Ugaidi Tanzania Unafanikiwa

Ugaidi Tanzania Unafanikiwa

Duh yaan watu watekwe wauwawe tukae kimya kweli hapana ata shetani atashangaa

Mimi kinachonishangaza ni pale wabunge wetu wanapojadili majanga ya watu kutekwa, kuuawa na wengine kuteswa huko bungeni; serikali wa kupitia kwa Naibu spika inatoa kauli kuwa bungeni sio mahala pa kupeleka malalamiko , wabunge wenye malalamiko juu ya uhalifu huo wapeleke malalamiko yao polisi!!!!! Hapo ndipo ninapojiuliza huu uongozi ni wa kuwalinda watu na usalama wao au ni wa kuwalinda watawala peke yao? Inaelekea huyu naibu spika haguswi kabisa na matatizo haya na pengine anajua kinachoendelea na ndio maana anapuuza!
 
FaizaFoxy-Huyu naye aliyeua Askari wetu saba kwa mkupuo naye ni gaidi?Ni kwa sababu ni Tanzania tu.Nilikuwa naangalia magazeti ya leo.Karibu yote ni siasa tu.Gazeti moja au mawili ysmeandika tena si kwa uzito.Shooting ya polisi Saba at a time ni habari kubwa kwa wanaotambua umuhimu wa Askari.Kuna vurugu mkoani pwani vyombo vya habari viko bize na siasa na habari za Simba na Yanga..
Link Kwanini tukatae kuwa mauaji ya polisi huko Mkuranga sio ugaidi?
 
Gaidi hawezi fanya kitu bila demand na time frame.

Gaidi lazima aseme nataka nifanyiwe hivyi ndani ya muda fulani bila hivyo nitafanya hivi zaidi.

Gaidi gani anaua kimya kimya bila hitaji lolote? Huyo siyo gaidi ni kibaka mamboleo
 
Mimi kinachonishangaza ni pale wabunge wetu wanapojadili majanga ya watu kutekwa, kuuawa na wengine kuteswa huko bungeni; serikali wa kupitia kwa Naibu spika inatoa kauli kuwa bungeni sio mahala pa kupeleka malalamiko , wabunge wenye malalamiko juu ya uhalifu huo wapeleke malalamiko yao polisi!!!!! Hapo ndipo ninapojiuliza huu uongozi ni wa kuwalinda watu na usalama wao au ni wa kuwalinda watawala peke yao? Inaelekea huyu naibu spika haguswi kabisa na matatizo haya na pengine anajua kinachoendelea na ndio maana anapuuza!
Naibu spika ni rafiki ya watekaji pia majambazi hataki wabunge wajadili uovu wao.
 
Blog za mapishi,nenda ukalale kibibi! Can't differentiate BTW Islam and terrorism... J,Bush

Qur'an 28:55. Na wanapo sikia upuuzi hujitenga nao na husema: Sisi tuna vitendo vyetu, na nyinyi mna vitendo vyenu. Salamun Alaikum, Amani juu yenu! Sisi hatutaki kujibizana na wajinga.
 
Nadhani serekali/polisi inatakiwa kuwa karibu na raia. Kuwa karibu na raia, ni pamoja na kutatua matatizo yanapotokea, kama vile, mauwaji au kutekwa kwa raia nk. Kwahivi sasa, naona hakuna TRUST Kati ya raia na vyombo vya salaama. Raia wana ogopa vyombo vya usalaama na vyombo vya usalaama sidhani kama wanaona hili ni tatizo. Kuaminiana Kati ya raia na vyombo vya usalaama, utasaidia saana kupunguza au kutokomeza ujambazi/ugaidi unao nyemelea nchi yetu.
 
Kuna ugaidi wa aina mbili; na ni kweli, moja ya ugaaidi huo hauleti tija kuutangaza kwa sababu wanaofanya aina hiyo ya ugaidi wanafanya kwa lengo la kutaka kutangazwa! Hivyo basi, unapotangaza, mission inakuwa accomplished!

Kwa mfano, ni kawaida sana kuona ISIS wanakata watu vichwa na kujirekodi kisha ku-release videos husika! Hawa wanafanya hivyo kwa lengo la kutaka publicity na kusambaza propaganda zao! Hawa ukiwaongesha kwenye TV inakuwa umewasaidia kufanikisha malengo yao... kueneza propaganda na hofu!!

Haya yanayotokea Tanzania sioni kama yana ufanano na aina ya ugaidi niliousema hapo juu!!! Hawa ni magaidi waoga na hakuna hata mmoja miongoni mwao mwenye hamu ya kufahamika japo na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa let alone askari polisi! Hawa hawafanyi wafanyayo kwa lengo la kutafuta publicity... inawezekana lengo lao ni kujenga hofu!!!

Kwavile hawana ujasiri wa kutaka wafahamike; kutangaza kwamba hao ni majambazi kunawapa ahueni kwa sababu bado wangependa kutenda uhalifu wao bila kufahamika! Hawa kuwatangaza wazi wazi kwamba ni magaidi kunawajengea hofu kuliko ujasiri kwa sababu wanafahamu Watanzania wanaweza kuvumilia kuishi na jambazi mtaa mmoja kuliko na gaidi anayeishi mtaa wa 7 !!!
 
Kinachoendelea sasa hivi Tanzania ni ugaidi (terrorism).

Lengo la ugaidi ni kuwatia watu hofu na kufikisha ujumbe kwa wengi kwa njia ya hofu.

Matukio yanayoongelewa sana kwenye vyombo vya habari na mitandao yote ya kijamii mpaka nchi za nje kwa sasa ni hayo, kuanzia watu kutekwa, kutolewa bastola hadharani, mauaji ya Kusini huko, watu kukutwa kwenye viroba, kupotea kwa watu na mengi mengineyo, yote yanaashiria ugaidi.

Magaidi hujitokeza na kusema sisi ndiyo tuliyoyafanya hayo ili waogopwe au matakwa yao yatimizwe au hukaa kimya na kuwachochea kivingine kwa lengo hilo hilo.

Matukio ya ugaidi yanapotokea pia hujitokeza wengine ambao hutumia fursa hiyo kufikisha ujumbe wao kwa njia tofauti.

Kwa yanayotokea Tanzania, ukweli ni kuwa, kuna wanaofanya huo ugaidi wa kutisha na kuna wanaotumia huo gaidi kama ni fursa kwao kufikisha ujumbe wao ama kwa kuongezea ugaidi mwingine au kwa kuendeleza hofu kwenye jamii na vyombo husika.

Watanzania tunachotakiwa kufanya ni kukaa kimya na kufunga hii mijadala yote na kuwacha kuripoti matukio yote ya kigaidi ili kushindana na ugaidi.

Gaidi kama matukio yake hayaongelewi kazi yake inakuwa haijafanikiwa.

Au leta mawazo yako ni njia gani zitumike kutatuwa hili tatizo "linalotukabili".

Kwa muono wangu, kila tunapoyaongea na kuyasambaza ndiyo furaha ya magaidi na ndiyo lengo lao, wengi wajawe na hofu.

Kwanini? Mie sijuwi.
Sijuwi=sijui
 
Kinachoendelea sasa hivi Tanzania ni ugaidi (terrorism).

Lengo la ugaidi ni kuwatia watu hofu na kufikisha ujumbe kwa wengi kwa njia ya hofu.

Matukio yanayoongelewa sana kwenye vyombo vya habari na mitandao yote ya kijamii mpaka nchi za nje kwa sasa ni hayo, kuanzia watu kutekwa, kutolewa bastola hadharani, mauaji ya Kusini huko, watu kukutwa kwenye viroba, kupotea kwa watu na mengi mengineyo, yote yanaashiria ugaidi.

Magaidi hujitokeza na kusema sisi ndiyo tuliyoyafanya hayo ili waogopwe au matakwa yao yatimizwe au hukaa kimya na kuwachochea kivingine kwa lengo hilo hilo.

Matukio ya ugaidi yanapotokea pia hujitokeza wengine ambao hutumia fursa hiyo kufikisha ujumbe wao kwa njia tofauti.

Kwa yanayotokea Tanzania, ukweli ni kuwa, kuna wanaofanya huo ugaidi wa kutisha na kuna wanaotumia huo gaidi kama ni fursa kwao kufikisha ujumbe wao ama kwa kuongezea ugaidi mwingine au kwa kuendeleza hofu kwenye jamii na vyombo husika.

Watanzania tunachotakiwa kufanya ni kukaa kimya na kufunga hii mijadala yote na kuwacha kuripoti matukio yote ya kigaidi ili kushindana na ugaidi.

Gaidi kama matukio yake hayaongelewi kazi yake inakuwa haijafanikiwa.

Au leta mawazo yako ni njia gani zitumike kutatuwa hili tatizo "linalotukabili".

Kwa muono wangu, kila tunapoyaongea na kuyasambaza ndiyo furaha ya magaidi na ndiyo lengo lao, wengi wajawe na hofu.

Kwanini? Mie sijuwi.
Huwezi kutatua tatizo kwa kupretend hamna tatizo.kunakitu kinaitwa "solving problem technique"unakifahamu?
 
Itakuwa walishakaa kimya mno mpaka imefikia hatua hii ni mambo yanajisema yenyewe. Kwanza bado serikali ipo kimya kwa kusema sio ugaid ni majambazi. Hakuna chombo cha serikali kilichoreport ni ugaidi.
 
Kinachoendelea sasa hivi Tanzania ni ugaidi (terrorism).

Lengo la ugaidi ni kuwatia watu hofu na kufikisha ujumbe kwa wengi kwa njia ya hofu.

Matukio yanayoongelewa sana kwenye vyombo vya habari na mitandao yote ya kijamii mpaka nchi za nje kwa sasa ni hayo, kuanzia watu kutekwa, kutolewa bastola hadharani, mauaji ya Kusini huko, watu kukutwa kwenye viroba, kupotea kwa watu na mengi mengineyo, yote yanaashiria ugaidi.

Magaidi hujitokeza na kusema sisi ndiyo tuliyoyafanya hayo ili waogopwe au matakwa yao yatimizwe au hukaa kimya na kuwachochea kivingine kwa lengo hilo hilo.

Matukio ya ugaidi yanapotokea pia hujitokeza wengine ambao hutumia fursa hiyo kufikisha ujumbe wao kwa njia tofauti.

Kwa yanayotokea Tanzania, ukweli ni kuwa, kuna wanaofanya huo ugaidi wa kutisha na kuna wanaotumia huo gaidi kama ni fursa kwao kufikisha ujumbe wao ama kwa kuongezea ugaidi mwingine au kwa kuendeleza hofu kwenye jamii na vyombo husika.

Watanzania tunachotakiwa kufanya ni kukaa kimya na kufunga hii mijadala yote na kuwacha kuripoti matukio yote ya kigaidi ili kushindana na ugaidi.

Gaidi kama matukio yake hayaongelewi kazi yake inakuwa haijafanikiwa.

Au leta mawazo yako ni njia gani zitumike kutatuwa hili tatizo "linalotukabili".

Kwa muono wangu, kila tunapoyaongea na kuyasambaza ndiyo furaha ya magaidi na ndiyo lengo lao, wengi wajawe na hofu.

Kwanini? Mie sijuwi.

Kwanza nianze kwa kusema umeandika upumbavu mtupu.

Pili kinachotokea Tanzania si "ugaidi" bali kuna kila dalili serikali ndiyo inayofanya mambo hayo kupitia usalama wa taifa halafu unataka watu wakae kimya huku maisha yao yako hatarini.
 
"Kutekwa" huwa ni vitani, hao waliotekwa walikuwa vitani?

Au unatekwa kwa watu kutaka "ransom", hao unaosema waliotekwa kuna "ransom" iliyokuwa "demanded"?

Hao unaosema walitekwa hao wala hawaingii katika kigezo cha ugaidi. Ugaidi ni kama matukio ya Kusini, ugaidi ni kama kutumia hao waliotekwa kusambaza habari za kutisha watu.

Tukio la Roma, hili baada ya kumsikiliza Ally leo nimeona kumbe ni mtu anaemtukana Rais, unamtukana Rais unategemea vijana wanaompenda wakuachie tu? Wacha Rais hebu mtu akutukane wewe tu mbele ya marafiki zako tuone kama utamuachia au marafiki zako watamuachia bila ya kumuadabisha.

Huo siyo ugaidi.

Sheria ifuatwe basi lakini kuchukua sheria mikononi mwako nnje ya mahakama ni kosa.
 
Ni mjadala ambao inabidi kwanza tujue sababu.

Kuna ugaidi wa kugeuza mtazamo, pia hatujauzungumzia.
Mwalimu unakuja na subtopic, theni unataka wanafunzi waje na full topic well done ss, ilitakiwa uelezee kiunagaubaga ili ueleweke sasa hapa unakiri udhaifu wako. Si ungekuja na mada complete kuhusu huo ugaidi wa kugeuza mtizamo.

HAKIKA TUKIKAA KIMYA MAWE YATASEMA. Wacha watu tufungukeee [emoji12] [emoji12] [emoji12] [emoji12] [emoji12]
 
Back
Top Bottom