Ukiishi kwa ndugu, rafiki, jirani zingatia haya

Ukiishi kwa ndugu, rafiki, jirani zingatia haya

Kinachouzi umefanya uchunguzi umegundua mke ndio mpumbavu unakubaliana na hali

Unamwambia " Aisee dogo fanya tu mwisho wa mwezi huu nenda home shemeji yako hakutaki "


Halafu ni mdogo wako wa mwisho huyo tumbo moja kamaliza chuo kasema ngoja niondoke kijijini niende kwa Braza niangalie channel zinaendaje na mimi nitoke
😂 kama masikhara hivi jibu jepesi ambalo linamuachia dogo maumivu mazito. Hapo juu kuna member anakwambia halafu baada ya bro kufariki unakuta shemeji anaanza kulalamika mnamtenga.
 
[emoji23] kama masikhara hivi jibu jepesi ambalo linamuachia dogo maumivu mazito. Hapo juu kuna member anakwambia halafu baada ya bro kufariki unakuta shemeji anaanza kulalamika mnamtenga.
[emoji1][emoji1] mambo wanatengeneza wao halafu wanakuja kulalamika wanatengwa
 
Jitahidi kwenda sawa na mama mjengo,unaamka asubuhi unasaidia kazi ndogondogo ndo unaanza shughuli zako za kuingia zoom,siyo unaamka tu hujasafisha hata choo unaingia zoom, utsfurushwa mapema,unafgia uwanja unatoatoa majani,kama maji ni ya kuchota basi unachota,unasafisha bafu,wafanye watoto wakupendw kwa kuwasaidia homework,unawahimiza shule,unawafundisha fundisha,jitahidi kila unapoamka unafanya jukumu walau moja la kifamilia kama miongoni mwa niliyoyataja ndo uanze harakati zako,na ukitaka hela za nauli ongea na mama mjengo kwanza,hapo hata ukisema unataka kuhama watakuzuia,
 
Usiwe mtu wa kushinda nyumbani masaa 24 huku ukitazama tamthilia katika runinga.

Hakikisha unawahi kutoka asubuhi na kurudi jioni ratiba yako ya chakula iwe dinner tu, lunch na breakfast kapambanie huko mtaani.

Pia katika hustle zako kwa chochote unachopata kumbuka kubeba hata kilo tano za mchele, matunda hata nyama kilo tatu peleka home.

Na hakika hutochokwa na mambo yatajipa tu.
Mkuu hapa anazungumziwa mgeni ambaye ameenda kuangalia life linaendaje eneo hilo sio mgeni ambaye ameenda mapumziko ya kikazi 😂.

Mchele kilo tano na nyama kilo tatu kama ndio zinapima "ustaarabu" wa mgeni mbona kama ni kumbebesha mzigo hustler. Upo sahihi lakini kwa kiasi kikubwa ingawa pia baadhi ya familia kushiriki chakula ni muhimu sana. Mfano mama angu ni lazima ushiriki mezani la sivyo uwe na sababu maalum.
 
Kinachouzi umefanya uchunguzi umegundua mke ndio mpumbavu unakubaliana na hali

Unamwambia " Aisee dogo fanya tu mwisho wa mwezi huu nenda home shemeji yako hakutaki "


Halafu ni mdogo wako wa mwisho huyo tumbo moja kamaliza chuo kasema ngoja niondoke kijijini niende kwa Braza niangalie channel zinaendaje na mimi nitoke
Hili ni kosa. Ndo hapo nnaposema mwanaume unahitaji hekima kudeal na mambo ya nyumbani kwako. Kama umeona kosa lazma uchunguze shida iko wapi na udeal nayo kiume. Kama n mke wako, deal nae maana hajakupanda kichwani, vivyo hivuo kwa mdogo wako.
Muhimu hakuna anaepata free pass ya kufanya anavotaka
 
Bangida mkuu angalia kama hii issue ya ndugu yake sister hapa, unaona wazi kabisa mgeni kaanza kutaftiwa sababu siku ya kwanza, unaweza tabiri huko mbeleni ni nini kitatokea.

Mwanaume inatakiwa uwe neutral. Sasa kama ulishamuonyesha mwanamke kama huyo umempa thamani zaidi kuliko ndugu utajikuta unachezea za uso.

NB: utanisamehe Joannah kwa kumtumia sis wako kama mfano mbaya.
Hapa nakuelewa. I think watu wengi hawajaelewA msimamo wangu. Simaanishi kwamba mke afanye anachotaka kwenye mji, hapana! Issue yangu ni kwamba, ndani kuna utaratibu na huo utaratibu utatakiwa ufuatwe. Na pia haimaanishi mke anapokosea asionywe, la hasha hata yeye rungu linamkuta.
What im saying ni kua, nyumba haitakiwi kuendeshwa kwa madharau from pande zote. Ukiona wawili wanshindwana ni jukumu lako kama mwanume kufanya ucchunguzi na kudeal logically na tatizo lililopo. Kama ni mke, akutane na vyake, kama ni ndugu na yeye pia.
Ninachiendelea kukataa ni madharau.!
Na pia ndugu, kama umeamua kuoa lazma umemchunguza mwenza wako na mapungufu yake unayajua, na kama umekubali kuendana nayo sidhani kama unashindwa kudeal nayo
 
Bangida mkuu angalia kama hii issue ya ndugu yake sister hapa, unaona wazi kabisa mgeni kaanza kutaftiwa sababu siku ya kwanza, unaweza tabiri huko mbeleni ni nini kitatokea.

Mwanaume inatakiwa uwe neutral. Sasa kama ulishamuonyesha mwanamke kama huyo umempa thamani zaidi kuliko ndugu utajikuta unachezea za uso.

NB: utanisamehe Joannah kwa kumtumia sis wako kama mfano mbaya.
Hapana usijali, mimi mwenyewe sikupendezwa na vitendo alivyonisimulia Mimi nimemsaidia kuona aibu.ni tabia mbaya kwa kweli Mambo madogo yanaanzaga hivihivi mwishowe bifu kali
 
Hapa nakuelewa. I think watu wengi hawajaelewA msimamo wangu. Simaanishi kwamba mke afanye anachotaka kwenye mji, hapana! Issue yangu ni kwamba, ndani kuna utaratibu na huo utaratibu utatakiwa ufuatwe. Na pia haimaanishi mke anapokosea asionywe, la hasha hata yeye rungu linamkuta.
What im saying ni kua, nyumba haitakiwi kuendeshwa kwa madharau from pande zote. Ukiona wawili wanshindwana ni jukumu lako kama mwanume kufanya ucchunguzi na kudeal logically na tatizo lililopo. Kama ni mke, akutane na vyake, kama ni ndugu na yeye pia.
Ninachiendelea kukataa ni madharau.!
Na pia ndugu, kama umeamua kuoa lazma umemchunguza mwenza wako na mapungufu yake unayajua, na kama umekubali kuendana nayo sidhani kama unashindwa kudeal nayo
Hapa tumeelewana chief na hiyo ndio concern yangu usiwepo upande ambao umejihesabia haki. Mpaka/utaratibu ni muhimu kwenye hii case, Mme asimame kama mme na kiongozi wa familia, Mke asimame kama mke na mtekelezaji wa miongozo toka kwa mme hivyo hivyo mgeni asimame kama mgeni na afuate taratibu za wenyeji.
 
Tatizo la Wanawake wanapoolewa wanahisi kuwa wao ndio wamemzaa huyo mume na siku mume akifariki wanataka na hao ndugu wa mume kusaidiwa malezi ya watoto. Hakika watoto wa mitaani hawatoisha katika jamii kwani matendo ya Wanawake husababisha visasi baadae.
Yeye kwa madai yake ndugu za mumewe pale hawamthamini wanamchukulia Kama Kaka Yao ndio kila kitu na yeye Ni nothing,Sasa anadai atapambana nao bega kwa bega wapunguze Uhuru,eti Uhuru umezidi..huyo mgeni eti alivyofika siku mbili tatu akaenda kwenye shoe rank akaanza kuchafua viatu vya braza akajichagulie,,,Sasa bibie kamaind
 
Hapana usijali, mimi mwenyewe sikupendezwa na vitendo alivyonisimulia Mimi nimemsaidia kuona aibu.ni tabia mbaya kwa kweli Mambo madogo yanaanzaga hivihivi mwishowe bifu kali
Hakika tuko pamoja na uendelee kumrekebisha anavyokosea na kumpongeza anavyopatia.
 
Yeye kwa madai yake ndugu za mumewe pale hawamthamini wanamchukulia Kama Kaka Yao ndio kila kitu na yeye Ni nothing,Sasa anadai atapambana nao bega kwa bega wapunguze Uhuru,eti Uhuru umezidi..huyo mgeni eti alivyofika siku mbili tatu akaenda kwenye shoe rank akaanza kuchafua viatu vya braza akajichagulie,,,Sasa bibie kamaind
Daah kweli hatari sasa dogo anachukua viatu vya Braza na Braza wala hana noma ha mind wala nini sasa shida iko wapi hapo

. viatu ni vitu vidogo sana na si vya kwake huyo ni mchoyo
 
Hapa tumeelewana chief na hiyo ndio concern yangu usiwepo upande ambao umejihesabia haki. Mpaka/utaratibu ni muhimu kwenye hii case, Mme asimame kama mme na kiongozi wa familia, Mke asimame kama mke na mtekelezaji wa miongozo toka kwa mme hivyo hivyo mgeni asimame kama mgeni na afuate taratibu za wenyeji.
Naam naam naaam. Hii ndo sawa.
Familia lazma ikae iweke muongozo kwenye kila kitu. Hapo mdo kutakua na amani na maendeleo. Na kila upande ukisimamia eneo lake kutakua hakuna muingiliano wa majukumu na amani itatawala.
 
Mambo ya kusemana vyakula ni umaskini tu, usukumani kwetu njoo utakunywa maziwa yakutosha utakula nyama zakutosha utakula wali wa kutosha alaf hakuna anae jali. Ukiwa unaondoka unapimiwa na debe kadhaa za mpunga. Ujanja ujanja ndio kitu pekee hatutaki baki nao huko huko kwenu
 
Haya yote mnayasema tu! Matoto ya siku hizi ni kama majinga fulani hivi! Hayawezi kujituma tena yanataka yaishi kama yalivyokuwa yanaishi kijijini! Hizo ni ng'ombe zikae huko huko kijijini!
Mkuu kwa hii comment utakua na roho mbaya sana, mchoyo na mkatili.
 
Toka niko Advance niliapa sitokuja kuishi kwa jamaa/ndugu mara zote nikiwa safarini ninafikia hotel hata kama nipo mkoa wenye ndugu ninaenda kuwasalimu tu na kuondoka.

Maana familia nyingi za kibongo hazina utaratibu mzuri mgeni na heshima zako watakulalisha na watoto vikojozi, utasimangwa kwenye chakula n.k
Hapa mada inaongelea kama mtu anatafuta maisha na hana njia nyingine zaidi ya kuishi au kufikia kwa ndugu. Unafikiri kuna anaependa kukaa kwa ndugu?
 
Kuishi kwa ndugu, mambo ya kufanya
1. Siku zote amka mapema na ufanye shughuli za kimsaada kwenye mji huo, kwa mfano kufagia, kusafisha mabanda ya kuku n.k. wjatever it is, lakini asubuh na mapema ikukute nje.
2. Jitahidi kutoka nje na kuzunguka kitaa ukitafta mishe ndogo ndogo za kukupa vijisenti ili usipauke kisoro
3. Usiwe na mazoea yaliyopitiliza hasahasa Kwa shemeji au wifi yako. Kaa kwa step wacha kiherehere
4. Ukipata chochote huko duniani, kamwe usirudi mikono mitupu, hata ndizi za buku zinaeza sindikiza wali maharagwe hapo ndani. Always provide some input kuwapunguzia mzigo.
5. Kuwa msafi, kuwa msafi kuwa msafi!
6. Fuata sheria zao, kwa mfano kuwahi kurudi, kusali n.k. kama una sheria zako kazipeleke kwenu, hapo ni kwa watu, wacha kisebengo cha kupanga masharti.
7. Hakikisha wale watoto kina "junia" hawakuzoei, wale wana mambo ya kiwaki unaweza mkata kelebu akatema meno. Jiepushe nao
8. Beki 3 ana mbolea iliopitiliza, ukipanda mbegu nakuapia lazma izae matunda. Mkwepe!
9. Kuwa mstaarabu
Hapo kwa kina Junior ndio penyewe na pagumu sana. Junia anaweza kukulamba kofi bila sababu halafu unajikuta unapaniki na kumpa 👊 ya kichwa!
 
Mambo ya kusemana vyakula ni umaskini tu, usukumani kwetu njoo utakunywa maziwa yakutosha utakula nyama zakutosha utakula wali wa kutosha alaf hakuna anae jali. Ukiwa unaondoka unapimiwa na debe kadhaa za mpunga. Ujanja ujanja ndio kitu pekee hatutaki baki nao huko huko kwenu
Ukiona watu wengi wanalalamikia wageni ujuwe wapo maeneo ambayo hayazalishi vyakula. Ni ngumu kusikia mtu wa Mwanza,Mbeya,Moro au Iringa analalamika.

Kwa Dar ni sahihi kabisa maana hao bei ya mlo mmoja kwa familia ya watu 4-6 inaweza kuwa ya siku 1 au 2 kwa Mbeya,Iringa au Mwanza.
 
Kuwa mwema - jua mipaka yako, wajibika, watendee kwa haki.

Usitake sana kutendewa haki, siyo kwenu hapo na upo kwa muda tu.

Jitambue.
 
Ni kujiongeza tu kwa kile kinachowezekana hata kama kujiongeza kwako hakutaonekana we jitahidi tu.
 
Back
Top Bottom