Hili nalisikia kwako kwa mara ya kwanza...Kama una ufahamu zaidi tuwasiliane. Ninavyojua miradi ni miwili tofauti. Nipo tayari kukupa contact zangu.
nakusalimu sana Dr.nina kaswali nakuomba sana unijibu
Mbona ujenzi wa hii barabara ya feri kibada via tungi umesimama kabisa au inasubiriwa 2015 kampeni hii barabara ya katini faraja kwa wengi ila ndio mbaya sana
Hongereni kwa hatua mliyofikia, ni mfano wa kuigwa na inanipa wepesi kama mwakilishi wenu.
Binafsi ninawashukuru sana NSSF kwa uwekezaji mkubwa katika Jimbo la Kigamboni. Ujenzi wa Daraja, ujenzi wa nyumba 600 za Toangoma, mradi wa Azimio na ule utakaoanza hivi karibuni eneo la Dungu ni mchango mkubwa sana kwa wana-Kigamboni.
Nitakuwa mchoyo wa Fadhila kama sitawapongeza NHC pia kwa uwekezaji wa kasi maeneo ya Kibada na hivi karibuni kwenye eneo la Mwongozo.Ukweli lazima tuuseme na tutoe pongezi panapostahili.
Ni mradi wa ujenzi wa nyumba takribani 7000. Mradi huu ni ubia kati ya kampuni ya Azimio na NSSF. Bw Iqbal ni mwenye eneo hilo na mmoja wa wakurugenzi wa kampuni ya Azimio.
Dkt Faustine Ndugulile MB-Mbunge Kigamboni
Si Kweli! Uvumi unaotoka na kutakuwa na taarifa sahihi. Mradi wa Mji Mpya wa Kigamboni ni mradi wa Serikali wa kujenga Mji mbadala pembezoni mwa DSM. Wazo la Mji Mpya wa Kigamboni ni zuri na wananchi wanaliunga mkono. Matatizo yapo kwenye utekelezaji. Matatizo yenyewe ni kama yafuatayo:
1. Sheria zinazosimamia mchakato huu ni nzuri (Sheria ya Ardhi na.4 ya mwaka 1999 na Sheria ya Mipango Miji na.8 ya 2007). Wanaovunja Sheria ni watendaji wa Wizara ya Ardhi na sio wananchi. Wananchi wanataka Serikali ifuate Sheria.
2. Ushirikishwaji: Watendaji wa Wizara ya Ardhi wanataka haki ya mwananchi kama mmiliki wa ardhi ianze na kuishia katika kulipwa fidia pekee. Wananchi wanataka wawe wadau katika mradi huu na kupewa kipaumbele cha kwanza kwenye ardhi yao.
3. Kumekuwa na usiri na sintofahamu kuhusu haki, Stahili na hatma za wananchi wa Kigamboni: Wananchi wanataka washirikishwe kikamilifu na haki zao ziwekwe wazi na waziafiki.
4. Ucheleweshaji mkubwa wa mradi: Kwa muda wa miaka Sita wananchi wa Kigamboni hawajanipa, hawakarabati, hawawezi kuuza Nyumba wala viwanja vyao na hawakopesheki kwenye mabenki. Hali inayoletea unyonge na kudumaza maendeleo yao binafsi.
Matatizo haya yakitatuliwa, mradi unaweza kupokelewa vizuri zaidi na wananchi.
Tanzania: Minister Trumps Fairness in Land Allocation in Dar
19 August 2014
Tanzania: Minister Trumps Fairness in Land Allocation in Dar
Summary NEPOTISM will not be entertained in the land allocation programme as the allotment will be carried out in transparency, the Minister for Lands, Housing and Human Settlements, Prof Anna Tibaijuka, has stated. "Yono Auction Mart won the tender to allocate the lands to Kigamboni and Kurasini following the announcement by the ministry," she said adding; "Residents should not listen to propaganda from people who have been discouraging others from buying shares." Prof Tibaijuka said when completed, the Kigamboni project would tremendously benefit people who reside in the area and that the government was seeking the fund for the project.
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
Govt suspends plans on Kigamboni satellite city - IPP Media
By Felix Andrew
30th May 2014
Kigamboni Satelite city
Prime Minister Mizengo Pinda told the August House here on Wednesday evening that the process will resume after issued that have to do with involvement of the key stakeholders, including the residents in the area and leaders of Temeke Municipality have been solved.
Pinda was contributing to the budget estimate debate for the Ministry of Lands, Housing and Human Settlement Development which was tabled on Tuesday.
The Premier said there was a need to look again into the whole process of establishing Kigamboni satellite city in order to enable it to be implemented well.
Let us take this issue and involve a wider section of the people like the councilors and other stakeholders so that they become aware of the entire process, he said.
Mh. MBunge Dr F. Ndugulile kulikuwa na hoja hii ya Mhe.Waziri mkuu Bungeni ,lakini majuzi tena Waziri Tibaijuka ameibuka na hoja tofauti.
Swali langu je unataarifa na mwenendo wa hii shughuli ya Wizara na nini maoni yako kwenye ukinzani wa misimamo hii ya Serikali.
CC. Prof Anna Tibaijuka
Hoja za Kamati ya Bunge hazijafanyiwa kazi. Kauli ya Waziri Mkuu haijafanyiwa kazi. Maagizo ya Spika hayajafanyiwa kazi.
Kuna tatizo la baadhi ya viongozi wanaopenda kutumia vyombo vya habari "kushughulikia na kutatua" matatizo ya wananchi bila kushirikisha wananchi wenyewe.
Inashangaza sana viongozi hawa wanashindwa kuelewa "ushirikishaji wa umma" ni moja ya msingi muhimu kabisa katika dhana ya utawala bora.
Bwana Akbaru ndio mmemshindwa kabisa anafuga mapori anatunyima fursa wakulima wadogo kwa sasa kisarawe,kijaka,kimbiji,mbutu ,mwasonga yote kahodhi maeneo!! Si mbunge si tibahijuka si kikwete wote mmewekwa mifukoni na Akbaru! Huyu Akbaru ni nani asiyeguswa? Huyo shombe shombe kawarubuni wazee na kununua ekari moja kwa laki moja hadi laki na nusu hayaendelezi kwa zaidi ya miaka 10 anaweka mapori tu na mbunge pamoja na tibahijuka wanamshangilia!!! Kwa sasa ardhi ya kulima hakuna tumekimbilia tundwi na huko bagamoyo kuna akbaru mwingine wa msoga yani sheeedaa!
Mkuu naomba ujibu hii hoja hapa chini maana ina mashiko
Sheria ipo wazi mtu asipoendeleza eneo kwa mda wa miaka mi3 ananyang'anywa huyu akbaru ana mapori kayafuga zaidi ya miaka 10 bila kuendeleza hata hasipojibu ujumbe kaupata vizuri.