Ukiacha Dar es Salaam, mikoa iliyobaki ujanja wao ni mchana tu, ikifika saa tatu usiku kila mtu yupo kwake

Ukiacha Dar es Salaam, mikoa iliyobaki ujanja wao ni mchana tu, ikifika saa tatu usiku kila mtu yupo kwake

Sio kweli ikishafika 8 kwenda 9 watu wanapungua kwa 50% hata movement zinapingua kwa karibu 60%
Kusema ziko sawa na mchana huo ni uwongo kwa halakati zangu kea wiki kazima nipite zaidi ya mara mbili usiku mnene
Jambo kubwa ni kuwa hapo saa 24 siku 7 za wiki hukosi daladala la kukufikisha au kukusaidia kukufikisha sehemu yoyote ya jiji la dar
Yaan hapo buguruni chama sheri ni kama lango KUU La DSM
Sasa kwa usiku kupungua 50% kuna tofauti gani?
 
Huwa napata tabu sana nikienda mkoani.

Kule ikifika saa 11 jioni wanapika chakula cha usiku.

Kama ni familia mtakuwa na masaa mawili ya stori baada ya hapo kila mtu anaenda kulaza ubavu wake.

Mkoani ni kitu cha kawaida kuona muuza duka anafunga biashara saa 1 jioni.

Saa 3 usiku kule ni usiku wa manane na ndio mida ambayo hata wezi wanakuwa na confidence ya kufanya uhalifu wao bila kusanukiwa.
 
Huwa napata tabu sana nikienda mkoani.

Kule ikifika saa 11 jioni wanapika chakula cha usiku.

Kama ni familia mtakuwa na masaa mawili ya stori baada ya hapo kila mtu anaenda kulaza ubavu wake.

Mkoani ni kitu cha kawaida kuona muuza duka anafunga biashara saa 1 jioni.

Saa 3 usiku kule ni usiku wa manane na ndio mida ambayo hata wezi wanakuwa na confidence ya kufanya uhalifu wao bila kusanukiwa.
Hiyo ni afya kubwa kwa watu wa mkoani au hujagundua kuwa karibia wote wakazi wa dar wana kauchizi, na waliowengi ni wezi, usimwamini mtu dar ata ndugu yako anakuibia halafu anageuza kuwa halali yake.
 
Mikoani mmepoa sana,kuna mikoa ikifika saa tatu huwezi kuona mtu nje,still wanaamka saa moja, mnakuwa mbafanya nini ndani muda wote.

Saa sita za usiku DSM kuna watu ndio wanajiandaa watoke
Saa saba usiku wauza chipsi bado wanamenya viazi.

Juzi kuna mtuhumiwa kampiga na kitako cha bastola mwenzake saa 12 asubuhi wakiwa kwenye club ya usiku.

Mnalala sana mikoani
Huu ni upuuzi na ushamba.
 
Sasa mtalalaje mapema na foleni yote ile mpaka saa nne za usiku mtu yupo kwenye daladala anaenda kwake, kazini katoka saa kumi jioni na akifika nyumbani mpaka amelala ni saa sita usiku halafu saa kumi asubuh tena yupo kwenye dalala anaenda kazini.
Ndiyo maana wakazi wa dar wengi wanalala kwenye madaladala kama unabisha kesho panda daladala saa kumi na moja asubuh then angalia asilimia ngapi ya abiria wapo macho kama sio wote wameuchapa.
Na walio ndani ya gari binafsi kama ni mke na mume, hawatazamani hata kuangaliana kuongea kila mtu yuko bize na simu au mmoja kalala, stressed life.
 
Ndo maana mnaongoz kulialia humu jukwaan kwa kugongewa madem zenu due hampati muda wa kupumzika na kula vyakula laini laini..mwsho wa siku kimoja Chali.....sie wa mikoani ni show show
Huu ni ukweli mchungu. Asilimia 90 wako kwenye ndoa ama.mahusiano kama picha tu.Kwenye foleni zao angalia tu ndani ya gari, kama si mmoja wao amelala basi anachati, au wameweka sura mbuzi, nuru ya uso haipo, uchovu mkubwa, kazini stressi, kurudi usiku wa manane, foleni kubwa, haridhishwi kitandani, mtu kwa siku analala masaa 2 tu, kula yenyewe wanakula fast food au junk foods, machipsi yai, wikend hakuna kupumzka, ni kwenda kujirusha kula mapombe na junk foods, matokeo kiriba tumbo na unene uliopindukia, matatizo ya afya mengi kama nguvu za kiume, presha sukari, hapo ndio mtu anaanza tena kubugia madawa kujaza sumu mwilini, hapo sijazungumzia pollution kama air and land polution za huko dar na noise pollution, ni mtu mmoja huyo anayapata haya yote halafu mnasema ni ujanja kwamba mji umechangamka kumbe watu ni nusu maiti zinazotembea.
 
Wapi? Tusidanganyane na kutiana moyo
😀 Mnafanya watu waliopo nje ya Dar na hawajakaa Dar wahisi ukiamka unakunywa chai Serena au Hyatt, wanazoziona katika movie. Kwako una furniture za ulaya, bafu kubwa lina jaccuzzi na sehemu ya steaming,ki shower amazing. Ukienda beach unakodi yatch, unakunywa beer saafi imported,sehemu nzuri

Kumbe UHALISIA bana asubuhi vitumbua au mihogo ya mia mia kwa mama Mwaju, chai ya rangi. Kuoga unatoka na kopo lako la sabuni maji katika ndoo, mavi unayamwagia maji system ya kuflash haipo au maji hayaendi katika system. Mtu anaweza hisi pisi kali unaimiliki kumbe ni mjasiriamwili unapiga,na wengine wanapiga ila una picha yake.


Huyu sio wewe, ila ndio 80% ya life hapa Dar.

Kuhusu night life ni kweli kuna tofauti, ila nimezurura mikoa kadhaa, naijua nightlife ya Mwanza,Arusha,Mbeya na sehemu kadhaa inategemea na mapendeleo yako na hadhi yako.

Hii mada ni aidha ya mtu ambae ni mdogo, au ana experience ndogo katika mambo ya starehe na kuzunguka nchi hii. Nimeenda mpaka vijijini iringa nakuta sehemu unakesha na watu wanakula monde, na ukitaka kuichapa unauliza wakulungwa😀
 
Kwamba kukesha ndio ujanja, hakuna mtu asiependa kutulizana usiku ila kwakuwa imebidi tu
Mtu anaamka saa 10 alfajiri analala saa 7 usiku sio kwa kupenda
Jamaa alietoa mada sio mtu wa night life bana, au alienda sehemu muda mfupi. Akataka kwenda kula bata jumatatu au jumanne usiku.

Hata Dar ukiona mtu anakesha mpaka asubuhi katika starehe, mara nyingi ni fala, mwizi au anatumia fedha za kupewa (baba,mama e.t.). Mjanja akienda club saa tano au sita saa 9 au kumi anasepa niamini, waliobaki ni aidha kuna issue maalum ni wachache wengi ni mafala, waomba bia,machawachawa,wezi, malaya(wabovu). wale smart,visu wanakuwa walishachukuliwa 😀

Mitandaoni watu wana mikwara sana, hawaulizi kujua. Inaweza isifikie Dar kwa sababu ya population na infrastructure ila kila sehemu ina night life yake. Night life issue kubwa ni ku refresh tu vinywaji,chakula n.k
 
Mikoani kuna Uzi sana...sana tatu unatafuta chakula kwa tochi!
Mkoa gani ulitafuta chakula kwa tochi? Au unaongelea aina ya chakula,ulikosa chips kavu? Kama ulikuwa Arusha ungeenda Granmelia ipo pale mkuu ina hadhi ya nyota tano kama Serena unapokunywa chai. Au kama ni masikini masikini ungeenda maeneo Shivers/Mrina ungepata nyama choma na mad* wa kununua.

Tabora ungeenda hata Tabora Belmonte ni nyota tatu haifikii Hyatt unapokula mchana ila ingefidia kidogo, wazungu weusi wenzako huwa wanalala pale pia, kama ni masikini masikini unataka wa kununu ukachakate ungeenda Oxygen Lounge/Club nadhani bado ipo nilipita muda kidogo.

Mwanza zipo sehemu kibao, Iringa zipo.....Mbeya pia nimeshacheki night life yao.

Issue ni hela hamna, au nyie ni madogo na night life mnaigiza mnataka mkute watu weengiii muanze ukenge ukenge 😀 sababu mmeshazoea kufuata mikumbo ya msafara wa mamba.

Halafu watu wa hivi na mitazamo hii hata hapa Dar ndio nyie tunawakimbia club kubwa tunaenda katika vi bar vya nje sababu brother brother nyiiingiii ni bia ya saba zote za mizinga,na kusimulia historia za zamani, ulegend wa kibwege oooh hapa Kino mi legend, babu yangu sijui hivi, wakati watu wanataka kula life kwa kidogo kilichopatikana.

Ukiwasha sigara, haujafika hata katikati anaitaka, unampa nzima anaiweka mfukoni anasubiri unayovuta. Mwishowe unambwatukia dogo kuwa na adabu, kwanza nani kakuita hapa....umeshapata bia na sigara. Ondoka

NB SIO LAZIMA UWE WEWE NDIO WATU KIBAO WALIVYO
 
Hapa mjini kuna watu wachache wana ishi na kuna watu wengi wana survive binafsi ningekuwa na survive ningeenda kulima mpunga ndani ndani huko mlimba kuliko kulala saa sita na kuamka saa kumi kwenda kuteseka kila siku joto wewe, foleni wewe, mafuriko ww, wizi ww kwanini usiende kijijini😁
 
Mikoani mmepoa sana,kuna mikoa ikifika saa tatu huwezi kuona mtu nje,still wanaamka saa moja, mnakuwa mbafanya nini ndani muda wote.

Saa sita za usiku DSM kuna watu ndio wanajiandaa watoke
Saa saba usiku wauza chipsi bado wanamenya viazi.

Juzi kuna mtuhumiwa kampiga na kitako cha bastola mwenzake saa 12 asubuhi wakiwa kwenye club ya usiku.

Mnalala sana mikoani
Kama una ela Dar mchana ni muda wa kulala.
 
Sema moderator kaedit cha habari kilikuwa kinasema "ntu" Sasa mtu unauza chips maana yake hela mnaisaka kwa tochi sisi huku samoja tushafunga hesabu😂trilion moja kwa siku
Naunga mkono hoja. Saa7 una menya chips manake watu wa huko wanashida sana. Muda wa kulala na familia wee Bado unafanya kazi. Mchana unatosha kabisa kuingiza Hela.
 
Wanawake asilimia kubwa wanaojiona asilimia wazuri Tanzania nzima wanakimbilia Dar.

Wa levels zote za maisha.
Sio leo mkuu. Hayo maisha ni yablong time way back.
Leo hii pisi kali zimejaa kila kona upcountry side.
Malaya ndio wnakimbilia Dar, wasio na kazi za kufanya na wasio jua kuwa Dar haiangalii sura kama huna mchongo utachapika sana na utatepeta kinoma noma
 
Back
Top Bottom