Uchumi wetu unaweza kuanza kuanguka mwishoni mwa 2023: Rais Samia anahitaji "National Security Advisor" aliyebobea sana

Uchumi wetu unaweza kuanza kuanguka mwishoni mwa 2023: Rais Samia anahitaji "National Security Advisor" aliyebobea sana

Inashangaza sana pale ambapo kupanda kwa bei za vitu kunahusishwa na kufungua nchi, mfano; mazao kuuzwa nje ya nchi kulilenga kuongeza pato kwa mkulima, lakini ajabu bei ya mbolea nayo inapanda kila siku, sasa hapa kuna haja gani ya kuhangaika kuzunguka dunia yote kwa kisingizio cha kufungua nchi wakati hapa ndani mambo ndio kwanza yanazidi kujifunga?

Namshauri Rais aache kufanya kazi kwa kukariri, habari ya kufungua nchi sasa imeshafeli; kuna tatizo kubwa sana la ukosefu wa ajira, halafu on top of that gharama za maisha zinazidi kupanda, atulie chini na wataalamu wa uchumi wamuoneshe namna mambo yanavyotakiwa kwenda, kuliko kuendelea kupanda ndege kila siku wakati impact ya hizo safari zake kwa mtanzania wa kawaida ni zero.

Kikwete licha ya kupanda ndege miaka yake yote bado uchumi wa nchi ulikuwa mbaya na tatizo la ajira lilikuwepo, huu ushauri anaopewa ni vyema sasa atulie chini achanganye na zake, atuoneshe yeye kama yeye ana kitu gani kwenye kichwa chake, anataka kuiona Tanzania inaelekea wapi kwa mipango mipya ipi, sio hii ya kufungua nchi kila siku huku mambo yetu ndani yanazidi kuwa magumu.
Sasa mtu aliyeokota Urais anaweza kuwa na vision gani zaidi ya kuwasikiliza akina vasco da gama wabembeaji kule jamaica?
 
Inashangaza sana pale ambapo kupanda kwa bei za vitu kunahusishwa na kufungua nchi, mfano; mazao kuuzwa nje ya nchi kulilenga kuongeza pato kwa mkulima, lakini ajabu bei ya mbolea nayo inapanda kila siku, sasa hapa kuna haja gani ya kuhangaika kuzunguka dunia yote kwa kisingizio cha kufungua nchi wakati hapa ndani mambo hii ya kufungua nchi kila siku na kuhutubia kila aendako huku mambo yetu ndani yanazidi kuwa magumu.
kabla ya kukosoa au kulaumu ni vyema ukaangalia sababu ya mfumuko wa bei nini, maana hili ni tatizo la dunia nzima kwa sasa likihusianishwa moja kwa moja na kupanda kwa bei za nishati, sasa tukianza kumlaumu mama bila hoja ya msingi tutakua tunamuonea, ht Biden huko kichwa kinamuuma ameamuru kutolewa kwa mafuta kutoka kwe hifadhi ya taifa lkn wachumi wanasema haitasaidi sana km OPEC na wazalishaji wengine wa nishati hawataongeza uzalishaji, japan nao wanafikiria kutumia hifadhi yao ya mafuta kudeal na hali,
 
Uzi fikirishi sana...

Hii nchi inahitaji reforms upya... Kwanza maendeleo yanashindwa kufika chini kwasababu hapo kati kuna milolongo ya watu wengi sana ambao ndio wanakwamisha vitu vingi...

Yaani mfano.. decision tu ya kujenga darasa ina msururu wa watu kibao hadi darasa likamilike... Na wote wanataka kitu kidogo..

Ni kupambana tu,,, serikali ni mimi na wewe..
 
Shikamoo mama. Pole na majukumu. Bado ninaamini kuwa wewe una utu. Endelea kuwa na utu na siyo ulegevu. Majizi ni mengi kuliko idadi za pikipiki zilizoko mkoa wa Katavi. I love you. Naomba nikupe ushauri.

Data zinaonyesha mambo yafuatayo:


Siku njema. Ngoja nipate kwanza breakfast.
kwasasa nchi nyingi dunian zinaendelea na shughuli za uchumi na hazina mpango wa kurejesha lock down za kitaifa hali ya kiuchumi 2023 itakuwa nzuri kuliko mwaka jana na mwaka huu
 
kwasasa nchi nyingi dunian zinaendelea na shughuli za uchumi na hazina mpango wa kurejesha lock down za kitaifa hali ya kiuchumi 2023 itakuwa nzuri kuliko mwaka jana na mwaka huu
hio ni issue nyingine ila mi nlikua najibu tu kuhusu hii issue ya inflation anayolaumiwa
 
hio ni issue nyingine ila mi nlikua najibu tu kuhusu hii issue ya inflation anayolaumiwa
Ikiwa kama unahitaji kuweka ziada ya taarifa bonyeza kitufe cha edit kwenye comment yako kisha utaongezea au ujumbe wako kuweeka kwenye utaratibu mwengine na kuuweka tena.
 
Uzi fikirishi sana...

Hii nchi inahitaji reforms upya... Kwanza maendeleo yanashindwa kufika chini kwasababu hapo kati kuna milolongo ya watu wengi sana ambao ndio wanakwamisha vitu vingi...

Yaani mfano.. decision tu ya kujenga darasa ina msururu wa watu kibao hadi darasa likamilike... Na wote wanataka kitu kidogo..

Ni kupambana tu,,, serikali ni mimi na wewe..
kuna baadhi ya vitu lazima viwepo katika hatua flani hivi ya maendeleo na kila nchi lazima ipitie vitu hivyo, kuna baadhi ya reforms zinahitaji gharama kubwa kuzimaintain ukilonganisha na faida zitazoleta kwa wakati huo lkn reforms hizohizo zikifanyika miaka 20 au 25 baadae zinaweza kuwa na tija kulingana na level ya maendeleo ya wakati huo so sometimes huenda tukawa tunademand too much may be
 
Ikiwa kama unahitaji kuweka ziada ya taarifa bonyeza kitufe cha edit kwenye comment yako kisha utaongezea au ujumbe wako kuweeka kwenye utaratibu mwengine na kuuweka tena.
sijaelewa unamaanisha nn bosi
 
Inashangaza sana pale ambapo kupanda kwa bei za vitu kunahusishwa na kufungua nchi, mfano; mazao kuuzwa nje ya nchi kulilenga kuongeza pato kwa mkulima, lakini ajabu bei ya mbolea nayo inapanda kila siku, sasa hapa kuna haja gani ya kuhangaika kuzunguka dunia yote kwa kisingizio cha kufungua nchi wakati hapa ndani mambo ndio kwanza yanazidi kujifunga?

Namshauri Rais aache kufanya kazi kwa kukariri, habari ya kufungua nchi sasa imeshafeli; kuna tatizo kubwa sana la ukosefu wa ajira, halafu on top of that gharama za maisha zinazidi kupanda, atulie chini na wataalamu wa uchumi wamuoneshe namna mambo yanavyotakiwa kwenda, kuliko kuendelea kupanda ndege kila siku wakati impact ya hizo safari zake kwa mtanzania wa kawaida ni zero.

Kikwete licha ya kupanda ndege miaka yake yote bado uchumi wa nchi ulikuwa mbaya na nchi ikageuzwa shamba la bibi, huu ushauri anaopewa ni vyema sasa atulie chini achanganye na zake, atuoneshe yeye kama yeye ana kitu gani kwenye kichwa chake, anataka kuiona Tanzania inaelekea wapi kwa mipango mipya ipi, sio hii ya kufungua nchi kila siku na kuhutubia kila aendako huku mambo yetu ndani yanazidi kuwa magumu.
Hana mipango yeyote yeye kamezeshwa kuwa hela yeyote inayotoka huko kwa mabeberu apite nayo kwa ajili ya kujenga madarasa na zahanati na barabara
 
Kuna mtu alisema advisor ni Bill Clinton labda kama zilikuwa story za mtaani.
Mengi uliyoweka naunga mkono kwa kugonga kistuli changu maana sina meza ningegonga kama wabunge. Sijasikia ukigusia bandari ya Bagamoyo itakayokuwa na miundo mbinu ya kisasa kuliko zote nchini.Naona kama tunaingizwa mkenge kiasi kwamba ikisha kamilika mchina ataanza kudai deni lake la sivyo tumalizane kwa kufunga bandari zote na kumwachia yeye peke yake. Naona mbeleni mchina akiwa anaingiza bidhaa kutoka nchini kwake na kuzitawanya nchini huku akizuia uzalishaji wa ndani unaofanana na bidhaa anazotaka ziingie. Mpaka sasa haijulikani nani mkweli kati ya waziri Mwambe aliyesema mkataba haukuwepo, JK (Aliyeweka jiwe la msingi, na Magu(RIP) aliyesema mkataba ni mbovu.
Hii bandari haiwez kujengwa Abadan jiulize kikwete tu aliyeleta huo mradi hakuweza kusaini na kuruhusu ujenzi itakuwaje huyu mama aiseee . Usalama wa Taifa sio wapuuzi kias hicho waruhusu mama aingie mkataba wa ovyo kiasi hicho hili hataweza na akijifanya anataka kulazimisha mambo watamkolimba
 
kabla ya kukosoa au kulaumu ni vyema ukaangalia sababu ya mfumuko wa bei nini, maana hili ni tatizo la dunia nzima kwa sasa likihusianishwa moja kwa moja na kupanda kwa bei za nishati, sasa tukianza kumlaumu mama bila hoja ya msingi tutakua tunamuonea, ht Biden huko kichwa kinamuuma ameamuru kutolewa kwa mafuta kutoka kwe hifadhi ya taifa lkn wachumi wanasema haitasaidi sana km OPEC na wazalishaji wengine wa nishati hawataongeza uzalishaji, japan nao wanafikiria kutumia hifadhi yao ya mafuta kudeal na hali,
Tell me, mpaka leo huko kufungua kwake nchi ameshatengeneza ajira ngapi? una data zozote? na hii idea ameiokota kwa Kikwete, sasa tell me again, Kikwete licha ya kuzurura ulimwenguni kote alisaidia nini kupunguza tatizo la ajira zaidi ya wale wapiga dili waliokuwepo wakati wake?

Kabla hujaja na habari ya soko la dunia [ kisingizio chenu kila wakati], tell me, serikali ina mpango gani wa kuikwamua nchi na mtanzania kutoka hapa alipogota sasa, mpaka bei ya nyama imepanda nayo tulaumu mfumuko wa bei duniani licha ya n'gombe wote tulionao?! tell me kuna mpango gani?
 
hahaa hatari
Miaka 5 itaishia hivyo hivyo, ubelgiji, ufaransa, uingereza, marekani, canada, denmark, urusi, china .....n the list goes on huku nyie mnapigiwa story za madarasa tu😅 mama katoa bil. Flani kwa ajili ya shule mara kwa ajili ya darasa😅

Term ikiisha deni ni 150 trillion! Huku kilo ya nyama ni 20,000/= ndo mtajua hamjui😅😅😅
 
Tell me, mpaka leo huko kufungua kwake nchi ameshatengeneza ajira ngapi? una data zozote? na hii idea ameiokota kwa Kikwete, sasa tell me again, Kikwete licha ya kuzurura ulimwenguni kote alisaidia nini kupunguza tatizo la ajira zaidi ya wale wapiga dili waliokuwepo wakati wake?

Kabla hujaja na habari ya soko la dunia [ kisingizio chenu kila wakati], tell me, serikali ina mpango gani wa kuikwamua nchi na mtanzania kutoka hapa alipogota sasa, kuna mpango gani?
lkn mi nlikua najibu hoja yako kuhusu inflation tu brother, km haya uliosema hapo ndo yamesababisha hii inflation ya sasa sawa, naona umeshanitafutia upande tayari dah!
 
Shikamoo mama. Pole na majukumu. Bado ninaamini kuwa wewe una utu. Endelea kuwa na utu na siyo ulegevu. Majizi ni mengi kuliko idadi za pikipiki zilizoko mkoa wa Katavi. I love you. Naomba nikupe ushauri.

Data zinaonyesha mambo yafuatayo:

1. Mwaka 2022 yawezekana kukawa na njaa Kali sana nchini.
2. Maisha yamepanda sana kwa sasa. Kwa sasa wafanyabiashara wanapandisha bei ya vitu namna wanavyotaka na wanavyojisikia.
3. Biashara nyingi ambazo ni formal zinasinyaa lakini taratibu sana tena sana.
4. Jitihada za kuipunguza na kui-manage informal sector hazipo tena. Kumbuka hii informal sector yetu ina athari mbaya zaidi kwenye uchumi, hasa mapato.
5. "Covid ya 2022" imekaribia.
6. Kodi zinaushambulia uchumi wakati uzalishaji umepungua.

Tusipotafuta majawabu ya hizi hatari sita hapo juu, kuna hatari ya uchumi wetu kuanza kuanguka mwanzoni mwa October 2023 na inaweza kutuchukua muda mrefu kurudi katika hali ya kawaida. Naomba nikupe tips zitakazokusaidia katika majadiliano ya kutafuta solutions. Ninaweza kuwa niko wrong pia.

1. Food security ni neno pana sana. Food security ni usalama wa taifa. Kama ningekuwa mkurugenzi wa usalama wa taifa let's say 2005, ningekuwa na mpango wa ku-forestate taifa kwa angalau miti bilion moja kwa miaka 16. Ningetengeneza misitu mikubwa sana ya kitaifa na maziwa makubwa (siyo ya kwangu. Namaanisha lakes) ambayo ni artificial. Ningetafuta masoko ya kudumu ya chakula nje ya nchi kwa miaka 16 kwa bei ambayo ni nafuu sana. Leo tungekuwa na "investors wa kati na wakubwa" wenye production capacity kubwa ya mazao ya kilimo. Ingawa tumechelewa, njia ya haraka ni investment ya serikali kwa wakulima wakubwa na wa kati wanaoweza kuzalisha chakula. Majeshi yetu yangeweza kufanya hii kazi kwa kuanza na vijana wa JKT na wale wanaozurura mijini bila kazi.

2. Kama usipoweka policy na sheria pamoja na mikakati madhubuti ya kupunguza gharama za maisha hasa bei za vitu, tutajuta kama taifa muda si mrefu.

3. Tuweke mfumo mpya wa kutambua transactions na ku-document supply chain kwenye uchumi wetu.

4. Pesa zetu za ndani zisitumike kwenye mbinu za covid zilizofail. Pesa za ndani ni pamoja na mikopo kutoka kwa wazungu. Usije ukafunga uchumi hata kidogo kisa covid. Taifa litasinyaa. Usalama wa nchi yetu utayumba kabisa au kuanguka.

5. Sina uhakika kama nchi yetu ina mtu anayeitwa "National Security Advisor". Kama yupo, kuna haja ya kumfukuza kazi. Ila kama hayupo, teua haraka. Yeye ata-design mpango wa muda mfupi kwa ajili ya 2022 to 2024 akilenga kutatua hizi changamoto zilizofungamana na masuala ya usalama wa nchi. Lakini atatengeneza mpango wa muda mrefu, yaani wenye phase mbili za utekelezaji wa miaka minane minane. Hata hivyo, njia pekee ya kumpata mtu wa namna hiyo, ni lazima iwe ya uwazi na isiyo na upendeleo wa aina yeyote.

Siku njema. Ngoja nipate kwanza breakfast.
Aruhusu Fao la kujitoa mzunguko wa fedha urudi kama kipindi cha JK .
Kujiajiri kutaongeza mzunguko
 
kuna baadhi ya vitu lazima viwepo katika hatua flani hivi ya maendeleo na kila nchi lazima ipitie vitu hivyo, kuna baadhi ya reforms zinahitaji gharama kubwa kuzimaintain ukilonganisha na faida zitazoleta kwa wakati huo lkn reforms hizohizo zikifanyika miaka 20 au 25 baadae zinaweza kuwa na tija kulingana na level ya maendeleo ya wakati huo so sometimes huenda tukawa tunademand too much may be

Mkuu wala sio tuna demand too much,,
Mfano kwa hayati Jiwe kuna vitu alivipeleka bila kufuata huu mlolongo mrefu na vilikamilika kwa wakati na kwa ubora (Japo alitoka nje ya sheria kidogo), ila vilikamilika...
Sasa tulitakiwa tu ku-assess wapi JPM alikosea na kurekebisha kidogo na kutungia sheria ili mambo yaende...

Waandishi wakiwa wengi stori kukamilika huwa ni ngumu sana..
 
Back
Top Bottom