Uchaguzi KKKT: Askofu Malasusa achaguliwa kuwa Askofu Mkuu wa KKKT kuchukua nafasi ya Dkt. Fredrick Shoo

Shoo hajaondolewa, bali amemaliza muda wake.
Hongera nyingi kwa Dkt. Malasusa, halafu hata watabiri hawakumtabiria kabisa huyu.
 
Katoliki maaskofu wanapigiwa Kura? Au wanapiga bila kupingwa?
From the best of my knowledge

Maaskofu wa katoliki wanateuliwa na papa baada ya mchakato mrefu.

Pia, hawana hicho cheo cha Askofu mkuu. Badala yake kila askofu ana mamlaka kamili kwenye jimbo lake. Anawaongoza maparoko, mapadri na watawa wengine ndani ya jimbo lake tu. Ni kama wabunge.

Kuhusu uchaguzi, upo wakati wa kuchagua viongozi wa Baraza lao la maaskofu (TEC). Lakini viongozi hao wa TEC hawana ukuu juu ya maaskofu wengine. Ni kama viongozi wa kamati za bunge.

Pia kuna baadhi ya maaskofu wana cheo cha ukadinali, mfano Pengo na Rugambwa. Hawa wanawajibika Vatican na sio viongozi wa maaskofu wengine. Ni kama mawaziri miongoni mwa wabunge.
 
Huu uzi una uwongo mwingi, hii nafasi huwa maxmum ni vipindi viwili . Shoo amemaliza muda wake. Kama mambo ya kanisa huyajui kaa tulia kwa nidhamu. Kwani ulitaka Kanisa litoe msimamo wa kukufurahisha wewe.
Kanisa la Mungu litaongozwa na roho mtakatifu. Panapo fukamoshi litatafuta maji ya kuzima na si kuweka petroli. Kanisa halipo kwenye ushindani. Bali lipo kurekebisha tabia, kuleta suluhu na kumcha Mungu.
 
Sawa.Hata kkkt vigezo ni hivyo.Na kwa maelezo haya inamaana na huko RC upo uchaguzi hata kama ni wa siri lakini upo kwani mmoja huchaguliwa kutoka miongoni. Hivyo scrutiny ipo labda mseme ni ya siri
 
Na maaskofu wasio makadinali wanawajibika wapi?
 
Malasusa alikuwa anamuogopa sana Askofu Mwaikali tu pale. Ndio maana wakafanya figisu zote za dunia kumtoa uaskofu Mbeya, na kisha jamaa kutimkia Kanisa la Kilutheri Afrika ya Mashariki (KKAM).
Ameen!Kama mazuri.
 
Wakatoliki wanaamini kwamba baadhi ya wale mitume 12 wa Bwana Yesu walikuwa ni maaskofu wa maeneo mbalimbali mfano Mt Petro sasa mbona tukisoma Biblia tunaona walipiga kura???

23.Matendo ya Mitume 1:23-26 Wakaweka wawili, Yusufu, aitwaye Barsaba, aliyekuwa na jina la pili Yusto, na Mathiya.

24.Kisha wakaomba, wakasema, Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, tuonyeshe ni nani uliyemchagua katika hawa wawili,

25. ashike mahali katika huduma hii na utume huu, alioukosa Yuda, aende zake mahali pake mwenyewe.

26.Wakawapigia kura; kura ikamwangukia Mathiya; naye akahesabiwa kuwa pamoja na mitume kumi na mmoja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…