Uchambuzi huru: Hotuba ya Rais Samia Suluhu ya Aprili 22, 2021

Unaweza ukawa na hoja nzuri,lkn wewe ukaathiriwa na lugha za kifedhuri,nafkiri ni malezi au makuzi,
 
Sasa kama Nyerere alishindwa umewahi kujiuliza alishindwaje wakati nchi ina viwanda, ndege zake, miradi ya Uzalishaji Umeme n.k lakini toka Mwinyi hadi JK hatukuwa na ndege hata moja ikiruka? Hatukuwa na kiwanda zaidi ya Mengi na Bakhresa yaani miaka 30 tuna matajiri wawili wenye viwanda vikubwa nchi nzima wengine wote Matapeli. ATC, Reli ya kati, reli ya Kasikazini vimekufa barabara zote za vumbi isipokuwa Dar. Au umesahau list ya Mafisadi Papa aloisoma Mengi. Nikukumbushe kitu hivi Magufuli kawezaje kurudisha uhai wa vitu vyote kwa kutumia zaidi pato la kodi zetu? Kuna watu wanasema Magufuli aliiba sana fedha. Ebu waulizeni hizo fedha kaziweka benki gani ya ndani au nje? Au kazikwa nazo! Bila shaka hawana jibu..
 
Dira na Mwelekeo alochukua!
Naheshimu maoni yako.

Ila kwa mtazamo wangu ambao unazingatia wakati tulionao sasa diplomasia ya uchumi lazma ipewe kipau mbele,hivyo kwa mwelekeo aliouchukua naona yuko sahihi...
 
Labda kamaanisha " mfano mbaya"!
Tatizo.lenu nyote ni kutosoma Katiba na Sheria. Kama Sheria ya Mitandao imepitishwa na Bunge, mlitegemea yeye aachie tu watu wafanye wanavyotaka kwa sababu mnataka kutukana? Upinzani walitakiwa kupigania sheria hiyo iondolewe lakini badala ya kuipinga Sheria, wao wakapingana na Utekelezaji wa sheria na rais ilihali Sheria ipo Kikatiba. Huoni kama Uzwazwa huo, mimi nitapigana na Sera za Uwekezaji sina tatizo na Mama Samia. Akichukua mkondo wa Magufuli nitampa support zangu 100% lakini hili la Wachina sijui wajenge Bandari, wapewe Masharti rahisi waje kuwekeza? Hell no China kuna mapori kibao wakawekeze kwao, sisi tutaenda kununua huko huko Porini walikowekeza..
 
Ndugu yangu asante mno mno kwa uchambuzi makini. Mimi nafarijika sana kuona wapo Watanzania (nikiwemo) ambao tunajiepusha na ushangiliaji wa kitumwa.

Hotuba ya jana ya Rais imeegemea mno nguzo zilizojishikiza kwa wengine. Ni kana kwamba Watanzania hawawezi kuwa na jawabu la utatuzi wa changamoto zao, na badala yake majibu yatatoka nje ya sisi. Kwa heshima naikataa dhana hiyo kwa nguvu zote.

Nilifarijika alipozitaja taasisi zetu za ndani akilenga kuzijengea uwezo wa kuzalisha mbegu zetu ili kuondoa upungufu wa mbegu za mazao nchini ambapo alionesha kuwa TARI na ASA zitaongezewa uwezo.

AGALIZO: - katika kufanya hayo anapaswa kujua kuwa wengi wa watafiti kutoka taasisi hizo ni MAWAKALA WAAMINIFU wa makampuni makubwa ya mbegu ambayo pia yanamiliki teknolojia ya uzalishaji wa mbegu zilizofanyiwa uhandisi-jeni (GMOs). Suala la chakula ni jambo nyeti na linahitaji umakini wa kutosha. Tusisahau chakula ,inaweza kutumika kama silaha (food weapon).

Ni sharti tuongeze mshikamano na sote tuseme kwa kauli moja "TANZANIA IS NOT FOR SALE"'
 
Kwakweli na mimi niseme wazi, napenda diplomacy ya mama kabisaaa kwa dhati ya moyo, ila itikadi yake naitilia shaka sana.

Tulishajaribu hizo awamu zikatuzalishia matatizo makubwa sana hadi kupelekea wakati mwingine kushindwa kulipa mishahara. Serikali ilikosa nguvu, mabepari wakapata nguvu.

Mh. Rais aamini kuwa sera ya free economy haikuanza katika initial stages za development ambapo nchi yetu ipo kwa sasa. Hata hayo mataifa hayakuanza ki hivyo walianza na protection kwanz kisha unapofikia market level ndipo una free economy siyo kabla ya kujenga mifumo kwanza.

Sera hiyo ilianzishwa miaka ya 1990s hasa baada ya mataifa makubwa kuona kwamba imekuwa ngumu ku exploit resources za nchi zinazoendelea na ndiyo iliyozalisha ukosefu wa ajira kwa vijana wetu japo watu wachache watabakia kuwa na ukwasi mkubwa huku social service zikishindwa kujiendesha.

Naelewa sababu kubwa ya Mh. Kuamini hivyo kwakua ameshakaa kwenye NGOs na kupata impartation ya kutosha kuhusu sera hizo, hata mimi nilisha pata hizo impartation na narlewa anachokisema mama lakini ndiyo maana nilikimbia huko nakuamua kutovuruga mtazamo wangu wa African spcialism mfumo ambao unalandana na culture pamoja na makuzi yetu.

Nimwombe tena Mh. Rais akubali kutengeneza hybrid na achukue mrengo wa China na Scandnavia ambao unaendana kidogo na siasa ya mwafrika. Aachane na sera za America zilizoletwa kiakili kupitia imani ya kilokole na NGOs...Hao wanatengeneza masoko yao through Corporate zao na kila mara wana peleka uncertainty kwa group kubwa la majoritarian ambao wanageuka kuwa omba omba na kuishi kwa hisani ya hao wachache wenye economic muscles and consolidated power...

Kwa jinsi tulipofika, gap litajionyesha haraka sana na hili kama hatutakuwa makini italigharimu chama chetu na tutarudisha mambo ya mitandao na rushwa za wazi kwenye kupata nafasi za uongozi wa kisiasa na waki serikali. Naomba tusije tukarudi kwenye kile kipindi cha watu kushindwa kuvaa sare za chama kwakua majority wanaona kuwa wamekuwa betrayed!
 
Naheshimu maoni yako.

Ila kwa mtazamo wangu ambao unazingatia wakati tulionao sasa diplomasia ya uchumi lazma ipewe kipau mbele,hivyo kwa mwelekeo aliouchukua naona yuko sahihi...
Ndugu yangu, kwa wazungu hicho kinachoitwa "diplomasia ya uchumi" kinamaanisha wewe kutoa malighafi ziende kwao na wewe uwe mpokezi wa "finished products" kutoka kwao ikiwemo mitumba.
Tuwe makini sana na ufunguaji milango ya kukaribisha wawekezaji kwani wengi ni WAPORAJI na wajengaji wa kwao. KAMWE HATUTAENDELEZWA NA WAWEKEZAJI.

#TANZANIAISNOTFORSALE!
 
Naunga mkono hoja ya kudhibiti mbegu za nje

Tutumie mbegu asili
 
Lakini Hayati rais Magufuli na mwelekeo mpya wa CCM tumeona mafanikio ya Ujamaa. Sisi wenyewe tuliishi Kijamaa zamani.
Ujamaa haujawahi kuwa na faida yeyote ile kwa wanainchi zaidi ya kuzalisha wazembe na wavivu (kifikra na kiutendaji). Magufuli mwenyewe kachemka na ujamaa wake. Unamwita mtetezi wa wanyonge! really? really?. Wanyonge gani ambao wanapapiganiwa ilihali watoto (wanafunzi) zao wanaendelea kukaa chini kwenye vumbi? Wanyonge gani ambao wanapiganiwa ilihali bei ya bidhaa zinazogusa wanyonge zilikuwa zikipanda bei kila kukicha (mfano, mafuta ya kula na sukari).
 
SWALA LA UKUSANYAJI kodi na swala la WAZAWA litamugarimu sana, tayari wafanyabiashara kadhaa hawataki kulipa kodi wakidai walishalipa enzi za hayati, next ni nkuona mishahara inaingia tarehe 40
 
Shukran Mkuu labda niwashtue Watanzania kwa.mfano mmoja tu.

Sisi tunalima Parachichi za Asili (organic) na zinauzika sana Ulaya na soko ni kubwa sana. Huko Ulaya Parachichi zetu zinauzwa kwa bei mara 3 ya parachichi zinazotoka Amerika ya kusini kwa sababu zao ni za mbegu za Maabara. Lakini basi nia shaka kubwa kama Wakulima wetu wanapewa bei mara 2 au 3 zaidi ya Parachichi za SA. Nachelea kusema sii ajabu kabisa tunapewa bei sawa na za huko South.. Lakini tunaweza.ku negotiate kupandisha bei maana hakuna sokoni mwenye Parachichi kama zetu.

Sasa itokee eti na sisi tuanze kuzalisha kwa wingi sijui na huo Ukulima wa Kisasa, tutakuwa tunashindana na South Amerika maana hakuna tofauti ya ladha, na hakika hatutapata soko tena maana wenzetu wameanza zamani. Tunauza Parachichi zeru nje sio kwa sababu ya wingi bali ni kutokana na ladha ya Uasilia wa zao hilo.
 
Ujamaa haujawahi kushindwa ila unashindishwa kwa gharama kubwa ili uonekane haufai. Kisichofaa ni kukopi na kupesti mfumo wa wengine na badala yake uyatafakari mazingira yako kisha uutekeleze ujamaa wako.

Nchi za Scandnavia na baadhi ya nchi za Latin America zinatekeleza aina yao ya ujamaa na wanenda mbele vizuri.

Wakati tunataka kusema ujamaa haufai, tujiulize ni ubepari upi unafaa. Tulifuata baadhi ya masharti yao ya ubepari wa hovyo, na mwishowe tulikwama sawa-sawa. Tusijidanganye, ni lazima tuwe na itikadi yetu kwa maendeleo yetu, sio vinginevyo.

#TANZANIAISNOTFORSALE"!
 
Hili siyo tatizo kama ndivyo why wao hawatengenezi madini yao? Kwanini wanakuja kwetu kuyatumia kwa technology yao?

What is your point here?

Hakuna anayekataa wawekezaji lakini wasiturudishe kwenye ule uchafu wa ufisadi na power mongering.

Naombeni sana msiturudishe kwenye umangungo, hatutakubali katu asilani, I promise mark my words...This country belong to all of us na lazima kuwe na maridhiano ya pamoja tusiwe dragged tu kama vile we have no say...

Tunatoa tahadhari kwasababu so far we know the aftermath ya hao wawekezaji ambao hawako guided...Kabla hawaja consolidate power na wealth, we shall stand firm to protect our dignity!

Naamini kabisa hii transition itatupa mwelekeo kama nchi, msije mkampoteza Mh. Kwa tamaa za miradi binafsi, hili hatutalikubali please and please come rain come sunshine....
 
Tatizo kuna watu ambao walishatengeneza miradi yao, they never think for the society they think for their own fame and prestige...Hawaamini kwamba tumeshatoka huko...Mh. akileta model kama za Arabic countries okay, za China sawa, za Scandnavia well and good siyo America wala UK
 
Mkuu.mimi.huwa.sichoki.kutoa darasa maana unazungumza tu kutokana na matango ulolishwa. July mwaka jana Tanzania imeingia Uchumi wa Kati na labda umesahau kuwa Magufuli alipoingia Madarakani Thamani ya Tsh ilikuwa Us Dollar 1 kwa Tsh 2,345. Miaka sita leo nambie Tsh. Inabadilishwa kwa kiasi gani?

Nikukumbushe pia kwamba toka Mwinyi hadi JK thamani ya Tsh ilikuwa ikishuka kwa asilimia 50 miaka mitano na asilimia 80 - 100 kwa miaka 10. Hapo utanambia sababu zipi zilikuwa?

Ujamaa, Ujamaa ni nini? Maana halisi ya Ujamaa ni kuwawezesha wananchi kupata mahitaji yao Muhimu kama Elimu Bure, Afya Bure, kuwasaidia wasojiweza na kiuchumi.kuhakikisha zile Commanding heights zinamilikiwa na Serikali. Nchi za Scandinavia wanafanya hivyo, Canada wanafanya hivyo. Na ranks za kidunia za maisha bora ya raia wake zinaongoza nchi hizo za Kijamaa! Ujamaa sio kila kitu kiwe mikononi mwa Serikali, Laa hasha isipokuwa Priority ya Uwekezaji nchini atatazamwa kwanza raia kwa sababu atawatoa katika Umaskini jamii inayomzunguka..
 
ASANTE SANA. Hicho ndicho tunachopaswa kufanya, na sio kuiga sera za kiuaji zinazopambwa na media kubwa kama BBC na CNN. Hao huzipigia chapuo sera za kibepari lakini nchi zao zina mafukara wa kutupwa.

#TANZANIAISNOTFORSALE!
 
Mkandara bwana.

Hujui kuwa Deni la Taifa chini ya Magufuli limekua kwa rate ya kutisha?

Hujui kuwa ndani ya miaka mitano ya kukaa madarakani, Magufuli kakopa zaidi au kwa kukaribiana na ukopaji wa Kikwete alioufanya ndani ya miaka kumi?

Lakini pamoja na hayo Magufuli katapanya pesa kwenye miradi inayotutia hasara, hiyo ATCL unayoisema, tayari tumeshakula hasara ya Bilion 153 ndani ya miaka mitano na tayari tumeshalipa shirika ruzuku ya bilion 150 ndani ya miaka mitano. Wakati huohuo Shirika bado halina safari zozote za maana nje ya nchi.

Lakini pia kuna miradi mingine isiyo na tija, tumetumia pesa za walipa kodi kuifanya, kwa mfano Ujenzi wa uwanja wa ndege kijijini Chato wakati makao makuu ya mkoa, yaani Geita hakuna uwanja.

Kufufua reli ya kati bila kutatua tatizo lililofanya reli hiyo ikafa in the first place itaresult kwenye tija ndogo.
 
Ndugu yangu kazi kubwa ya mabepari ni kuupotosha ulimwengu kwa kuhakikisha wanaupaka ujamaa kinyesi kwa gharama yoyote. Wanajua kuwa siku kila mtu akijua yaliyomo kwenye ujmaa na dunia ikaongozwa kwa misingi hiyo, itawazibia wao mianya ya uporaji.

Hata hizo nchi zinazojiita za kibepari zinatekeleza baadhi ya vipengele vya ujamaa otherwise pasingekalika. Mfano mzuri wa waliojifanya kupuuza vipengele hivyo ni utawala wa Trump. Alipuuza, lakini sote tumeona kilichotokea USA, palimshinda na akatupiwa virago na wapiga kura wa Marekani.

Ubeparini itikadi ya kijambazi, full stop.

#TANZANIAISNOTFORSALE!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…