Wakuu habari zenu!
Mi ninatatizo hili na sijui ni kwa nini ninalo ila nataka nijue kama kuna tiba yake maana linanitia wasiwasi mno.
Natanguliza shukrani wakuu...
Mkuu Nikhili, ebu rudia kuuusoma uzi wa jinsi ya kujieleza kwa daktari hapo juu, nahisi utaweza kusaidia sana hata kama si kwa daktari ila unafupisha kiasi iweze kuleta hata muungano wa mawazo. ila wewe umeelezea hivi kwa ufupi kila mtu ataanza kukuelezea tu kitu kinachohusiana na damu, unaona hata mtaalamu Mzizimkavu ashateremka nondo za tatizo lake mwingine pia atakuja na tatizo lingine na kulishusha mpaka chini kwa maelezo mwisho hataweza kukusaidia wewe,mie na hata wengine. Ila kwa kifupi kinyesi kuchanganyikana na damu si dalili nzuri kwa kusema ivo tuuu....na unatupa maswali zaidi kuliko majibu ya kusaidia mfano naanza...lilianza lini, je damu inaanza kabla ya choo, au baada ya choo au inachanganyika kabisa kama ulivyosema, je kuna maumivu yoyote unayasikia kabla .wakati na baada ya kujiasaidia, au hata muda wote, je unahisi maumivu au uvimbe wa tumbo, je ushawahi kutapika damu au manjano, je ushawahi umwa kichocho,au kuongezewa damu au kunywa pombe kali kwa muda mrefu, au unahisi na manjano ya macho.......kwa kifupi atleast useme yale unahisi yanaweza kusaidia ili kupunguza maswali na watu waweze kulenga tatizo zaidi..ila narudia tena damu kutoka na njia kubwa mara nyingi si dalili nzuri maana kuna magonjwa mengine yanahitaji medical attention na kufanya invstigation zaidi na za haraka...pole kwa maelezo