Uchambuzi wa Kiufundi naunga mkono nchi yetu kununua umeme kutoka inje nchi kuliko kusafilisha hadi kaskazini

........kujenga miundo mbinu ni muda na gharama baasa miaka 15 to 20 wataweza kutawanya kooote .....sio project miezi 6 mkuuu oohhh sikia tuuu....kulipa fidia tu njia kupitisha....bado cost kusafirisha....umbali huo.....feasabilitu study zipo ukiwa access utaziona miradi yote na expansipn zake....hapo hakuna siasaa mkuu
 
Sasa utashangaa Tanzania itaiuzia umeme Kenya kutoka Nyerere Dam kupitia hapo Arusha……😅
 
Sasa utashangaa Tanzania itaiuzia umeme Kenya kutoka Nyerere Dam kupitia hapo Arusha……😅
Ni jambo la muda mrefu! Kulingana na bajeti ya wakati huo!
Kwasasa mikoa ya kaskazini ipate huduma kwanza kwa bajeti ndogo!

Baadae miundombinu ile ile inaweza tumika kuuzia umeme inje siyo dhambi kwa wakati ujao
 
Mkuu shukrani kwa Ufafanuzi, Ila Investment ya Rufiji basin cost us an arm and a leg..

Tungeingia permanent supply contract na hizo nchi mbona hizi kelele zinazotoka sasa zisingekuwepo?

1Milion trees and wildlife, Ecosystem disturbance and Bilions of USD, may be 4?
Just to be told we cant be self sufficient...

Nadhani Rais Samia kaamua kumfichia JPM mapungufu yake big time.

Its always cheaper to rent than to own...lakini yanakuja na gharama zake, vitu kama political instability... Ethiopia isnt that stable.

Tunatokaje hapa tulipo, dead stuck if at all Rufiji wasn't a permanent power solution.
 
Wakati huo nchi itakuwa ishajipanga kwa bajeti inaweza kufanya hivyo!
Na ikauza na huko kenya kwa kutumia miundombinu hiyohiyo watayochukulia kwa sasa!
 
Hoja dhaifu kabisa katika utetezi, hivi unataka kutuambia hiyo mikoa ya kasikazini haina nguzo au mtandao wa umeme?
Je, zile zinazotumika katika hiyo span ya Nyumba ya Mungu na Pangani haiwezi kuunganishwa na ile ya JNHEPP. Ingelikuwa kwamba hayo maeneo hayajawahi kuwa na umeme na gharama ya nguzo na kujenga mtandao wa umeme kutokea JNHEPP hadi huko kasikazini ningekubali kuwa gharama ni kubwa. Lakini ukweli ni kuwa tayari hayo maeneo Yana mtandao wa umeme na kutokana upungufu wa umeme kutoka vyanzo vya Pangani na Nyumba ya Mungu inabidi kuunganishwa na umeme wa ziada kutoka JNHEPP hivyo haihitaji kujenga mtandao mpya, zaidi ya kuunganisha span ya Morogoro to Tanga au Pwani to Tanga.
 
Hapoo tinaemda sawaa....kaficha mengi sanaa....Mwamba alikuwa hadhauriki....ingawa in long run unawaza nchi huru miaka 60 plus hatuna own umeme zaidi 50%? Ndio maana Mwamba hakupenda hizooo....but gharama sanaa....ukiwa nao mwingi hautumiki so what? Kujenga njia miaka 10 hafi zaidi njia moja tu....miaka 30 njia 3 tu....kununua miaka 2 unapata umeme wa jirani....kupanga kuchagua.......opportunity cost
 
Kwa hoja yako mikoa ya mipakani yote inapaswa tununue umeme nje ya nchi/jirani mfano mikoa mikoa iliyombali zaidi kuliko hiyo ya kaskazini kutoka vyanzo ya taifa ni Mara, mwanza na kagera...!?

Na kwa mantiki yako hao wenzetu wanadhibiti vipi gharama na ufujaji na hadi kusambazia sisi?
Mf: kutoka ethiopia-kenya- hadi tz

Muhimu: kwa nionavyo kujijengee uwezo wa kutosheleza mahitaji yetu wenyewe, kama ethiopia alivyoweza..

Kwakuwa tumetumia gharama ya kimazingira na pesa nyingi sana kutekeleza mradi wa JK nyerere.
 
Mkuu kama unatafuta teuzi basi jipange upya uje na hoja zilizoshiba haswaa and not these skinny shits.....Acha kuleta siasa kwenye mambo ya kitaalamu na msingi sana kwenye hili taifa.

Jitahidi sana uwe unafikiria mara mbili mbili ikibidi hata kufanya tafiti kidogo na sio kutumia mihemko.
 
Wewe boya kweli, kwa hiyo unafikiri hapo wizarani kuna malaika, hapo kuna binadamu wengine vilaza kama wewe tu.

Na unaweza kuta kuna bosi mmoja tu ndio anahamua kulishikia bango hata kama kuna wataalamu walishauri tofauti na yeye.
 
Nilikuwa naangalia cost wa china kutengeneza 33KV from Rufiji to Arusha ...600km ngoma ni nzito....1km ina cost $50k....zodisha 50k x 600 ni 30mil $....kama 7T project....miaka 5 hafi 7...kumbuka budget Tanzania ni 50T..2025 to 26.
 
SWALI DOGO: Kuna transmission lines (400kv) zilizojengwa toka Iringa kupitia Singida Babati hadi Arusha katika mradi wa East Africa Power Pool; hizo hazitoshi kufikisha umeme kaskazini?
 
Iko hivi umeme kutoka vyanzo vikuu vya umeme wa uhakika Rufiji na mikoa mingine ukitaka kuusafirisha kwenda mikoa ya kaskazini unakuwa unazungumzia mradi wa wastani wa 800km ~900Km

kwanini kujichosha ilihali kwa jilani anao umeme
Kwa hiyo fundi, huu umeme wa uhakika ni tofauti na umeme tunaotumia sasa? Kwanini ili uusafirishe unahitaji njia mpya kwa makilomita unayoyasema? Kumbe siku zote nchi haina njia za kusafirishia umeme mkubwa Kama huu mpya? Ila naonaga yale maguzo ya chuma yenye miguu minne inasemekana ndio yenye umeme mkubwa je, huu mpya umekataa kupita humohumo ukafika japo singida?
Kwako fundi
 
Kama miaka yote hatuna umeme huko kaskazini, hiyo haraka ya kununua umeme kutoka nje ya nini au kuna nini hasa mpaka muone leo kuna haja ya kununua umeme kutoka nje ya nchi?

Kama kujenga miundo mbinu kuusambaza umeme itachukua miaka 5 hadi 10, kwanini tusifanye hivyo kwa kutumia hizo pesa za kutaka kuagiza umeme kutoka nje?

Sisi wadanganyika hatuna haraka, tumeishi maisha haya ya bila umeme na maji miaka yote na tupo, kwanini leo nyie watu wachache mjifungie huko mtoke na majibu rahisi kama haya, kwamba tununue umeme kutoka nje kwa sababu gharama za kusambaza umeme wetu ni ghali sana.

Kwani gharama za kujenga hilo bwawa Rufiji ni ndogo?

Mbona tuliamua kulijenga?

Malengo ilikuwa ni tujitosheleze sisi kwanza, kwa nishati humu ndani, kisha ziada ndio tuuze nje.

Mimi sijali wewe ni Engineer au Fundi mchundo, mimi sioni kama hiki unachokisema kiko sawa.

Hakuna mradi rahisi, hata SGR siyo rahisi lakini tulijenga na tunaendelea kujenga, kuna mradi wa UDART sio rahisi lakini bado tunaujenga.

Aliyekwambia sisi hatujui kujenga miundombinu kuusambaza huo umeme ni ghali ni nani?

Kama umeme umeshazalishwa wa kutosha na hauna pa kwenda, tusifunge mashine zote au tusimamishe uzalishaji tuanze kutengeneza miundo mbinu ya kuusambaza humu nchini kwanza.

Sidhani kama Magufuli alitaka kujenga bwawa lile ili tufanye biashara, alichoka na vilio vya shirika letu la umeme Tanesco, kusema umeme hautoshi, mara bwawa la Mtera limekauka, mara IPTL mafuta, na upuuzi kama huo, na ndio maana walikuwa wanatupa nishati hiyo kwa mgao.

Kwanini leo muanze kutupanga na kutufundisha biashara badala ya kutafuta njia za kutusambazia umeme?

Kule Kagera, kuna kampuni ya ABB walijenga zile nguzo kutoka uganda sidhani hata kama miaka sita ilifika. Tuwaite hawa watujengee miundombinu ya kuusambaza.

Miaka ile IPTL inaanzishwa tuliambiwa hadith kama hizi, kwamba IPTL itazalisha umeme wa kutosha na utakuwa ni muarobaini kwa tatizo letu la umeme nchini, kumbe ilikuwa miradi ya wezi wachache. Kila siku hesabu zinabadirika.

Wakaja wajanja wengine Richmond, SONGAS yale yale.

Kuna Mbunge mmoja anajiita Dr. Kasheku Musukuma, anasema kuna wapigaji nchi hii, wakitaka kupiga wanakunja na gia za usomi. Wana kuja na maelezo meeengi, kutafuta namna ya kujustfy upigaji wao, kisha wanatokomea gizani.

Kuhitimisha hoja yangu, Sisi hatuna haraka, kama kujenga miundo mbinu ni miaka 5 au 10, jengeni tutasubiri umeme wetu wenyewe.

Huo mnaotaka kuuleta wenyewe auhitaji miundo mbinu ya kuuingiza nchini?

Ikiwa huo nao utahitaji miundombinu, basi nashauri tujenge miundombinu yetu, iwe ya juu au aridhini lakini tuwe na mfumo wetu, tutumie umeme wetu, hatuna haraka.
 
Hakuna hawa ni wale wapigaji tu kama KILIMO KWANZA, walikuja hivi hivi tukaambiwa FAO, OXFARM, World Bank sijui nani kamwaga pesa, njaa nchi hii itakuwa historia.

Wakazila zote, na matrekta sijui waliuza hata huwezi kupata majibu, waka mute.

Hizi hadithi nchi hii sio ngeni, tumezisikia sana, kisha wanapiga wana mute.
 
Samico Tanzania
Uje Ujibu
Hoja Mambo Haya Mazito Na Ujanja Hautakiwi
Umeme Tunao Chekwaa Kwanini Tununue Nje, Tutengeneze Miundombinu
Zanzibar Unapita Baharini Tushindwe Kuufikisha Tanga Jirani
 
WEWE JAMAA MUONGO SANA.

BASI WEKA UZALISHAJI WA MABWAWA HAYO TUONE HUO UPUNGUFU
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…