Tetesi: Ubaguzi wa ajira kwenye Serikali ya Mapinduzi Zanzibar

Tetesi: Ubaguzi wa ajira kwenye Serikali ya Mapinduzi Zanzibar

Magufuli ndio raisi mbovu hajawahi kutokea Tanzania,hivi sasa watanzania wamegawanyika kidini na kikabila mambo kama haya hayajawahi kuwepo Tz,Mauaji ya kisiasa ni kitu kipya kabisa TZ

Kwa ufupi Magufuli anaigawa TZ vipande vipande tusibiri tuone nini kitatokea,,
Nyinyi ndio wale watanzania wa nyuma ya keyboard. Tanzania mliyonayo akilini ni ile ya 1985, yanayotokea Dar na kwenye miji mikubwa ndio kipimo chenu cha nchi ambayo Mungu ametujalia.

JPM atakumbukwa kwa miaka mingi ijayo, kwa sababu hashughuliki na maslahi pekee ya watu wa mijini ambao siku zote hawana shukrani.

JK anaonekana malaika baada ya kuondoka pale magogoni, huo ni ushahidi wa uwepo wa watu wengi kama wewe mkuu chabuso.
 
Dah!! Tunaelekea wapi na Tanzania yetu... Yameanza visiwani huko bara yananukia au yalishafika sema hatujashtukia... Ila malipo ya hawa wanaharamu watayapata hapa hapa duniani
 
Mwal Nyerere alishasema mkianza kuwabagua wabara mtakuja upemba na uunguja, Waache kuwabagua wabara lasivyo dhambi hii itawatafuna daima

Kama wanavyobaguliwa wachaga na wakaskazini .Hii ni sera ya Laanatullahi Nyerere na CCM yake
 
Nyinyi ndio wale watanzania wa nyuma ya keyboard. Tanzania mliyonayo akilini ni ile ya 1985, yanayotokea Dar na kwenye miji mikubwa ndio kipimo chenu cha nchi ambayo Mungu ametujalia.

JPM atakumbukwa kwa miaka mingi ijayo, kwa sababu hashughuliki na maslahi pekee ya watu wa mijini ambao siku zote hawana shukrani.

JK anaonekana malaika baada ya kuondoka pale magogoni, huo ni ushahidi wa uwepo wa watu wengi kama wewe mkuu chabuso.

Si ndio akatujengea international airport kule Chato ili tupate watalii wengi wa kwenda kuvuta ugolo , na pia usisahau vile vi wonder vya ugolo kule Chato
 
Ubaguzi uko kwenye damu, acha kusingizia siasa....nafanya shughuli zangu Zanz nayashuhudia yote haya ila tunawaona mapoyoyo tu maana hata wakinibagua hawanipunguzii chochote ....ila kwa kujifanya watu wa dini sasaaaa!!!!!

Tatizo unatoa huduma Kwa mapadri tu
 
Si ndio akatujengea international airport kule Chato ili tupate watalii wengi wa kwenda kuvuta ugolo , na pia usisahau vile vi wonder vya ugolo kule Chato
Mkuu, viwanja vya ndege vinajengwa nchi nzima, pesa inatumika kwa faida ya wengi na sio wachache wenye mawazo ya kibinafsi kama wewe.

Endeleza kejeli za mitandaoni wakati watu wanapiga kazi ya maana kila kona ya Tanzania.

Secularism unayoipinga huwezi kuizuia, labda ufe halafu uzaliwe kwenye dunia nyingine.
 
Wacha unafiki huo wewe. yaani kila siku unaleta habari za kizushi hata aibu huoni.. Naweza kusema ajira za SMZ wanofaidika nazo wapemba. kwani ajira zote zinazotoka Pemba basi kama wazee wako wanatoka Unguja huwezi kupata hata uwe CCM lakini wao wapemba ajira za Unguja sehemu yeyote ya Unguja wanaomba hizo ajira.. Kama ubaguzi haukuanza leo musisi wa ubaguzi huo seif Sharif wakati alipokuwa waziri wa Elimu na waziri kiongozi kwa pale alidhihirisha chuki zake za wazi kwa watu wa Unguja.

Hakuna watu wabaguzi dunia hii kama Wapemba na Mission yao kubwa sana umuona mtu wa Unguja yuko chini na hafanikiwi hilo la kuitetea zanzibar ni ujanja wa kuwahadaa watu wachache wa unguja kutokujua nini kiko kenye nyoyo zao. lakini waunguja wengi wanaanza kutambua hayo. kwa hivyo wacha kueneza propaganda za kipuuzi
Usilolijua ni bora ukae Kimya....
Pumbavu
 
Hii kitu ipo sana na si zanzibar hadi bara. Hata kama una vigezo vimejitosheleza.. bado watademand loyalt flan kutoka kwako either pesa au kuwa mwanachama.
Bara imekuwa iki copy mambo mengi ya dhulma kutoka Zanzibar, angalia chaguzi za hivi karibuni Bara.
 
Ubaguzi uko kwenye damu, acha kusingizia siasa....nafanya shughuli zangu Zanz nayashuhudia yote haya ila tunawaona mapoyoyo tu maana hata wakinibagua hawanipunguzii chochote ....ila kwa kujifanya watu wa dini sasaaaa!!!!!

Hata Tanganyika kumejaa ubaguzi na zarau kwa Wazanzibari.
 
Ni kweli kabisa mie rafiki zangu wengi wamepata ajira kupitia njia hyo mpka uwe na card ya ccm yaani kuna kipengele unajaza number ya card ya ccm. Hasa ajira za walimu nimeshuhudia live. Jamaa wanaigawa Zanzibar kabisa.
Umeona . Kuna wengine walitaka kupindisha taarifa hizi
 
Matatizo ya uajiri mpya yanaanzia kwenye "short lists" hii ni hatua ya mwanzo ya kuwatoa wapinzani, hatua nyengine ni "veting" ambayo hufanywa na usalama wenye maslahi na UVCCM. Mrejesho wa veting zao huwaacha watu fulani wenye asili ya maeneo fulani (hasa wapemba) na familia zenye kuhisiwa kuwa na Upinzani. Taarifa zinasema waathirika wakubwa ukiacha watu kutoka Pemba, ni watu wa kaskazini ya Unguja na watu wa majimbo yenye nguvu kubwa za upinzanio na mjini hasa watu wenye asili ya kiarabu.
 
Nyinyi ndio wale watanzania wa nyuma ya keyboard. Tanzania mliyonayo akilini ni ile ya 1985, yanayotokea Dar na kwenye miji mikubwa ndio kipimo chenu cha nchi ambayo Mungu ametujalia.

JPM atakumbukwa kwa miaka mingi ijayo, kwa sababu hashughuliki na maslahi pekee ya watu wa mijini ambao siku zote hawana shukrani.

JK anaonekana malaika baada ya kuondoka pale magogoni, huo ni ushahidi wa uwepo wa watu wengi kama wewe mkuu chabuso.
JPM atakumbukwa kwa:-"hawa msiwavunjie wamenipigia kura,hawa wavunjiwe hawajanipigia kura,hawa wafukuze kazi vyeti vyao feki,huyu mwacheni kabila letu moja,huyu mpigeni risasi anapingana na mawazo yangu"...

Kwa ufupi JPM atakumbukwa kwa kuirejesha nyuma Tanzania kidemokrasia,na kupindisha haki za msingi kwa kila mtanzania,Tanzania ya leo kila mtanzania kajiininamia kwa msongamano wa mawazo,wale wenye uwezo wameanza kukimbilia Finland kwenda kutafuta ukimbizi,wengine waliobakia wamejawa na hofu ya maisha yao..

"Raisi wa ajabu haijawahi kutokea Tanzania":-TAL
"Tanzania inaongozwa na watu washamba" :-ZZK
 
Kuna taarifa za ubaguzi wa ajira ndani ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa wapinzani na hasa watu kutoka kisiwa cha Pemba. Taarifa hizi zinaendelea kuzagaa na kutolewa katikati ya lawama za wakubwa kufumbia macho taarifa hizo au kukanusha bila uthibitisho wa ziada.

Taarifa zinadokeza kuwa mara baada ya kufanyika uchaguzi wa marudio wa Machi, 2016 , mikakati ilipangwa kuhakikisha wapinzani hawapati nafasi za kuajiriwa na vile vile kuhakikisha watu walidhaniwa kuwa wapinzani wanaondolewa katika vitengo nyeti. Taarifa zinadokeza kuwa zoezi hili limefanyika kwa asilimia zaidi ya 90%

NAMNA UBAGUZI UNAVYOFANYWA.

Taarifa zinaeleza kwamba zoezi la uajiri wa nafasi mpya, linaratibiwa vyema kwa kushirikisha vyombo vya usalama (usalama wa taifa) na UVCCM, Vijana wa UVCCM waliomo serikalkini na mawakala wao kwenye TISS wametengeneza mtandao kuhakikisha kila nafasi inashikiliwa na mwana CCM au wanaoitwa ":watu wetu". Mkakati huu umepangwa na kupata baraka za ofisi moja Kupitia Ofisi ya Makamo wa pili wa Rais wa Zanzibar.

Taarifa zinasema kuwa kumekuwa na hamisha hamisha ya wafanyakazi hasa wa utumishi kwenye vitengo ambao waliokuwepo huondolewa na kuchomekwa watu wa mfumo ili kufanikisha suala hili. Kuna idara nyingi na hata taasisi zenye bodi na mashirika zinaingiliwa majukumu yake na Utumishi mkuu kwa watu kuhamishwa na mamlaka ya bodi hizo kunyanganywa kwa kisingizio cha "Utumishi Mkuu"

Zipo taarifa kuwa hata zile nafasi zinapotangazwa zilizohitajika zijazwe na watu kutoka Pemba kwa mfano, hupelekwa watu kutoka Unguja au Bara ambao wanaaminika kuwa wako upande wa Utawala na kuchukuwa nafasi hizo.

MAJIBU MEPESI.
Kupitia tuhuma hizo, Waziri wa nchi ofisi ya Makamo wa pili wa Rais( Mh Muhamed Aboud) amewahi kutolea ufafanuzi suala hili na kubainisha kwamba hakuna ubaguzi na mchakato unakuwa wa wazi ambapo hutangazwa na wenye sifa ndio wanaajiriwa jee huo ndio ukweli ?

Taarifa zinasema hilo sio tatizo, Sheria ya Utumishi wa ummma imeeleza vyema kuhusu mchakato ambapo nafasi hutangazwa na wenye sifa ndio wanatakiwa kuajiriwa, Hapa tatizo si mchakato, Tatizo ni DHAMIRA, inaelezwa kuwa mkakati ni kuwa hata kama mtu ana sifa ilimradi ni Mpinzani anatafutiwa mazingira ya kuachwa. Zipo taarifa kuwa imefika mahali watu wana sifa na wameshachaguliwa na kuhojiwa halafu wanaachwa baada ya kufanyiwa "veting" na kile kitengo kinachoitwa "GSO" Veting hio inasemwa inaelekezwa kwenye siasa na kupekuliwa asili ya familia ya mtu. Hapa ndipo vijana wa mfumo wa UVCCM wanapohusishwa.

Viongozi ama kwa kutojuwa au kwa makusudi hawataki kujiridhisha kadhia hii. Mfano wa karibuni ni uajiri wa walimu na nafasi zinazotangazwa kupitia mashirika na taasisi za Serikali.

ATHARI
Athari ya kwanza ni kuajiriwa watu ambao hawana uwezo na nyengine ni kuigawa jamii. Katika hili Kule Zanzibar , jamii ya watu wa Pemba imeathiriwa sana. Zipo taarifa kuwa ukiwa Mpemba hata kama ni CCM huaminiwi na wako wengi wamekosa kuajiriwa kwa kudhaniwa kuwa wapemba wote ni wapinzani. (huu sio ukweli)

Tetesi hizi ni nyeti. Imefika wakati maofisa wanaohusika na uajiri huwaeleza watu wazi wazi kuwa "...wewe unazo sifa lakini huwezi kuajiriwa, huwa wanasema tatizo liko kwa watu wenu ambao wametoa taarifa kuwa hufai..." Hii ndio hali ilivyo.

Mwandishi amepataa tetesi hizi kupitia kwa vyanzo muhimu na sasa taarifa hizi zimezagaa kule Zanzibar.

MWISHO.
SMZ inatakiwa kuondowa dhana hii kwa vitendo, Kwenye jamii hizi taarifa zpo na hazipaswi kupuuzwa. Wazanzibari wenyewe wanafahamiana na huwa unaambiwa Zanzibar hakuna siri. Ikiwa Mkakati huu upo basi kwa haraka uondolewe kwa maslahi ya Taifa.




Kishada.
HAYA MAMBO MBONA MNAYASEMA LEO WAKATI MUANZILISHI WA MAMBO HAYO NI SHEIKH SEIF SHARIF HAMAD .
Baada ya mapinduzi kulikuwa hakuna huyu mpemba na huyu muunguja na ndiyo maana hata scholarships za elimu ya juu vijana wengi wa kipemba na unguja walinufaika. Wakati Sheikh Seif aliposhika madaraka ya kuwa Cheif Minister wa SMZ pamoja na ujumbe wa CC, Alianza mkakati wa kuhakikisha vijana toka pemba wanaajiriwa na kupewa madaraka bila kuwepo na uwiano na wenzao. Baadaye ndipo ilipojulikana kuwa bwana huyu alikuwa anatengeneza mfumo ndani ya mfumo rasmi ili kutekeleza azma yake ya kuutaka urais wa zanzibar. Sasa leo kilio hiki ni cha nini?
SIKU ZOTE DHAMBI INA MALIPO YAKE NA HAPA KAMA KWELI SUALA HILI LIPO SMZ BASI MWENYE KUBEBA ZIGO HILI NI SEIF SHARIF.
MTENDA AKITENDEWA SIKU ZOTE HUHISI KUWA ANAONEWA.
 
Mkuu, viwanja vya ndege vinajengwa nchi nzima, pesa inatumika kwa faida ya wengi na sio wachache wenye mawazo ya kibinafsi kama wewe.

Endeleza kejeli za mitandaoni wakati watu wanapiga kazi ya maana kila kona ya Tanzania.

Secularism unayoipinga huwezi kuizuia, labda ufe halafu uzaliwe kwenye dunia nyingine.

Si ndio hata chato mnajenga mupate kusafirisha ugolo??
 
HAYA MAMBO MBONA MNAYASEMA LEO WAKATI MUANZILISHI WA MAMBO HAYO NI SHEIKH SEIF SHARIF HAMAD .
Baada ya mapinduzi kulikuwa hakuna huyu mpemba na huyu muunguja na ndiyo maana hata scholarships za elimu ya juu vijana wengi wa kipemba na unguja walinufaika. Wakati Sheikh Seif aliposhika madaraka ya kuwa Cheif Minister wa SMZ pamoja na ujumbe wa CC, Alianza mkakati wa kuhakikisha vijana toka pemba wanaajiriwa na kupewa madaraka bila kuwepo na uwiano na wenzao. Baadaye ndipo ilipojulikana kuwa bwana huyu alikuwa anatengeneza mfumo ndani ya mfumo rasmi ili kutekeleza azma yake ya kuutaka urais wa zanzibar. Sasa leo kilio hiki ni cha nini?
SIKU ZOTE DHAMBI INA MALIPO YAKE NA HAPA KAMA KWELI SUALA HILI LIPO SMZ BASI MWENYE KUBEBA ZIGO HILI NI SEIF SHARIF.
MTENDA AKITENDEWA SIKU ZOTE HUHISI KUWA ANAONEWA.
Sasa kama Seif Sharif kayaanzisha CCM ndio wayaendeleze,sasa hapo kutakuwa na tafauti gani kati ya Seif Sharif na CCM Zanzibar!??.

Kwani mkiwakosesha ajira wapemba na Wazanzibari wasio na asili ya Kiafrika anaepata tabu nani Seif Sharif au wazanzibari na familia zao
 
HAYA MAMBO MBONA MNAYASEMA LEO WAKATI MUANZILISHI WA MAMBO HAYO NI SHEIKH SEIF SHARIF HAMAD .
Baada ya mapinduzi kulikuwa hakuna huyu mpemba na huyu muunguja na ndiyo maana hata scholarships za elimu ya juu vijana wengi wa kipemba na unguja walinufaika. Wakati Sheikh Seif aliposhika madaraka ya kuwa Cheif Minister wa SMZ pamoja na ujumbe wa CC, Alianza mkakati wa kuhakikisha vijana toka pemba wanaajiriwa na kupewa madaraka bila kuwepo na uwiano na wenzao. Baadaye ndipo ilipojulikana kuwa bwana huyu alikuwa anatengeneza mfumo ndani ya mfumo rasmi ili kutekeleza azma yake ya kuutaka urais wa zanzibar. Sasa leo kilio hiki ni cha nini?
SIKU ZOTE DHAMBI INA MALIPO YAKE NA HAPA KAMA KWELI SUALA HILI LIPO SMZ BASI MWENYE KUBEBA ZIGO HILI NI SEIF SHARIF.
MTENDA AKITENDEWA SIKU ZOTE HUHISI KUWA ANAONEWA.

Unao ushahidi wa unayoyasema??Yaan Y nyinyi mnawachukuwa wagalatia walioforge vyeti kutoka Tanganyika kwa sababu tu wapate kuwapigia kura CCM na mnawaacha ndugu zenu waislamu Kwa sababu ni wapinzani.
 
HAYA MAMBO MBONA MNAYASEMA LEO WAKATI MUANZILISHI WA MAMBO HAYO NI SHEIKH SEIF SHARIF HAMAD .
Baada ya mapinduzi kulikuwa hakuna huyu mpemba na huyu muunguja na ndiyo maana hata scholarships za elimu ya juu vijana wengi wa kipemba na unguja walinufaika. Wakati Sheikh Seif aliposhika madaraka ya kuwa Cheif Minister wa SMZ pamoja na ujumbe wa CC, Alianza mkakati wa kuhakikisha vijana toka pemba wanaajiriwa na kupewa madaraka bila kuwepo na uwiano na wenzao. Baadaye ndipo ilipojulikana kuwa bwana huyu alikuwa anatengeneza mfumo ndani ya mfumo rasmi ili kutekeleza azma yake ya kuutaka urais wa zanzibar. Sasa leo kilio hiki ni cha nini?
SIKU ZOTE DHAMBI INA MALIPO YAKE NA HAPA KAMA KWELI SUALA HILI LIPO SMZ BASI MWENYE KUBEBA ZIGO HILI NI SEIF SHARIF.
MTENDA AKITENDEWA SIKU ZOTE HUHISI KUWA ANAONEWA.

Ina maana kwanza unakiri kuwa haya yapo na ni sawa kufanywa.

Kwa hiyo haya ndio malipo ya Seif Sharif sio? halafu tunajiapiza kuwa tuna utawala bora na umoja ?

Kuna hio dhana kuwa Seif alipendelea lakini cha kushangaza tokea Baada ya Mapinduzi inajulikana ni nani waliojazwa kwenye serikali hadi leo hii. Sidhani kama hao wapinzani walipata nafasi yoyote. Hebu tuambie baada ya mapinduzi hadi leo kwenye vikosi, wizarani, mashirika, nk. nani wanaongoza kwa wingi ?.

Acheni ubaguzi kwa maslahi ya Taifa.

SMZ ijisafishe kwa ubaguzi kama upo.
 
Sasa kama Seif Sharif kayaanzisha CCM ndio wayaendeleze,sasa hapo kutakuwa na tafauti gani kati ya Seif Sharif na CCM Zanzibar!??.

Kwani mkiwakoseha ajira wapenda na Wazanzibari wasio na asili ya Kiafrika anaepata tabu nani Seif Sharifu au wazanzibari na familia zao
Msameheni huyo ndio wale wale.
 
Kuna taarifa kuwa licha ya hao watu kutoka Pemba kukosa fursa ndani ya Serikali kwa takribani miongo zaidi ya mitatu (1990- 2000, 2018)na kabla ya Mapinduzi, Jamii za watu wa Pemba zina wasomi imara na wataalamu ambao hujitafutia kwa njia zao pasi kutegemea serikali.

Hapa tunazungumzia huu ubaguzi wa ajira. Kwa nini wapinzani wabaguliwe ?
 
Ina maana kwanza unakiri kuwa haya yapo na ni sawa kufanywa.

Kwa hiyo haya ndio malipo ya Seif Sharif sio? halafu tunajiapiza kuwa tuna utawala bora na umoja ?

Kuna hio dhana kuwa Seif alipendelea lakini cha kushangaza tokea Baada ya Mapinduzi inajulikana ni nani waliojazwa kwenye serikali hadi leo hii. Sidhani kama hao wapinzani walipata nafasi yoyote. Hebu tuambie baada ya mapinduzi hadi leo kwenye vikosi, wizarani, mashirika, nk. nani wanaongoza kwa wingi ?.

Acheni ubaguzi kwa maslahi ya Taifa.

SMZ ijisafishe kwa ubaguzi kama upo.
Mkuu kuna wakati wa utawala wa Aboud Jumbe Mwinyi nusu ya mawaziri wake walikuwa wanatoka Pemba,hata Seif Sharif kutokana na maneno yake mwenyewe , Aboud Jumbe ndie aliemleta katika siasa..

Ubaguzi ni kitu kibaya,hakuna alie amilika kila mtu anafanya makosa,katika siasa,wanasasa wanafanya mambo mengi ya maamuzi kwa maslahi yao binafsi,..lakini haina maana kuwa makosa yaliyofanywa yaendelezwe au kurudiwa,ijengeni Zanzibar yenu,piganieni mnachokitaka,acheni kubaguwana
 
Back
Top Bottom