Ukitaka kuishi vizuri Dar es Salaam ishi Kigamboni

Ukitaka kuishi vizuri Dar es Salaam ishi Kigamboni

Viwanja vinauzwa KIGAMBONI mwembe mdogo karibia na chuo cha afya kigamboni college

1. Umbali kutoka ferry mpk site ni killometer 23

2. Viwanja vimepimwa ila vipo katika michakato ya hati kwahy ukinunua unapata kwa jina lako rasmi

3. Umeme umefika tayar kumetulia hali ya hewa ni safi sana

Meter 8* 22 mil 1.5

Meter 15*20mil 2.5

Meter 35*35 mil 5

Kuhusu punguzo ondoa shaka kila kitu ni maelewano.
IMG_4794.jpg
 
Sehemu yoyote ambayo gharama za nyumba ya kupanga ni ndogo kuna kitu kinasababisha. Kuna rafiki yangu pale DIT alipanga kule ili akae ghetto kali na hapendi kelele za mtaani ila kero za usafiri zilimfanya ahame baada ya miezi mitatu.

Ukitaka kukaa sehemu ambayo una projects za online au working from home hiyo Kigamboni ni sawa. Na usiwe mpenda bata za usiku wakati huna usafiri binafsi. Ile ni sehemu ya kujichimbia
 
Kuna maeneo K'mboni kuna wezi hatari, watu wanavamiwa ndani na kupigwa mapanga...
 
Kigamboni nizuri sana ila maji chumvi sijawahi ona, unababuka sana ,waweke maji dawasa nahakikisha hakuna atakayeshindwa kaa kigamboni
 
Kigamboni (sasa ni wilaya) ni sehemu ya jiji la Dar es Salaam ambayo tofauti na maeneo mengine ilichelewa kuendelezwa kimiundombinu mpaka kufika miaka ya 90 .Watu walichelea kuishi huko kutokana na kupaona ni maporini palipostahili kuishi wanyama.

Hivi leo,mambo ni tofauti sana,mji unakua kwa kasi ya ajabu, barabara zinajengwa kutangulia makazi ya watu,ni sehemu pekee katika jiji la Dar es Salaam ambako ukiingia unasahau kuhusu foleni za barabarani , hali ya hewa ni nzuri kutokana kutokuwepo kwa ujenzi holela wa nyumba, ni karibu sana na city centre na kuna fursa nyingi za kuanzisha biashara.

Binafsi nilifika kwa mara ya kwanza na kuhamia kigamboni mwaka 2015 kutoka Survey maeneo ya karibu na Mlimani city nilipoishi kwa takribani miaka minne,ila mpaka kufikia leo sijawahi kujutia kuishi huku wala kuwaza kuhamia mahali pengine katika mji huu kutokana na sifa nilizozitaja hapo juu na kwa bahati nzuri Mungu amenijaalia kujenga kakibanda huku huku.

Kwa ambao hawajawahi kufika huku hudhani kwamba Kigamboni ni kisiwa na kwamba usafiri pekee wa kufika huku ni wa kuvuka maji kwa pantoni, la hasha! Kigamboni si kisiwa bali imetenganishwa na sehemu nyingine ya jiji kwa sehemu ya bahari iliyoingia nchi kavu (ghuba) ambayo ni bandari ya Dar es Salaam na Kwa sasa ukiachilia usafiri wa wa pantoni kuna daraja na baraba mbili ambazo unaweza kupita bila hata kuiona hiyo bahari.

Karibuni sana Kigamboni.
Uzuri wa Kigamboni ni kuwa hata kama unafanya kazi mjini, foleni unapishana nayo kwa kushangaa upande wenye foleni.
 
Kuna watu wana-comment humu bila kuwa na details..
1: Kigamboni maji ya dawasa yapo
2: maeneo yenye wezi ni yapi hayo?
Kigamboni ni sehemu nzuri sana..nilihamia kutoka mbezi ya Kimara 2014..mpaka leo sijafika uko
 
Kigamboni (sasa ni wilaya) ni sehemu ya jiji la Dar es Salaam ambayo tofauti na maeneo mengine ilichelewa kuendelezwa kimiundombinu mpaka kufika miaka ya 90 .Watu walichelea kuishi huko kutokana na kupaona ni maporini palipostahili kuishi wanyama.

Hivi leo,mambo ni tofauti sana,mji unakua kwa kasi ya ajabu, barabara zinajengwa kutangulia makazi ya watu,ni sehemu pekee katika jiji la Dar es Salaam ambako ukiingia unasahau kuhusu foleni za barabarani , hali ya hewa ni nzuri kutokana kutokuwepo kwa ujenzi holela wa nyumba, ni karibu sana na city centre na kuna fursa nyingi za kuanzisha biashara.

Binafsi nilifika kwa mara ya kwanza na kuhamia kigamboni mwaka 2015 kutoka Survey maeneo ya karibu na Mlimani city nilipoishi kwa takribani miaka minne,ila mpaka kufikia leo sijawahi kujutia kuishi huku wala kuwaza kuhamia mahali pengine katika mji huu kutokana na sifa nilizozitaja hapo juu na kwa bahati nzuri Mungu amenijaalia kujenga kakibanda huku huku.

Kwa ambao hawajawahi kufika huku hudhani kwamba Kigamboni ni kisiwa na kwamba usafiri pekee wa kufika huku ni wa kuvuka maji kwa pantoni, la hasha! Kigamboni si kisiwa bali imetenganishwa na sehemu nyingine ya jiji kwa sehemu ya bahari iliyoingia nchi kavu (ghuba) ambayo ni bandari ya Dar es Salaam na Kwa sasa ukiachilia usafiri wa wa pantoni kuna daraja na baraba mbili ambazo unaweza kupita bila hata kuiona hiyo bahari.

Karibuni sana Kigamboni.
100%
 
Sijawahi penda kuishi Kigamboni
Na suala la kuvuka maji daily ndo kabisaa

pamoja na daraja bado i dont prefer hata kuwa na kiwanja cha kuzugia
 
Hiyo ilikua zamani sio sasa,gari zinakwenda kibada ,kongowe saivi nyingi tu ,mpaka za kariakoo kupitia darajani
Hapana sio kweli,mie juzi nilikuwa uko maeneo ya mji mwema,kufika saa tatu hakuna gari hata moja,ni vibajaji tu
 
Hewa inazidi hii ya huku kwangu? Maana mi nakaa jirani na msitu wa pande,hadi feni nilishazing'oa nikauza coz hazina kazi. Pametulia huwezi sikia hata bodaboda zaidi ya milio ya ndege na batamzinga wangu
 
hapana mku, kigamboni hapafai kabisa, kama ni kwa sababu ya bahari tu sawa lkn kuna changamoto ya usafiri sana, nilifikia huko niliona tabu zake, nilitakiwa kuamka saa 9 usiku kwenda stendi ya Magufuli mbezi, siwezi kuishi mbali na kituo cha mabasi ya kwenda mikoani.
Mpango mzima sasa ni Mbezi, Luguruni, kibamba, kiluvya na kibaha.
Hiyo standy, kama unaitumia tu kurahisisha unapoenda mkoa, na siyo kibiashara inakupoteza,
Ni sawa kutegemea nyumba ya kupanga sababu tu, iko magomeni.

Kaa popote unapoona panaendana na shuguri zako za kiuchumi, kuna siku badala ya kufikilia kwenda mkoa na basi, utaona nafsi inakutuma kutafuta usafiri wa kwako.
 
Ndio napotaka kununua kiwanja huko.. Hata iwe maporini kabisa
Hongera kuna fikra za mtandaoni ukizifuata huwezi kujikomboa Dar, wengi tunapasifia kinondoni kawe, kwenye nyumba za kupanga, bora ujenge huko kigamboni kongowe miembe saba kibaha, alafu rudi upange magomeni, utakua na cha kujivunia mjini.

Kuna watu niliwakuta mjini enzi hizo Standy ya magari ya bagamoyo iko pale kariakoo mnafani, mpaka leo wako na maisha yaleyale, ilimradi wanaishi Kariakoo.
 
Hongera kuna fikra za mtandaoni ukizifuata huwezi kujikomboa Dar, wengi tunapasifia kinondoni kawe, kwenye nyumba za kupanga, bora ujenge huko kigamboni kongowe miembe saba kibaha, alafu rudi upange magomeni, utakua na cha kujivunia mjini.

Kuna watu niliwakuta mjini enzi hizo Standy ya magari ya bagamoyo iko pale kariakoo mnafani, mpaka leo wako na maisha yaleyale, ilimradi wanaishi Kariakoo.
Mji unakuwa Kigamboni size yake kama wilaya mbili za Dar. So kujaa itachelewa ila na maendeleo yamewahi fika
 
Ukipata muda tembea kuanzia Mji mwema Hadi Mikwambe uone viwanja vilivyopo barabara hio peke yake achana na zile hotels za baharini. Ikifika weekend napata shida niende wapi. Kigamboni sihami tena nazidi kusogea mbele kule nishafika Dege eco village

Hiyo ni trip tosha.

Asante kwq mualiko Bataringaya, ntaufanyia kazi.

Hapa nasubiria kiepe na shrimps.....😋😋

Kasie The Foodie.
 
Viwanja vinauzwa KIGAMBONI mwembe mdogo karibia na chuo cha afya kigamboni college

1. Umbali kutoka ferry mpk site ni killometer 23

2. Viwanja vimepimwa ila vipo katika michakato ya hati kwahy ukinunua unapata kwa jina lako rasmi

3. Umeme umefika tayar kumetulia hali ya hewa ni safi sana

Meter 8* 22 mil 1.5

Meter 15*20mil 2.5

Meter 35*35 mil 5

Kuhusu punguzo ondoa shaka kila kitu ni maelewano.View attachment 1821559

Luna wataalamu wa kusoma uoto wa asili wa ardhi na kubaini kipindi cha masika maji yanatuama hapo ama yanapita au yanaingia ardhini kwa mida mfupi.

Nilipewaga hilo somo miaka 7 iliyopita kwa sasa sikumbuki vizuri kudadavua ila ukiwasikiliza ukashika hupotei.
 
Back
Top Bottom