UCHAMBUZI: Hoja za NECTA kufuta utaratibu wa kutangaza shule bora na wanafunzi bora hazina mantiki kwa 100%

UCHAMBUZI: Hoja za NECTA kufuta utaratibu wa kutangaza shule bora na wanafunzi bora hazina mantiki kwa 100%

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
11,550
Reaction score
40,697
Siku ya leo, Baraza la Taifa la Mitihani Nchini Tanzania (NECTA) limetangaza matokeo ya kidato cha nne na kufuta utaratibu wa muda mrefu wa kutoa orodha na mtiririko wa ubora wa shule kulingana na kiwango cha ufaulu na pia limefuta utaratibu wa kutangaza wanafunzi bora wa mitihani hiyo. NECTA imetoa sababu kuu mbili za wao kufanya hivyo, ambazo ni;

-Kutangaza shule bora ni kutangaza biashara kwa shule hizo.

-Hakuna usawa baina ya shule moja na nyingine katika mazingira ya utoaji elimu hivyo hawapaswi kushindanishwa.

Kwa kuwa JF ni Kisima cha maarifa na uchambuzi huru, Mimi binafsi hapa hapa nitazipinga hoja zote hizo mbili kwa kuchambua kwa kina hoja kwa hoja.

1. Hoja ya kutangaza biashara
Kwanza kabisa hoja hii imekaa kiupande mmoja, ni hoja ya kibaguzi kwa 100% na kuumiza wasiohusika kwa 100%. It is a double standard decision. Sababu za kibiashara zimewalenga wamiliki wa shule binafsi (zimewabagua) na hapo hapo zinazinyima fursa shule za serikali pasipo sababu (zime wahukumu pasipo kuhusika).

Pili ni hoja ya nusu nusu mno, kwa kuwa NECTA hiyo hiyo ndio imekuwa ikitoa hadharani matokeo yote ya shule moja moja yenye kuakisi ubora wa shule husika, hata kama NECTA haitaweka mtiririko rasmi wa ubora bado mtu yoyote makini (hata asiye makini) anaweza kuchambua na kuonyesha zipi ni shule kumi bora zaidi kulingana na mtiririko wa kimatokeo ulivyo.

Na katika hili, mtu au taasisi tofauti (vikiwemo vyombo vya habari) vinaweza kuja na uchambuzi wenye kukinzana na kuzaa upotoshaji. Kifupi tu, NECTA imejivua jukumu lake na sasa inakwenda kuruhusu mtu au taasisi yoyote kujitangazia ubora wake kimatokeo, hata kama ni kwa upotoshaji. Na tutegemee matangazo ya kibiashara (yenye chembechembe za upotoshaji) kwa kwa kutumia matokeo ya NECTA yakichipuka na kuongezeka maradufu. Mwisho katika hili, NECTA haipaswi kukwepa kuteketeleza majukumu yake, kisa tu inaogopa kivuli cha kuonekana inatangazia biashara shule bora. Vipi kama shule hizo 10 bora ningekuwa ni shule za serikali tu?

2. Hoja ya mazingira yasiyolingana katika utoaji elimu hapa nchini
Nadhani huenda hii ni hoja ya kipumbavu kupita maelezo kuwahi kutolewa na NECTA. Kwanza kabisa kuweka hoja sawa, sote yanapaswa kufahamu kuwa, NECTA haiwajibiki popote katika kutengeneza, kuboresha au kuyapima mazingira ya utoaji elimu hapa Tanzania, hivyo hawapaswi kuyasemea chochote mazingira hayo maana sio jukumu lao.

Pili NECTA wanawajibika kuandaa, kusimamia, kusahihisha na kutoa matokeo ya mitihani. Kama NECTA wanaona na kuamini kuwa mazingira ya utoaji elimu hapa Tanzania hayako sawa baina shule na shule na yanaathiri matokeo yao, ni kwanini waandae mitihani mmoja kwa wote au usahihishaji na utoaji wa alama za ufaulu uwe sawa?

Kwanini suala la utofauti wa mazingira baina ya shule moja na nyingine liwe ni hoja wakati wa kutangaza ubora wa shule tu, lakini isiwe ni hoja ya msingi wakati wa kutunga mitihani, kusahihisha na kuweka alama za ufaulu?
 
Mimi nakasirika sana, kwanini shule za kanisa zinafanya vyema kuliko za kata? Shule inaitwa Taifa, performance yake kama Taifa Stars ✨, halafu shule inaitwa St. Francis performance yake kama Argentina 🇦🇷 mabingwa wa dunia.

Hamjui inaumiza kiasi gani. Afadhali hata UMUGHAKA ana option, either afe yeye au afe Rehema
 
NECTA walitaka shule binafsi zijitangaze vipi ili kupata wanafunzi wengi kama sio kutumia ubora wa matokeo ya ufaulu wa mitihani ya NECTA?

NECTA inaogopa shule kushindana katika kutoa elimu bora?

NECTA haiamini matokeo ya mitihani yao kama kipimo muhimu na sahihi cha kuzipima shule katika kutoa elimu bora?
 
Siku ya leo, baraza la taifa la mitihani nchini Tanzania (NECTA) limetangaza matokeo ya kidato cha nne na kufuta utaratibu wa muda mrefu wa kutoa orodha na mtiririko wa ubora wa shule kulingana na kiwango cha ufaulu na pia limefuta utaratibu wa kutangaza wanafunzi bora wa mitihani hiyo...
Mimi naona wapo sahihi kwa 100% kufuata upumbuvu huo kwa kuwa ubora wa Elimu aliyo ipata mtu tutaupima mtu anapo kuwa mtaani anavyo mudu mazingira yake na kusaidia wengine.

Watu wanaiba mitihani na kuweka mikakati ya udanganyifu na wengine wamefaulu mpka kuitwa maprofefa lakini anadai chuo kikuu alichokuwa anafanyia kazi ambapo ni chuo kikuu maarufu palikuwa jalalani kwa sababu tuu ya kacheo ka uwaziri.
 
Mvaa Kobaz kawekwa pale kwa mikakati maaalum. Yaaan Mekkha akae kusoma shule za Vatican zilizojazana top ten?
Halafu baadae Sheikh akae kusoma shule za Istiqama 10 zilizopo mkiani🤣🤣 mnajisumbua nyie.
 
Mimi naona wapo sahihi kwa 100% kufuata upumbuvu huo kwa kuwa ubora wa Elimu aliyo ipata mtu tutaupima mtu anapo kuwa mtaani anavyo mudu mazingira yake na kusaidia wengine...
Uko nje ya mada kabisa.
Hoja hapa ni kuhusu NECTA kusitisha utaratibu wa kutangaza shule bora na wanafunzi bora katika mitihani yao.

Wewe unajadili kuhusu uhalisia wa mwanafunzi kufaulu mtihani wa NECTA dhidi ya Akili halisi ya mwanafunzi na Elimu ya kuyamudu maisha ya kila siku mtaani.
 
Mkenda ni smart na izo hoja ulizoweka anaweza pangua zote hata Mimi binafsi naweza kuzipangua.

Unajua umafia wa kweny biashara iwe bidhaa au elimu? Unajua izo shule wanafunzi wanalipa shilling ngapi then uje kufananisha na elimu bure? Mkenda na wenzie michezo yote wanaijui wapo kweny game kitambo hawajai kurupuka sio rahisi.

Mazingira ya izo shule na st kayumba unayajua.

Nakupa home work 👉 Kaangali motisha ya walimu wa izo shule kabla ya wanafunzi then uje hapa kuleta jibu.
 
Mkenda ni smart na izo hoja ulizoweka anaweza pangua zote hata Mimi binafsi naweza kuzipangua.

Unajua umafia wa kweny biashara iwe bidhaa au elimu? Unajua izo shule wanafunzi wanalipa shilling ngapi then uje kufananisha na elimu bure? Mkenda na wenzie michezo yote wanaijui wapo kweny game kitambo hawajai kurupuka sio rahisi.

Mazingira ya izo shule na st kayumba unayajua.

Nakupa home work 👉 Kaangali motisha ya walimu wa izo shule kabla ya wanafunzi then uje hapa kuleta jibu.
Bado hujajadili hoja hapo juu na wala hujajibu hoja. Uko nje ya mada.

Kama mazingira ya kielimu ni tofauti, kwanini NECTA watunge mtihani mmoja kuwapima wote?
 
Bado hujajadili hoja hapo juu na wala hujajibu hoja. Uko nje ya mada.

Kama mazingira ya kielimu ni tofauti, kwanini NECTA watunge mtihani mmoja kuwapima wote?
Serikali imejidhatiti kwa watu wote tambua na utoaji elimu uko katika kiwango kidogo kuanzia mazingira na Mishahara kwa walimu kwa maana iyo kiwango dunia cha elimu kinachotolewa kwa upande wao .

Ukija kw wanafunzi wa private haswa top ten niambie ada wanayolipwa na hata hata wanafunzi wazazi wao wanaweza kuwapeleka kusoma hata marekani pesa ipo ila sio hawa St kayumba wengi hali mbovu wakina sie..
Jaribu kuzunguka katika shule kati ya KEMOS na tafuta ambayo imefeli sana then angalia mazingira .
..
 
Huu uamuzi wa hovyo kwa namna fulani utapunguza morali miongoni mwa walimu na shule zetu, hawa jamaa simply wanataka iwe business as usual, mkifaulu wengi mtajua wenyewe, na mkifeli wote mtajua wenyewe, hawajui maana ya motisha kabisa.

Pia, huu uamuzi kwa upande mwingine naona utaziathiri zaidi zile shule zinazofanya vibaya, kwani sasa matokeo yao mabovu yatakuwa siri, walimu hawataona aibu shule zao kufelisha wengi, wakuu wa wilaya na mikoa hawatawajibika, wala hapatakuwepo na jitihada zozote za kubadilisha hali.
 
Serikali imejidhatiti kwa watu wote tambua na utoaji elimu uko katika kiwango kidogo kuanzia mazingira na Mishahara kwa walimu kwa maana iyo kiwango dunia cha elimu kinachotolewa kwa upande wao .

Ukija kw wanafunzi wa private haswa top ten niambie ada wanayolipwa na hata hata wanafunzi wazazi wao wanaweza kuwapeleka kusoma hata marekani pesa ipo ila sio hawa St kayumba wengi hali mbovu wakina sie..
Jaribu kuzunguka katika shule kati ya KEMOS na tafuta ambayo imefeli sana then angalia mazingira .
..
Sote tunajua mazingira ya kielimu yakiwa bora basi matokeo yataakisi hivyo. Kwa hiyo sio hoja hapa.

Hoja ni kwanini tuzinyime credit shule zilizofanya vizuri?

Kwanini tujenge chuki dhidi ya shule zilizoboresha mazingira ya utoaji elimu?

Kwanini tuzihukumu (tuzitungie mitihani) shule zote sawa sawa wakati tunajua mazingira ya kutoa elimu ni tofauti?

Kwanini tuzinyime fursa ya kushindana shule za serikali?
 
Sote tunajua mazingira ya kielimu yakiwa bora basi matokeo yataakisi hivyo. Kwa hiyo sio hoja hapa.

Hoja ni kwanini tuzinyime credit shule zilizofanya vizuri?

Kwanini tujenge chuki dhidi ya shule zilizoboresha mazingira ya utoaji elimu?

Kwanini tuzihukumu (tuzitungie mitihani) shule zote sawa sawa wakati tunajua mazingira ya kutoa elimu ni tofauti?

Kwanini tuzinyime fursa ya kushindana shule za serikali?
Tambua kwa namna yeyote ile huwezi kulinganisha sasa tuje kweny za serikali zimazofanya vizuri kama Tabora boys ,ilboru.

Je izo shule zinareflect jamii za izo shule zilipo kwa watu wa mkoa wa shule izo zilizopo ndo wanajua sana...point👉 serikali kupitia mitihani ya elimu ya msingi wale vipanga ndo wanaenda kujumuika kutoka shule tofauti kwa hao wanaandaliwa sawa na kuchukua wachezaji wakali kuweka timu moja then upambanisha na timu Haina wachezaji class ya juu.

Ni kwamba hata uchukue za serikali tayar ilboru Wanaenroll vipanga kutoka sehemu nyingi za Tanzania ..private nao wamechukuw vipanga ivyo ivyo Tena na kuwajengea mazingira mazuri Zaid.

Katika kuja kucompara tayar ushajua wa kwanza atakuwa yupi maana wale weny akili wote wamawekwa sehemu moja.

Labda private wao na list yao na government yao ..hata hao government wale vipanga wanakuwa wako shule kama kibaha, ilboru ,Tabora boys& girl wawe na list yao ya kupambana ..Shule za kata ziwe na list yao.
 
Uko nje ya mada kabisa.
Hoja hapa ni kuhusu NECTA kusitisha utaratibu wa kutangaza shule bora na wanafunzi bora katika mitihani yao.

Wewe unajadili kuhusu uhalisia wa mwanafunzi kufaulu mtihani wa NECTA dhidi ya Akili halisi ya mwanafunzi na Elimu ya kuyamudu maisha ya kila siku mtaani.
Enzi zetu waliokosa nafasi Shule za Serikali walikwenda Private kama Sangu, Highland etc. Hizi mbwembwe za kutangaza results kwenye Makamera hazikuwepo.
 
Mkenda ni smart na izo hoja ulizoweka anaweza pangua zote hata Mimi binafsi naweza kuzipangua.

Unajua umafia wa kweny biashara iwe bidhaa au elimu? Unajua izo shule wanafunzi wanalipa shilling...
Sasa why watunge mtihani mmoja kama wanajua Kuna disparity ya quality?

Huyo Mkenda smart kwa lipi? Hakuna hata SoMo la kilimo au viwanda sekondari alafu wanaongelea Tanzania ya viwanda na kilimo wanadhank man power inatokea wapi?

Acheni exaggerate watu wanao under perform, hoja ni kwamba kama una grade basi wangeweza sema Serikali top 10 na private top 10!! Hapo angekua smart.

Nakumbuka walikua wana grade matokeo ya form 6 kwa shule zenye wanafunzi below 40 na above 40 Ili kulinganisha sample zinazofanana.

Sasa kuacha gap ndio Kila mtu ata claim ameongoza kitaifa maana anajua hauna namna ya kuthibitisha!! Mtarudi Tena kuanza kukemea ilihali tatizo mmelileta wenyewe.
 
Back
Top Bottom