Ukisikia kujilipua ndo huku. Ml 60 hisa za CRDB bank, liwalo na liwe!

Ukisikia kujilipua ndo huku. Ml 60 hisa za CRDB bank, liwalo na liwe!

Wakuu, Maisha bila kujilipua hayaendi. Kifupi kama unanifuatilia nilijichanga UTT AMIS na kuweza kupata kiasi cha 60ml sasa nimetoa hiyo hela yote na kununua hisa za CRDB. Kifupi, liwalo na liwe nikipata sawa na nikikosa sawa. Mungu jaalia. Nitaleta mrejesho baada ya Mwaka kupitia.
Mkuu Huko Sio Kujilipua.Ila nakutakia kila la heri.Portifolio yako ya Investment Ikoje?
 
Sio kweli kwani nao UTT wanawekeza kwenye hisa na sehemu zingine thus wanapata gawio
Bank kwa sasa zinaface challenges zifuatazo
1.SACCOS zimekuwa nyingi
2.Kausha damu
3.Wakala wa Pesa za simu
4.Wakala wa mifumo mingine ya Pesa mfano NALA
HAYA MAMBO YA HISA KWA KAMPUNI ZA HAPA BONGO SIO YA KUHISI ULAJI KAMA KWA WENZETU AMBAO WAPO WAZI KWENYE FINANCIAL STATEMENTS ZAO
UTT AMIS ina maana kuliko hizo shares za CRDB
 
Sio kweli kwani nao UTT wanawekeza kwenye hisa na sehemu zingine thus wanapata gawio
Wao wana wataalamu wa kuweza kujua wawekeze mahali gani baada ya kufanya uchambuzi wa kina. Na hawaweki mayai yote sehemu moja..
 
Wao wana wataalamu wa kuweza kujua wawekeze mahali gani baada ya kufanya uchambuzi wa kina. Na hawaweki mayai yote sehemu moja..
Wameweka NMB na CRDB only we angalia ikishuka moja wapo ya hizo utashangaa. Stability yao inatokana na faida ya hatifungani. Hisa ndo zinaboost zaidi. Umoja 50 hisa 50 hatifungani, Wekeza Maisha 50 hisa 50 hatifungani na fixed,watoto etc. Bond na liquid ni fixed income option only hakuna jipya
 
Sio kweli kwani nao UTT wanawekeza kwenye hisa na sehemu zingine thus wanapata gawio
Sio kila hela UTT wanawekeza kwenye hisa. Fedha zinazokusanyw akwenye Mfuko wa Bond na liquid wanawekeza kwenye Bond za serikali na bank peke yake ndiposa ukiwekeza kwenye mifuko hii No risk ipo mifuko wanayowekeza kwenye hisa pia ,, UTT sio sawa na wewe kwasababu Wana mtaji mkubwa na wanaweza kuhimili KUWEKEZA kwa muda mrefu mpaka wapate faida
 
Yes for general bank profit, but not in terms of dividend for share holders, better to invest your money UTT mara mia..!! Huyu mwache atarudi kauza shares azipeleke UTT tena, hajafanya study vema, ndio maana kaandika kujilipua, mtu wa kujilipua ni mtu wa ku bet, yaani sio msomi au hajui soko la fedha vema, kazi yake ni ku bet bet tu..!!
Yani katoa hela ambapo ana uhakika wa kupata 12% halafu kapeleka wanakompa 3% 🤣
 
Vigezo vya kuiva kwake kwa miaka mingapi umesoma? Ukute Ni miaka 20
Sasa miaka 20 kuna tatizo gani kama unapewa hio 15.49%? Unajua hio hela ni bei gani kwenye 60M?

Kwa hesabu ni kama 9.3M risk free kila mwaka. Hio hela ukiipata hujalipa ada za wanao na kupunguza makali ya maisha? After 20 years unapewa hela yako ikiwa intact.

Kumbuka still bado una kazi ambayo ilikuwezesha kupata hizo 60M.
 
Back
Top Bottom