Labda tumetazama video tofauti maana kama ni ile uloiweka, Yahya Kassim anazungumzia kundi la Wazanzibar na wale wanaodai utengano, wasiotaka muungano huu kwa madai ya serikali 3. Ameileza hofu ya Wazanzibar na matakwa ya Wazaniabr ya kwamba wale wanaosema hakuna hofu sii wakweli na katoa mifano.....Sasa ikiwa wewe umeelewa tofauti, basi ipo kazi kubwa sii kwangu tu bali mijadala mingineyo yote utaitafsiri upendavyo.Mkuu Mkandara
Nimekuwekea video ili uache utaratibu wako wa kuwatisha Watanganyika ni wamoja ndani ya muungano, nje ya hapo wataanza Ukurya na Unyakyusa. Nimekuweke uone hali ya Zanzibar kama alivyosema Yahaya Kassimu. ''muungano ukivunjika na ninyi manrudi kwenu,pale mnapaita tu, Wallahi mtaondoka'' .
Je, huoni tatizo hapo? Ni akina nani wataondoka.
Pili, nimekuwekea usikilize wakikiri kuwa ndani ya muungano wanapata kila wanachodai.
Wewe unapata wapi ushujaa wa kusema wanaonewa ikiwa wao wenyewe wanasema hakuna uonevu.
Tatu, maelezo yako umekubaliana na Warioba. Usichokitaka ni jina Tanganyika.
Unaposema tumeweza kuendesha S2 bila matatizo unajidanganya.
Suala la muungano lina mtatizo na wewe ndiye muumini wa Tanganyika kuvaa koti.
Huwezi kuwa na JMT ndani yake Tanganyika ikafanya kazi. Haliwezekani,ndilo tatizo la miaka 50. Utatengaje shughuli za waziri au katibu mkuu katika kushughulikia Tanzania na Tanganyika.
Hesabu zinakataa, mantiki hairuhusu. Unagoma tu lakini unaelewa ukweli.
Muundo uliousema ndio waWarioba, kinachokutisha ni kuzinduka kwa Tanganyika. Unafahamu uwepo wa Tanganyika utaondoa loophole za kutumia herufi ZAN katika kuiba, kudoea. Hilo ndilo linakutesa, na umeshalisema hapa JF(Kumbu kumbu ipo). Unakumbuka kauli ya ''wazanzibar hawajui, wataumia sana Tanganyika ikirudi""
Kuhusu ulinzi na usalama, nimekuuliza makusudi ili kukuonyesha misaada na mikopo si muhimu kuliko wanachokipata. Hawana bajeti ya ulinzi na usalama ambayo kwa bilioni 400 ingechukua zaidi ya Bilioni 150. Ukiweka na wizara zingine wasiokuwa nazo, znz ingebaki bila bajeti ya kulipa mshahara wa sheha.
Leo yote hayaonekani kinachoonekana ni pesa kutoka Washington.
Nikupe mfano kwa hili, kuna mtu alikuwa anamuomba mwenyezi mungu amsaidie kupata kazi.
Amesali usiku kucha kwa miaka 2 bila kupata kazi.Kwa miaka 2 alikuwa na afya akitembea kutafuta kazi.
Baada ya miaka 2 akaacha kumuomba mungu kwasababu hajamsaidia katika maombi ya kupata kazi. Akasema hakuna haja ya kuendelea na swala au maombi yake.
Masikini ya mungu, kumbe huyu jamaa hakujua mungu alikuwa anasikiliza na kujibu swala na maombi yake. Kwa miaka 2 hakuugua hata siku moja. Kuna uwezekano angepata kazi na kuugua kipindi hicho na pesa zote za mshahara kuishia katika matibabu. Mungu alimsaidia kumwepusha na maradhi kwasababu maradhi ndilo tatizo lililomkabili, si kazi.
Mfano huo ni sawa na wazanzibar,wanaona kukopa washington ni fahari kama yule mtu aliyekuwa anatafuta kazi. Hawajui kuwa kutokuwa na bajati za ulinzi na usalama, mambo ya ndani, mambo ya nje, elimu na mzigo wa kubeba muungano ni mkubwa kuliko kupata pesa kutoka kwa Christine Lagard zenye riba. wapo mgongoni wakiendelea na safari na hawaoni, wanachotaka ni kutembea chini waonekane wanaweza.
Muda umefika, wapewe nafasi ya kukopa IMF na kupata misaada kutoka Uarabuni na Ulaya bila kikwazo. Wapewe mamlaka za kumiliki wizara zao, wapewe kila wanachokitaka.
Sisi tunaizindua Tanganyika, ni nafuu kuzuia pesa zetu kwenda znz kuliko kuwakataza kukopa.
Tanganyika ni muhimu kwa wakati huu kuliko wakati mwingine.
Hakuna wa kuizuia, wapo wa kuichelewesha. Tanganyika itazinduka katika meza ya majadiliano au kinyume chake wazanzibar watalipa gharama kubwa kuizindua.
Hakuna kurudi nyuma ni Tanganyika tu. Hilo litatokea iwe mwaka huu au kesho lakini lazima litokee na wznz waelewe hivyo.
Likitokea mezani ni nafuu kwao, wakisubiri tuwatake waizindue Tanganyika wataumia sana.
Hata swala la Mkataba kwa maana ya ndani ni kuwepo na mamlaka kamili baina ya serikali hizi ili kila serikali iweze kupanga na kuchagua maendeleo yao. CUF kama chama hata kikishinda uchaguzi wa Znz, ndani ya mfumo huu hawawezi kupewa mamlaka hayo ya kidemokrasia ili wao waendeshe shughuli za serikali ya Zanzibar, hivyo kwa kushindwa kupata suluhu kwa miaka yote ndio maana wametaka kuchukua mamlaka hayo kupitia marekebisho ya katiba yao ambayo inawapa mamlaka kama nchi. (NB: Katiba iliyopo haitambui ukweli kwamba Zanzibar ni nchi!) na kwa kufanya marekebisho hayo inaiwezesha Zanzibar wawe na mamlaka ya shughuli za serikali yao kama ilivyo Tanganyika ina mamlaka hayokwa miaka 50 ya Muungano. Wazanzibar wengi wameelewa na kukubali kupokea marekebisho hayo kimsingi.
Sasa kuitaka Tanganyika ambayo hadi sasa hivi ina mamlaka kamili ya kuendesha shughuli zake haileti maana zaidi ya Ukorofi, ni swala potofu la walozoea vya kunyonga tunashindwa vilivyochinjwa kihalali! kwa sababu Zanzibar imehitaji mamlaka ambayo hawana kama republic ndani ya muungano na sio fair kwa nchi kutokuwa na mamlaka ktk demokrasia ya kweli. Hivyo basi ni muhimu kutazama undani wa kuwapa mamlaka haya kutaathiri vipi muungano na hakuna njia isipokuwa kuweka mambo yote ndani ya Muungano (wizara zote) ila mamlaka ya kuendesha shughuli za serikali ndio yapewe hizo serikali zilizopo hadi chini kabisa na sio kila kitu kiwe chini ya serikali ya CCM. Bado huelewi!
Nakuomba muulize mtu yeyote anayeishi ktk nchi zenye Muungano, swala sii serikali ngani maana zipo nyingi, huu ni muundo tu unaotazama ukubwa wa nchi, watu, rasilimali, uwezo wa nchi na kukata ktk matabaka mengi ili kurahisisha ufanishi wa shughuli za maendeleo. Je nini haswa sababu za mamlaka kamili ya ki republic kutolewa kwa nchi (sub soveregn countries)? - sidhani kama unaweza kunambia kwa unagaubaga maana inaonyesha huna unachojua juu ya hili. Sidhani kama unaelewa a republic ndani ya muungano inatakiwa kuwa na mamlaka gani na kwa shughuli gani na mambo ya Utawala huwa chini ya nani..
Tunaposema serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (JMT), ina maana a National REPUBLIC of Tanzania ambayo kama nilivyokwisha sema toka Malecela, Sumaye, Lowassa na leo Pinda ni mawaziri wakuu ambao kwa uhalisia wametumikia serikali kwa maslahi ya Tanganyika kwa muda wote wakiwa madarakani kutokana na kuendelea kutumia mfumo usiouwiana na mabadiliko ya Kisiasa na Kuchumi. Lakini tunaliona kosa tu pale Zanzibar wanapotaka nao kuwa na kiongozi wa shughuli za serikali yao ambaye ana mamlaka kamili kama kwetu.
halafu swala la mikopo kwani Tanganyika inapokopa nje hailipi riba? kwani haiwfanyi makosa hayo hayo unayoyafikiria kwa Zanzibar maana unachowacheka ni sawa na Nyani asoona makalio yake mwenyewe. Ikiwa mambo yote yatakuwa ya Muungano, serikali kuu italazimika kupitia bunge la JMT kupitisha mikopo yote na kwa uhakika kila mmoja wetu atahusika, hii ni katika kuondoa Usiri wa CCM ambao wanautumia kwa maslahi yao au ya chama. Umeona wapi chama tawala kina miradi ya biashara kama sii mfumo mbaya wa Utawala halafu wewe unatazama UZanzibar na Utanganyika! Damn vipofu kweli hawaambiwi tazama, hupewa fimbo wakapapasa ardhi!...