Elections 2015 UKAWA na Lowassa unganeni mchukue nchi, wakati ndio huu, mkipuuzia huu ushauri basi tena!

Elections 2015 UKAWA na Lowassa unganeni mchukue nchi, wakati ndio huu, mkipuuzia huu ushauri basi tena!

Naona Team Lowasa mnaweweseka na Lowasa wenu. Nani alikwambia UKAWA wanatafuta ushindi kwa njia haramu? Lowasa ni mchafu na UKAWA ni watu wasafi hawako tayari kuchafua njia na nia yao ya kujenga Tanzania iliyo safi kwa kuungana na uchafu. Lowasa ni fisadi na sera za UWAKA ni kuwaondoa mafisadi akiwemo Lowasa itakuwaje wawe na nia hiyo halafu wamchukue fisadi kupambana na mafisadi. Ni njia haramu kuwa naye kwenye mapambano. Mtafutie kwingine na si WAWAKA

Hizi ni hoja nyepesi. Mimi wala siop timu Lowassa kama unavyodhani. Mimi maisha yangu hayamtegemei mwanasiasa, kwani ninaweza kuishi popote duniani kwani Mungu amenibariki. Kinachoniuma ni mfumo kandamizi wa CCM hadi wananchi walio wengi hawapati mahitaji ya msingi kwa miaka nenda rudi. Sasa hali imekuwa mbaya zaidi hasa kiusalama (rejea vamizi kwenye vituo vya polisi hapa nchini).

Huo uchafu wa Lowassa unaouongelea ni upi ambao Magufuli au viongozi wengine wa CCM hawana? Aceni kudanganya watu ili mkoloni mweusi CCM aendelee kutunyonya. UKAWA wanatakiwa kuelewa kwamba ushindi ni strategies na ikipatikana opportunity unachukua na ukiacha ujue imekula kwako. Lowassa na opportunity kwa UKAWA na Watanzania wote kwa ajili ya kuondoa mfumo kandamizi wa CCM.
 
fuvu la paka

Unahisi kwa moyo wote huyo uliyemtaja yuko kwa ajili ya kuwatumikia wananchi? mi nadhani wangemtumia huyo kama daraja la kuvukia kuwatumikia wananchi?

Waswahili walisema adui muombee njaa
 
Last edited by a moderator:
Umezungumza lakini ujue nafasi ya makamu wa rais ipo kikatiba. kuibadilisha ni lazima uitishe bunge.

Clemence, hilo wanaweza kutafuta mtu mwenye influence kwa upande wa Zanzibar ili awe mgombea mwenza wa Lowassa. Na hilo litatoa nafasi kwa Prof. Lipumba kugombea ubunge Tabora ili aje kuwa waziri wa Fedha.
 
fuvu la paka

Kama lengo ni kuiondoa CCM nakubaliana na wewe. Lakini kama ni kuwatumikia wananchi kuna mambo mengi sana ya kuyachunguza kabla ya kufikia hapo.....kumbuka Lowasa ana marafiki akina Karamagi, Rostam, na mafisadi underdogs wengi mno ambao sidhani kama Ukawa wanaweza kukubali kuungana nao.....labda Lowasa atangaze kuachana nao kitu ambacho hana ubavu nacho.
 
Last edited by a moderator:
Kama tutaendelea kujidanganya kwamba UKAWA pekee yao watachukua hii nchi basi tutakuwa watu wajinga zaidi duniani..

No way, lazima mtu mwenye nguvu kutoka chama tawala ajiengue nao then ajiunge na wapinzani hapo ndipo kutakuwa na urais wa upinzani kushinda chama tawala. Tumeyaona hayo yakitokea kwenye nchi zetu nyingi tu za kiAfrika. UKAWA tukitaka kwenda Ikulu ni lazima tukubali kushirikiana na Lowassa.. Ni dhahiri EL ana mtaji wa watu wengi sana nyuma yake, kuli'ignore kundi kubwa hivo lililopo nyuma yake utakuwa ni ujinga wetu na kamwe tusitegemee kwenda Ikulu tena miaka ya karibuni..

Wale wanaobeza UKAWA kushirikiana na EL watakuwa ni wapumbavu wasiotakia upinzani mafanikio.. Narudia, kama viongozi wa UKAWA wanaweza kunegotiate na EL wafanye hivyo haraka..

Tena wasichelewe, asikudanganye mtu, nimegundua wananchi wengi hawaujui ufisadi wa LOWASA ni kama hadithi za kusadikika na kufikirika tu.
Huyu mtu ameivumilia sana CCM, na ana kitu kikubwa sana cha kuongeza kwenye upinzani.
 
Uzi wako una mantiki nzuri sana, sema UKAWA wanaanzaje kumsafisha kwa wananchi ili aeleweke vizuri?
Mkuu kusafisha Lowasa ni kazi ndogo tu ni hivi "NDG WANANCHI LOWASA SI FISADI ILA ALIBEBESHWA MZIGO WA DHAMBI WA CHAMA ILI CHAMA CCM KIENDELEE KUTAWALA,ILA UKWELI NDG WANANCHI SISI KAMA UKAWA TULIKUWA TUNAMCHAFUA NDG LOWASA ILI CCM WAMWACHIE AJE HUKU UPINZANI TUENDELEZE MAPAMBANO YA KUKING'OA HIKI CHAMA KONGWE,PIA NDG WANANCHI KUMBKENI SIASA NI MCHEZO WA KIHUNI HIVYO TULIMUHTAJI SANA LOWASA AONGOZE MAPAMBANO HAYA KWANI LOWASA NI MTU SAFI,SAHIHI,TUNAMPENDA NA TUNAMUAMINI ATATUPELEKA KTK MABADILIKO YANAYOTARAJIWA NA UKAWA" hili ndio dodoki pekee la UKAWA kwa lOWASA mkuu!!
 
mkuu kusafisha lowasa ni kazi ndogo tu ni hivi "ndg wananchi lowasa si fisadi ila alibebeshwa mzigo wa dhambi wa chama ili chama ccm kiendelee kutawala,ila ukweli ndg wananchi sisi kama ukawa tulikuwa tunamchafua ndg lowasa ili ccm wamwachie aje huku upinzani tuendeleze mapambano ya kuking'oa hiki chama kongwe,pia ndg wananchi kumbkeni siasa ni mchezo wa kihuni hivyo tulimuhtaji sana lowasa aongoze mapambano haya kwani lowasa ni mtu safi,sahihi,tunampenda na tunamuamini atatupeleka ktk mabadiliko yanayotarajiwa na ukawa" hili ndio dodoki pekee la ukawa kwa lowasa mkuu!!

mkuu, nitafute baadae upate kinana mbili...
 
Narudia tena. LOWASSA ni Asset na Ukawa ni Asset. Hivyo,Lowassa (Asset) + Ukawa (Asset) = USHINDI WA URAIS + WABUNGE + MADIWANI. Wenye uelewa wataona hilo.


👏👏👏👏 excellent perception...!!!

Nitashangaa sana Dr. Slaa agome kuungana na Lowassa ktk kuikomboa nchii hii.. nitamuona Dr. Slaa hajui siasa..na sio mtu kabisa...


Ukawa + Lowassa...NI USHINDI TU...

I bet, there is no way CCM can come close to win tht combination...!!!

Yaani USHINDI ni kabla hata ya October...


Ukawa + Lowassa ni UKOMBOZI WA WATANZANIA...

Lazima Dr. Slaa ageuze mawazo ya mgando sasa, awe kama MBOWE.. maana Mbowe is very very clever ktk mtaji wa kisiasa kama Lowassa, na ana spirit ya ushindi wa wazi....

I know, kwa sasa Mbowe au Prof. Lipumba hawana shida ya kuungana na Lowassa, tatizo ni Dr. Slaa...

Lazima Dr. Slaa akubali haraka, aone kama Kenya walivyofanya na UKAWA + Lowassa, CCM ni kifo...!!!

Yaani hakuna namna CCM itapona hapo...!!!

Yetu macho, CCM byebyeee....
 
Serena-Naomba ieleweke kwamba mpaka sasa majimbo ya CHADEMA hasa za maeneo wanakokaa wasukuma (Kanada ya Ziwa) kwa kiasi kikubwa yatarudi CCM kwasababu ya Magufuli kuwa msukuma. Asiyetaka kukubaliana na mimi asubiri October


Mimi sikubaliani na wewe juu ya Wasukuma ,Wasukuma wa sasa wanamwamuko mno kuliko kipindi cha nyuma wako tayari kuonekana wanamuunga mkono Magufuli kwa sasa na wakati wakapeni na wakajitokeza kwa wingi kurudisha kadi za vyama vya upinzani lakini siku ya kupiga kura wanapigia upinzani.

Kwa mfano matokeo ya Ubunge 2010 Ilemela na Nyamagana walishinda Chadema dhidi ya CCM iliyokuwa na Masha na Dialo wasukuma. Jimbo la Kwimba mhindi aliwashinda wazawa wa Kwimba kwenye mchakato wa CCM ktk kura za maoni.

Uchaguzi wa Serikali za mitaa 2014 hasa kwenye maeneo ya wakazi walio na mchanganyiko na kabila nyingine pia wazawa (wasukuma) waliopeperusha bendera ya ccm dhidi ya Chadema walishindwa vibaya.

Wanachotakiwa UKAWA wawe na ilani inayouzika kwa urahisi kwa makundi yote wakulima, wafugaji, wafanyakazi, wavuvi, Elimu, Afya na hasa ileeze nini watafanya kuwaondolea wananchi hali hii ngumu ya maisha. Kwa mfano mwaka huu wasukuma wanaolima pamba kama zao la biashara bei ni mbaya kuliko kipindi cha Mwinyi na Mkapa ambapo kipindi hicho pamba ilikuwa dhahabu yao.
Msimu huu bei ya pamba kwa kilo ni sh800 (ongezeko la sh 100 ya bei ya mwaka jana) na bei hii tangu msimu wa mwaka 2011 haijawahi kuvuka hapa.Kipindi cha Mkapa walikuwa hawanunui mbegu za pamba lakini kwa sasa mbegu wanauziwa.

Una hoja hasa kwenye sera na ilani lakini naomba usiwapumbaze CHADEMA na UKAWA kwa matokeo ya serikali za mitaa, kwani unajua influence ya Magufuli kwa kanda ya ziwa??? kama unafikiri utani, wewe subiri October 2015.
 
Sijawahi kuona ushauri wa hovyo kama huu wa kwako hapa.

Hakuna haja ya kuiondoa ccm madarakani ikiwa tutaweka wagombea wale wale mafisadi walioua nchi yetu. Ukiitoa ccm kwa kuwa imekuwa fisadi na mafisadi ndio hao hao kina Lowasa, halafu unampa uongozi wa nchi fisadi gumegume yule yule Lowasa, utakuwa ama una maradhi ya akili ama huna msingi wala sababu ya maana ya kutafuta mabadiliko. Utakuwa unatafuta mabadiliko kwa maslahi yako binafsi na si ya umma kitu ambacho UKawa hakikubaliki.

LAWASA AKIGOMBEA URAISI KWA CHAMA CHOCHOTE HATUMPIGII KURA SISI WATANZANIA HALISI TUNAOTAKA TANZANIA YETU ASILIA.

Hueleweki unapoongelea Lowasa awe mgombea wa UKAWA, huku references and standards zako zote ziko ccm!. Kwa kuwa ccm wote ni mafirauni na hakuna msafi, basi ukawa wasimamishe tu hilo fisadi nao? Wewe vipi lakini?

UKaWA inachukua nchi without haja ya mkono wa mafisadi!.

Hii kumtengenezea njia mwenye safari ya matamanio, imebuma, tafuta mlango mwingine. Labda jaribu kwa Zito au IPPT Maendeleo!, Ukawa kumejaa nahata hivyo access denied!.
 
Ndugu Wananchi,

Mimi kama mdau wa siasa na mzalendo kwa nchi yangu naomba nitoe ushauri ufuatao kwa UKAWA pamoja na Lowassa. Najua kuna watu inaweza ikawa ngumu sana kuelewa point yangu, lakini wenye ufahamu na mambo ya siasa na mapinduzi wataona point yangu.

Huu ushauri wangu umezingatia hali ya uchumi wa watanzania ambayo imeendelea kuwa maskini huku viongozi wakizidi kutajirika sana (mfano familia ya Rais wa sasa). Naelewa pia kuna watu watakuja hapa na fikra ya ufisadi wa ndugu Lowassa na kwamba hafai kupokelewa UKAWA. Hivi hawa ukiwauliza waweze kuthibitisha huo ufisadi wa Lowassa wanao majibu? Na je ni nani ndai ya CCM ambaye ni msafi?

Je huyu Magufuli ni msafi kiasi gani? Ni kwa vipi tumesahau juzi taarifa za CAG jinsi alivyolidanganya Bunge na upotevu wa billions zaidi ya 500? na je si ni huyu huyu Magufuli ndiye aliyehusika kwenye sakata la uuzaji wa nyumba za serikali? akimuuzia girlfriend wake na kaka yake ambao hawakuwa watumishi wa serikali kinyume cha utaratibu?

Nauliza tena, je ni nani MSAFI ndani ya CCM? Jibu ni HAKUNA MSAFI CCM. Na kwa wale wanaotegemea kuona mabadiliko yoyote hasa ya kiuchumi chini ya kiongozi yeyote ndani ya CCM hao wanajidanganya. Kwa CCM hata uwe msafi kiasi gani ukishaingia utakuwa unafanya matakwa ya CCM ya kulindana hasa ya kulinda wenye pesa na si kwa ajili ya wananchi.

Kwa hakika CCM haipo kwa ajili ya wananchi, kwani chini ya CCM tangu Uhuru, hakika hatujapata nafuu yoyote japo tuna rasilimali nyingi kama madini, maziwa , mafuta na gesi sasa. Naomba wananchi wenzangu mfungue macho na kuona jinsi muswada wa gesi na mafuta ulivyopitishwa juzi kwa hati ya dharura ili kulinda maslahi ya watu na si wananchi.

Ni wakat sasa wananchi wajue kwamba ADUI yao mkubwa ni CCM na mfumo wake na si watu, kwani watu hata wawe wazuri kiasi gani, lkn akishaingia ndani ya CCM, huyo mtu kwisha habari yake.

Baada ya huo utangulizi, sasa naomba niongelee kilichonisukuma mimi kuchukua muda kuandika thread hii. Awali ya yote naomba niseme kwamba mimi sina chama lakini ni mwenyeji wa Kanda ya Ziwa. Na kwasababu natoka eneo moja na Magufuli, wengi wangetarajia mimi pia niwe kati ya watu wanaofurahia uteuzi wake.

Naomba niseme kwamba, kwanza Magufuli ni mtendaji mzuri pamoja na kwamba ana udhaifu wake lakini kwa ccm yeye kidogo ana nafuu. Hatahivyo, pamoja na utendaji wake kuwa na unafuu, lakini HATALETA MABADILIKO yoyote, kwani akishaingia kwenye uongozi, yeye naye ataishia kufanya kama chama kinavyohitaji.

Na kwa msingi huo, mabadiliko ya maana katika nyanja zote yataletwa na chama mbadala na si ndani ya CCM.

Hivyo basi, Ombi langu kwa UKAWA ni kwamba wampokee Lowassa kupitia CHADEMA na Lowassa apewe nafasi ya kugombea Urais kupitia UKAWA. Naomba nirudie tena, Lowassa apewe nafasi ya kugombea URAIS. Hii ndio njia pekee ya kuitoa CCM na kuleta mfumo mpya utakaoleta mabadiliko hapa Tanzania.

UKAWA, kama kuna mtu mwenye value added kwenye mchakato wa kumtoa mkoloni mweusi madarakani ni Edward Lowassa, na wakati ndio huu na mkiacha tu hii nafasi, basi mtaendelea kuwa wapinzani miaka nenda rudi na mbaya zaidi hata wabunge watapunguakwa kasi sana mwaka huu. Hakuna mtu yeyote anayeweza leta thamani kwenye UKAWA na kuipa Ushindi toka CCM mbali na Lowassa pekee.

Faida ni kwamba CHADEMA tayari kina msingi nchi nzima na wafuasi wengi sana. Lowassa naye ana back up ya watu wengi sana na hata baadhi ya viongozi wa CCM katika ngazi zote watakuja naye. Naomba ieleweke kwamba Lowassa anapoingia CHADEMA atakuta mfumo ambao nao uko tayari, kwahiyo atafanya kazi ndani ya huo mfumo, na hivzo mambo ya CCM hatakuwa na impact kwenye mfumo atakaoukuta CHADEMA na UKAWA.

Na ukizingatia mfumo wa CHADEMA unavyojali wananchi, hivyo watanzania tutafaidika sana hasa kiuchumi. Lowassa akiwa mgombea Urais wa UKAWA atasaidia sana hata majimbo mengi ya ubunge kwa Wana UKAWA.

Mapendekezo yangu kwa wagombea wa UKAWA ni huu hapa:

1. Lowassa agombee urais kupitia CHADEMA.

2. Prof. Lipumba agombee Umakamu wa Urais.

3. Dr. Slaa akagombee ubunge ili aje awe waziri mkuu.

NB1: Naomba ieleweke kwamba mpaka sasa majimbo ya CHADEMA hasa za maeneo wanakokaa wasukuma (Kanada ya Ziwa) kwa kiasi kikubwa yatarudi CCM kwasababu ya Magufuli kuwa msukuma. Asiyetaka kukubaliana na mimi asubiri October. Na kura za urais vivyo hivyo. Na kwa msingi huo, ni lazima CHADEMA na UKAWA wawe na target ya kura za nyanda za juu kusini, kusini, kati na kaskazini. Na watu wa kusaidia UKAWA kukusanya kura za kutosha katika maeneo hayo ni Lowassa (Kaskazini, Kusini, kati, na nyanda za juu kusini) na Lipumba hasa kanda za magharibi na Kusini.

Najua kuna watu watakuja na hoja hapa ya Muungano kuhusu nafasi ya urais na makamu wake. Hapa UKAWA walenge kuondoa mfumo wa CCM na hivyo wanatakiwa watu wenye ngu (influencial people). Na kwa kuzingatia hilo, kwa CUF ukiondoa Lipumba anakuja Hamad amabye anagombea Zanzibar. Na kwasababu hiyo, wana-UKAWA wa Zanzibar wakubali tu wagombea wote watokee Bara, kwani matunda ya mfumo wa UKAWA utawafaidisha wananchi wote.

NB2: Lowassa atasaidia pia urais wa Seif Hamad kwa upande wa Zanzibar, kwani kuna wtu kule ambao hawajakubaliana na maamuzi ya CCM ya kuwaondoa akina Bilal. Na pia Lowassa na Karume ni kitu kimoja.

Naomba nimalizie kwa kusema kwamba hii ndio nafasi pekee ya CCM kuondolewa madarakani. Na njia pekee ni kupitia kwa Lowassa na UKAWA. Chadema na UKawa kubalini huu ushauri na hakika watanzania tuko nyuma yenu, kwani tunaamini kwamba uchumi wa Tanzania utabailika kwa mfumo ulio nje ya CCM na CHADEMA na UKAWA wanaweza kutumia nafasi hii sasa ya kumkubali Lowassa ili tupate mabadiliko.

UKAWA mnatakiwa kuwa makini, acheneni na propaganda za watu wengi hapa JF na mkubaliane na hali halisi. Wakati ndio huu na mkiuachia basi watanzania wasahau mabadiliko kwa kipindi kirefu sana.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki UKAWA.

Ahsanteni.
Ni mimi Mpenda nchi.


Hapana, nadhani ukweli tuusimamie, Lowasa sio mwadilifu! Basi hilo lituongoze na si vinginevyo
 
Lowasa ni CCM na katika wakoloni waliotuweka mpaka hapo tulipo. Lowasa alikuwa anatafuta madaraka ili aendelee kuimarisha himaya yake ya kutuibia Watanganyika kwa hiyo hatuwezi kuhamisha hiyo himaya yake na kuinganisha na wapambanaji wanaotaka kumwondoa huyo mkoloni mweusi. Tutakuwa tunajiangusha wenyewe. Jiulize kwa nini CCM wamemuondoa, ni kwa sababu ni mchafu. Wamemwondoa maana walijua wakimweka UWAKA watamponda na kuwaangusha kwa hiyo wametafuta kujisafisha japo bado ni wachafu. UKAWA wanazo siraha za kutosha hawahitaji mtu mchafu kuja kuwapigania. Kwa hiyo kama Watanzania wanahitaji mabadiliko waje bila Lowasa
Hizi ni hoja nyepesi. Mimi wala siop timu Lowassa kama unavyodhani. Mimi maisha yangu hayamtegemei mwanasiasa, kwani ninaweza kuishi popote duniani kwani Mungu amenibariki. Kinachoniuma ni mfumo kandamizi wa CCM hadi wananchi walio wengi hawapati mahitaji ya msingi kwa miaka nenda rudi. Sasa hali imekuwa mbaya zaidi hasa kiusalama (rejea vamizi kwenye vituo vya polisi hapa nchini).

Huo uchafu wa Lowassa unaouongelea ni upi ambao Magufuli au viongozi wengine wa CCM hawana? Aceni kudanganya watu ili mkoloni mweusi CCM aendelee kutunyonya. UKAWA wanatakiwa kuelewa kwamba ushindi ni strategies na ikipatikana opportunity unachukua na ukiacha ujue imekula kwako. Lowassa na opportunity kwa UKAWA na Watanzania wote kwa ajili ya kuondoa mfumo kandamizi wa CCM.
 
 excellent perception...!!!

Nitashangaa sana Dr. Slaa agome kuungana na Lowassa ktk kuikomboa nchii hii.. nitamuona Dr. Slaa hajui siasa..na sio mtu kabisa...


Ukawa + Lowassa...NI USHINDI TU...

I bet, there is no way CCM can come close to win tht combination...!!!

Yaani USHINDI ni kabla hata ya October...


Ukawa + Lowassa ni UKOMBOZI WA WATANZANIA...

Lazima Dr. Slaa ageuze mawazo ya mgando sasa, awe kama MBOWE.. maana Mbowe is very very clever ktk mtaji wa kisiasa kama Lowassa, na ana spirit ya ushindi wa wazi....

I know, kwa sasa Mbowe au Prof. Lipumba hawana shida ya kuungana na Lowassa, tatizo ni Dr. Slaa...

Lazima Dr. Slaa akubali haraka, aone kama Kenya walivyofanya na UKAWA + Lowassa, CCM ni kifo...!!!

Yaani hakuna namna CCM itapona hapo...!!!

Yetu macho, CCM byebyeee....

Good observation.
 
Tena wasichelewe, asikudanganye mtu, nimegundua wananchi wengi hawaujui ufisadi wa LOWASA ni kama hadithi za kusadikika na kufikirika tu.
Huyu mtu ameivumilia sana CCM, na ana kitu kikubwa sana cha kuongeza kwenye upinzani.

Na hata hao wapinzani wake (CCM) watakosa hoja ya kumwita fisadi maana walikula wote.. Watamwitaje EL fisadi wakati wao wote ni mafisadi. Hii ndio move pekee ya UKAWA kuweza either kuchukua nchi au kupata wabunge wengi ambao watatupa Waziri Mkuu na Spika wa Bunge..
 
Lowassa fisadi hajawahi kuwa upande wa wananchi,
 
Lowasa ni CCM na katika wakoloni waliotuweka mpaka hapo tulipo. Lowasa alikuwa anatafuta madaraka ili aendelee kuimarisha himaya yake ya kutuibia Watanganyika kwa hiyo hatuwezi kuhamisha hiyo himaya yake na kuinganisha na wapambanaji wanaotaka kumwondoa huyo mkoloni mweusi. Tutakuwa tunajiangusha wenyewe. Jiulize kwa nini CCM wamemuondoa, ni kwa sababu ni mchafu. Wamemwondoa maana walijua wakimweka UWAKA watamponda na kuwaangusha kwa hiyo wametafuta kujisafisha japo bado ni wachafu. UKAWA wanazo siraha za kutosha hawahitaji mtu mchafu kuja kuwapigania. Kwa hiyo kama Watanzania wanahitaji mabadiliko waje bila Lowasa

Watu wengine bwana!, hivi ni nani ambaye yuko ukawa na ana nguvu huko hakuwahi kuwa CCM? CCM ina mfumo wake na CHADEMA wana mfumo wao. Si Mbowe wala Dr. Slaa ambaye hakuwahi kuwa mwana-CCM huko nyuma. Wote wametokea huko, lkn mfumo uliopo CHADEMA na ile spirit ya Lowassa ya kufanya kazi ni muhimu sana. Halafu pia mmekalia uchafu uchafu wa Lowassa ni upi??? Hivi kuwa tajiri haupaswi kugombea uongozi wa nchi? Je ni nani wa kulaumiwa kama alikuwa halipi kodi kwenye biashara zake? si ni serikali hiyo ya CCM?
 
Lowasa ni CCM na katika wakoloni waliotuweka mpaka hapo tulipo. Lowasa alikuwa anatafuta madaraka ili aendelee kuimarisha himaya yake ya kutuibia Watanganyika kwa hiyo hatuwezi kuhamisha hiyo himaya yake na kuinganisha na wapambanaji wanaotaka kumwondoa huyo mkoloni mweusi. Tutakuwa tunajiangusha wenyewe. Jiulize kwa nini CCM wamemuondoa, ni kwa sababu ni mchafu. Wamemwondoa maana walijua wakimweka UWAKA watamponda na kuwaangusha kwa hiyo wametafuta kujisafisha japo bado ni wachafu. UKAWA wanazo siraha za kutosha hawahitaji mtu mchafu kuja kuwapigania. Kwa hiyo kama Watanzania wanahitaji mabadiliko waje bila Lowasa


Kombe la dunia 2010 Suarez alidaka mpira uliokuwa unaingia golini dakika ya mwisho kabisa ya mchezo.. Unajua nini kilifuata?? Alipewa kadi nyekundu, wapinzani wake wakapiga penalt na wakaikosa, then unajua nini kingine kilitokea?? Mwisho wa mechi akina Suarez wakaibuka kidedea.. Wakati mwingine lazima ukubaliane na facts na kucheza rafu ndogo ndogo ili tu mpate ushindi.. Mara nyingi kwenye mpira anayetafuta suluhu au ushindi kwa hali na mali inawalazimu mpaka kufanya mbinu chafu ili washinde, wanajidondosha kwenye 18 ili wapewe hata penalt..

Tuendelee kujidanganya kwamba ni rahisi kuishinda CCM bila rafu na mbinu yeyote ile.. Ila kumbuka, kinachoongoza nchi si mtu bali ni system na sera. Hata unayemwona msafi UKAWA akipelekwa CCM anaweza kugeuka mchafu kuliko, nani alitegemea ZZK atakuwa hivi alivyo?? Kama umekubaliana na scenario hiyo, basi pia hata yule mchafu CCM anaweza kuwa msafi akiingia UKAWA..
 
Back
Top Bottom