Ukitaka kujipima kama una upendo wa kweli na uvumilivu basi fuga mbuzi wa kienyeji

Ukitaka kujipima kama una upendo wa kweli na uvumilivu basi fuga mbuzi wa kienyeji

Tuliletewa jike na mwanae kumbe yule mama alikuwa na mimba akazaa dume tukakampa jina Champion, tulikuwa tunacheza naye sana baba akaamua kumuhasi/asi (hapo sijui lipi sahihi) jamaa alivyokuwa akawa na kiburi na dharau sio ya kawaida majani ya jana hali, hataki kufungwa kamba hivyo mama na dada yake wanafungwa yeye yupo pembeni yao na kulikuwa na mti umepinda vizuri kwamba alikuwa anaweza kuupanda hivyo yeye aliupanda akala majani, majani ya jana wakala mama na dada champion. Tusipomuona inabidi tumuite na anaitika kabisa Mee halafu anakuja mbio Kama mtoto anavyoitwa na akija hata Kama kakuudhi inabidi utabasamu lasivyo anakupiga pembe [emoji3][emoji3][emoji3], baadae akawa ukisahau jiko wazi anaingia anakula chakula chochote atakachokikuta ispokuwa nyama na samaki tu. Baadae akawa kero mtaani anaingia nyumbani kwa watu akikuta wanakula na yeye anataka Kula wakimnyima anapindua meza, hawakuchinjwa wote wala kuuzwa maana watoto tulikataa yote, na mwisho mzee aliwagawa baada ya watoto wote kuondoka nyumba, hadi Sasa bado tunamuongelea champion ambaye mdogo wangu aliinama kumfunga kamba kwa hasira jamaa akarudi nyuma Kama hatua saba hivi akaja speed akampiga kichwa mdogo wangu akaanza kuvuja damu puani na mdomoni Mungu NI mwema dogo alipona, visa NI vingi ila niishie hapa maana mmenikumbusha mbali.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]Aiseee..
 
Ao wajinga wanakuaga na kiongoz wao mjinga kuliko wako wao, yani ukiwafungua tu ye anaongoza to njia kwa speed kwenda kula mazao ya watu, dawa yao kamba asa iyo kamba ukute wako wa 3 ndo shughuli inakua ngumu mara wakuvute uku mara uku wakikushinda ujue kesi iyo, mazao ya watu washakula,

Basi nilikua nkiwatuliza kimbelembele na mfunga kamba kwenye lisho alafu namtia fimbo nyingi hadi asira yangu ipoe.... Kuna wakati kimbelembele alikua beberu mkorofi ukimchapa anageuka anaruka anataka akupige, basi nkawa nampa kolabo mwanangu mmoja, nafimbo zetu ndefu mmoja mbele mwingine nyuma akigeuka akupige fimbo akigeuka uku fimbo.....

Ila mikoa mingine noma Mbuzi 50 walipikutika mwezi mmoja, yani mbuzi anapatwa na kichaa, ukimpasua unakuta hadi irizi,

Pia kuna watu noma, waroho ata mbuzi kajifia hadi anaanza kuaribika ila wanakula tu....
Waliwah kumuaibisha mzee mmoja,walikuwa na kamba afu akawashika kwa pamoja ili akawafunge malishoni,sasa ile tabia yao ya mwingine anaenda huku,mwingine mbele mwingine nyuma mzee akawa amekomaa kuwashikilia ili wasimkimbie alijikuta wamemfunga miguu akakosa balance akajipiga chini
 
Nishawah kulea kamoja mama yake alikufa
Kila napoenda kako miguun nikienda dukan ananifata nikimuacha nikamfungia analia balaaa
Nikilala anakuja kuniamsha
Nilikuwa namnywesha maziwa na kumuogesha nilimpenda sana alivyojua akachukuliwa
 
Pamoja na mabaya yote,mnayoeleza, kijana ukitaka kutoboa Maisha haraka achana na kufunga kuku ,fuga mbuzi. Haeagi haraka , wanazaliana kwa wingi na chakula chake ni Cha bure. Tafuta Kambi weka uzio Anza kuwafuga
 
Tuliletewa jike na mwanae kumbe yule mama alikuwa na mimba akazaa dume tukakampa jina Champion, tulikuwa tunacheza naye sana baba akaamua kumuhasi/asi (hapo sijui lipi sahihi) jamaa alivyokuwa akawa na kiburi na dharau sio ya kawaida majani ya jana hali, hataki kufungwa kamba hivyo mama na dada yake wanafungwa yeye yupo pembeni yao na kulikuwa na mti umepinda vizuri kwamba alikuwa anaweza kuupanda hivyo yeye aliupanda akala majani, majani ya jana wakala mama na dada champion. Tusipomuona inabidi tumuite na anaitika kabisa Mee halafu anakuja mbio Kama mtoto anavyoitwa na akija hata Kama kakuudhi inabidi utabasamu lasivyo anakupiga pembe [emoji3][emoji3][emoji3], baadae akawa ukisahau jiko wazi anaingia anakula chakula chochote atakachokikuta ispokuwa nyama na samaki tu. Baadae akawa kero mtaani anaingia nyumbani kwa watu akikuta wanakula na yeye anataka Kula wakimnyima anapindua meza, hawakuchinjwa wote wala kuuzwa maana watoto tulikataa yote, na mwisho mzee aliwagawa baada ya watoto wote kuondoka nyumba, hadi Sasa bado tunamuongelea champion ambaye mdogo wangu aliinama kumfunga kamba kwa hasira jamaa akarudi nyuma Kama hatua saba hivi akaja speed akampiga kichwa mdogo wangu akaanza kuvuja damu puani na mdomoni Mungu NI mwema dogo alipona, visa NI vingi ila niishie hapa maana mmenikumbusha mbali.
Kipindi tukiwa na mbuzi wengi,ilitokea kambuzi kamoja kadogo dogo kakazaa ila kakawa hakataki kumnyonyesha mwanae,ile kukachunguza vizuri tukagundua matiti yake yalikuwa magumu na ukiyakamua yanatoa vitu vizito vizito hv,basi ikabid tuachane nako

Ikabid kile kitoto tuanze kukipatia maziwa ya ng'ombe baada ya muda kilinenepa kweli na kikawa kinashinda ndani kama paka hadi tukawa tunakivalisha nguo na cheni ya kimsalaba tulikifunga shingoni

Pale nyumban kile kimbuzi tulikipenda sana,ilikuwa mtu akichukua lile kopo lake la kukanyweshea maziwa ukikaonesha kanakufata kwa kukimbilia kakizani unataka kukipatia maziwa,chuchu yake tulikuwa tunatumia zile kopo za mafuta ya cherehani

Siku moja wakati kameshaanza kuchangamka kakawa kanapiga misele ya nje na nyumbani,bahati mbaya kakagongwa na gari na kakafariki pale pale,kwanza waliokaona walishangaa kuona mbuzi ana cheni
Siku hyo tulipata huzuni sana pale nyumban,tulikazika na tukakatengenezea kaburi,tulipata shida sana kuzoea kwamba hakapo tena nyumban
 
Kwa sisi waislamu tunafundishwa kuwa kwanini Mungu alituma mitume na hao mitume asili ya kazi zao ilikuwa kuchunga mbuzi na wanyama wengine.

Tunafundishwa kuwa Allah aliwaandaa hawa mitume kwa kuwapa kazi ya kuchunga wanyama kwanza kabla ya kuwapa utume ili wawe na mioyo ya uvumilivu ili waweze kulea na kuhamiliana na wanadamu watakao kuwa wanawaongoza.

Tazama historia ya mitume wengi utaona kazi zao wa uchungaji wa wanyama na hasa mbuzi.
Allah alijua kuwa ikiwa wataweza kuchunga wanayama na hasa mnyama msumbufu na kisirani kama mbuzi basi kwa binadamu itakuwa rahisi.
 
Ao wajinga wanakuaga na kiongoz wao mjinga kuliko wako wao, yani ukiwafungua tu ye anaongoza to njia kwa speed kwenda kula mazao ya watu, dawa yao kamba asa iyo kamba ukute wako wa 3 ndo shughuli inakua ngumu mara wakuvute uku mara uku wakikushinda ujue kesi iyo, mazao ya watu washakula,

Basi nilikua nkiwatuliza kimbelembele na mfunga kamba kwenye lisho alafu namtia fimbo nyingi hadi asira yangu ipoe.... Kuna wakati kimbelembele alikua beberu mkorofi ukimchapa anageuka anaruka anataka akupige, basi nkawa nampa kolabo mwanangu mmoja, nafimbo zetu ndefu mmoja mbele mwingine nyuma akigeuka akupige fimbo akigeuka uku fimbo.....

Ila mikoa mingine noma Mbuzi 50 walipikutika mwezi mmoja, yani mbuzi anapatwa na kichaa, ukimpasua unakuta hadi irizi,

Pia kuna watu noma, waroho ata mbuzi kajifia hadi anaanza kuaribika ila wanakula tu....
Ha ha ha.....kama nakuona vule[emoji1787]
nmetamani nitembelee jamii za wafugaji nijionee hivi vituko[emoji38]
 
Nimewavunja sana hao miguu, mbuzi na ng'ombe nimechunga sana.
Bora ufuge kondoo kuliko hao vicheche.

Wakishazoea kulisha shamba fulani, ukiwa njiani unawaswaga wanatimua mbio hata kama ni umbali wa kilometa 3 mbele. Inabidi ukimbizane nao na lazima utakuta wameshaharibu tu.

Raha ya kufuga hao ni nyama, baba alikuwa akichinja kila wiki mbuzi.

Nb: ukitaka kuwa mfugaji wa hutu "tushenzi" basi uwe na eneo kubwa vinginevyo kila siku utaitwa kwa mwenyekiti au mtendaji kujibu mashitaka ya kuharibu mazao ya watu.[emoji23][emoji23][emoji23]
Ha ha ha ......hawa wadudu ni wasumbufu pro max[emoji38]
 
Waliwah kumuaibisha mzee mmoja,walikuwa na kamba afu akawashika kwa pamoja ili akawafunge malishoni,sasa ile tabia yao ya mwingine anaenda huku,mwingine mbele mwingine nyuma mzee akawa amekomaa kuwashikilia ili wasimkimbie alijikuta wamemfunga miguu akakosa balance akajipiga chini
Ni kosa kubwa mno kuwaburuza wote Kwa pamoja kwenda kuwafunga , huwa wanakataa kabisa , na ukigeuka kuangalia Yani unaona kabisa Kwa kiburi na dharau hataki , aheri umchukue mmoja mmoja japo Napo ni kibembe tuu , kuja kumaliza kumfunga ushampiga vibao vya kutosha
 
Back
Top Bottom