Sakata la wauguzi huko mkoani tabora waliokuwa wakibishana juu ya matumizi ya vifaa vilivyoisha muda wake limeibua maoni mengi sana ya watu!
Wengi wao wameishia kulitazama kwa juu juu na kumuona yule afisa binti mwenye Rafudhi ya KIJITA mix na KIKURYA kwamba ndiye mkosaji na yule mwingine yuko sahihi
Ukitaka kuwaelewa vizuri wahudumu hawa kwanza kabisa fanya kama unaheshimu mawazo ya kila mmoja wao kama ifuatavyo!
A) Anaepinga vifaa vilivyoisha visitumike!
Mawazo ya afisa huyu yapo sahihi lakini sehemu pasipo sahihi! Naposema usahihi wake ni sahihi pasipo sahihi namaanisha aliyemwambia (Binti) Je, alikuwa mtu sahihi kufanya maamuzi yoyote ya kubadilisha? Je kulikuwa na mbadala?, Je taarifa za ukomo wa matumizi mganga mkuu wa hospital alikuwa nazo? Je Shifting ya Jana yake siku hiyo walitumia nini? Kwanini havikuondolewa kama vimeisha muda wake? Ukitafta majibu ya hayo unaona kabisa yule afisa alikuwa sahihi lakini pasipo sahihi!
B) Afisa aliyetaka vitumike!
Huyu ukimtafakali kwa juu juu huwezi kuona jambo lakini kuna jambo, ukichimba unaona naye anajambo, unaona kabisa huyu kwa maoni yake hakukuwa na mbadala hivyo yupo sahihi! Au amechoka kusubili,
Huyu afisa anaishi kwenye falsafa ya Funika kombe mwanaharamu Apite!
Falsafa hii ndiyo falsafa ya serikali isiyojali maisha ya watu!
Yamkini huyu binti anataarifa zote za ukosefu wa vifaa tiba, na yamkini hakuna jitihada za kupata Leo au kesho!
Pia huwezi kuacha kujiuliza maswali haya! Kama vifaa tiba vipya vipo kwanini asingetoa vipya? Kwanini vilivyoisha vilibakia kuwepo hospitali hapo? Je anamkomoa nani? Na anamlinda nani?
Ukitafakali kwa kina sakata hili utagundua wote wapo sahihi lakini tofauti ni kwamba!
1. Aliyekataa anatetea taaluma yake.
2. Yule binti anayeruhusu anatetea Tumbo lake!
Na Mara nyingi serikali ya kimasikini imezungukwa na watu wanaotetea matumbo kuliko wanaoetetea taaluma zao!
Mifumo ya ugavi na manunuzi vifaa tiba katika hospital na ofisi za umma imejaa milolongo mireefu ambayo ni kero kwa maafisa! (Wanachoka bora liende)
Hivyo Dawa ya hawa watumishi ni kuwahamisha ili wasije tegeneza bomu la kuhatarisha maisha yao na ya wagonjwa!
Mkosaji mkubwa katika sakata hilo nimsambazaji wa vifaa tiba, ni mganga mkuu ambaye hakuviondoa vifaa vilivyoisha muda wake hospitalini, ni serikali yenye wajibu wakupeleka vifaa tiba kwa wakati!
Sakata hilo ni kipande kidogo sana cha Uozo mwingi uliopo mahospitali karibu yote Tanzania!
Huyo binti ni kielelezo cha wahudumu walio wengi Tanzania ambao wanaijua serikali hivyo wameamua kwenda nayo kama ilivyo!
Yule kijana akiadhibiwa itavunja moyo, na yule binti akiadhibiwa napo itafedhehesha Mioyo!
Nina uhakika 100% Report ya waziri itaishia kukanusha kwamba hakukuwa na vifaa tiba vilivyoisha na wale wahudumu watahamishwa kwa migogoro binafsi!
Tunaoumia ni SISI!
Updates
Wahudumu wote waliokuwa wanabishana kuhusu matumiz ya vifaa vibovu wamesimamishwa kazi!
Hapo ndipo utaelewa huyo wa kiume kosa lake ni lipi!
Ukitaka kulielewa hilo kosa rudia kusoma Uzi huu hapo juu!
Bahati mbaya hata kabla ya uchunguzi kuanza tayali waziri kashakanusha kwamba HAKUNA KIFAA TIBA KILICHOISHA MUDA WAKE NCHI NZIMA!
Wengi wao wameishia kulitazama kwa juu juu na kumuona yule afisa binti mwenye Rafudhi ya KIJITA mix na KIKURYA kwamba ndiye mkosaji na yule mwingine yuko sahihi
Ukitaka kuwaelewa vizuri wahudumu hawa kwanza kabisa fanya kama unaheshimu mawazo ya kila mmoja wao kama ifuatavyo!
A) Anaepinga vifaa vilivyoisha visitumike!
Mawazo ya afisa huyu yapo sahihi lakini sehemu pasipo sahihi! Naposema usahihi wake ni sahihi pasipo sahihi namaanisha aliyemwambia (Binti) Je, alikuwa mtu sahihi kufanya maamuzi yoyote ya kubadilisha? Je kulikuwa na mbadala?, Je taarifa za ukomo wa matumizi mganga mkuu wa hospital alikuwa nazo? Je Shifting ya Jana yake siku hiyo walitumia nini? Kwanini havikuondolewa kama vimeisha muda wake? Ukitafta majibu ya hayo unaona kabisa yule afisa alikuwa sahihi lakini pasipo sahihi!
B) Afisa aliyetaka vitumike!
Huyu ukimtafakali kwa juu juu huwezi kuona jambo lakini kuna jambo, ukichimba unaona naye anajambo, unaona kabisa huyu kwa maoni yake hakukuwa na mbadala hivyo yupo sahihi! Au amechoka kusubili,
Huyu afisa anaishi kwenye falsafa ya Funika kombe mwanaharamu Apite!
Falsafa hii ndiyo falsafa ya serikali isiyojali maisha ya watu!
Yamkini huyu binti anataarifa zote za ukosefu wa vifaa tiba, na yamkini hakuna jitihada za kupata Leo au kesho!
Pia huwezi kuacha kujiuliza maswali haya! Kama vifaa tiba vipya vipo kwanini asingetoa vipya? Kwanini vilivyoisha vilibakia kuwepo hospitali hapo? Je anamkomoa nani? Na anamlinda nani?
Ukitafakali kwa kina sakata hili utagundua wote wapo sahihi lakini tofauti ni kwamba!
1. Aliyekataa anatetea taaluma yake.
2. Yule binti anayeruhusu anatetea Tumbo lake!
Na Mara nyingi serikali ya kimasikini imezungukwa na watu wanaotetea matumbo kuliko wanaoetetea taaluma zao!
Mifumo ya ugavi na manunuzi vifaa tiba katika hospital na ofisi za umma imejaa milolongo mireefu ambayo ni kero kwa maafisa! (Wanachoka bora liende)
Hivyo Dawa ya hawa watumishi ni kuwahamisha ili wasije tegeneza bomu la kuhatarisha maisha yao na ya wagonjwa!
Mkosaji mkubwa katika sakata hilo nimsambazaji wa vifaa tiba, ni mganga mkuu ambaye hakuviondoa vifaa vilivyoisha muda wake hospitalini, ni serikali yenye wajibu wakupeleka vifaa tiba kwa wakati!
Sakata hilo ni kipande kidogo sana cha Uozo mwingi uliopo mahospitali karibu yote Tanzania!
Huyo binti ni kielelezo cha wahudumu walio wengi Tanzania ambao wanaijua serikali hivyo wameamua kwenda nayo kama ilivyo!
Yule kijana akiadhibiwa itavunja moyo, na yule binti akiadhibiwa napo itafedhehesha Mioyo!
Nina uhakika 100% Report ya waziri itaishia kukanusha kwamba hakukuwa na vifaa tiba vilivyoisha na wale wahudumu watahamishwa kwa migogoro binafsi!
Tunaoumia ni SISI!
Updates
Wahudumu wote waliokuwa wanabishana kuhusu matumiz ya vifaa vibovu wamesimamishwa kazi!
Hapo ndipo utaelewa huyo wa kiume kosa lake ni lipi!
Ukitaka kulielewa hilo kosa rudia kusoma Uzi huu hapo juu!
Bahati mbaya hata kabla ya uchunguzi kuanza tayali waziri kashakanusha kwamba HAKUNA KIFAA TIBA KILICHOISHA MUDA WAKE NCHI NZIMA!