Ujumbe huu uwafikie Askari wa JWTZ

Ujumbe huu uwafikie Askari wa JWTZ

Sehemu husika ni kwenda kumripoti kwa wakubwa zake ni ishu nyepesi tu lazima ashughulikiwe ipasavyo.
Utaratibu wa kuonana na wakubwa wao upoje? Maana kuingia kambini ni lazima ukutane na walinzi getini ambao Wana vyeo vidogo na watakuhoji, na obviously wakiona unataka kumchoma mwenzao watakuzuia kuingia.
 
Onyo zuri mwenye akili timamu asikie na kuelewa.
Nadhani ingekuwa busara kama ange weka full story lakini hapo tutamuhukumu mwanajeshi bila kujua upande wa pili ilikuwaje... Mimi sidhani kama huyo mwanajeshi ni punguani aanze kumpiga TU mtu bila sababu...huyu Kuna kitu kakikoroga...haki vile​
 
Una umri gani?
Cheo chako?

Ukinijibu nitakuambia nilipo uje, tuone kama utayaweza.
Poti lazima awe na nidham.
Mkuu weka namba yako ya simu au email nikisema nikazichukue Kwa mods wa Jf ntakua nimekuonea weka hapa ila Ombii langu wewe si ni kidume usiandike contact za Uongo lengo langu ni kukufundisha serikali ipo....
NB.
No beef
 
Utaratibu wa kuonana na wakubwa wao upoje? Maana kuingia kambini ni lazima ukutane na walinzi getini ambao Wana vyeo vidogo na watakuhoji, na obviously wakiona unataka kumchoma mwenzao watakuzuia kuingia.
Siyo lazima useme unawaeleza unahitaji kuonana na mkuu wa kambi lazima wakupe utaratibu
 
Na kwa bahati mbaya, wengi hawana elimu
Hilo sasa mkuu ni tatizo jingine!
Tusifuge vifuani mwetu nadharia ama dhania hiyo ya jumla jumla ambayo haina ukweli wowote.

Kuhusu elimu ya kitaaluma isichukuliwe katika kuthamanisha maisha halisi ya mtu mzima.
Kuna watu hawajasoma hata "a" lakini maisha yao ni standard, utu na yenye hekima tupu.

"Elimu" kama mnavyodhania kustaarabisha watu, basi leo hii nchi yetu Tz ingekuwa na maisha mazuri na bora kabisa karibia kulinganishwa na pepo ya firdausi namna ilivyojaliwa jiografia nzuri na rasilimali chekwa kwa raia wake!

Sasa watunga sera na mafisadi waliotufikisha tulipo, ni kada ya wajinga na mambumbumbu wasio na elimu?

Matendo ya hovyo hufanywa na mtu yeyote baradhuli bila kujali idadi ya madarasa ya taaluma yaliyopo kichwani mwake.
 
Wakiweza na wao kuwaelewesha wahasibu wao na makamamanda kuhusu usumbufu wanaoupata waazazi wao kwenye matibabu.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]bongo wanajeshi wanakula Hela za Bure tu,ila hawana lolote ndo maana wanaleta ubabe mtaani
Wakipelekwa Mozambique kupambana na ugaidi, wanarudishwa wakiwa mizoga. Badala watumie huu wakati wa Amani kujiimarisha, wanaoutumia kutengeneza chuki na raia wasio na silaha.
 
Ungekuja kutoa malalamiko yako sehemu husika ili upate haki yako jeshi ni la wananchi ni mali yenu sote.
Shida siyo kutoa malalamiko,yaani mtu anipige makofi,nije nitoe malalamiko,dawa ni kupambana kadri unavyoweza,kama utapigwa sawa,kama utampiga sawa.Wananchi waache unyonge,mwanajeshi akikuzingua eti anataka kukupiga,usipigwe kizembe,pambana kadri unavyoweza.Hakya-Mungu siwezi kukubali uniaibishe hadharani,halafu niende kwa wakubwa ukaombe msamaha faraghani,aisee sikubali.
Jiulize kwanini Rostam Aziz alipotuhumu mahakama kuwa haziko huru,aliambiwa na chama cha majaji,aombe radhi vilevile alivyotuhumu,yaani kama aliita vyombo vya habari kutuhumu,basi aite vyombo vya habari kukanusha na si vinginevyo,angesema akanushe faraghani,nani angejua kakanusha?
Narudia tena,mwanajeshi asiye na nidhamu,akinizingua,namimi namzingua,ni heri tupambane nionekane nimepambana,siyo kupigwa kizembe.
 
Back
Top Bottom