Ukiwaelewa na kuwajua wanawake huwezi kuoa

Ukiwaelewa na kuwajua wanawake huwezi kuoa

Mwanadamu hatabiriki, kumjua kiwango cha kusema unamjua mtu hilo suala halipo. Ndiposa waswahili wanasema hujafa hujaumbika. Kwamba mtu/watu hubadilika.

Ndiposa kwenye kuoa, ukipata mtu mmeelewana, mkakubaliana...ndoa ifungwe.

Mambo yakibadilika, ndoa ikawa ndoana, ukiweza vumilia, ukishindwa achana naye kisha anza upya. Maisha ni safari imejaa hekaheka

Mwanadamu habadiliki.
Mwanadamu unayemuona kabadilika ni yule ambaye ulikuwa hujamjua uhalisia wake.
Wewe ndiye unamuona kabadilika lakini yeye hajabadilika ila anaonyesha hulka yake halisi.
 
Matokea ya 50 kwa 50 mkuu , tumempigania mtoto wa kike mpaka ikapitiliza tukamsahau mtoto wa kiume , sasa inakua ni ngumu mtoto huyo wa kiume kuishi ya mtoto huyo wa kike aliyepiganiwa kwa kila namna .
Kipi kifanyike?
 
Rais wetu tu single Maza!
Sasa tunashangaa nini kuwa na utitiri wa ma single Maza au vijana wa kiume kukataa ndoa?!
 
Mfalme sulemani alisema kadri unavyokua na maarifa ndio unakua na huzuni. Ukiyajua ya viongozi wa dini utaacha kwenda kusali
Naunga mkono hoja
Bora hata nisingesoma seminari. Maana inanifanya niskip kwenda church mara Nyingi. Ingawa naamini katika Mungu
 
Mwanadamu habadiliki.
Mwanadamu unayemuona kabadilika ni yule ambaye ulikuwa hujamjua uhalisia wake.
Wewe ndiye unamuona kabadilika lakini yeye hajabadilika ila anaonyesha hulka yake halisi.
Hoja yako hii wala sikubaliani nayo, bila shaka wakati ni mwalimu mzuri, ukipata maisha marefu utaikumbuka hoja hii na utakubaliana na nilichojadali awali.

Nikutakie heri
 
Kwema Wakuu!

Kuna namna mbili za kutokuwa interested na Ndoa.
Mosi, kutowaelewa na kutowajua kabisa wanawake.
Pili, kuwaelewa na kuwajua sana wanawake.

Hiyo ya pili ndio zaidi. Watu wengi wanaowajua wanawake kindakindaki huishia kuwa bachelor sugu. Hawaoi.

Wapo wanaume wenye kila sifa ya kuoa lakini hawataki kufanya hivyo kutokana na uelewa wao mkubwa kuhusu wanawake.

Jioni njema

Kuamua kuishi maisha ya kutooa sio tatizo sababu kuna matowashi wasiooa,

Lakini Kugoma kuoa huku unataka na unafanya matumizi ya waliooa ni woga, kutojiamini, kutotaka kuwajibika na kushindwa kutumia akili kama mwanaume

Wanaume wamepewa mamlaka ya kuwa vichwa ili waweze kuongoza wanawake, kuongeza uzao, kutunza na kulea, kuzalisha Mali na kuendeleza kujenga ufalme wa Mungu.

Sasa mnataka msioe ili iweje. Ili mzalishe jamii ya panya road, mashoga na wasagaji?
 
Hapo kwenye kuachana ndipo maumivu makali anakutana nayo mwanaume maana mali zake zinagawanywa wakati za mwanamke haziguswi., kumbuka sheria ya ndoa haitambua kipato na mali za mwanamke. Kwa mwanaume kuoa ni kamali

Hoja hii nzuri sana na inatafakarisha mno.

Kabla sijafunga ndoa, mentor wangu aliniambia kuhusu life span na life cycle ya ndoa. Kwenye life span alisema, ndoa inaweza kuishi kwa dakika moja hadi miaka 100. Yaani ndoa ni kiumbe chenye uhai.

Na kiumbe hai hufa. Hivyo hili la kufa kwa ndoa lazima niliweke kwenye mipango kazi wa ndoa, kwamba ndoa ikifa dakika ya tatu nijue nafanyaje...vivyo hivyo ikifa at 3 months, 7 years, 20 years...
Kwamba ndoa ikifa kilichokufa ni ndoa, sio wanandoa. Kuna mengi.

Ni mentorship ambayo vijana wengi hawana, mbaya zaidi hawatii bidii kutafuta haya maarifa toka kwa watu sahihi.
 
Kuamua kuishi maisha ya kutooa sio tatizo sababu kuna matowashi wasiooa,

Lakini Kugoma kuoa huku unataka na unafanya matumizi ya waliooa ni woga, kutojiamini, kutotaka kuwajibika na kushindwa kutumia akili kama mwanaume

Wanaume wamepewa mamlaka ya kuwa vichwa ili waweze kuongoza wanawake, kuongeza uzao, kutunza na kulea, kuzalisha Mali na kuendeleza kujenga ufalme wa Mungu.

Sasa mnataka msioe ili iweje. Ili mzalishe jamii ya panya road, mashoga na wasagaji?

Nimekaa pale nione majibu ya maswali uliyouliza
 
Yanini kununua n'gombe mzima wakati nikitaka nyama zimejaa tele buchani
 
Kwema Wakuu!

Kuna namna mbili za kutokuwa interested na Ndoa.
Mosi, kutowaelewa na kutowajua kabisa wanawake.
Pili, kuwaelewa na kuwajua sana wanawake.

Hiyo ya pili ndio zaidi. Watu wengi wanaowajua wanawake kindakindaki huishia kuwa bachelor sugu. Hawaoi.

Wapo wanaume wenye kila sifa ya kuoa lakini hawataki kufanya hivyo kutokana na uelewa wao mkubwa kuhusu wanawake.

Jioni njema
Mkuu kwa heshima na taadhima nashukuru sana kwa hili Andiko Ila tafadhari mkuu next time uje na nondo za kutosha km kawaida yako sio unatuwekea summary tu ungetushushia mapoint hapa wengine tuchukue notice za hao mabechala Sugu wanaogoma kuoa sababu wamewajua wanawake kwa asilimia 100 na 1
 
Yanini kununua n'gombe mzima wakati nikitaka nyama zimejaa tele buchani
Sasa huyo Ng'ombe si unamtafuna kila unapotaka hizo nyama za buchani hata mkia unakuta ushaachwa kwenye Supu huko unakuta firigisi hakuna moyo hakuna bandama hakuna mapupu yote hapo kwenye mabanda ya supu huko, ushaona sasa ukibeba Ng'ombe wako ukamweka ndani kila kitu unakikuta anacho Wewe ni kubonyeza tu
 
Kuamua kuishi maisha ya kutooa sio tatizo sababu kuna matowashi wasiooa,

Lakini Kugoma kuoa huku unataka na unafanya matumizi ya waliooa ni woga, kutojiamini, kutotaka kuwajibika na kushindwa kutumia akili kama mwanaume

Wanaume wamepewa mamlaka ya kuwa vichwa ili waweze kuongoza wanawake, kuongeza uzao, kutunza na kulea, kuzalisha Mali na kuendeleza kujenga ufalme wa Mungu.

Sasa mnataka msioe ili iweje. Ili mzalishe jamii ya panya road, mashoga na wasagaji?

Nina mke na mpango wangu ni kuwa na Wake Watatu

Sema Inshallah
 
Back
Top Bottom