Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania watoa tahadhari ya uwepo wa tishio la shambulio la kigaidi

Mahaba Niue haya, elewa swali!
 
Si la kupuuzia hili, hao wamarekani wakitoaga onyo ni jambo la kuchukulia serious.

Kampala walitoa onyo zikalipuliwa sehemu mbili mwaka jana.

Nahisi ngoma hii itakuwa mlimani city, masaki, oysterbay au posta.
mmeanza kazi!!
 
Serikali iombe usaidizi kwa US na Kenya maana wote wana uzoefu na mambo haya.

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Majuha mpo wengi. Chanjo za korona zimewaharibu vichwa.
 
Jukumu la ulinzi na usalama wa nchi ni la kila raia. #Kuanzia mleta taarifa, mimi, wewe na yule tuilinde kizalendo nchi yetu pendwa ya mababu na mabibi dhidi ya uadui wa ndani au nje.🙏🙏🙏
 
Maskini mimi at least sehemu tajwa huwa siingiagi!

Wakigusia Mwendokasi wamenimaliza maana ndiyo anga zangu huko.
Waongo mkuu kipindi cha Magufuli walizui raia wao kuja Tanzania kwasababu kuna vitisho vya ugaidi, wakasema tena Tanzania kuna ugonjwa wa Ebola, kwaiyo awa ndugu zetu Tahadhari zao ni za kitapeli, kipindi cha Magufuli walitoa tahadhali nyingi sana na hakuna tukio lolote lilotokea Dar
 
Yaani jamaa wanajuaje kwamba kuna kuna tukio la ugaidi kama si wao ndo wanalipanga..... the logic is clear
Wana informants huko huko Al Shabaab..... Kenya nakumbuka walikua na snipers wawili huko Al Shabaab Sasa yule informant wa CIA ndani ya Al Shabaab akawachoma. Jamaa mmoja alichinjwa Mombasa mwenzie akatwangwa risasi akiwa kwenye gari.

So tokea tukio lile litokee ndio watu wakafahamu Al Shabaab Ina mapandikizi kutoka mataifa mengi Ili kulinda maslahi Ya nchi zao. So ukiona Tanzania haijalipuliwa trust me Kuna informant kule ana divert hizo mission!!
 
Mbona issue ya Garissa walionya na ikatick..... Tusipende ujuaji! wao Wana intelijensia kuliko nchi zetu maskini hizi sio sisi ikitokea mikutano ya Chadema ndio eti taarifa za intelijensia zinafanya kazi!!
 
Umesema kweli. Na mikutano ya hadhara izuiwe. Ugaidi sio mzuri, watu wasio na hapoteza maisha
 
Tahadhari hii imetolewa leo 25/01/2023! Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania umewatahadharisha wananchi au Raia wa Marekani waliopo nchini Tanzania [emoji1241] kwamba kuna viashiria vya shambulio la kigaidi kufanyika nchini, toka vikundi vya kigaidi ambavyo haikuvitaja rasmi.

Kwa maeneo waliyoyataja hapo chini;

......

By U.S. EMBASSY ,
DAR ES SALAAM
JANUARY25, 2023

SECURITY ALERT – U.S. EMBASSY DAR ES SALAAM, TANZANIA

Location: High traffic areas frequented by Westerners in Dar es Salaam and elsewhere in Tanzania

Event: Locations frequented by U.S. citizens and other Westerners in Dar es Salaam and elsewhere in Tanzania continue to be attractive targets to terrorists planning to conduct attacks. Terrorist groups could attack with little or no warning, targeting hotels, embassies, restaurants, malls and markets, police stations, mosques, and other places frequented by Westerners.

Actions to Take:

Be alert to your surroundings.Practice personal security measures.Stay alert in locations frequented by tourists/Westerners.Keep a low profile.Visit our website for Travel to High-Risk Areas .S. citizens who travel abroad should always have a contingency plan for emergency situations.  Review the Traveler’s Checklist .

Assistance:

U.S. Embassy Dar es Salaam, Tanzania
686 Old Bagamoyo Road, Msasani,
P.O. Box 9123
Dar es Salaam, Tanzania
+255 22 229 4000

drsacs@state.gov

Je, ni imetokea tu au ni mpango maalumu?
 
Zuio la mikutano linaweza likafuatia,japo siyo sehemu za mikutano si sehemu zitembelewazo na US citizenens na Westerners wengine.
Ngoja serikali iende na biti muone.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…