Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

Habari ndugu wafugaji wenzangu.

Naomba msaada wa kuelekezwa dawa kabambe ya kuua viroboto katika banda la kuku wa kienyeji na viroboto vilivyowapamba kuku wenyewe.

Asanteni sana

Jaribu akheri powder,isipofanya kazi tumia paranex ni soln form.
 
Wakuu nawasalimu.
Mwenye ujuzi wa namna ya kupambana na ugonjwa wa kuku hasa vifaranga wa kuvimba vichwa na macho na pia macho kuwa na utando mweupe anisaidie tafadhali.

case yako mkuu iko too general,nakushauri tafuta mtaalam karibu yako awaangalie kujua tatizo..
 
Kama kutakuwa na mtu wa kunisaidia kuokoa vifaranga vyangu maana vipo kumi na tano jamani.

"Nlikuwepo":bolt:

Natumai vifaranga vyako vinaendelea vyema,ila next time vifaranga usiviweke sakafuni hii hupelekea kupata pneumonia.,wawekee sodust,pumba ya mpunga au hata majan makavu atleast 10 cm height.
 
Natumai vifaranga vyako vinaendelea vyema,ila next time vifaranga usiviweke sakafuni hii hupelekea kupata pneumonia.,wawekee sodust,pumba ya mpunga au hata majan makavu atleast 10 cm height.

mkuu mbona kama height ya 10cm ya matandiko ni mengi sana au unamaanisha 10mm?
 
Natumai vifaranga vyako vinaendelea vyema,ila next time vifaranga usiviweke sakafuni hii hupelekea kupata pneumonia.,wawekee sodust,pumba ya mpunga au hata majan makavu atleast 10 cm height.

Nimekuelewa vyema mkuu,wako poa sasa.

"Nlikuwepo":bolt:
 
Mkuu chama2chawa sio 10mm.height inatakiwa iwe kubwa hata zaidi ya hiyo niliotaja coz faida zake ni kama zifuatazo..!kutobadilisha mara kwa mara, kunyonya unyevu,kuua imelea vya magonjwa,kutunza joto.
 
Msaada wakuu nimenunua kuku wa kienyeji watatu kwa ajili ya kuanza ufugaji na nina jogoo mmoja tatizo langu hawa kuku wanataga mfululizo hawalalii mayai nimekusanya mayai zaidi ya 60 naengine ninakula lakini hawaonueshi kulalia nifanyeje ili haya mayai nipate vifaranga?
 
Msaada wakuu nimenunua kuku wa kienyeji watatu kwa ajili ya kuanza ufugaji na nina jogoo mmoja tatizo langu hawa kuku wanataga mfululizo hawalalii mayai nimekusanya mayai zaidi ya 60 naengine ninakula lakini hawaonueshi kulalia nifanyeje ili haya mayai nipate vifaranga?

ili mayai yalaliwe na kukutotolewa mpe kuku ambaye anatabia ya kulalia mayai Baada ya kumaliza kutaga
 
Wakuu tujuzane
Nimeona wafugaji wengi wa Ng`ombe wanafanikiwa saana wakiwa karibu na Madktari wa Mifugo hiyo na changamoto kuwa ndogo kwao.Hasa pale wanapokuwa katika hatua za Mwanzo.Kipindi cha mpito kama miaka miwili hivi.Then muda unavyokwenda Mfugaji anakuwa anaongeza uwezo na kupunguza kumuita Dokta kira mara.

Sasa hembi nijuzeni kwenye ufugaji wa Kuku.
Ningependa kujua wapi Unaweza kupata Dokta/mtaalam wa Upande wa Ufugaji wa Kuku,na je mfano kama je inawezekana kuingianae mkataba wa kumlipa kwa mwezi Mshahara na allowance ya mafuta ili kila wiki kwa uchache awe anakuja site.
Kwa wazoefu inawezaku cost kiasi gani?

Maana mie kwa muono wangu,naona hii ndio move nzuri kwangu kuanza nayo.Ili nikianza nianze kwa mfumo wa kuwa karibu sana na Mtaalam.Maana expection ni kuanza na Kuku 4000 wa kienyeji kwenye free grazing kwenye hekari zangu kama 15 hivi.Kwa Kutenga groups in each Acre

Wadau naomba mchanganuo hapo na njia nyepesi,Manual readings ninazo nyingi ila kuwa na trainer on site ni bora zaidi pia
 
ili mayai yalaliwe na kukutotolewa mpe kuku ambaye anatabia ya kulalia mayai Baada ya kumaliza kutaga

Asante mkuu ila naona kama kuku wangu wote hawana tabia hiyo sijui naweza kuwalazimishaje wayalalie ipi yasiniharibikie?maana nimemlazimisha mmoja apalie naona analalia usiku tu mchana halalii kabisa
 
wapo kuku chotara ambao wao wanataga tu hawana hulka ya kuatamia,sasa nakushauri tafuta kuku wakienyeji au chotara ambao wanatabia ya kulalia mayai,kisha hao wasio atamia watumie kama kuku wa kukuzalishia mayai tu,sasa hayo mayai unaweza ukawawekea kuku wale wenye tabia ya kuatamia.
 
Aisee hembu niambine mwenzenu mbumbumbu.
Hivi Kuku wa Kienyeji kwa Kiingereza wanaitwaje?
Na hawa Juju wengine(maana hata jina lao sijui niwekeje)wanaitwaje?

Sasa akili yangu inaniambia
-Kuku wa Kienyeji wanaitwa LOCAL CHICKEN
-Sasa hawa wengine(tumezoea kuita wakizungu)inakuwaje,maana FOREIGN CHICKEN mhhh,hapa huwa nacheka mwenyewe

Hembu mtujuze wataalam
 
Wana Jf Mungu awabariki na abariki kazi za mikono yenu. Uzi huu wa Kubota na michango ya wachangiaji wengine nitaifanyia kazi
 
Msaada jaman naomba nijue jinsi ya kutambua kanga dume na kama mtu anajua kanga huanza kutaga baada ya muda gani msaada jaman
 
Amani iwe nanyi!Nikitambo sijachangia uzi huu sio kwa sababu sikuwa na interest nao la hasha!Kwa kipindi kile uzi huu ulikuwa kama functionless kwangu kutokana na mazingira yangu hayakunuruhusu kabisa kufuga kibiashara ingawa nilikuwa natamani kufuga.Nikaona ni busara niweke uzi huu mkuu kama hazina hivyo kuamua kujiweka bize kutafuta njia za kujikwamua na mazingira yale,katika njia za kufanikisha hilo nimejukuta kwa miaka miwili iliyo pita nimepitia katika wakati mgumu na maisha yakukatisha tama sana ndugu wana jf hatahivyo,namshukuru MWENYEZI MUNGU kwa sasa ninavyo andika hii post nipo mahali ambapo naweza kufuga na kuwekeza katika miradi mingine,na nimeanza kufanya hivyo kwani hivi sasa nina kuku wakubwa kumi na nne na vifaranga kumi na tatu napia natarajia mnamo tarehere mbili mwezi huu kuwa na vifaranga wengine 25-30 kwani kuna kuku watatu wamelalia mayai thelathini.Nafikiri huu ndio umekuwa wakati wangu muafaka wa kutafuta hazina yangu ambayo ni hii thread,nashukuru kwa sasa uzi una michango mingi tofauti na hapo awali nilipo ishia ulikuwa na pages 13 ila kwa sasa una pages 43 naomba niwapongeze kwa hilo na naomba msikate tamaa kutuelimisha.Nimesomo pages zote na sasa nitaendelea kutoa mrejesho wa maendeleo ya ufugaji wangu ingawa ni mvivu kidogo kuandika ila nitajitahidi kadri ya uwezo kwa hili kuhakikisha nami natoa nilichokipata kwa manufaa ya wenzangu.MUNGU akubariki Kubota MUNGU awabariki Mama Joe,Chasha, Liverpoolfc,MamaTimmy,Guta,Fidel80,Aza,Asigwa,Chamilitary,Ankoeli,Poutry Sayuni na wengine wote ambao nimewasahau.

Umefanya kilicho chema mkuu
 
Zanzibar Spices
huyohuyo mtaalam wa mifugo ulie nae karibu atakushauri we ongea nae vizuri tu.
 
Back
Top Bottom