Uchambuzi wa Kiufundi naunga mkono nchi yetu kununua umeme kutoka inje nchi kuliko kusafilisha hadi kaskazini

Uchambuzi wa Kiufundi naunga mkono nchi yetu kununua umeme kutoka inje nchi kuliko kusafilisha hadi kaskazini

Ethiopia, Uganda, Zambia watu Plan B yao ya umeme wamenunua wapi?

Unasema huwezi kuzima umeme kufanya matengenezo mboma wanazima kilamsiku, hata Dar ilikuwa kwenye mgawo juzi tu hapa.

Unazungumza kuhusu ukame, kwani Ethiopianumeme wao ni Nuclear??

Wanatumia Bwawa na tena Ethiopia ninmchi ambayo inakabiliwa na ukame kuliko sisi?
Na Ethiopia wana ukame bongo inasubiri

Ova
 
Bro kuna mnyama anaitwa pimbi huwa anasahau maelezo kila baada ya dakika tano!
Sasa wewe binadam ambacho kinakufanya usielewe ni nini?

Utafanyaje matengenezo ya kudumu pasipo kuwepo na umeme mbadala ili usevu wananchi wakati wa matengenezo?

Kazi ya kutengeneza mabwawa inahitaji siyo chini ya misimu miwili ya mvua!
Wakati huo hao wananchi watatumia nn pasipokuwepo na umeme mbadala?
Nadhani pimbi wa kwanza ni mtu wa maamuzi huko na ninyi ni vipimbi vidogo dogo ambao mna vimdomo vya Kasuku.

Mwanzo tulikuwa busy kutetea nchi ijitoe kwenye umeme wa kununua Kagera na Rukwa.

Leo tunapambana kununua umeme Ethiopia.

Ila kwa huyu bibi ndio kabisaaa. Pigeni tu
 

Attachments

  • 20250306_140427.jpg
    20250306_140427.jpg
    103.7 KB · Views: 2
  • Screenshot_20250310_134331_YouTube.jpg
    Screenshot_20250310_134331_YouTube.jpg
    133.6 KB · Views: 2
Iko hivi umeme kutoka vyanzo vikuu vya umeme wa uhakika Rufiji na mikoa mingine ukitaka kuusafirisha kwenda mikoa ya kaskazini unakuwa unazungumzia mradi wa wastani wa 800km ~900Km

Unajua kama kuna line za 400kV zimeshajengwa, zinaunga Arusha, Namanga, Babati, Singida mpaka Dodoma ? Hizo 800km mpaka 900km unazipata wapi ?

Hilo jambo linahitaji maelezo ya kitaalamu zaidi ambayo huyapati.
 

Hizo ni data za 2023 peak ya matumizi ya umeme ilikua ni 1400MW, na capacity 1900MW

Mpaka January 2025 capacity ishaongezwa 3000+ MW na inategemea kufika mwisho wa mwaka kufika 4000MW.

Umeme ni mwingi sana, kuusambaza ni issue nyengine
Sasa Kuna faida gani yakuzalisha bidhaa kwa wingi ili hali hamna marketing strategy ya kuwafikishia wateja?

Ni uzembe wa kipumbavu,yaani unafungua kiwanda cha sababuni halafu unakwepa kuingia gharama za usagirishaji wa bidhaa zako kwenda sokoni ili hali wateja wana hitaji then unaamua kuacha bidhaa yako store nakupasia wateja kwa kampuni nyingine ?
 
Gharama za kusafirisha umeme kwa umbali huo ni kubwa mno ukilinganisha na kuuchukulia hapo kenya .
Wanaposema umeme wa Ethiopia haina maana uko huko Ethiopia! Ni uko hapo jilani kenya wastani wa km 250km~300km tu

Unajua kama kuna line ya 400kV, imefika Namanga ikitokea huku, na imeunga line za Babati, Singida mpaka Dodoma ?

Halafu zinaunga mpaka Mbeya, yaani muunganiko upo kwa namna yoyote kwa ndani kwetu tu huwezi kupata hiyo 800km au 900km.
 
Kule kwetu Rukwa tunatumia umeme wa Zambia all those years na hata kukitokea changamoto gridi ya taifa sisi huwa tunapeta tu tunabaki kuwashangaa

Na Sasa hivi inapelekwa 400kV, kwa ajili ya ku upgrade kutoka kwenye 66kV.

Tapping ikitokea Tagamenda Substation, Iringa.
 
Wachina hawajui hata kiswahili wanapiga kazi wewe hiyo lugha inakusaidia nini ndugu yangu! Mimi ni fundi sijasoma kama wewe ndugu lakini nina uzoefu wa hizi kazi zina gharama kubwa mno.

Ila Kiswahili ni lugha yako, ulitakiwa ukijue vizuri. Hata hao Wachina wamenipa lugha ya kiapaumbele ndio maana wamefika hapo walipo.
 
Kule kwetu Rukwa tunatumia umeme wa Zambia all those years na hata kukitokea changamoto gridi ya taifa sisi huwa tunapeta tu tunabaki kuwashangaa
Na kwa kweli ule umeme Huwa haukatiki mara kwa mara.... Nimefanya kazi huko kipindi Fulani nimejionea....
 
SWALI DOGO: Kuna transmission lines (400kv) zilizojengwa toka Iringa kupitia Singida Babati hadi Arusha katika mradi wa East Africa Power Pool; hizo hazitoshi kufikisha umeme kaskazini?

Hapa ndipo Kuna hoja wanatakiwa watuambie. Hizi zinafanya kazi gani ? Sababu zipo na tunazijua vizuri.
 
Sasa Kuna faida gani yakuzalisha bidhaa kwa wingi ili hali hamna marketing strategy ya kuwafikishia wateja?

Ni uzembe wa kipumbavu,yaani unafungua kiwanda cha sababuni halafu unakwepa kuingia gharama za usagirishaji wa bidhaa zako kwenda sokoni ili hali wateja wana hitaji then unaamua kuacha bidhaa yako store nakupasia wateja kwa kampuni nyingine ?
Wewe sio mfanyabiashara, take yako ni ya Ki layman.

Labda nikueleweshe taratibu utaelewa.

Una maduka yako mawili moja lipo Dar na jengine lipo mwanza, kwenye maduka unauza mchele, Huku dar una machine yako ya kukoboa huo mchele, ila mwanza Huna, kutokana na Gharama za kuleta Mpunga Dar, ukaamua kule kule mwanza upeleke machine ya mtu mwengine akukobolee mpaka utakapopata machine yako. Ungeleta Mchele Dar ukobolewe halafu urudishwe mwanza Gharama zingekuwa kubwa.

Outsourcing kupunguza gharama ni common practise kwenye biashara.

Cha muhimu hapo ni sisi huo umeme wetu tuuze Nchi za jirani sehemu ambayo miundombinu yetu ipo vizuri, mfano sasa hivi kuna Mradi wa Takriban Trilioni 1 kupeleka umeme Zambia.
 
Hapa ndipo Kuna hoja wanatakiwa watuambie. Hizi zinafanya kazi gani ? Sababu zipo na tunazijua vizuri.
Hiyo transmission line ya 400kv kutoka grid ya taifa inapeleka umeme mikoa ya kati na kanda ya ziwa ina kiwango chake cha kubeba mwisho Megawatts 550~600MW

Kuna ongezeko kubwa la umeme hasa maeneo ya migodini linalotegemea hiyo line!

Ukiamua kuibebesha mzigo mwingine wa mikoa ya kaskazini haitakubali kubeba lazima gridi itatoka kila mara na kupelekea mgao wa kijinga kabisa!

Njia ya uhakika ni kujengwa powerline nyingine itakayolisha mikoa ya kaskazini ambacho ndicho serikali inafanya kwa kuzingatia gharama za mradi!
Kuchukua hapo Namanga kenya inaonekana ni gharama nafuu zaidi kuliko kujenga power line mpya kutoka Rufiji
 
Unajua kama kuna line ya 400kV, imefika Namanga ikitokea huku, na imeunga line za Babati, Singida mpaka Dodoma ?

Halafu zinaunga mpaka Mbeya, yaani muunganiko upo kwa namna yoyote kwa ndani kwetu tu huwezi kupata hiyo 800km au 900km.
Hiyo transmission line ya 400kv kutoka grid ya taifa inapeleka umeme mikoa ya kati na kanda ya ziwa ina kiwango chake cha kubeba mwisho Megawatts 550~600MW

Kuna ongezeko kubwa la umeme hasa maeneo ya migodini linalotegemea hiyo line!

Ukiamua kuibebesha mzigo mwingine wa mikoa ya kaskazini haitakubali kubeba lazima gridi itatoka kila mara na kupelekea mgao wa kijinga kabisa!

Njia ya uhakika ni kujengwa powerline nyingine itakayolisha mikoa ya kaskazini ambacho ndicho serikali inafanya kwa kuzingatia gharama za mradi!
Kuchukua hapo Namanga kenya inaonekana ni gharama nafuu zaidi kuliko kujenga power line mpya kutoka Rufiji
 
Mkuu, unaongelea changamoto ya kusafirisha kama vile Kaskazini ni mikoa mipya inayohitaji kuanza michakato ya ujenzi wa miundombinu ya usafirishaji wa umeme.

Mpaka sasa mikoa hii inatumia umeme wa Gridi ya taifa, kwahiyo hakuna hizo gharama za ujenzi, fidia wala muda kama ulivyotueleza hapa.

Nakubaliana na wewe kwenye point mbili ambazo ni unafuu wa umeme unaotoka Ethiopia kuliko tunaozalisha sisi, na pia suala la kuepuka gharama za upotevu unaotokana na conduction resistance.

Lakini tukirudi kwenye uhakisia, hatukustahili kununua umeme huu, badala yake tujenge powerstations hata kama ni kwa muda mrefu lakini tutakua na uhakika wa kutumia umeme wetu.

Serikali inatushika kwa kutaja hasara ya 32 B kwa kupoteza hizo 17 MW zinazopotea kwenye usafirishaji wa kuelekea kaskazini, lakini wasichotueleza kwamba hiyo ni hasara ya kimahesabu na sio hasara halisia. Ni sawa na mtu alieweka mkeka kwa gharama ya elfu 10 kubetia timu fulani ishinde apate Millioni 1, katikati ya mechi akaamua kusitisha ubashiri wake baada ya kusahwishiwa na laki 3 kwa kuhofia timu yake ingepoteza. Huyo mtu anaweza kusema amepata hasara ya laki 7 kwasababu asingesitisha angepata milioni, lakini kiuhalisia anakua kapata faida ya laki mbili na 90.

Hicho ndicho tunafanya sisi pia, tunaepusha kupoteza 17 MW ambazo zitabaki kama ziada tu kwenye gridi na badala yake tunaenda kununua 100 MW ambazo pamoja na kuwa za bei rahisi, lakini zitakua na gharama zaidi ya hiyo 32 B tunayopoteza. Kwa hesabu za mtaani tunakua tumepata hasara zaidi.

Nadhani uamuzi sahihi ulikua kujifunza teknolojia wanayotumia wao kufikisha umeme wao Namanga kwa gharama nafuu na sisi tuanze kujichanga kutengeneza miundombinu yetu ifikie ubora huo, ikiwemo kujenga hizo Substations za HVDC.
 
Hiyo transmission line ya 400kv kutoka grid ya taifa inapeleka umeme mikoa ya kati na kanda ya ziwa ina kiwango chake cha kubeba mwisho Megawatts 550~600MW

Kuna ongezeko kubwa la umeme hasa maeneo ya migodini linalotegemea hiyo line!

Ukiamua kuibebesha mzigo mwingine wa mikoa ya kaskazini haitakubali kubeba lazima gridi itatoka kila mara na kupelekea mgao wa kijinga kabisa!
Kwani zile High voltage transmission lines zinazoenda migodini zimeunganishwa kwenye hiyo line?

Maana ninazifahamu za Buzwagi na Bulyanhulu ambazo nilidhani zinajitegemea na ndio maana zina vituo vyake vya kupozea kwa maana zinachukua umeme moja kwa moja kwenye vituo vya kufua umeme. Geita pia inachukua moja kwa moja Nyakanazi kule.

Huo mzigo zilioongeza ni upi?
 
Hiyo transmission line ya 400kv kutoka grid ya taifa inapeleka umeme mikoa ya kati na kanda ya ziwa ina kiwango chake cha kubeba mwisho Megawatts 550~600MW

Kuna ongezeko kubwa la umeme hasa maeneo ya migodini linalotegemea hiyo line!

Ukiamua kuibebesha mzigo mwingine wa mikoa ya kaskazini haitakubali kubeba lazima gridi itatoka kila mara na kupelekea mgao wa kijinga kabisa!

Njia ya uhakika ni kujengwa powerline nyingine itakayolisha mikoa ya kaskazini ambacho ndicho serikali inafanya kwa kuzingatia gharama za mradi!
Kuchukua hapo Namanga kenya inaonekana ni gharama nafuu zaidi kuliko kujenga power line mpya kutoka Rufiji
Unajua kama Arusha tayari Kuna 400kV ? Na imeungana na na line za Babati, Singida mpaka Dodoma ?
 
Na wewe kasome power loss na power factor katika transmission!

Hapa nimetumia lugha rahisi kabisa ili hata mwananchi wa chini aelewe!

Ukitaka niongee lugha za umeme mwanzo mwisho wengi wasingeeelewa!

Hata nchi zilizoendelea zinanunua kutoka inje, Tanzania haitakuwa ya kwanza!

Na kingine ambacho huwezi kukijua unapoongezea umeme kutoka inje unakuwa umeongeza flexibility katika gridi ya taifa .
Note; Gridi ipo lakini huo umeme wa kutoka inje ni plani B, wakati Plan A Ikiendelea taratibu hatua kwa hatua.
Jf haina mwananchi wa kawaida, kuna watu wenye taaluma na uelewa mpana. acha uchawa.
 
Hiyo transmission line ya 400kv kutoka grid ya taifa inapeleka umeme mikoa ya kati na kanda ya ziwa ina kiwango chake cha kubeba mwisho Megawatts 550~600MW

Huko Ethiopia inatoka line ya voltage ngapi na inabeba power kiasi gani ?

Fafanua kitaalamu hili jambo, sio kwa mtindo huu unao ufanya wewe.
 
Kuna ongezeko kubwa la umeme hasa maeneo ya migodini linalotegemea hiyo line!

Ukiamua kuibebesha mzigo mwingine wa mikoa ya kaskazini haitakubali kubeba lazima gridi itatoka kila mara na kupelekea mgao wa kijinga kabisa!

Ongezeko kwa kiwango cha 400kV kuzidiwa au ?

Ethiopia unatoka umeme wa Volt ngapi kuingia kwetu ? Ni 765kV au 1000kV ?
 
M
Unataka kuniambia wewe unaakili kuliko wizara waliotathimini wakaona wakachukulie kenya!
Wakati mwingine Vijana tunahoji vitu vingine havina hata msingi!

Nimekutolea mfano ungekuwa wewe ungesafilisha maji kutoka Dar upeleke dodoma wakati Dom kuna mtu anatafta wateja kwa gharama nafuu?
Mkuu usisubstute wizara hapo, lazmz ujue ufisad unaofanyika nchi mbalimbali dunian ni vitengo vinavvyofanya chini ya wizara na maraisi. Hivyo tujkite kwenye hoja bila kujali wizara. Maana ujue kwa hapa kwetu wizara wala serikali hazikosei mfano issue ya DP world.
 
Mkuu, unaongelea changamoto ya kusafirisha kama vile Kaskazini ni mikoa mipya inayohitaji kuanza michakato ya ujenzi wa miundombinu ya usafirishaji wa umeme.

Mpaka sasa mikoa hii inatumia umeme wa Gridi ya taifa, kwahiyo hakuna hizo gharama za ujenzi, fidia wala muda kama ulivyotueleza hapa.

Nakubaliana na wewe kwenye point mbili ambazo ni unafuu wa umeme unaotoka Ethiopia kuliko tunaozalisha sisi, na pia suala la kuepuka gharama za upotevu unaotokana na conduction resistance.

Lakini tukirudi kwenye uhakisia, hatukustahili kununua umeme huu, badala yake tujenge powerstations hata kama ni kwa muda mrefu lakini tutakua na uhakika wa kutumia umeme wetu.

Serikali inatushika kwa kutaja hasara ya 32 B kwa kupoteza hizo 17 MW zinazopotea kwenye usafirishaji wa kuelekea kaskazini, lakini wasichotueleza kwamba hiyo ni hasara ya kimahesabu na sio hasara halisia. Ni sawa na mtu alieweka mkeka kwa gharama ya elfu 10 kubetia timu fulani ishinde apate Millioni 1, katikati ya mechi akaamua kusitisha ubashiri wake baada ya kusahwishiwa na laki 3 kwa kuhofia timu yake ingepoteza. Huyo mtu anaweza kusema amepata hasara ya laki 7 kwasababu asingesitisha angepata milioni, lakini kiuhalisia anakua kapata faida ya laki mbili na 90.

Hicho ndicho tunafanya sisi pia, tunaepusha kupoteza 17 MW ambazo zitabaki kama ziada tu kwenye gridi na badala yake tunaenda kununua 100 MW ambazo pamoja na kuwa za bei rahisi, lakini zitakua na gharama zaidi ya hiyo 32 B tunayopoteza. Kwa hesabu za mtaani tunakua tumepata hasara zaidi.

Nadhani uamuzi sahihi ulikua kujifunza teknolojia wanayotumia wao kufikisha umeme wao Namanga kwa gharama nafuu na sisi tuanze kujichanga kutengeneza miundombinu yetu ifikie ubora huo, ikiwemo kujenga hizo Substations za HVDC.
Endelea kubeti tu kunaweza kukutoa
 
Back
Top Bottom