Ukienda mikoa hii kwa nenda kufanya kilichokupeleka, hawapendi watu wanaopenyeza mambo ya uchawa kupitiliza, Case study ni Zuchu

Ukienda mikoa hii kwa nenda kufanya kilichokupeleka, hawapendi watu wanaopenyeza mambo ya uchawa kupitiliza, Case study ni Zuchu

Nadhani wote mmesikia kilichomtokea Zuchu huko Mbeya, Sio kosa lake, Hakujua kwamba yupo eneo tofauti kabisa, Alikuwa akipigia sana debe viongozi bila kujua kufanya hivyo ni kuamsha hisia kali wasizozipenda wanambeya wasiopenda mambo ya kutukuza sana viongozi (Uchawa)

Na kama unaingiza mambo ya uchawa basi jua kubalance, usizidishe.

1. Kilimanjaro - Pamoja na mazingira magumu ya kuwa upande wa upinzani, Vyam vilivyoweza kuleta upinzani mkubwa nchini huwa vina viongozi wa mkoa huo kuanzia TLP, NCCR, CHADEMA, n.k. ni watu ambao wamefikia levels za juu zaidi kwenye mambo ya upinzani.

2. Mbeya - Huku watu wanapenda sana haki ndio maana hii Nchi unapozungumzia watetezi wengi wanatokea huko, Kina Nay wa Mitego kakulia huku, Mwabukusi, Mawakili wa vyama pinzani, n.k. Kwa mwaka huu pekee kuna kijana kakamatwa huko kwa kosa la kuchoma picha, kuna mchungaji kafungwa kwa kumkosoa Rais, n.k. Unavyopanda stejini fanya kilichokuleta maana mzunguko wa pesa ni mdogo viingilio vinatafutwa kwa taabu.

3. Mara - Nje ya kuwa maarufu kwa kumtoa Nyerere kiongozi alielitanguliza taifa bila kujipendelea mkoa wake pamoja na kuacha alama ya mkoa uliojitolea zaidi kwenda kuipigania nchi Kagera, Ni watu wenye misimamo yao hawapendi mambo ya uchawa uliopitiliza.
Na mara upande wa wakurya tu tarime ila musoma, serengeti butiama na musoma vijjn hapo ndio homes of chawaz.
 
Sugu nlikuwa naye sangu,alinizidi darasa kdg na wakina mponjoli mwalakasuka
Watu wa mbeya wastaarabu ila ujingjing hawataki

Ova
Mwaka Gani hiyo Sangu mkuu,ulimkuta Mwakyulu?!Isote?,Bukuku?umenikumbusha mbali sana!
 
Back
Top Bottom