Ukitaka kujipima kama una upendo wa kweli na uvumilivu basi fuga mbuzi wa kienyeji

[emoji23][emoji23][emoji23] Mbuzi hawana maana kabisa
 
Pale kilimahewa mwanza mlimani enzi hizo bado mlima una nyumba chache, tukawa tunachunga mbuzi wa babu mlimani kule, sasa tukawa tunakawaida ya kuwachapa viboko vya hatari endapo tu mbuzi akifanya kosa la kugoma kutembea pindi tuvutapo kamba, tulikuwa wajukuu kama wanne hivi, sasa mbuzi akigoma tu unatoa taarifa kwa wenzio oyaa wangu kagoma basi anafungwa kwenye mti kamba fupi tunakata stiki za kutosha tunamshambulia balaa ha ha sometime tulikuwa tunawasingizia kuwa wamegoma ili tu,, tuwakate stiki.. mbuzi walikuwa na adabu kichizi
Sasa ukiwa mlimani mtu aliyeko bondeni anaona kila kitu, stori ikamfikia babu siku babu akatuvizia akapanda juu ya mti tuliokuwa tunawafunga pale ili kuwa stiki.. tumeanza kuwapiga tu babu akashuka kwenye mti huo huo aisee tulitembezewa stiki πŸ˜€ nafikiri mbuzi walifurahia sana ile revenge yao.
Kwa sasa nina mbuzi kama 26 juzi mchunga mbuzi aliniambia baba naomba uniongeze fedha maana mbuzi ni wengi na wana sumbua hasa muda huu bado mazao yako shambani,, nilipanda dau fasta hata sikutaka kubisha. Mbuzi ni noma aseeπŸ˜€
 
Unasingizia viumbe vya watu..
 
Hongereni
Mwezi uliopita nilijitia kiherehere kununua ng’ombe wa kienyeji, alitaka kunipa kesi ya mauaji baada ya kumpiga jirani

Nimeishia kumchinja siku ya Eid,
Sitaki tena mnyama Mwenye miguu minne kwangu
Aaah Rudisha bhana Ile avatar 😁
 
[emoji16][emoji16][emoji16]
 
Kusema ukweli ni wasumbufu mno,nilikuwa nao kama wanane hivi siku walipovamia shamba la shemeji yangu na kurarua mihogo ndio siku nilimpigia jamaa wa vingunguti aje awachukue kwa bei aloitaka mwenyewe
 
Hawa wadudu wasumbufu sana. Nakumbuka mzee ashawahi kuwa na ugomvi na mbuzi wake[emoji16][emoji16]

Yule mbuzi alikuwa korofi korofi tu halafu akimpiga bibi anakuja juu. Kuna siku tupo jikoni tunakula yule beberu kama kawaida yake anapiga wenzie walisahau kumfunga kamba, mzee ile kutupia jicho akaliona ni lile beberu, akanyanyuka kwa hasira akalikamata ndevu akamuwasha kofi, akamng'ata sikio mpaka akamega kipande.
Nyumbani wakaona sasa hiyo mbuzi tuchinje tu maana ukiachana na kutokuwa na maelewano mazuri na boss wake, lakini pia ingeweza kumletea uchizi mwenye nyumba[emoji16][emoji16]
 
Wapuuzi sana hao viumbe.
 

Attachments

  • Mbuzi.mp4
    810.3 KB
Kuna mbuzi Moja kubwa kama ndama ilikuaga libabe la wababe Lina KENGELE πŸ˜ŠπŸ€“ shingoni limbuzi la mizimu...
 
Kuna mbuzi Moja kubwa kama ndama ilikuaga libabe la wababe Lina KENGELE [emoji4][emoji851] shingoni limbuzi la mizimu...
Tulikuwa nayo kama hiyo. Hata bandani kwake huingii mpaka ulifunge na lilikuwa halifunguliwi. Mbuzi ni wakorofi sana[emoji16]
 
Ndo maana
Ninao kama 60 hawa Nala, Dodoma Mbuzi ni mchafu, msumbufu, mkeraji, ana sura mbaya anaweza kukufanyia jambo ukataka kumdunda akaleta majonjo ya kuudhi mara mbili ukapiga akafa
Wanasema unaweka sura ya mbuzi
 
Kuna wale wa pale Mbezi beach tank bovu wanajichunga wenyewe na Barabara wanavukia kwenye zebra Kila siku asubuhi na jioni bila kukosea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…