Ujenzi wa Reli ya SGR uishie Tabora

Ujenzi wa Reli ya SGR uishie Tabora

Acha iishe tuu reli ni muhimu sana, na zisipotumika hapo zitaishia kujenga matundu ya choo for same amount of money
 
Mlikuwa wapi kulisemea hili mwanzoni mpak now mradi upo on-air
Yaani ulitaka amkosoe JPM? Hajitaki? Angeishia kutukanwa na kuitwa kila aina ya majina, na wasiojulikana nao wangemtembelea! IRA UDSM ilivunjwa yote na maprofesa wake kutukanwa kisa tu walimshauri "Mungu Mtu" yale asiyotaka kusikia kuhusu mradi wa Rufiji! Prof. wangu wa UDOM alitukanwa hadharani kisa tu aliongea ukweli kuhusu Makinikia
 
Hela hatuna, tusikope sana ili kupunguza kutumia na madeni.

Tabora ni karibu sana na Burundi, Rwanda, DRC, Mwanza na Uganda. Tujenge bandari kavu kuubwa pale Tabora ili watu wa Mwanza, Uganda, Rwanda, Burundi, DRC na Kigoma wachukulie Tabora mizigo yao itakayoletwa na SGR hapo.

Tukipata faida hapo tutaendelea na ujenzi hadi Mwanza, Burundi Rwanda na DRC kama tulivyokuwa tumepanga.

Hii itasaidia kuepuka uharibifu wa barabara kutoka dar hadi Tabora lakini na kupunguza umbali na gharama kwa watu wa DRC, Rwanda, Burundi kufuata bidhaa zao Dsm.
Mkuu kavulata , kwanza asante kwa mawazo yako. Sii wengi humu wanajua how SGR can operate profitably!. Ili SGR iweze kuleta faida ni lazima iwe na kitu kinachoitwa linkages. Mfano hiki kipande cha Dar Moro ambacho kiko tayari, kiteendeshwa kwa hasara muda wote hadi SGR itakapo link na Rwanda, Burundi, Uganda na DRC.

Karibu mitaa hii

Pia kasome
P
 
Yaani we acha tu. Tushakula hasara ya matrillioni dah! Sijui haya makosa ni ya bahati mbaya au makusudi. Maana taarifa zote zipo bandarini na watu wote wanajua mizigo mingi ambayo inapita Bandarini ni ya Zambia na DRC congo. Na mizigo ni ya Cobalt na Copper. Na hayo madini yapo Zambia na huko Katanga congo. Sijui nani wakukosoa hilo kosa. Dah! Matrillioni tuliokopa hayatarudi. Ilitakiwa sgr itoke Dar-Kapirimposhi-Lubumbashi (ipite kwenye migodi ya Copper na Cobalt) ndio kuna mizigo ya mamiiliona ya Tani.


Inabidi watu warudie kudesign ramani ya sgr iende sehemu ya mizigo mingi..
Ipo TAZARA, kwa nini isitumike kwa ufanisi?
 
SGR inakwenda kuwasaidia Wapiga Kura Mwanza. Full stop!
Chuki ilikuwa kubwa mno mno mno dhidi ya kanda nyingine, hasa kaskazini, Mashariki na kusini, nchi ilikuwa ikijengwa upande mmoja zaidi. Tulishuhudia miradi mikubwa ikimiminwa kuelekea kanda moja na idadi ya mikoa ikiongezwa upande huo. Hata kuhamia Dodoma kwa nguvu ilikuwa kusogeza huduma karibu na kanda pendwa sio vinginevyo.
 
Mkuu kavulata , kwanza asante kwa mawazo yako. Sii wengi humu wanajua how SGR can operate profitably!. Ili SGR iweze kuleta faida ni lazima iwe na kitu kinachoitwa linkages. Mfano hiki kipande cha Dar Moro ambacho kiko tayari, kiteendeshwa kwa hasara muda wote hadi SGR itakapo link na Rwanda, Burundi, Uganda na DRC.

Karibu mitaa hii

Pia kasome
P
Ahsante mkuu, hata mm kuna uzi humu niliwahi kuandika kuhusu ni nini kitasafirishwa kwenye SGR ili tupate faida? Tukumbuke kuwa faida ya SGR itakokotolewa baada ya kutoa faida iliyokuwa ikitokana na usafirishaji kwa njia malori, mabasi ya abiria na reli ya kati (opportunity costs). Ndio maana mimi nikapendekeza reli hii ghali sana kujenga na kuendesha ya SGR ingeishia morogoro, Dodoma, Singida au Tabora tu kusaidia kuondoa msongamano wa malori bandari ya DSM na "Bagamoyo" kwa kuisogeza mizigo Morogoro, Dodoma, Singida au Tabora ili biashara ya malori, mabasi na reli ya kati isife
 
Kila mjinga leo anatoa ushauri wa kichekesho.
Kuna ombwe pahala ukiona hivyo. Itafika pahala kila mtu atajitengenezea ndama wake wa dhahabu na kumfanya Mungu wake.
 
Kwasasa cobalt bado inasafirishwa na malori kwenda afrika ya kusini kupitia bandari ya Durban. Mzigo wa Cobalt na Copper ni mwingi kiasi kwamba bandarini Dar hawawezi kuhandle.

Na mzigo wa Copper na Cobalt upo mwingi na wa kutosha. Kuanzia copper belt ya Zambia kufika Katanga mpaka Kolwezi mpaka kufika kwenye migodi ya cobalt. Sasa hii reli yetu wamefanya makosa makubwa. Wanapeleka reli kigoma ujue upande wa pili ni uvira na hakuna mzigo na ni mbali sana toka Katanga kwa hiyo mzigo wa cobalt tutaukosa. Na sgr watapeleka karema- katavi ambapo upande wa pili ni Kalemie ambapo hakuna mzigo na ni mbali toka migodi ya Cobalt ya Katanga na kolwezi kama 1000km. Na hapo hujapiga hesabu ya kununua meli kubwa ya mizigo ziwa Tanganyika, na pia Congo inabidi wajenge bandari kubwa upande wao wa Kalemie. Yaani kiufupi mradi wa sgr ukikamilika hautapata mzigo mkubwa wa kurudisha hela na madeni na riba. Nenda kafatilie uzalishaji wa Copper na Cobalt na maeneo ambayo migodi ipo huko zambia(Copper belt) na congo (katanga, Lubumbashi, kolwezi) halafu fatilia geography ya congo. Kisha linganisha na sgr ya inayojengwa ndio utaelewa jinsi sgr inavyopotea
Wanasema reli ni huduma hata kama faida isipokuwepo, tutasafirisha ng'ombe na wapiga kura wetu.
 
Unajua upande wa pili wa ziwa Tanganyika kuna mji wa uvira ambao hauna mzigo wowote wa maana yaani ni hasara juu ya hasara. Mizigo mingi ipo usawa wa Zambia kuelekea Lubumbashi, kolwezi na Katanga kwenye migodi ya Cobalt na Copper. Sasa ishu ni uzembe wa kujipanga kutarget huo mzigo. Maana Africa kusini ni mbali mno ukilinganisha na Dar. Yaani tunacha mizigo ya maana ya mamiliona ya Tani halafu mwishoni tutashindwa kulipa deni
Tunatakiwa tujue Kwanza sababu ya uelekeo wa sgr kuwa huo na sio huko unakosema, pengine Kuna sababu za maana zaidi kuliko unavyofikiria
Hata hivyo kutoa mawazo mbadala baada ya mradi kuanza hakusaidii taifa, mawazo yako ungeyaibua kabla ya upembuzi yakinifu watu wakajadili hapa pengine wangeyaona wahusika.
 
Nenda kaangalie ramani ya Congo, Zambia na Tanzania. Halafu angalia umbali kati ya Katanga, Kolwezi kuja Dar kupitia Kapirimoshi zambia. Halafu angalia njia na umbali toka Katanga kuja uvira kisha kigoma kisha Dar. Angalia route ipi ni fupi. Kumbuka hii ni biashara na mzigo ukipita route fupi ndio gharama ya usafiri inapungua. Na mzigo mwingi upo Zambia kwenye copper belt na Cobalt ya congo kwenye migodi iliyopo Katanga mpaka Kolwezi. Hebu kaangalie ramani ndio utaelewa makosa ya sgr
Ungekuwa ujinga uliopitiliza kujenga SGR kando ya TAZARA kuelekea Zambia tena kama ulivyo kujenga SGR na barabara nzuri kandokando ya reli ya kati hadi Mwanza. SGR, barabara na reli ya kati lazima zicheze pamoja kwenye uwanja mmoja kila mtu na nafasi yake ili kupata synergism. Lazima kuwe na kazi Meli, kazi ya SGR, kazi ya Barabara na kazi ya reli ya kati, maana vyote ni vyetu na hatutaki vife. Kuna kodi, ajira na huduma kwenye meli, SGR, malori na reli ya kati pia. Do not strengthen the weakest by weakening the strongest.
 
Jpm kapotea.


Hii ni biashara, kwenye biashara ya usafiri tunaangalia mizigo inayosafirishwa. Na tunaangalia potential ya kuwepo uhakika wa mizigo ya kusafirisha. Kwa takwimu za bandarini. Mizigo mingi inatoka Migodi ya Zambia na Congo na ndio inapita Bandarini. Sasa ilitakiwa sgr ijengwe kuifuata migodi ya Zambia na Congo. Hicho kilichofanywa kupeleka reli kanda ya ziwa na kigoma ni kupoteza hela na hakuna mizigo ya kurudisha hela na madeni na riba.


Sasa hivi mizigo ya migodini inapitia Durban afrika ya kusini.
Wazo mama la kujenga SGR kuelekea mwanza haikuwa biashara na faida bali huduma ya haraka sana ya bei nafuu kutoka mwanza kuja Dsm.
 
Hela hatuna, tusikope sana ili kupunguza kutumia na madeni.

Tabora ni karibu sana na Burundi, Rwanda, DRC, Mwanza na Uganda. Tujenge bandari kavu kuubwa pale Tabora ili watu wa Mwanza, Uganda, Rwanda, Burundi, DRC na Kigoma wachukulie Tabora mizigo yao itakayoletwa na SGR hapo.

Tukipata faida hapo tutaendelea na ujenzi hadi Mwanza, Burundi Rwanda na DRC kama tulivyokuwa tumepanga.

Hii itasaidia kuepuka uharibifu wa barabara kutoka dar hadi Tabora lakini na kupunguza umbali na gharama kwa watu wa DRC, Rwanda, Burundi kufuata bidhaa zao Dsm.
Reli ikiishia tabora,hatutapa mapato ya fedha za kugeni wacha tuimalize tu hadi kigoma

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
Mradi wa sgr umetutia madeni. Halafu mradi ukikamilika utatutia madeni zaidi. Pia ramani ya mradi imekosewa. Reli ya sgr inatakiwa iende sehemu ya mizigo mingi. Na mizigo mingi ni shaba ya Zambia, na madini ya cobalt na shaba yaliyopo Lubumbashi/kolwezi/katanga DR Congo.

Sasa hii reli naona imepotea uelekeo wa mizigo mingi mno kwa hiyo haitarudisha hela. Kwa hiyo ni madeni juu ya madeni halafu riba. Mizigo mingi ipo kusini kwa Congo na Zambia. Halafu reli inaelekea mashariki mwa Congo

Hao Rwanda na Burundi hawana mzigo wa maana kuzidi Zambia na Cobalt na Copper ya Drc congo. Ilitakiwa SGR iende kwenye mizigo ya maana huko kwenye migodi ya zambia na Congo.

Hii sgr inayojengwa imekosewa kabisa. SGR ilitakiwa iwe Dar-Kapirimposhi-Lubumbashi(ikiwezekana ipite kwenye migodi ya Copper na Cobalt iliyopo Kolwezi, Mutanda huko Drc ndanindani)
Akili ndogo kweli
 
Mzigo wa Rwanda, Congo DRC, na Zambia unaoingia kupitia bandari kwa mwaka ni tani ngapi kwa kila mmoja?
Umeandika kitu Cha kufikirisha Sana, maana huwezi kukosoa bila kuwa na data ya mizigo inayotoka sehemu husika.
Mwenye data atuletee Kwanza hapa tuone
 
..Dar to Kapirimposhi ni reli ya Tazara.

..Tujiulize kwanini reli hiyo inaendeshwa kwa hasara?
Kabisa, reli ya TAZARA ni Ipo vizuri kuliko Reli ya Kati, lakini inaendeshwa kwa hasara kubwa, na hii reli ya TAZARA inafika hadi huko Kapirimposhi
 
Reli ikiishia tabora,hatutapa mapato ya fedha za kugeni wacha tuimalize tu hadi kigoma

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
Hapa tunaongelea ukosefu wa hela ya kujengea SGR yote sawa na mpango. Ndio maana tunashauri badala ya kuicha hela yetu ipotee bure kwa kutokamilika kwa ujenzi na badala ya taifa kukopa zaidi ili kujenga SGR the least evil ni kukamilisha ujenzi hadi Tabora tu. Pale Tabora zitafutwe ekari kama 1000 hivi za kujenga bandari kavu ya mizingo ya Mwanza na vitongoji vyake, kigoma, DRC, Rwanda, Burundi ili kupunguza umbali wa kuja bandari ya dsm. Tukifanya hivyo kutakuwa na faida zifuatazo:
1. Wateja wetu wataishia Tabora tu.
2. Barabara zetu kutoka dam hadi tabora zitapunzika sana.
3. Biashara ya malori, mabasi na reli ya kati ambayo yalikuwa yakose kazi itaendelea.
4. Mji wa Tabora utaendelea kiuchumi na kijamii.
5. Ajira itakuwa kubwa kanda ya kati pale
6. SGR itafanyakazi kuliko kutelekezwa kabisa.
7. Madeni ya ujenzi wa SGR yatapungua
8. Tutapata uzoefu wa kuendesha SGR (pilot study)
9. Faida tutakayopata itamalizia vipande vilivyosalia (capacity building)
 
Mradi wa sgr umetutia madeni. Halafu mradi ukikamilika utatutia madeni zaidi. Pia ramani ya mradi imekosewa. Reli ya sgr inatakiwa iende sehemu ya mizigo mingi. Na mizigo mingi ni shaba ya Zambia, na madini ya cobalt na shaba yaliyopo Lubumbashi/kolwezi/katanga DR Congo.

Sasa hii reli naona imepotea uelekeo wa mizigo mingi mno kwa hiyo haitarudisha hela. Kwa hiyo ni madeni juu ya madeni halafu riba. Mizigo mingi ipo kusini kwa Congo na Zambia. Halafu reli inaelekea mashariki mwa Congo

Hao Rwanda na Burundi hawana mzigo wa maana kuzidi Zambia na Cobalt na Copper ya Drc congo. Ilitakiwa SGR iende kwenye mizigo ya maana huko kwenye migodi ya zambia na Congo.

Hii sgr inayojengwa imekosewa kabisa. SGR ilitakiwa iwe Dar-Kapirimposhi-Lubumbashi(ikiwezekana ipite kwenye migodi ya Copper na Cobalt iliyopo Kolwezi, Mutanda huko Drc ndanindani)
Ipo Reli ya Tazara, inakufa tu pale. Wafanyabiashara weengi wanaiogopa sababu ya Delay ya mizigo. Kumbuka Biashara ya Reli kusafirisha mizigo inaua biashara ya Malori ambayo meengi ni ya viongozi katika hizi nchi, yaaani Zambia na Tz.....
 
Back
Top Bottom