Ufufuaji wa Misukule: Ina tofauti gani na Maigizo?


Kuwa na watu kama hao kwa sasa ni ngumu kidogo mkuu!
mi huwa nashangaa sana kuwaona kina TB joshua wakijeweka kundi moja na kina Paulo wa enzi zile
 
Kuwa na watu kama hao kwa sasa ni ngumu kidogo mkuu!
mi huwa nashangaa sana kuwaona kina TB joshua wakijeweka kundi moja na kina Paulo wa enzi zile

Kwa Lugha rahisi tunaweza kuwaita Manabii wa uongo sasa Kwani kwa sasa hatuwezi kua na watu Kama wale!

Vipi Kuhusu Imani zetu Maana Kama hatuwezi kua na watu Kama wale ina Maana kwa walimwengu wa Leo Imani zetu ziko chini sana ya kiwango na kwa Maana hiyo uzima wa milele kuuona ni kazi!?
 

Ni kazi kubwa sana kuuona huo uzima wa milele kwa kupitia hawa watumishi wafufua misukule! cha muhimu ni kila mtu kukomaa kwa imani yake haswa ile ya mwanzo..
 

si ajabu shule umeenda, halafu una comment huu ujinga !
Haishangazi, maana mna nunua picha dukani kisha mnatundika sebuleni halafu mnawaambia watoto wenu: huyu ni BWANA WETU !
 
si ajabu shule umeenda, halafu una comment huu ujinga !
Haishangazi, maana mna nunua picha dukani kisha mnatundika sebuleni halafu mnawaambia watoto wenu: huyu ni BWANA WETU !

umekumbusha mbali sana mkuu!
ni kipindi cha muvi ya YESU, akili fupi nyingi huamini yule ndiye YESU
 
Ni kazi kubwa sana kuuona huo uzima wa milele kwa kupitia hawa watumishi wafufua misukule! cha muhimu ni kila mtu kukomaa kwa imani yake haswa ile ya mwanzo..

Mkuu Samahani kwa maswali Yangu!
Tunaweza ifikia Ile Imani ya mwanzo iwapo ata Hawa wanatuongoza hawana huo uwezo Kama punje ya mbegu ya Aladari? Tunaweza kweli?

Ndio Maana Mimi wakati mwingine Hua naamini Ufufuo Upo kwa Yule mtoa uhai! Sisi sio watoa uhai na Imani zetu ni chini sana Kama ulivyosema kua ni kazi. Sasa tutaweza Vipi kufufua watu ingawa Maandiko yametupa nafasi ya kufanya hivyo?
 

maandiko hayazungumzi juu ya kufufua misukule!
labda kama wafu na misukule inamaana moja
 
Kuna mtu alisema wanaombea wagonjwa na wanapona,sasa swali la kujiuliza kwanin wasiwe wanaenda hospital moja kwa moja? Na kama umate umate si watapewa na ndugu wa wagonjwa?

Si na mikocheni walikua wanafufua misukule?iliishia wapi?
 
Ni kazi kubwa sana kuuona huo uzima wa milele kwa kupitia hawa watumishi wafufua misukule! cha muhimu ni kila mtu kukomaa kwa imani yake haswa ile ya mwanzo..

Mbona inakuuma sana misukule ikifufuliwa? Nina wasiwasi kuwa unawachukua wewe, wakati watu wanafurahi wachawi kupigwa mpaka wanawaachia watu waliowaiba wewe unachukia, mwanga nini wewe? Na mtakoma mnajifanya dunia ndio yenu hii msijue kuwa ni ya Mungu.

Mungu aumbe watu wake nyie mkawafiche kwenye dali na kwenye uvungu wa nyumba, mwisho wenu umefika.
 
Maisha ya kimwili Si bora Kama maisha ya kiroho! Ni Vema kuponya Roho kwanza kuliko mwili!

Unaiponyaje roho, halafu ukitumia Roho yenye herufi kubwa maana yake ni Roho ya Mungu, roho ya mwanadamu inaanza kwa herufi ndogo.
 


Ndg yangu katika Kristo umenena vizuri, utafanya utafiti. Wakati wautafiti wako na kushauri umuombe sana Mungu akusaidie na akupe ufahamu upate maarifa. Maneno ya Mungu yanatuambia kuwa watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Tena siku za mwisho kutakuwa na manabii wa uongo. Utawajuaje hawa manabii wa uongo,Yesu mwenyewe anatuambia kwa matendo yao. Sasa jiulize wakati wa Yesu hakukua na wachawi au misukule? Kwanini Yesu hakuhangaika na misukule?
 

Unaonyesha kuwa unaielewa biblia, unaunajua kuwa Yesu alimtokea tomaso kumtoa mashaka yake. Sasa na watumishi wa leo wanawajibu wakuwatoa mashaka waumini.
 
hivi ule mpango wake wa kumfufua Amina Chifupa uliishia wapi?
 
usishangae haya yanaweza tokea kabisa sikuhizi binadamu tu wanyama sana unambadilisha binadamu mwenzako kuwa mnyama (msukule) na kumtumikisha kazi zako kama punda , ni kweli kabisa baadhi ya binadamu hawafi kwa mapenzi ya mungu bali ni ya binadamu so kumrudisha mtu kama huyo yawezekana
 
Unaiponyaje roho, halafu ukitumia Roho yenye herufi kubwa maana yake ni Roho ya Mungu, roho ya mwanadamu inaanza kwa herufi ndogo.

Umeenda mbali sana kimawazo mkuu!

Sasa mbona sijasikia hao wachawi wakiteketezwa? always ni misukule tuu wasiokuwa na ndugu wala origin yoyote ile,
Wengine wanatoka mochwari,
ref: gwajima akiwa arusha, kuna msukule alisema ametoka mochwari, hapo jiulize alitokaje?

hakuna aliyemwona akitoka? Maigizo igizo tu!
Hakuna ushaidi wa kisayansi kudhibitisha haya maufufuo..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…