Ukiwajua Polisi Tanzania, hutawashangaa kabisa na taarifa zao

Ukiwajua Polisi Tanzania, hutawashangaa kabisa na taarifa zao

Yes I have one I know, PhD, MAsters Moshi Technical, Ilboru, UDSM, ARDHI, lakini Kwa taarifa ni kwamba jeshi la polisi halitaki kuwatumia watu wa namna hii kwenye Administration Ili kuimplicate policy change isipokua wanatumia kama operation officers wa kutumwa tu na vilaza, ambao elimu hawana!
Uliza Elimu ya Kamishna Suzan Kaganda na sasa Yuko wapi?
Duuh Hatari sana!
 
Nmewahi kusoma riwaya ya habibu anga pamoja na mambo mengi ila utendaji wa nchi na namna nchi inavyo operate hasa kwa police ni kama wanatupiwa lawama...

Wanakuwa wanajua kabisa kinachoendelea ila wanakuwa na maelekezo ambayo inabidi jamii iyakubali hata kama hawayataki..

Kwa sasa jamii yetu inauhasama ambao hausemwi wa kutokuaminiana kati ya taasisi ya police na raia ila huenda hata police wanaonewa tu...

Sasa kwa hali ilivyo usishangae matukio kama ya wale w TRA tegeta yakaja kujitokeza tena kwa ukubwa..

Nini kifanyike?
Kwanza police wazuie hao watu wasiojulikana nnaamini kwa strong security system ya police hakuna tukio litafanyika wasijue au wasihusishwe..

Pili mifumo ya kipolice isomane ili kuepusha mtuhumiwa kukamatwa na kuachiwa wakati anakesi au anatafutwa sehemu nyingine..

Tatu wapungeze kama si kuondoa taarifa zenye ukakasi kama hizi.. ambazo hata ambae hajaufuta umande anaona amepigwa na kitu kizito kichwani..


Upo msemo wa kiswahil usemao
USIMSHIKE KIPOFU MKONO WAKATI MNAKULA ATAJUA UNAKOMBA MBONGA..
Umemaliza ! 👍🙌
 
Nina mkasa unaofanana na wako, na Mimi nilifungua taarifa chang,'ombe lakini mtuhumiwa walimkata wakamwachia kwa dhamana Ila ishu yangu ilifunguliwa jalafa na Dci na waliokuwa wanashugulika ni FCU Cha ajabu hawana taarifa zozote kwamba mtuhumiwa alishakamatwa Chang'ombe hata nilipowaambia bdo hawakuweza kuwasiliana
 
Polisi wana laana hao jamaa mie mtoto wangu yeyote atakaye kuja kuwa polisi mimie sie baba yake nitamkataaa hadharani
Angalia maisha Yao baada ya Kustaafu! Fanya utafiti kidogo tu utajua karma is real! Mwingine anajitengenezea kaburi huko,huku akiwa hama maelewano na familia yake kabisa anaitwa 7sita
 
Angalia maisha Yao baada ya Kustaafu! Fanya utafiti kidogo tu utajua karma is real! Mwingine anajitengenezea kaburi huko,huku akiwa hama maelewano na familia yake kabisa anaitwa 7sita
Umenichekesha sana Hahaha 🤣
Hivi yule jamaa alishakamilisha ule mradi wake ??!
Dunia ina mambo ya ajabu 😱
 
Duuh Hatari sana!
Lengo ni kuhakikisha kwamba wajinga wanawasimamia polisi wasomi! Unakuta Askari polisi let's say RPC au OCD, Ni msomi mzuri wa Sheria kama Muliro! Anajua namna mifumo inavyofanya kazi, lakini juu yake amewekwa DC na RC mwenye kichwa kama Cha chalamila! Na amepewa title ya Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa au WILAYA na yeye ndiye anayetoa maelekezo, Nini kifanyike na Nini kisifanyike, jua kwamba OCD na RPC asubuhi anatoa taarifa (briefing) ya Hali ya usalama kwenye eneo lake Kwa huyu kilaza aliteteuliwa Kwa kulipa fadhila au jinsi alivyofanilisha wizi wa kura nk nk.
Hakuna mtu anayepinga au kupindisha Maagizo ya Mwenyekiti! Matokeo yake Ndio haya wanaagizwa Cha kufanya na wajinga wajinga.
 
Nimeona watu wanashangaa polisi kuja na taarifa za mtu aliedhaniwa katekwa kuwa kafa kwenye ajali ....siko hapa kuwatetea polisi ..wala kushutumu lakini ningependa kuongea Kwa uzoefu wangu ...kuhusu polisi Tanzania...

Niliwahi kuwa na kesi ya mtu alienitapeli ...polisi Chango"mbe nikapewa Askari wa upepelezi tukawa tunamtafuta Kwa karibu miezi miwili...now wakati tunamtafuta huyo mtu tulishirikisha hadi kitengo cha cyber. Askari hao niliopewa kupitia"connection ya mtu powerful "kwahiyo sikuwa na wasiwasi na kuwa labda hawana nia au wamehongwa...walikuwa serious kazin....sasa cha kuchekesha ni kuwa Kwa kipindi ambacho "mtuhumiwa wetu" tunamtafuta...huyo mtuhumiwa akaenda Fanya matukio mengine ya kitapeli akakamatwa polisi Magomeni...akaachiwa...huku Sisi bado "tunamtafuta"..na mtuhumiwa baadae akaenda kumshitaki mtu mwingine polisi Kilwa road waliotapeliana...huku Sisi tunamtafuta...baadae kabisa akafanya tukio lingine akakamatwa polisi Oysterbay ndo tukaja kupata taarifa.

Kichekesho kingine ni jinsi polisi walivyokuwa wanachukulia hayo matukio kama tofauti na yanajitegemea na sio Ku combine matukio na kufungua kesi moja with strong evidence...na jinsi kila kituo kinamgombea mtuhumiwa....baadae nikaja gundua structure ya polisi ya ni ya kizamani Sana ...na Sheria zinaunda jeshi la polisi za kizamani sana....Kwa ufupi mahitaji ya kuwa na chombo cha Ku deal na organised crime ya mwaka 2024 yako tofauti kabisa na muundo wa jeshi la polisi....lilivyo sasa...

So sometimes tunawauliza polisi maswali na lawama nyingi wakati kiukweli hili jeshi la polisi Lina operate kama Tanzania bado uko miaka ya sabini tunawapa lawama nyingi sana bila kukaa chini na kuangalia namna ya kuwa na chombo vya mahitaji ya sasa na Sheria za sasa dunia inabadilika sana.

Leo ukiibiwa simu ndani ya mwendokasi..taratibu inasema uende polisi pale ulipopandia mwendokasi...yaani kama umepanda mwendokasi kimara ukaibiwa simu labda Magomeni itabidi urudi kimara kuandika jalada wakati pengine mwizi kateremkia posta...huu ni mfano Tu wa dunia inavyo kwenda na polisi walivyo baki kizamani.​

Jeshi la polisi linahitaji overhaul kabisa
Haaaa.. hata wewe muuza ngada unashitaki kutapeliwa 🙄 kanuni ya wauza ngada inasema hakuna kushitakiana kwa mambo ya utapeli wa aina yoyote songa mbele....ila kwa kuongeza mimi binafsi nawajua majambazi walio pata ajira polisi dar es salaam huku kule kigoma walikuwa ni majambazii yanayo tafutwa na polisi kwa miaka mingi .. jeshi la polisi linaongozwa kipumbavu sana ...mtu yoyote anaye ingia kituo cha polici ni lazima system zimtambue kikompyuta kabla ya kupatiwa huduma yoyote iwe ni kushitaki au kushitakiwa nk na mifumo yote ya serikali hadi mahospitalini ilitakiwa iwe connected na usalama wa taifa hivyo mambo ya PF3 yasinge itajika sana maana ukifika hospital unaingizwa kwenye system kutambulika ...kama ni muhalifu polisi inapokea alert 📢 kuwa hupo hospitalini wanatia team kuku aresti nk
 
Solution ni ku-digitalise mfumo, kila data iingizwe kwenye mfumo isomeke nchi nzima. Kama details za huyo aliyekutapeli zingekuwa kwenye mfumo wa taarifa za jinai za kidigiti za polisi, data ikiingizwa kituo cha polisi kilwa, inatakiwa ipige alarm pale kituo cha polisi Magomeni kuonyesha kwamba the suspect amekuwa located kilwa. Pia isomane na vituo vya uhamiaji, akiwa anafanya michakato ya kuvuka boda, afisa uhamiaji akiwa ana-process, jina likiingia tu katika mfumo, alarm ilie ili afisa huyo afanyie clearance za alarm husika. Isomane na magereza, Mahakama....

Isomane na mochwari kwamba ukiingia mwili wa mtu aliyekufa pasipo kujulikana, cha kwanza police na Hospitali wachukue DNA ya mtu huyo, iingie kwenye mfumo, ili akija ndugu au mtu kumtafuta ndugu, mtu huyo aliyekuha kutafuta nduguye atoe DNA, ikifanana na ya marehemu, basi mfumo nchi nzima unaweza kusema labda yuko mochwari mbeya, Nkasi, au Buzebazeba kutokana na DNA data iliyojazwa.

Hii itapunguza kutafutana manually katika mochwari coz mwananchi hawezi kutembelea mochwari za nchi nzima. Hata akifanikiwa, atatoka na ugonjwa mwingine kutokana na kuangalia watu waliokufa nchi nzima

Once I heard kwamba kuna utaratibu wa kutengeneza Database ya taifa zima ya DNA unafanywa na ofisi ya mkemia mkuu wa serikali. Matukio kama ya ghorofa la kariakoo, DNA ingetosha kufanya utambuzi. Matukio ya watu kuungua na moto mpaka kufa, majivu au mabaki yakiingia katika DNA database, wanatambulika

There is a need to create a digital cobweb ya jinai, na taasisi zote zinazo process jinai.

Suala la kuibiwa simu liwe reported anywhere, tena online, kama mtu ana IMEI number, imsome mwizi alipo pa po hapo bila kusubiri issue za watu wa Cyber, na mfumo uwe unaampa taarifa aliyeibiwa timely, papo hapo.

Therefore, there us a need to establish a sophisticated department of IT at the Police Force
Baadhi ya mifumo ipo tayari ila baadhi kweli hadi tuweze kuifikia itahitaji miaka mingi sana kwa hapa tulipo.

Mfano hili la DNA kwa sasa tu kupata majibu ya DNA inachukua muda, hivyo bado swala la muda hatutakuwa tumelitatua.

Ishu kama ya kuibiwa simu, hapa kuna mambo mengi sana zaidi hata ya hao polisi. Kwanza simu iwe na settings za uhakika na taarifa zake mwenye simu husika awe nazo.

Simu inaweza kupatikana hata bila ya kuwatumia polisi lakini bado ni changamoto sababu ya settings na uwepo wa data ya internet.

Ebu fikiria tu watu wengi wana simu janja na bado hata hawafahamu emails zao walizosajilia hizo simu.

Bado tunahitaji kuwa na elimu kwa jamii hasa ya masuala ya ulinzi wa taarifa binafsi, matumizi ya vifaa kama simu janja na mambo yanayohusiana navyo.

Ila ni kweli pia jeshi letu la polisi linahitaji maboresho hasa ili kuendana na wakati huu wa uhalifu wa kidigitali
 
Umenichekesha sana Hahaha 🤣
Hivi yule jamaa alishakamilisha ule mradi wake ??!
Dunia ina mambo ya ajabu 😱
Amekamilisha na ameshanunua Jeneza na kuteua Mwenyekiti wa kamati ya Mazishi. Kiufupi anateswa na Spirit haunting! Yani nafsi za watu zinamlilia jinsi alivyozikatili! Nimekutana na mwanafamilia mmoja akanidokeza kwamba, mke ameshaondoka nyumbani sababu jamaa ni mkorofi kuliko anavyoonekana kwenye screen!
 
Nimeona watu wanashangaa polisi kuja na taarifa za mtu aliedhaniwa katekwa kuwa kafa kwenye ajali ....siko hapa kuwatetea polisi ..wala kushutumu lakini ningependa kuongea Kwa uzoefu wangu ...kuhusu polisi Tanzania...

Niliwahi kuwa na kesi ya mtu alienitapeli ...polisi Chango"mbe nikapewa Askari wa upepelezi tukawa tunamtafuta Kwa karibu miezi miwili...now wakati tunamtafuta huyo mtu tulishirikisha hadi kitengo cha cyber. Askari hao niliopewa kupitia"connection ya mtu powerful "kwahiyo sikuwa na wasiwasi na kuwa labda hawana nia au wamehongwa...walikuwa serious kazin....sasa cha kuchekesha ni kuwa Kwa kipindi ambacho "mtuhumiwa wetu" tunamtafuta...huyo mtuhumiwa akaenda Fanya matukio mengine ya kitapeli akakamatwa polisi Magomeni...akaachiwa...huku Sisi bado "tunamtafuta"..na mtuhumiwa baadae akaenda kumshitaki mtu mwingine polisi Kilwa road waliotapeliana...huku Sisi tunamtafuta...baadae kabisa akafanya tukio lingine akakamatwa polisi Oysterbay ndo tukaja kupata taarifa.

Kichekesho kingine ni jinsi polisi walivyokuwa wanachukulia hayo matukio kama tofauti na yanajitegemea na sio Ku combine matukio na kufungua kesi moja with strong evidence...na jinsi kila kituo kinamgombea mtuhumiwa....baadae nikaja gundua structure ya polisi ya ni ya kizamani Sana ...na Sheria zinaunda jeshi la polisi za kizamani sana....Kwa ufupi mahitaji ya kuwa na chombo cha Ku deal na organised crime ya mwaka 2024 yako tofauti kabisa na muundo wa jeshi la polisi....lilivyo sasa...

So sometimes tunawauliza polisi maswali na lawama nyingi wakati kiukweli hili jeshi la polisi Lina operate kama Tanzania bado uko miaka ya sabini tunawapa lawama nyingi sana bila kukaa chini na kuangalia namna ya kuwa na chombo vya mahitaji ya sasa na Sheria za sasa dunia inabadilika sana.

Leo ukiibiwa simu ndani ya mwendokasi..taratibu inasema uende polisi pale ulipopandia mwendokasi...yaani kama umepanda mwendokasi kimara ukaibiwa simu labda Magomeni itabidi urudi kimara kuandika jalada wakati pengine mwizi kateremkia posta...huu ni mfano Tu wa dunia inavyo kwenda na polisi walivyo baki kizamani.​

Jeshi la polisi linahitaji overhaul kabisa
Naunga mkono hoja hii.....hasa kufanya overhaul ya jeshi la Polisi hilo ni muhimu Sasa.
 
Haaaa.. hata wewe muuza ngada unashitaki kutapeliwa 🙄 kanuni ya wauza ngada inasema hakuna kushitakiana kwa mambo ya utapeli wa aina yoyote songa mbele....ila kwa kuongeza mimi binafsi nawajua majambazi walio pata ajira polisi datmr es salaam huku kule kigoma walikuwa ni majambaz8 yanayo tafutwa na polisi kwa miaka mingi .. jeshi la polisi linaongozwa kipumbavu sana ...mtu yoyote anaye ingia kituo cha polici ni lazima system zimtambue kikompyuta kabla ya kupatiwa huduma yoyote hiwe ni kushitaki au kushitakiwa nk na mifumo yote ya serikali hadi mahospitalini ilitakiwa iwe connected na usalama wa taifa hivyo mambo ya PF3 yasinge itajika sana maana ukifika hospital unaingizwa kwenye system kutambulika ...kama ni muhalifu polisi inapokea alert 📢 kuwa hopo hospital nk
Mifumo mingi haisomani hata huko forodha tulimsikia mkubwa mmoja analalamika !!
🙏🤦🏽‍♂️
 
Amekamilisha na ameshanunua Jeneza na kuteua Mwenyekiti wa kamati ya Mazishi. Kiufupi anateswa na Spirit haunting! Yani nafsi za watu zinamlilia jinsi alivyozikatili! Nimekutana na mwanafamilia mmoja akanidokeza kwamba, mke ameshaondoka nyumbani sababu jamaa ni mkorofi kuliko anavyoonekana kwenye screen!
Hatari sana 😱
 
Lengo ni kuhakikisha kwamba wajinga wanawasimamia polisi wasomi! Unakuta Askari polisi let's say RPC au OCD, Ni msomi mzuri wa Sheria kama Muliro! Anajua namna mifumo inavyofanya kazi, lakini juu yake amewekwa DC na RC mwenye kichwa kama Cha chalamila! Na amepewa title ya Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa au WILAYA na yeye ndiye anayetoa maelekezo, Nini kifanyike na Nini kisifanyike, jua kwamba OCD na RPC asubuhi anatoa taarifa (briefing) ya Hali ya usalama kwenye eneo lake Kwa huyu kilaza aliteteuliwa Kwa kulipa fadhila au jinsi alivyofanilisha wizi wa kura nk nk.
Hakuna mtu anayepinga au kupindisha Maagizo ya Mwenyekiti! Matokeo yake Ndio haya wanaagizwa Cha kufanya na wajinga wajinga.
😳😱 !!
 
Nimeona watu wanashangaa polisi kuja na taarifa za mtu aliedhaniwa katekwa kuwa kafa kwenye ajali ....siko hapa kuwatetea polisi ..wala kushutumu lakini ningependa kuongea Kwa uzoefu wangu ...kuhusu polisi Tanzania...

Niliwahi kuwa na kesi ya mtu alienitapeli ...polisi Chango"mbe nikapewa Askari wa upepelezi tukawa tunamtafuta Kwa karibu miezi miwili...now wakati tunamtafuta huyo mtu tulishirikisha hadi kitengo cha cyber. Askari hao niliopewa kupitia"connection ya mtu powerful "kwahiyo sikuwa na wasiwasi na kuwa labda hawana nia au wamehongwa...walikuwa serious kazin....sasa cha kuchekesha ni kuwa Kwa kipindi ambacho "mtuhumiwa wetu" tunamtafuta...huyo mtuhumiwa akaenda Fanya matukio mengine ya kitapeli akakamatwa polisi Magomeni...akaachiwa...huku Sisi bado "tunamtafuta"..na mtuhumiwa baadae akaenda kumshitaki mtu mwingine polisi Kilwa road waliotapeliana...huku Sisi tunamtafuta...baadae kabisa akafanya tukio lingine akakamatwa polisi Oysterbay ndo tukaja kupata taarifa.

Kichekesho kingine ni jinsi polisi walivyokuwa wanachukulia hayo matukio kama tofauti na yanajitegemea na sio Ku combine matukio na kufungua kesi moja with strong evidence...na jinsi kila kituo kinamgombea mtuhumiwa....baadae nikaja gundua structure ya polisi ya ni ya kizamani Sana ...na Sheria zinaunda jeshi la polisi za kizamani sana....Kwa ufupi mahitaji ya kuwa na chombo cha Ku deal na organised crime ya mwaka 2024 yako tofauti kabisa na muundo wa jeshi la polisi....lilivyo sasa...

So sometimes tunawauliza polisi maswali na lawama nyingi wakati kiukweli hili jeshi la polisi Lina operate kama Tanzania bado uko miaka ya sabini tunawapa lawama nyingi sana bila kukaa chini na kuangalia namna ya kuwa na chombo vya mahitaji ya sasa na Sheria za sasa dunia inabadilika sana.

Leo ukiibiwa simu ndani ya mwendokasi..taratibu inasema uende polisi pale ulipopandia mwendokasi...yaani kama umepanda mwendokasi kimara ukaibiwa simu labda Magomeni itabidi urudi kimara kuandika jalada wakati pengine mwizi kateremkia posta...huu ni mfano Tu wa dunia inavyo kwenda na polisi walivyo baki kizamani.​

Jeshi la polisi linahitaji overhaul kabisa

Naunga mkono hoja kwa asilimia 100. Halijaandaliwa kufanya kazi kwenye dunia ya sasa.
Lina structure ambayo ni rigid na hair hairuhusu creativity.
Lina promote kulindana wao kwa wao hata kama kuna wengine wahalifu.
Halijaandaliwa kufanya policing kwenye mfumo wa siasa wa vyama vingi.
Sijui KPI zake, ila nachoka sana napoona matatizo yamekuwa mengi ila viongozi wamesheheni bashasha
 
Hoja dhaifu sana, kuna shahada plus G.P.A kali huko mitaani na zimekosa mwelekeo wa maisha (uelewa wako finyu kuhusu maisha) zimeamua kuendesha bodaboda na bajaji, wa kike wameamua yao!

Unahisi shahada,uzamili n.k ukiwa kwenye taasisi za kiusalama zina tija?? Hivi unapoambiwa tii amri ya mkubwa wako hapo shahada au div 1 inahusika vipi??

Unafahamu muundo wa mafunzo yao?? Pale div 1 au shahada inakusaidiaje?? Siku zote watawala (maboss)(vitengo) ni wachache na wanaofanyishwa kazi ni wengi.

Halafu nani aliyekudanganya ukipata div 1 au shahada kwa elimu yetu hii tunaoifahamu eti unajisifu una akili!

Nahisi hujatembea duniani na hujakutana na mikasa kuhusu elimu yetu! Unajua serikalini kuna first class ngapi?? Zimeleta tija??
Umesema mengi kiongozi

Ila AKILI ni tofauti na ELIMU Mkuu.
 
Back
Top Bottom