Ufafanuzi: Kwanini tuliona Lissu anafaa urais 2020 na sasa hafai Uenyekiti?

Ufafanuzi: Kwanini tuliona Lissu anafaa urais 2020 na sasa hafai Uenyekiti?

Mkuu Lissu hatakiwi awe Mwenyekiti kwa sababu makubaliano yasiyo rasmi ya Mbowe kuachiwa gerezani ni pamoja na mambo mengi, kumpa Mwenyekiti wa chama tawala free pass kwenye tiketi ya urais kwenye uchaguzi ujao.

Lissu kuwa Mwenyekiti wa Chadema ni threat zaidi kwa uongozi dhaifu wa CCM, katiba yetu mbovu na muungano wa Tanzania usio wa haki.

Infact Lissu huwa haropoki ila watawala wanajua fika hawawezi kumshinda kesi kwa kutumia kauli yake. Uongozi wa chama tawala unaukukumbuka mziki wa Lissu dhidi ya Magufuli kwenye uchaguzi uliopita mpaka Magufuli akaamua aweke mpira kwapani liwalo na liwe.

Mbowe has been so much compromised to go against the above, as a result Chadema is deeply stuck.

Hicho ndicho hakisemwi na chama tawala au na Mbowe & co.!!!
Lakini nadhani haya ni mafikirio tu, kwani ccm wanahitaji ruhusa ya Mbowe kuendelea kutawala? Tangu lini?

Hata Lisu akiwa Mwenyekiti, tutarudi humu humu JF kulalamika kivingine baada ya uchahuzi 2025.

Watasema Mbowe kamuhujumu Lisu, kwasababu chadema visingizio vimejaa, huwa vinasubiri muda tu vitolewe.

NChi hii hatufanyi uchaguzi, huwa tuna halalisha mtu aendelee kuwa madarakani kwa jina la demokrasoa za uchaguzi.

CCM sio wehu, wanafahamu hawashindi uchaguzi wowote, hivyo ili jamii za kimataifa waridhike, inabidi twende studio tuigize, na waone tumefanya uchaguzi. Na sterling (ccm) hauwawi.

Lisu ashinde, sawa lakini tupunguze promo, uchaguzi utaisha chadema iko hoi sana. Na haitakuwa chadema hii tuijuayo, utanambia muda huo ukifika.
 
Wajibu wangu ni kutoa shule ya siasa na utawala bure kabisa, Narudia kuwajibu nikisema,
Nani kakupa mamlaka haya?
Umehitimu wapi taaluma hizi?
Unapo kuwa tapeli wa kisiasa, hiyo nayo iwe ni sifa ya kujitangaza?
 
WAPIGA KURA HAPANA, MAJORITY OF THEM COULD BE OF "LOW IQ" particularly in this aspect, I say specifically in this aspect
Tunachokilalamikiaga kwa ccm, ndio ww unakitetea bila aibu hapa!
 
Tunachokilalamikiaga kwa ccm, ndio ww unakitetea bila aibu hapa!
Soma post ya Yeriko utajifunza kitu


Mwingine huyu hapa

Mimi kama Mimi, LISSU HAFAI KUWA MWENYEKITI, NI MROPOKAJI, UBABE, UJUAJI, NA HANA HEKIMA NA UVUMILIVU. Na akifanikiwa kuwa m/kiti Chadema ndio mwisho. Siomveni MABAYA lini siasa zake atagombana na wengi, wengi watahama/kupoteza morali.

Sauti kubwa huyu hapa


View: https://youtu.be/NU3b3IYQjhk?si=ZK_baFHAShSaIf9l
 
Kama Magufuli aliweza kuwa mwenyekiti wa ccm na uwezo mdogo vile wa kiutawala, Lisu anashindwaje?
Muulize Samia shughuli ya kujenga SGR, bandari keshagawa kakuta Magufuli (kanunua ship-to-shore cranes), kaongeza kina cha bahari, kaongeza ufanisi, umeme kukatika hadithi, wananchi wanapata huduma kwenye taasisi za serikali, ACCACIA (owners) wanenawa yaishe. To name a few things.

Magufuli level kubwa, huyo Lissu wako hatoshl kwa Mbowe tu.
 
Soma post ya Yeriko utajifunza kitu
Nisome kwakuwa anaendana na utashi wako?
 
Muulize Samia shughuli ya kujenga SGR, bandari keshagawa kakuta Magufuli (kanunua ship-to-shore cranes), kaongeza kina cha bahari, kaongeza ufanisi, umeme kukatika hadithi, wananchi wanapata huduma kwenye taasisi za serikali, ACCACIA (owners) wanenawa yaishe. To name a few things.

Magufuli level kubwa, huyo Lissu wako hatoshl kwa Mbowe tu.
Nasisitiza Magufuli hakuwa kiongozi mzuri, ni kweli alikuwa mtendaji mzuri kwenye miundombinu, ila hakuwa kiongozi mzuri. Sijui unaelewa ninachomaanisha? Mfano mrahisi, mchezaji nyota kwenye team si lazima awe team captain mzuri. Baki humo.
 
“Exactly, I can say, the methods za kuongoza chama cha upinzani Afrika ni tofauti kabisa na kugombea Urais kupitia chama cha upinzani Afrika ndio maana chadema imedumu licha ya vyama 28 vilivyosajiliwa kuanzia 1992 vimekufa vyote ikiwemo vyama vya juzi kama ACT kimeshindwa kujiendesha kimeamua kujisalimisha mikononi mwa Dola.
I can guarantee you, CHADEMA baada ya miaka mitano ijayo chini ya uongozi wa Mwenyekiti Mbowe; hutaitofautisha na hivyo vyama vingine unavyo vitolea mfano hapa.
Mbinu za uongozi wa kubembelezana na chama tawala wakati hali inapo ruhusu; halafu kuminywa wakati chama tawala kinapo pata kiongozi kichaa; na pasiwepo na njia mpya za kupambana na hali zote mbili; utategemea chama hicho kitakuwa na ufanisi gani?
Tegemeo la Mwenyekiti Mbowe lililo baki sasa ni kumshikilia Samia ili chama kipate nafasi kwenye serikali. Hakuna lingine zaidi ya hapo. Na wengi wenu mnao jitokeza hapa, kutetea uongozi wa Mbowe, mategemeo yenu ni hayo; kuingizwa kwenye ulaji, serikalini. hamna la ziada ya lengo hilo.
 
Nasisitiza Magufuli hakuwa kiongozi mzuri, ni kweli alikuwa mtendaji mzuri kwenye miundombinu, ila hakuwa kiongozi mzuri. Sijui unaelewa ninachomaanisha? Mfano mrahisi, mchezaji nyota kwenye team si lazima awe team captain mzuri. Baki humo.
Unaweza tofautisha uongozi na utendaji?

Kipimo cha uongozi ni utendaji.

Nyongeza nafasi ya raisi sio ya utendaji, ni decision making.

Ukiona vision zake zinaenda ina maana ana mechanism nzuri za strategic planning and supervision.

Unadhani mafanikio utokea tu kwa Kudra za mungu.

Hata hujui unachoandika, umesharudi kwenye akili zako hovyo za kila siku
 
Vita mbinu we umeona Mbowe na Mnyika wame-panic.

Ndio kwanza wanashawishi na wengine wenye nią kwenda kuchukua form.

Sana Mbowe anawaasa wanachama wao kutowashambulia wagombea waliopotoka kama Lissu wanao shambulia wenzao.

Lissu mchanga kwenye siasa
lisu ni mwanaharakati, aishi humo tu na sio mwanasiasa
 
Kwahiyo ina maana Mbowe ataishi milele? Yaani unaamini hakuna chadema bila Mbowe? Succession plan ikoje? Hivi leo Mbowe akifariki (God forbid) huoni power struggle itakua kubwa sana maana kutakua na vacuum kubwa.

Hapana, Tsvangirai hakuandaa successor alipofariki kukatokea vita ya madaraka hadi kusababisha Chamisa kuhama na wafuasi wengi na hivyo kuiua MDC-T. Same will happen Mbowe akifariki ghafla. Kuhusu Besigye, nguvu ya Bobi wine ndio ilikiua. Kumbuka Besigye ni jamii moja na Museveni ila Bobi Wine ni mugganda hivyo kura zikapigwa kikabila na ndio unaona Bobi wine akaizoa central yote ambayo zamani ilikua ngome ya Besigye. Nilitegemea unajua siasa za kimataifa kumbe upo shallow kiasi hiki!!

Kwamba dola Inamuogopa Mbowe ambaye yupo moderate? Unachekesha. Kama kuna chochote basi dola itafanya kila kitu kumdhoofisha Lissu ili kiendelee kuiburuza chadema maana wanajua Mbowe ni moderate sio radical kama Lissu ambaye ataleta serious opposition.

Nadhani mkuu ungekaa kimya tu, the more unaropoka unashusha credibility yako. Nilikua nakuheshimu sana ila tokea Lissu achukue fomu nimekushusha sana heshima yako. Acheni demokrasia iamue lissu akifeli si mtamtoa kwa kura 2029 why umuite anatumika na dola kisa kachukua fomu?
Kwanza hajajibu Maswali
 
Wewe Yericko na machawa wenzako msiwadanganye watu. Mna maslahi binafsi na kuendelea kuwepo kwa Mbowe ndani ya uongozi. Hamuutaki ukweli kuwa kwa sasa Chadema inahitaji ari mpya maana maslahi yenu yatakatizwa. Hakuna kingine cha zaidi.

Wewe hapa unapiga porojo ila ukweli unaujua. Mimi nikueleze tu kuwa kama mnataka Chadema iwe bai bai basi Mbowe aendelee kukalia tena kiti kwa kipindi hiki ambacho tayari mwenendo wake umedhihirisha wazi kuwa hana jipya tena la zaidi. Nakuhakikishia itakuwa bai bai na hayo maslahi yenu mtayapata kwa muda tu then mtaanza kugawana mifupa.

Wewe na wapuuzi wenzako mnataka kutuaminisha kuwa kwa miaka 20 sasa bado hamna imani na mtu mwingine zaidi ya Mbowe? Mbona sisi tunawaona wapo? Tena wenye ushawishi kwa vijana na makundi mengine? Chagueni moja, Kife au kipone. Mimi nilishaapa siwezi kuunga mkono mgombea anayepigiwa chapuo na maccm. This time Mbowe anapigiwa chapuo na maccm. Hicho ndiyo kifo cha dhahiri. Cha zaidi hata nyie mnaomuunga mkono Mbowe this time tukiwaangalieni ni watu machawa machawa tu wasio na jambo lingine la zaidi.

Yani mimi nije nimuunge mkono mgombea wa aina hiyo? Hapana. Nakuhakikishia kitakufa mkiendelea na huu ujinga anbao mmepewa muda wa zaidi ya mwezi mmoja kutafakari kwa kina.
 
Chadema ikiwa nyie ndio chamba kikuu Cha upinzani lakini pia milijipambanua kama chama Cha demokrasia ni wakati Sasa muidhihirishie Dunia wapi mnapractice hio demokrasia.Mbowe amehudumu miaka mingi inamtosha na apumzike.Haiwezekani eti Chadema nzima mwenye akili,uwezo na haki ya kukiongoza chama Cha Chadema awe mtu mmoja tuu....si kweli.Mchakato huu mkiufanya vibaya Kwa kumpigania huyo Mkurunziza wenu abakie tena madarakani hakika mtakuwa mmeimaliza kabisa Chadema mioyoni mwa Wananchi.Mruhusu ukomo wa madaraka,uhuru wa kugombea hizo nafasi za juu na mumpumzishe mh Mbowe abakie kuwa mshauri na mzee wa chama.
 
Ndugu umepatwa na Nini? Mbona unapwaya kiasi hiki? Kwenye andiko lako nimeelewa vitu viwili!

1. Kwamba mliruhusu Lissu agombee Urais hata kama hana sifa kwa kuwa mlijua atashindwa na baada ya siku 60 atarejea kuwa mtu wa kawaida. Kwanza haya ni matusi kwa chama Chako. Pili umeonesha hamjali maslahi ya nchi ukilinganisha maslahi ya SACCOS yenu!
2. Mbowe ataongoza milele!
Nadhani ONDOENI neno demokrasia kwenye jina la chama chenu kama mna mawazo ya kiimla kiasi hiki!
3. Wewe Yericko ni chawa unayefuata upepo tu hauna msimamo binafsi! Ulitupiga kamba hapa siku za mwisho za Dr. Slaa mpaka yeye mwenyewe akajitokeza kukusuta !
 
I agree 100% you have a valid points.

Mbowe anahitaji kuandaa successor, not only that anahitaji kuweka mfumo imara zaidi wa democracy ndani ya chama.

Lakini Lissu sio mtu mwenye uwezo wa kujenga chama, he is not leadership material.

My personal opinion sio lazima kila mtu akubaliane na mimi; Wenje, Mnyika na Lema wanaweza kuwa replacement nzuri ya mwenyekiti, makamu na katibu mkuu.

Not Lissu he is too emotional.
Kwahiyo mnamtaka mtu wa kucheka cheka na kuuma vidole pale atakapokutana na CCM? Mnamtaka mtu wa aina hiyo? Mbowe alidanganywa kuwa CCM itampa viti vya uwaziri walipokaa kwenye maridhiano na Samia. Bila hata kujua katiba ikoje akaingia mkenge. Huyo ndiyo mnataka kutuaminisha kuwa ana jipya la zaidi kuendelea kuongoza? Yani alidanganywa kama katoto kadogo na ndiyo chanzo kikubwa cha matatizo yanayoendelea ndani ya Chadema kwa sasa.

Sisi wengine tumeshasema hatumuungi mkono mgombea ambae CCM wanampigia chapuo. Mbowe aondoke wajitokeze watu wawanie hiyo nafasi apatikane mtu sahihi akiongoze chama kwenye nyakati mpya. Yani miaka 20 iliyopita kungekuwa na machawa kama leo Mbowe angeaminiwa kupewa chama akiongoze akiwa na miaka 40 tu? Hilo liyericko lipuuzi limeshavuka miaka 40 lakini na lenyewe bado halijiamini kuwa linaweza kuongoza Chadema kwenye ngazi yoyote zaidi limebakia kuwa lichawa la Mbowe. Kabla ya hizi porojo zake nilikuwa namuheshimu ila sasa nimemtambua ni mtu wa aina gani. Hovyo kabisa
 
Kwahiyo mnamtaka mtu wa kucheka cheka na kuuma vidole pale atakapokutana na CCM? Mnamtaka mtu wa aina hiyo? Mbowe alidanganywa kuwa CCM itampa viti vya uwaziri walipokaa kwenye maridhiano na Samia. Bila hata kujua katiba ikoje akaingia mkenge. Huyo ndiyo mnataka kutuaminisha kuwa ana jipya la zaidi kuendelea kuongoza? Yani alidanganywa kama katoto kadogo na ndiyo chanzo kikubwa cha matatizo yanayoendelea ndani ya Chadema kwa sasa.

Sisi wengine tumeshasema hatumuungi mkono mgombea ambae CCM wanampigia chapuo. Mbowe aondoke wajitokeze watu wawanie hiyo nafasi apatikane mtu sahihi akiongoze chama kwenye nyakati mpya. Yani miaka 20 iliyopita kungekuwa na machawa kama leo Mbowe angeaminiwa kupewa chama akiongoze akiwa na miaka 40 tu? Hilo liyericko lipuuzi limeshavuka miaka 40 lakini na lenyewe bado halijiamini kuwa linaweza kuongoza Chadema kwenye ngazi yoyote zaidi limebakia kuwa lichawa la Mbowe. Kabla ya hizi porojo zake nilikuwa namuheshimu ila sasa nimemtambua ni mtu wa aina gani. Hovyo kabisa
Una minutes za hiko kikao cha Mbowe kuahidiwa uwaziri na CCM au humu JF unadhani kumejaa watoto wa kusikiliza baseless accusations.

Halafu Mbowe wala CDM hawana shida na Lissu kugombea nafasi ya uenyekiti, sikiliza watu wenye kauli za chama. Hizo ndio legit mouth piece zao, katibu mkuu wao John Mnyika kasema nafasi za kuchuana zipo wazi kwa nafasi ya mwenyekiti.

Huku mitandaoni hadithi tu, msitengeneze story kama vile Lissu kawekewa mizengwe toka atangaze kugombea. Mbowe na CDM wala hawana shida mnazotaka kutengeneza.

Kilichombeba Lissu kipindi cha Magufuli ni mafisadi ya CCM kwenye kumchafua, kulinda maslahi yao. Otherwise Lissu sio wa vile zaidi ya kuwa ropo-ropo tu.
 
Ipo hoja inaendelezwa kutoka kwenye Makala yangu ya juzi licha ya kuijibu vizuri katika makala ile ya kwanini Tundu Lissu hana sifa ya kuwa Mwenyekiti wa Chadema taifa,

Wanajenga hoja ya kujirudia Kwamba Lissu chama kilionw anafaa kuwa Rais wa Jamhuri yenye Majeshi JWTZ, Usalama wa Taifa, TRA, TPA n.k ila mimi Yericko naona atapwaya kuwa Mwenyekiti wa chama chenye kanda 10 na majimbo kadhaa?

Wajibu wangu ni kutoa shule ya siasa na utawala bure kabisa, Narudia kuwajibu nikisema,

“Exactly, I can say, the methods za kuongoza chama cha upinzani Afrika ni tofauti kabisa na kugombea Urais kupitia chama cha upinzani Afrika ndio maana chadema imedumu licha ya vyama 28 vilivyosajiliwa kuanzia 1992 vimekufa vyote ikiwemo vyama vya juzi kama ACT kimeshindwa kujiendesha kimeamua kujisalimisha mikononi mwa Dola.

Urais kwa chama cha upinzani Afrika ni unpredictable kuupata ni 50/50 na ni tukio la siku 60 tu baada yapo mnarudi kujenga chama kwaajili ya miaka mitano ijayo, Hivyo uhakika wa uimara wa chama unatakiwa usijaribiwe, Ukuu wa chama ulindwe for Unlimited and Unwaveringly high standards, So we will protect the party with a much higher strength than anything.

Kwamaoni yangu Lissu hana sifa na ubora wa kuongoza chama kulingana na mapungufu yake mengi sana ambapo mengine niliyaeleza katika makala ile, Anayo nafasi ya kukua huko mbele akabadilika na kufaa kukiongoza chama cha siasa kinachokaribia kushika madaraka kama Chadema! Niwape siri, ndiomaana Chama kilikuwa tayari kumpa Lowasa kugombea Urais lakini KAMWE kisingeweza kumpa Lowasa uenyekiti wa Chama abadani…., Now i can tell you, Sir Mbowe will lead this party until CCM comes out of power and then its mission will be completed….

Mwezi August mwaka huu wa 2024 Lissu alitangaza kugombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Chadema, Mwezi October mwaka huu 2024 Lissu akatangaza kuwa atagombea Urais kwa tiketi ya Chadema, Mwezi wa 12 mwaka huuhuu 2024 Lissu katangaza kugombea nafasi na Mwenyekiti wa Chadema na kuondoa nia yake ya kugombea Umakamu Mwenyekiti wa Chadema, yaani hajui hata anataka nini?

Soma Pia: Tundu Lissu: Nimewasilisha kusudio la kugombea nafasi ya Mwenyekiti CHADEMA

Tumejifunza makosa ya vyama vilivyokuwa na viongozi imara lakini vikaingia kwenye mtengo wa wanaharakati uchwara wakishirikiana na wapambe wa dola walioanzisha nyimbo za kuweka ukomo wa uongozi, Sasa vimekufa, Chama cha Morgan Tvangirai Zimbabwe kimekufa, Chama cha Besyge Uganda kimekufa kwasababu ya ujinga wa mitego kwamba kiongozi huyu kakaa sana aondoke aje mwingine, bila kuangalia uimara wa kiongozi huyo namna anavyopamba na dola!

Dola inatulazimisha tufanye kosa la karne kwa kumuondoa Mbowe ili wao wanywe mvinyo kwa furaha pale Mbweni na Viunga vyake! Hatutafanya kosa hilo, sahauni kabisa!

Kisu hakionjwi kwa ulimi!

View attachment 3178483
Zikomo, mbona unatumia nguvu kubwa????
Uzuri wote tunajua.
 
Endeleeni kumsakama Lissu kwa kujifanya ana mapungufu na Mbowe na magenge yake hamna mapungufu.

Kuna dalili ya kuwasilisha orodha ya waliovuta mpunga kwa mama Abdul ili awaoneshe mlivyo dhaifu kuliko yeye.

Kikomo Cha unafiki umekaribia.

Kama kweli Mbowe ana Nia nzuri ya kukisaidia CDM bado anayo nafasi ya kukisaidia hata bila kuwa mkt Taifa, wenzie wameweza kwanini yeye asiweze? Akina zito wameweza, yeye je?

Ondoeni ubinafsi na uchawa wa kijinga
 
Back
Top Bottom