Ugali unaopikwa kwa Unga wa mahindi (dona) hatari kwa afya ya binadamu

Ingekuwa ni hivyo basi Wakenya wote wangekuwa wameshatangulia mbele ya haki,Kenya ni mwendo wa dona tu,haya makapi (unga mweupe/uliokobolewa)yanaliwa TZ
 
Sasa itabidi Watanzania wote wahamie USA ili waweze kula FDA approved dona, which is a good thing if you really think about it.
 
Peleka uongo kule babu zetu walikula dona na hawakuwa na cancer
 
Sasa mbona hauhaelezea vzuri?.
Inamaanisha mahindi yote ya dona yana hiyo sumu ya aflatoxin? Na pia hii ishu ya sumu kwenye kiini imegunduliwa recently au toka zamani ipo.?
Kama toka zamani basi pita hivi.
Dadavua.
 
Kuna mazoezi ambayo hayatajiwi kwa aina fulani ya watu hasa watu wenye umri kuanzia 35 na kuendelea.
 
kwa hyo wewe reference yako kubwa ni Wikipedia...sons vizuri michngo ya watu na kunareference nzuri zimetolewa...changanya na Wikipedia yako...usipoelewa basi wewe utakua ni jipu....itabidi Kigwangala aje akufanyie ziara ya kushitukiza
 
Hii taarifa itapokewa kwa mtazamo tofauti na wadau wa dona vs sembe






 
Ingekua kuna sumu zamani hyo wangekufa sana. Tulia we naona unataka kupiga dau watu wakoboe upate pumba.
 
Hebu weka chanzo cha habari yako tafadhali.
 
Babu yako kala dona, bibi yako kala dona, shangazi zako na wajomba zako wamekula na kukulia dona. Hiyo sumu haikuwaona. Au inabagua? Acha hizo. Kama hutaki kula dona kaa pembeni sisi twala. Unaogopa aflatoxin mbona kila siku unaosha kirungu huogopi ngoma?
 

Aflatoxin ni chemikali/sumu inayozalishwa Na vimelea vya aina ya fungus ambaye huota Na kustawi kwenye mbegu baada ya kuvuna halafu zisikaushwe kitaalamu. Hii sumu ndio moja ya vyanzo vya saratani. Haina maana ukila chakula au kinywaji chenye hii sumu ni lazima uugue. Kwa hiyo sio dawa ya kuweka Bali hutokea kwa sababu ya mchakato usiozingatia utaalamu ambavyo ndivyo tufanyavyo kwa mbegu zote huku kwetu!
 
Mkuu, unahoja nzuri sana. Hakika unga wa DONA una virutubisho vinavyohitajika mwilini. Japo la muhimu ni kuosha mahindi vizuri kabla ya kusagwa ikiwa yamewekwa dawa ya kuhifadhia.

Ukweli ni kwamba Unga wa SEMBE ni makabi tuuu.
 
visivo na sumu vimebaki viwili tu: k na O 2!
 
Wakuu alichosema huyu jamaa mleta mada sio kigeni kwangu maana niliwahi kusikia kitu kama hicho. Nilisikia kwamba ugali wa dona la mahindi linatengeza sumu ikiwa utakuwa unakula kila siku pamoja ya kwamba unga wa dona una virutubisho vya kutosha. Pamoja na hayo, unga wa sembe ni hatari zaidi.
 
ngoja ni google nirudi...........
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…