Ufyatu 100%: Sababu zinazotolewa hazina mantiki au mantiki hazina sababu?

Ufyatu 100%: Sababu zinazotolewa hazina mantiki au mantiki hazina sababu?

Kuna uzi Pascal Mayalla kafafanua kabisa kuwa IGA ni Sawa na MoU... memorandum of understanding tu.. makubaliano ya kidiplomasia zaidi ambayo hayana nguvu yeyote ya kisheria Hadi mtakapoingia mkataba halisi....

Umeuliza why hii inapingwa zaidi?
Hujui kuna watu wataathirika na biashara? Karamagi na Ticts?hakawalipa watu "wampambanie"?
Unaamini ni uzalendo wake Tibaijuka anaenda Hadi kwenye TV kupinga Dpworld? Huyu Tibaijuka aliepewa mgao escrow?? Hajapewa mgao na Karamagi??..

Huoni kuna kundi linatumia nguvu kupinga Dpworld Kwa sababu ambazo haziko clear??

Moja, hoja yako ya kuhusisha mkataba wa IGA na Ticts au makosa ya utawala uliopita siyo sahihi ni kama unahamisha nguzo za gori ili mpira uingie gorini.

Pili, IGA siyo MoU labda kama hujausoma au unautetea kwa sababu unazozijua mwenyewe.

Tatu, hujajibu swali langu la msingi Kwa nini DPW haiwekezi nchini kwa Sheria, Kanuni na Taratibu zilizopo kama makampuni mengine ya kibiashara? Kumbuka hata Ticts, unayoshutuma ukimhusisha Prof Tibaijuka, haikuwekeza kwa njia inayotaka kutumiwa na DPW ikitetewa kwa nguvu kubwa na Utawala ulioko madarakani. Kuna nini?

Bila majibu yenye ushahidi usio na mashaka, DPW ikiwekeza kupitia IGA, wakati wa kampeni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, mwakani, nitajitokeza mbele ya wapiga kura, wagombea wa chama tawala, ngazi zote, waeleze kilicho nyuma ya uwekezaji huo.
 
Mimi napinga unafiki
Wale waliokuwa wanamkosoa Magufuli...kina Tundu Lissu, Mbowe na Bagonza hutaniona kabisa nawashambulia...why?angalau wao walithibitisha kuwa wanamkosoa yeyote Yule aliepo madarakani...hata kama sikubaliani nao hoja siwezi waambia kaeni kimya...since hawakukaa kimyaa wakati wa Magufuli...
Hawa kina Pengo, Mwanakijiji, Slaa, Tibaijuka na wanafiki wengine lazima tuwavue nguo kila mara wanaponyanyua midomo yao....
Unafiki na kuchagua nani umkosoe sababu ya dini ni kitu kibaya zaidi kuliko mikataba mibovu
Tena hasa huyo kimbau mbau, Fido dido, vicks kingo wahedi
Mnafiki mkubwa wala sio mtanzania huyu
 
Tanganyika inalizwa misitu,loliondo ,gesi na bandari za bara zinafuata
Ile memorandum imesema, kuna park, safari place, lake zones, bandari ni baba lao.
So kupigwa tumepigwa vizuri tu.
Kumbuka iko mikataba 30 imesainiwa hii ni cha mtoto.
 
Ile memorandum imesema, kuna park, safari place, lake zones, bandari ni baba lao.
So kupigwa tumepigwa vizuri tu.
Kumbuka iko mikataba 30 imesainiwa hii ni cha mtoto.
Iwepo mikataba 100 au zaidi kama haikidhi matakwa na masharti ya uwekezaji tutaipinga kwa nguvu zote.

Na kwa sababu inaonekana dhahiri, kwa sasa, kuwa uwekezaji nchini unafanywa kinyume, Serikali ichukue uamuzi mgumu wa kuiweka wazi mikataba yote kabla haijatiwa saini. Km kuna minong'ono (Serikali haijakanusha na Bunge limekaa kimya) kuwa Loliondo/Ngorogoro amepewa mgeni kuwekeza baada ya kuondoa Wamasai. Muda si mrefu Wamasai walikohamishiwa kutazuka migogoro ya ardhi kama ilivyo Kilosa

Narudia tena, mimi nitahamasisha wenye mawazo kama mimi, kuwambia Wapiga kura kinachoendelea nchini kuhusu uwekezaji, kwa kile kinachoitwa "Demokrasia ya Uchumi" kumbe kichaka cha kuifirisi nchi utajiri wake wa asili. Hivi kwa nini Viongozi wa sasa hawajifunzi kwenye mikataba ya hovyo ya uchimbaji madini?

Na kama "demokrasia ya uchumi" inalingizia Taifa pato kubwa kwa nini Serikali inaendelea kukopa na kuomba misaada? Naomba jibu kutoka kwa watetezi wa hiyo Sera, badala ya wao kuimba nyimbo za mapambio na kusifia
 
Hiyo no 6 ..lazima kushindanisha??
Rais anaweza ona kampuni ipi sahihi ..
Kama Magufuli alivyokuwa anatuchagulia kampuni ipi zijenge nini na wapi..
Bwawa la Nyerere...alichagua yeye ..
Sgr alichagua yeye ..

Since Rais Yuko more informed na washauri Tele kaona Dpworld sahihi...

Wewe kaaa kimyaa kama ulivyokuwa kimyaa wakati Magufuli anafanya yote hayo Kwa utashi wake
Hayo mamlaka rais kapata wapi? He sio udikteta?
 
Kule tayari mkuu moto ushaanza.
Siwezi kushangaa kuwa moto huko walikohamishiwa Wamasai umeanza kuwaka kwa sababu uamuzi ulichukuliwa kisiasa. Mwanasiasa hudhani yeye ndiye anajua kila kitu hata kama anajua kusoma na kuandika tu. Ukimwuliza atalifanyia nini Taifa lake atakupa ahadi za uwongo ili kesho umpe kura ya kula tena.

Kwani nani hajui kuwa asili ya Mmasai ni kuwa na mifugo mingi? Je, Serikali ilichukua hatua gani au juhudi yoyote ya kuwaandaa ufugaji wa kisasa usiohitaji kuwa na kundi kubwa la mifugo, kabla ya kuwahamisha? Ni Serikali hiyo hiyo tunayoipinga kuingiza DPW kuwekeza nchini kwa mgongo wa nchi yao kwa kutumia mkataba (IGA) wa hovyo kabisa.
 
Hiyo no 6 ..lazima kushindanisha??
Rais anaweza ona kampuni ipi sahihi ..
Kama Magufuli alivyokuwa anatuchagulia kampuni ipi zijenge nini na wapi..
Bwawa la Nyerere...alichagua yeye ..
Sgr alichagua yeye ..

Since Rais Yuko more informed na washauri Tele kaona Dpworld sahihi...

Wewe kaaa kimyaa kama ulivyokuwa kimyaa wakati Magufuli anafanya yote hayo Kwa utashi wake
Kama Magufuri alifanya makosa unataka yaendelee?
 
Iwepo mikataba 100 au zaidi kama haikidhi matakwa na masharti ya uwekezaji tutaipinga kwa nguvu zote.

Na kwa sababu inaonekana dhahiri, kwa sasa, kuwa uwekezaji nchini unafanywa kinyume, Serikali ichukue uamuzi mgumu wa kuiweka wazi mikataba yote kabla haijatiwa saini. Km kuna minong'ono (Serikali haijakanusha na Bunge limekaa kimya) kuwa Loliondo/Ngorogoro amepewa mgeni kuwekeza baada ya kuondoa Wamasai. Muda si mrefu Wamasai walikohamishiwa kutazuka migogoro ya ardhi kama ilivyo Kilosa

Narudia tena, mimi nitahamasisha wenye mawazo kama mimi, kuwambia Wapiga kura kinachoendelea nchini kuhusu uwekezaji, kwa kile kinachoitwa "Demokrasia ya Uchumi" kumbe kichaka cha kuifirisi nchi utajiri wake wa asili. Hivi kwa nini Viongozi wa sasa hawajifunzi kwenye mikataba ya hovyo ya uchimbaji madini?

Na kama "demokrasia ya uchumi" inalingizia Taifa pato kubwa kwa nini Serikali inaendelea kukopa na kuomba misaada? Naomba jibu kutoka kwa watetezi wa hiyo Sera, badala ya wao kuimba nyimbo za mapambio na kusifia

Tulipokuwa tukilia kuhusu kuchezewa kwa chaguzi mlikuwa hamuelewi hatari ya kura kutoheshimiwa, kisa mliyemtaka ndio alikuwa anapora chaguzi. Kwa sasa hata ukihamasisha wapiga kura, mbegu ya kukaa madarakani bila ridhaa ya wananchi imeshaota. Hakuna anayeogopa tena wananchi. Na kibaya zaidi hata wananchi walio wengi hawako tena tayari kujitokeza kupiga kura kwenye chaguzi zisizoheshimiwa. Hivyo hata ukihamasisha hao wapiga kura hakuna chochote utafanya zaidi ya kupoteza muda.
 
Kama Magufuri alifanya makosa unataka yaendelee?
Yataondoka kwa kupiga porojo hapa jukwaani? Hamkujua madhara ya mbunge mbaya ya kiutawala aliyokuwa anapanda dhalimu kwa kujifanya mzalendo?

Sasa tumefika mahali viongozi wanafanya wanavyoona bila kuhofia wananchi wanasema nini. Tusubiri tu hadi mambo yazidi kuharibu ili tukisema tunaingia barabarani akili ziwe zimewarudia.
 
Hiyo no 6 ..lazima kushindanisha??
Rais anaweza ona kampuni ipi sahihi ..
Kama Magufuli alivyokuwa anatuchagulia kampuni ipi zijenge nini na wapi..
Bwawa la Nyerere...alichagua yeye ..
Sgr alichagua yeye ..

Since Rais Yuko more informed na washauri Tele kaona Dpworld sahihi...

Wewe kaaa kimyaa kama ulivyokuwa kimyaa wakati Magufuli anafanya yote hayo Kwa utashi wake
Na wakati Magu anafanya hivyo, were you happy about it, au kwa vile leo wewe ni Pro Sa100 unaona sawa yeye kuachagua kampuni as she's more informed? "Two wrongs don't make a right"!
 
Siwezi kushangaa kuwa moto huko walikohamishiwa Wamasai umeanza kuwaka kwa sababu uamuzi ulichukuliwa kisiasa. Mwanasiasa hudhani yeye ndiye anajua kila kitu hata kama anajua kusoma na kuandika tu. Ukimwuliza atalifanyia Taifa lake atakupa ahadi za uwongo ili kesho umpe kura ya kula tena.

Kwani nani hajui kuwa asili ya Mmasai ni kuwa na mifugo mingi? Je, Serikali ilichukua hatua gani au juhudi yoyote ya kuwaandaa ufugaji wa kisasa usiohitaji kuwa na kundi kubwa la mifugo, kabla ya kuwahamisha? Ni Serikali hiyo hiyo tunayoipinga kuingiza DPW kuwekeza nchini kwa mgongo wa nchi yao kwa kutumia mkataba (IGA) wa hovyo kabisa.
Ndo hapo nashangaa, mifugo yao ilikua huru huko walipokuwa.
Wamepelekwa huko wabondei nao wanalalamika mifugo mingi na tena kwanini sisi tuliopo hatukuboreshewa huduma before ila hawa wamepewa kila kitu?
Mziki unaanza.
Wale wananchi kule Wana swali la Msingi kabisa.
Ila jibu sasa
 
Tulipokuwa tukilia kuhusu kuchezewa kwa chaguzi mlikuwa hamuelewi hatari ya kura kutoheshimiwa, kisa mliyemtaka ndio alikuwa anapora chaguzi. Kwa sasa hata ukihamasisha wapiga kura, mbegu ya kukaa madarakani bila ridhaa ya wananchi imeshaota. Hakuna anayeogopa tena wananchi. Na kibaya zaidi hata wananchi walio wengi hawako tena tayari kujitokeza kupiga kura kwenye chaguzi zisizoheshimiwa. Hivyo hata ukihamasisha hao wapiga kura hakuna chochote utafanya zaidi ya kupoteza muda.
Unajadili kisiasa ukiegemea upande unaoushabikia au uanachama badala ya hoja za mada kuu. Huwezi kuniingiza kwenye gari hilo.

Nasimamia ukweli ninaouamini kuwa Wanasiasa wote ni wachumia tumbo, awe wa chama tawala au upinzani. Km wanasiasa wa upinzani baada ya utawala wa sasa kuruhusu mikutano ya hadhara wameusifia sana. Leo hii wanabweka hovyo, kisa!!!

Iwe mwanasiasa wa upinzani au chama tawala chaguzi za kitaifa zijazo, nitatumia ushawishi niliojaliwa kushawishi wapiga kura kuchagua mwenye mtazamo wa kitaifa na siyo wa yeye au chama chake.

ENOUGH IS ENOUGH WITH FAKE AND SELFISH POLITICIANS. Nia ninayo, uwezo ninao na sababu ninazo za kutosha kufanikisha lengo langu. Daima mbele nyuma mwiko
 
Na. M. M. Mwanakijiji
1. Hakuna Tanganyika; sijui ni kina nani wanazungumzia. Hadi hivi sasa hakuna nchi au taifa la Tanganyika. Hivyo Tanganyika haimo kwenye mjadala.
Katiba ya JMT 1977 ,151 (1) Inatamka '' Tanzania Bara maana yake ni eneo lote la Jamhuri ya Muungano ambalo zamani lilikuwa eneo la Jamhuri ya Tanganyika''

Kwa maana tunapoitaja Tanzania, lile eneo la Bara ndiyo ilikuwa Tanganyika. Huyu jamaa anayeitwa Tanganyika sijui alibatizwa au alisilimishwa lakini tunajua ni yule yule aliyeachwa na Mwingereza.
Tanganyika ipo midhali neno Bara lipo. Lakini Wazanzibar hawajiiti Tanzania visiwani tena, hili neno Bara ni Tanganyika. Ukiwa huna visiwani wapi utapata Bara? ni Tanganyika tu

Kwanini ni muhimu katika mjadala. Rais SSH alisaini MoU inayohusu Tanzania ( Zanzibar wakiwemo).
Katika kamati ya Bunge, kwa mujibu wa Mbunge Aida Kenani Wazanzibar walisema Bandari zao hazimo katika MoU. Hoja haijakanushwa na Bunge au Wazanzibar. Sasa kama Zanzibar haipo katika Tanzania tunabaki na Tanzania Bara ambayo ni eneo la iliyokuwa Jamhuri ya Tanganyika. Kwa maneno mengine MoU inahusu Tanganyika.

Kama Rais wa JMT anasaini suala la Tanzania Bara ambayo ni Tanganyika na kuiacha Zanzibar katika jambo la muungano (bandari kwa mujibu wa mkataba) kwa kutumia jina la Tanzania, huoni Tatizo hapo?
Mathalan DP wakitoa Dollar Bilioni 10 kwa Bandari, Zanzibar wanastahili kwasababu DP inatoa kwa Tanzania.

DP hao hao walileta ufanisi mapato ya Bandari ni ya JMT kwasababu yamesimamiwa na Rais wa JMT na kuandikwa kwa jina la JMT na Zanzibar watapewa ruzuku ya bajeti na 4.5% ya pato la bandari. Huoni tatizo hapo? Lakini DP wakitaifisha bandari au kudai malipo hilo litakuwa suala la Tanzania Bara ambayo ni Tanganyika, Zanzibar watatumia katiba yao. Huoni tatizo hapo?

Ni utaratibu ule ule mbovu wa gesi ya Tanganyika, Madini ya Tanganyika, utalii wa Tanganyika n.k. kuingiza pato la Taifa halafu Zanzibar wanapata mgao wa 4.5% kwasababu tu ya neno Tanzania. Lakini ukiwauliza gesi yao ipo wapi wanakwambia si jambo la muungano. Huoni tatizo hapo ? Huoni kwanini Tanganyika inahitajika kuwekwa wazi kwenye mambo mazito kama haya ya Bandari?

Ni utaratibu ule ule wa hovyo, kwamba, tunakopa kama Tanzania halafu wakati wa kulipa tunatumia hazina ya Tanzania Bara yaani Tanganyika. Huoni tatizo hapo?

Kama Tanganyika haipo , Hii Tanzania Bara iliyotajwa katika katiba ni kitu gani na kilianzia wapi?

The Boss JokaKuu Pascal Mayalla
 
Back
Top Bottom