Ujinga ni tatizo kuu hapa Tanzania

Ujinga ni tatizo kuu hapa Tanzania

Hapana wengi wanapinga bandari kupewa mwekezaji wanadai mambo ya usalama sijui nchi itauzwa n.k yaani sio tu mkataba uboreshwe hawataki kabisa DP world aje bandarini.

2. Wanadai tuliibiwa sana na wawekezaji yes ni kweli lakini kwa Sasa Kuna sheria nzuri zimewekwa mfano Ile ya 16% hisa kwa serikali, local content kwamba lazima ratio Fulani ya tender na ajira zitoke nchini, Kuna sheria kali za transfer pricing 2018 zimepunguza mianya ya kukwepa kodi walau kwenye haya makampuni ya nje etc. So mjadala uwe mkataba utakaoingiwa basi uwe na maslahi kwa nchi lakini sio kupinga mwekezaji apewe bandari.

3. Hao TPA ndio Wezi kuliko hata makampuni ya kigeni, so mbadala wa bandari usiwe TPA tena Bali muwekezaji serious otherwise tunachokwepa kubwa na DP ndio kinachoibiwa na hao wahuni wa TPA.
Kwa kifupi wapingaji hawana hoja za msingi
 
Hapana wengi wanapinga bandari kupewa mwekezaji wanadai mambo ya usalama sijui nchi itauzwa n.k yaani sio tu mkataba uboreshwe hawataki kabisa DP world aje bandarini.

2. Wanadai tuliibiwa sana na wawekezaji yes ni kweli lakini kwa Sasa Kuna sheria nzuri zimewekwa mfano Ile ya 16% hisa kwa serikali, local content kwamba lazima ratio Fulani ya tender na ajira zitoke nchini, Kuna sheria kali za transfer pricing 2018 zimepunguza mianya ya kukwepa kodi walau kwenye haya makampuni ya nje etc. So mjadala uwe mkataba utakaoingiwa basi uwe na maslahi kwa nchi lakini sio kupinga mwekezaji apewe bandari.

3. Hao TPA ndio Wezi kuliko hata makampuni ya kigeni, so mbadala wa bandari usiwe TPA tena Bali muwekezaji serious otherwise tunachokwepa kubwa na DP ndio kinachoibiwa na hao wahuni wa TPA.

Well sijui hao wengi lkn ukiona wengi wanapinga ina maana hawataki kwa nini muwalazimishe wakati wengi hawataki? Demokrasia ni kusikiliza wengi isitoshe tumeshaumizwa sana hivyo tutakuwa ni wajinga kama tusipotaka kuwa waangalifu kwani wanaotetea dp world ndio wale wale pia waliotetea kuuzwa kwa shirika la reli kwa wahindi, ndio wale wale waliotetea uwekezaji wa migodi ya dhahabu ambapo sasa yamebakia mashimo na hakuna tulichofaidika, hivyo its human kama ulishaumizwa kuwa mwangalifu …
 
Mbona Dp world Imepewa bandari kadhaa China. Nadhani issue iwe tu mkataba wa kimaslahi ila hata china wao maendeleo Yao yalikuja kwa mitaji ya kigeni.
Kama ni hivyo jengeni hoja kwa kushauri serikali sehemu pa kufanyia marekebisho kwenye mikataba siyo kuleta lawama jumuishi kama mleta mada...inakera sana.
Serikali nayo viongozi wanaleta mikataba mibovu inayoingia na hao wawekezaji huku wakitoa lawama kwa wafanyakazi wanaoendesha taasisi zinazodaiwa kushindwa kujiendesha kwa faida.

Ebu fikiria wanasiasa wanafanya makosa lakini hawachukuliwi hatua za kinidhamu alafu unataka mfanyakazi hapo TPA wao wawe Mungu walionee nchi huruma...Akina Musukuma hawalipi kodi kwenye biashara zao zote lakini ndiye wa kwanza kuilaumu wafanyakazi wa TRA na TPA...ukitaka kuwawajibisha viongozi wa juu wanapiga simu yenye vitisho.
 
Kwa hiyo bi Tozo alipelekwa wapi kujifunza uwekezaji?

Shida mnakwepa ukweli

1. Ukomo wa mkataba
2. Kwa nini Zanzibar hazihusiki?
3. Analeta mtaji kiasi gani kuwekeza
4. Mapato na kodi zetu zimekaaje?
5. Sharti la kupewa ardhi yoyote anayotaka na tuwalipe sisi tutakaowandoa anapopataka boss
6. Kutokuvunja mkataba hata akiboronga.

Hatupingi uwekezaji ila tunapinga mkataba mbovu
 
Kwa hiyo bi Tozo alipelekwa wapi kujifunza uwekezaji?

Shida mnakwepa ukweli

1. Ukomo wa mkataba
2. Kwa nini Zanzibar hazihusiki?
3. Analeta mtaji kiasi gani kuwekeza
4. Mapato na kodi zetu zimekaaje?
5. Sharti la kupewa ardhi yoyote anayotaka na tuwalipe sisi tutakaowandoa anapopataka boss
6. Kutokuvunja mkataba hata akiboronga.

Hatupingi uwekezaji ila tunapinga mkataba mbovu
Una uhakika hayo unayosema yapo hayajatolewa ufafanuzi?
 
Enzi za Mao, China ilikuwa nchi ya kikomunisisti iliyoamini katika Sera za Ukomunisti.

Pamoja na Ukomunisti wa China, Rais wa kwanza wa China, Mao aliamini kuwa ni lazima apeleke vijana nje ya China wakajifunze Dunia inaendaje na ikoje ili warudi kufanya mabadiliko China.

Moja ya vijana hao alikuwepo Den Xiapoing ambaye alikuja kuwa Rais wa China baada ya Mao. Den alipelekwa Ulaya na akajifunza sana namna uchumi wa Ulaya ulivyokuwa unaenda.

Alipokuja kurudi China, Den alianzisha mfumo wa Private Property na Uwekezaji wa Sekta binafsi katika mfumo wa Uchumi wa China. Kipindi chake ndo makampuni mengi ya Marekani yalienda kufungua viwanda na kufanya uwekezaji China.

Kwa wachina wengi walimuona Deng ni msaliti wa Mao kwa kuwa wengi walikuwa wanaamini kila kitu ni cha wachina na mwekezaji kutoka nje ni mwizi. Den aliwajibu haijalishi kama paka ni mweupe au ni mweusi ili mradi anakamata panya basi huyo anatufaa

Pamoja na wachina kupata shida kuelewa Sera za Den Xiapoing ila leo ndo wachina wanamsujudu kama The Father of Modern China.

Ukiacha China kuna nchi za Singapore na Umoja wa Falme za Kiarabu ambao Dubai ni nchi mojawapo za umoja huo.

Hizi nchi nazo miaka ya 1960 ilikuwa kama sisi! Ila watawala wao walipata akili kuwa kwa akili za kuwaza sisi ndo sisi hatutafika popote. Kupitia rasilimali ya mafuta Dubai walibadilisha Sera zao kuhamasisha uwekezaji wa sekta binafsi. Leo hii kila mtu Duniani anakwenda kutalii Dubai na si kwa sababu ya mafuta tu ila kutokana na namna ikivyojengwa , inavyopendeza na ilivyo na uchumi mkubwa na maendeleo makubwa.

Ukija Tanzania. Hapa ndo shida ilipo. Nchi hii ilianzishwa katika misingi ya kijamaa. Misingi hii iliwaaminisha watu kuwa kila kitu ni Serikali na Serikali ni kila kitu. Mfumo huu ambao unaamini katika state capture umedumaza akili za Watanzania wengi sana kiasi ambacho kuna Watanzania leo hawajifunzi hata dunia ikoje, inaenda wapi na itakuwa wapi miaka hata 50 mbele.

Akili hizi zinaamini kuwa Sera ya uwekezaji ni kuuza nchi, Uwekezaji ni uuzaji wa nchi. Sera hii imewafanya Watanzania kuwa nyuma sana. Nchi yetu kuwa nyuma sana, mifumo yetu ya huduma kuwa nyuma sana.

Leo hii Tanzania, unatoka Dar hadi Kigoma kwa masaa zaidi ya 15 kwenye treni ambayo muda wowote unaweza kuambiwa leo hakuna usafiri. Ndani ya hiyo treni vyoo vichafu, huduma ni mbovu ila mtanzania hana shida ili mradi tu inamilikiwa na Serikali

Leo hii nchi yetu ina bandari zinayoweza kuhudumia ipasavyo nchi hadi 8 zinazotuzunguka, ila meli zinakaa wiki 2 hadi 3 kushusha mizigo, wafanyabiashara wanapoteza mizigo yao, hakuna mapato makubwa nchi inaweza kupata na kufanya maendeleo makubwa ila watu wanaona sawa tu ili mradi iwe chini ya Serikali. Hawajali hata wakiambiwa meli zinakimbia zinaenda Bandari za nchi jirani ili mradi waone au wasikie Serikali ndo mmiliki. Huu ni ujinga uliotukuka sana.

Kibaya zaidi pamoja na ujinga huu wa Watanzania, nchi jirani zinazotuzunguka zinakimbia sana ili kukamata fursa za kiuchumi sisi tusiwe na kitu. Rwanda amejenga Bandari kavu kubwa sana ili mizigo ya Congo Mashariki ipite kwake . Bandari hii kawapa wawekezaji. Sasa Rwanda anajenga uwanja wa Ndege mkubwa zaidi Afrika Mashariki ambao utaendeshwa pia na Sekta binafsi.

Huku Kenya amejenga Bandari ya Lamu ambayo ataiendesha kwa sehemu kubwa kupitia sekta binafsi, Msumbiji kaomba vikosi vya Rwanda vilinde Bandari zake ili wawekezaji waweze kuwekeza na zifanye biashara. Hawa wakifanya haya Serikali ikichukua hatua kuboresha utendaji wa Bandari kuna watu wanaaza kusema nchi inauzwa.

Serikali ikiwasikiliiza hawa watu kuna hatari kubwa sana huko mbeleni nchi yetu kuja kuwa kituko cha mwisho zaidi kuliko hata sasa, kutokana na kusikiliza wajinga huku nchi ikitakuwa ikimbie iendane na mabadiliko ya Dunia ya sasa.

Kwa Dunia inavyokwenda sasa, Tanzania haipaswi kurudi nyuma tena! Ujinga usipewe tena nafasi Tanzania!
Acha mboyoyo, tuambie ni wapi watanzania wameukataa uwekezaji?

Wanachokataa ni utapeli kupitia bandari
 
Kwa Dunia inavyokwenda sasa, Tanzania haipaswi kurudi nyuma tena! Ujinga usipewe tena nafasi Tanzania!
Huelewi unachokiandika juu yake.

Uliambiwa kuwa "communist" ni kujitenga na dunia nyingine?

Huko kwenye "ubepari" kuna mahali popote wanaposema ni lazima kila nchi iwe na mfumo sawasawa na mkuu wa hao mabepari?

Sasa wewe unayekariri, nawala hutaki au huna uwezo wa kutumia akili zako na kudadavua lipi linalofaa kwa wananchi wa hapo ulipo, tuelewe wewe ndiye mtetezi mkuu wa ubepari?

Mbona hata huko kwenye ubepari bado kuna mambo ya kikomunist yanafanyika?

Uliambiwa kwa Tanzania kuwa nci ya kibepari kwelikweli ni lazima iuze kila kitu ilichonacho kwa hao mabepari watakaokuja kukuletea maendeleo hapa?

Huyo Deng, alipofungua nchi, wachina walibweteka kwa kujua mabepari wanaleta maendeleo?

Ni ajabu sana kwa mtu mwenye akili kudhanikwamba maendeleo yaliypo China yamletwa na watu kutoka nje. Hii akili siyo ya kawaida kabisa.

Mwisho, ngoja nikiri kwamba andiko lako refu sikulisoma. Lakini ninajua takataka ambazo wewe hupenda kuzitetea hapa JF.
 
Huelewi unachokiandika juu yake.

Uliambiwa kuwa "communist" ni kujitenga na dunia nyingine?

Huko kwenye "ubepari" kuna mahali popote wanaposema ni lazima kila nchi iwe na mfumo sawasawa na mkuu wa hao mabepari?

Sasa wewe unayekariri, nawala hutaki au huna uwezo wa kutumia akili zako na kudadavua lipi linalofaa kwa wananchi wa hapo ulipo, tuelewe wewe ndiye mtetezi mkuu wa ubepari?

Mbona hata huko kwenye ubepari bado kuna mambo ya kikomunist yanafanyika?

Uliambiwa kwa Tanzania kuwa nci ya kibepari kwelikweli ni lazima iuze kila kitu ilichonacho kwa hao mabepari watakaokuja kukuletea maendeleo hapa?

Huyo Deng, alipofungua nchi, wachina walibweteka kwa kujua mabepari wanaleta maendeleo?

Ni ajabu sana kwa mtu mwenye akili kudhanikwamba maendeleo yaliypo China yamletwa na watu kutoka nje. Hii akili siyo ya kawaida kabisa.

Mwisho, ngoja nikiri kwamba andiko lako refu sikulisoma. Lakini ninajua takataka ambazo wewe hupenda kuzitetea hapa JF.
Unaanza kwa kusema sielewi nilichoandika unamalizia kwa kusema hujasoma chote nilichandika. Ndo mana nikisema ujinga kwa watanzania ni tatizo nielewe ndugu.
 
Unaanza kwa kusema sielewi nilichoandika unamalizia kwa kusema hujasoma chote nilichandika. Ndo mana nikisema ujinga kwa watanzania ni tatizo nielewe ndugu.
Nimekueleza msingi wa nilichojibu. Hukusoma hilo?
Nimesoma mistari ya mwanzo nikaona hadithi ni zile zile za siku zote, sikujihangaisha tena kupoteza muda na andiko refu hilo lenye mambo yale yale ninayofahamu unayatetea kila mara humu.

Na kuhusu huo "ujinga" nilitaka kulisemea hilo, lakini nikaghaili.
Ngoja nikuache kwa sasa kuhusu hili la "ujinga."
 
Nimekueleza msingi wa nilichojibu. Hukusoma hilo?
Nimesoma mistari ya mwanzo nikaona hadithi ni zile zile za siku zote, sikujihangaisha tena kupoteza muda na andiko refu hilo lenye mambo yale yale ninayofahamu unayatetea kila mara humu.

Na kuhusu huo "ujinga" nilitaka kulisemea hilo, lakini nikaghaili.
Ngoja nikuache kwa sasa kuhusu hili la "ujinga."
Uwe na jioni njema
 
Ila ni kweli kabisa
Nchi ya kifala sana hii
Nimeshuhudia Warundi wakiingizwa usiku pale NIDA Chang'ombe kwenda kutoa alama za vidole, kulikuwa na afisa wa NIDA na Mlinzi wa SUMA JKT, kila Mrundi aliliwa jiwe tatu 300,000 daadeki, halafu kuna watu humu wanalilia uzalendo kwe kwe kwee😆😆

Kulikuwa na Warundi kama 28 hivi so do the maths.
 
Back
Top Bottom