Ipo haja ya kuweka CV ya kila mchangiaji hapa JF
 
Nimeliona live ZZK likishangilia walipokuwa wanatoa maoni ya Ofisi ya Waziri mkuu, si unajua walipopewa yale maonii ya taasisi zake walienda kuchakachua wakapeleka ya Pinda!!?? Najua mnajua msimamo wa Pinda na Serikali Tatu na Muungano pia!!! Chumia tumbo hili lilishanunuliwa siku nyingi, limekuwa lipole na zee kwa mawazo.
 
akiri ndogo kuongoza akili kubwa, kwa nini zisiwepo fikra kuwa anayeongezwa ni mtoto? anakimbilia mke? na mke kama anaongeza ni kuwa alikuwepo na si kuwa anazaliwa, kwa iyo mke(tanga-nyika) kama yupo kwa nini asije kulea watoto? kama ni kuunda nchi/kuzaa mtoto sio kuleta mke ni kuzaa kipya basi afikirie kuwa tunaleta mtoto aje kusaidia kuteka maji, kupika, kufua na kulinda nduguze! badala ya kujadili hoja ya warioba wanawaza wanawake...ivi kwa nini msieleze kama warioba alivosema, je waasisi wa muungano waliacha serikali mbili nchi mbili au waliacha serikali mbili nchi moja? je ukiwa na serikali mbili moja iko Tanganyika na nyingine zanzibar, je serikali ipi inashughulikia mambo ya wabara?au ile ile ya muungano ndo ya bara na wanzibar wachangie tu mambo ya wabara? je madini na gesi vilivo Tanganyika ni mali ya muungano ila vilivo upande wa pili ni vya wazanzibar, kuna fair distribution apo? This is what a layman/gentlemen must address and not marriage/sex issues!
 
Inaonekana somo la Warioba kuna viumbe halijawaingia.

January kaandka Twitter kuwa watatumia uwingi wao kuulinda muungano.

CCM hawaitamani Tanganyika yetu?

Muungano una matobo kibao bado unang'ang'aniwa wa nini?

Kuna Watu wanafaidika nao nini?

waulinde muungano kwa kujenga hoja hili tuwaelewe sio kuulinda kwa wingi wa watu
 
Kwa hiyo Zitto anapingana na makala yake moja, tena ya mwaka huu, akiunga mkono serikali 3?
 
Kwa uchangiaji huu napata jibu y wengi hawakumuelewa prof Shivji - majibu yake kwa warioba! Ipo haja ya kuweka CV ya kila mchangiaji hapa JF

alaf zije kwa order of age...tuanze na Dogo1, ah ahh!!
 
Hivi kweli maelezo ya Warrioba yote January hajaelewa kitu?Mbina kapangua hoja zote za gharama,ufanisi etc?Mods waache kuchanganya threads ili watu wajadili vipengele.
 
Rightly So...., una haki ya kuongelea na ku-challenge kila kitu ila kumuita mtu msaliti na coward sababu mawazo yake, yanayokukera ni kuingilia uhuru wa mawazo ya mtu
Kwa mtazamo huo huo kumuita mtu msaliti na coward ni uhuru wa mawazo. Hivyo ndivyo anavyomuona. Athibitishe au wewe thibitisha kwamba sivyo.
Zitto ni mbunge ni vema atoe mawazo yake bungeni ili aone kama yanaungwa mkono.
 
January Makamba ‏@JMakamba 10m Kilichofanyika Bungeni leo ni kuorodhesha matatizo ya ndoa (ambayo ni ya kweli) halafu kisha kusema kwamba kuongeza mke ndio jawabu lake.

January, we ndiye unataka kuwa rais kwa mawazo haya? Fanya uchambuzi kabla ya kuandika. Kwa kifupi ulichosema ni ugoro kwa vile kwa sisi watu wa vijijini mgogoro wa wanandoa unaweza kusababishwa na kazi nyingi kama, kulima, kuchota maji, kuhudumia wakwe wa umri mkubwa, n.k. hivyo kuoa mke mwingine huondoa matatizo.
 
Usipende kusikia unachokitaka tu, Lazima tuwe na mawazo tofauti tofauti, usitake watu wote wawe kama makondoo!
Kwani hayo mawzo ya Mzee Warioba ni yanani, sio maoni ya wananchi!???
Na nyie mnaosema "Warioba, Warioba, Warioba, Warioba, Warioba, ...." wakati wa kutoa maoni mlikuwa wapi!?
Je, mbona mnamsema Mzee Warioba peke yake!? Jaji Ramadhani, Almaamry, Prof. Baregu nk nk mpaka Daktari wetu mpendwa Mvungi (R.I.P) ambaye rasimu hii imegharimu maisha yake hamwasemi!?? Ccm kweli ni viumbe wa ajabu na huyu MM anayewasikiliza anakuwa mtu wa ajabu pia!


 
Relevancy yake imekuwa reduced to Zero..so watapiga mishemishe ya kuongelea CDM na kuichafua ili CCM waendelee kuwafund.
 
Zito na Makamba ni kama moshi na moto, wanaongozanaga kweli. Afu na staili yao ile ile ya vitwit, sijui hii era ya uongozi walii-recruit toka wapi.

Yaani CCM wakishakufanya mtu wao, baaasi wanahakikisha akili zako wanazing'oa halafu wanabandika zao zitakazokufanya uache kutumia ubongo badala yake utaanza kutmia nduu, manina sana CCM, na walaaniwe!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom