Ukizaa na mume wa mtu, jukumu la kulea mtoto ni lako mwenyewe!

Ukizaa na mume wa mtu, jukumu la kulea mtoto ni lako mwenyewe!

Ulichosema ni ukweli mtupu,,japobaadhi hawataelewa. Kwenye suala zima la kuzaa mwanamke ndio mwenye maamuzi.
Ukienda Ustawi wa Jamii kesi nyingi za matunzo ni za wanawake nyumba ndogo. Mapenzi yakiisha basi mwanaume haangaiki na kulea mtoto. Na wengi wanaingia kwa madai kuwa wanapendwa.Na wanawake wengi wanajua kuzaa ndio garantee yabkupata fedha au ndoa kwa mwanaume kiti ambacho wala hakina ukweli kwani mwanaume akikupenda hata kama huna kizazi ata stiki na wewe.

Wanawake wengi wanakuwa wahanga sababu ya kujipa upofu wa maneno mazuri wanayopewa wakati mapenzi yapo moto moto. Wanawake wenyewe ndo tunaweza kujikomboa katika hili. Tufanye maamuzi ya kuzaa kwa sababu tunahifaji lkn sio kwa sababi ya tamaa,, fedha au ndoa kutoka kwa mwanaume.



Sent using Jamii Forums mobile app
Wanawake sijui wana akili gani kuna single mother mmoja kazaa na mume wa mtu tena huyo mume ana wake watatu, yani mpaka leo namshangaa sijui tamaa ya pesa mzee mwenyewe ni muislam tena umri kama wa baba yake

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
Kwa mwanaume uzinzi ni starehe ambayo haimuathiri kama Dada zetu.
Ndio maana wazee wetu wa kale hawakuwa wajinga kumdhibiti Mwanamke dhidi ya kuziniwa ili Asipate madhara
Hata Mungu anajua hilo

Nyie endeleeni kuchagua dhambi zinazowafurahisha mnazilea
 
Kwani sex hufanyika kwaajili ya kutaka kuzaa tu ?

Je siyo kwaajili ya kupeana raha tu ?
Raha inayoweza kuleta watoto

Watu mjizuie ama muwajibike

Hata usipowajibika ni sawa pia
Mungu ana mkono mrefu sana
Narudia tumuogope Mungu sanaa
Usimkomoe mama wala mtoto
Waza mbele y Mungu utatoa utetezi gani
 
Wanawake sijui wana akili gani kuna single mother mmoja kazaa na mume wa mtu tena huyo mume ana wake watatu, yani mpaka leo namshangaa sijui tamaa ya pesa mzee mwenyewe ni muislam tena umri kama wa baba yake

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
Watu wamekubaliana wakajifunika duvet moja
Mbona unaumia wewe?
 
Hata Mungu anajua hilo

Nyie endeleeni kuchagua dhambi zinazowafurahisha mnazilea

Sio kila MTU anaamini habari za Mungu
Ila linapokuja suala la madhara halisi halitochagua muamini na asiye Amini.

Yule anayedhurika ndiye anapaswa kujikinga na kukingwa zaidi, hiyo ni kanuni ya Asili.
 
Raha inayoweza kuleta watoto

Watu mjizuie ama muwajibike

Hata usipowajibika ni sawa pia
Mungu ana mkono mrefu sana
Narudia tumuogope Mungu sanaa
Usimkomoe mama wala mtoto
Waza mbele y Mungu utatoa utetezi gani

Mungu hahusiki na maujinga yetu.
Mfanye maujinga alafu mumuingize Mungu kwenye upumbavu wenu.

Raha inapaswa uwe ndani ya Ndoa,
Nje ya hapo Mwanamke anajiingiza katika jina Baya la ukahaba au umalaya.
Na Matokeo yake atawajibika yeye zaidi, kiasili
 
Mwanamke aliyezaa na mume wa mtu hafai kuwa mke, uyo ni mtafuta maisha....... " alisikika jamaa mmoja katikati ya kundi la vijana"
 
Mungu hahusiki na maujinga yetu.
Mfanye maujinga alafu mumuingize Mungu kwenye upumbavu wenu.

Raha inapaswa uwe ndani ya Ndoa,
Nje ya hapo Mwanamke anajiingiza katika jina Baya la ukahaba au umalaya.
Na Matokeo yake atawajibika yeye zaidi, kiasili
Kwa muktadha wa mada hii aliye katika ndoa ni mume
Hivyo atulie na mkewe maisha yake yote
 
Sio kila MTU anaamini habari za Mungu
Ila linapokuja suala la madhara halisi halitochagua muamini na asiye Amini.

Yule anayedhurika ndiye anapaswa kujikinga na kukingwa zaidi, hiyo ni kanuni ya Asili.
Kama unapenda kumkinga himiza wenye viapo vya ndoa watulie ndani ya ndoa
 
Tatizo binadamu wa siku hizi ni wabishi sana...
 
UKIZAA NA MUME WA MTU, JUKUMU LA KULEA MTOTO NI LAKO MWENYEWE!

Anaandika, Robert Heriel

Unajizima Data sio!

Ati ooh! Alinidanganya Hana MKE, ooh! Sikujua kama kaoa. Wanaume ni Umbwa Koko!

Kama alikuambia Hana MKE si ungemuambia Ukoe wewe sasa ili uwe Mke wake. Mwambie apeleke posa nyumbani, taratibu za kindoa zifuate, iwe ndoa ya kimila au kiserikali au kidini. Kimila utaratibu ni simple Sana. Ukishaenda kutoa posa ukakubali tayari hiyo ni Ndoa.

Binti yangu epuka kujizima data. Mabinti WA siku hizi wengi ni wale wa liwalo na liwe. Wanayachezea Maisha yao kijinga.

Wengi wanajua kabisa Fulani ni mume wa mtu lakini kwa tamaa ya Pesa wanajilengesha Makusudi, na kujibebesha mimba, kisha baadaye wanaanza kusumbua Watu.

Acheni ubinafsi, eleweni kuwa mnawatesa Watoto wenu. Mtoto wako hawezi kulingana kihadhi na mtoto wa kwenye Ndoa. Hawezi kupata thamani kama angezaliwa ndani ya Ndoa. Mtoto wako utakayemzaa badala ya kuwa baraka anakuwa mleta tafrani Duniani.

Kwa nini usitafute Mwanaume wako akakuoa ndipo upate mtoto, uone jinsi ilivyoraha mtoto kulelewa na Baba na Mama. Wewe unazaa na waume za Watu alafu kama chizi ATI unasema ATI alinidanganya hana MKE. Hana MKE ulienda kwao akakutambulisha na Akaja kwenu kutoa Mahari ili useme alikudanganya. Wewe ndiye ulijidanganya.

Jukumu la KULEA MTOTO uliyempata Kwa Mume WA MTU ni jukumu lako ewe Binti yangu.

Hakuna Mwanamke yeyote mwenye Akili, MKE kamili atakayekubali Mume wake akuhudumie wewe au huyo mtoto wako. Na hiyo ipo Naturally ili ujutie Makosa uliyoyafanya, sasa Kwa nini umtese mtoto wako kisa ujinga wako. Ni Bora ukaacha kuzaa na waume za Watu.

ATI ili mtoto wako ahudumiwe ni mpaka vikao, sijui kupelekana Mahakamani, sijui kutukana na mume WA MTU. Kwa nini ujipe Shida? Yaani mpaka Mwanaume apate Pesa ya ziada ndio akupe wewe Pesa ya matumizi ya Mtoto. Lakini mtoto wako hayupo kwenye hesabu za Baba yake kisa Baba anafamilia Kuu anayoiangalia.

Binti yangu, epuka kuzaa na mume WA MTU kama unataka mtoto wako apate mapenzi kamili ya Baba na Mama.

Mke anayomamlaka na Haki zote kumzuia mume wake kutotoa Pesa yoyote nje ya familia. Sio ajabu Wake wakiona Waume zao wanawatoto nje wakapandisha gharama za Maisha ndani ya familia kama kuwapeleka Watoto shule za gharama na matumizi mengi yawe juu kusudi mtoto wako akose kabisa Pesa ya mume wake.

Sarah alimshawishi Ibrahimu kumfukuza Hajiri na mtoto wake waondoke katika nyumba. Ibrahimu Baba wa Imani Kwa mujibu wa Dini ya Uyahudi, uislam na Ukristo akamfukuza Hajiri na mwanaye. Kama Hicho kisa haujapata picha jinsi Hali ilivyo endapo utazaa na Mume WA MTU basi utakuwa unamatatizo.

Acha kuharibu Maisha yako. Acha kuharibu Maisha ya mwanao utakayemzaa. Zaa na Mwanaume wako.

Acha kuvuruga nyumba za Watu. Usiwe Mkosi na janga katika Maisha yako.

Epuka kuolewa MKE mwenza, hakuna kitu kama Hicho. Ni kujidanganya tuu. Ni tamaa zetu wanaume na ubinafsi wetu. Hakunaga mambo ya hivyo. Ni kuharibu Maisha tuu.

Ni Bora uwe mvumilivu na subira. Mpaka mume wako atakapofika ndio ufanye Maisha na kuanzisha familia Naye. Dunia ya sasa sio lelemama.

Ukivunja Kanuni za asili hata ungeunda sheria Kali vipi lazima mambo yazidi kuwa magumu.

Hakunaga msamiati usemao alinidanganya hana MKE. Huo ni Uongo mkubwa. Ulithibitishaje maneno yake.
Mwanaume yeyote kama upo serious naye na unahitaji awe Mumeo sharti umpe Kanuni zako kupima Nia yake. Mwambie afanye hima akuoe.

Elewa kuwa Mwana mpumbavu ni mzigo Kwa Mamaye, na hii inatokana na sababu kuwa Mama ndiye amebeba dhamana ya mtoto.

Nipumzike sasa

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Hatari sana wapambane na hali yao
 
Watu wamekubaliana wakajifunika duvet moja
Mbona unaumia wewe?
Mtoto anaumia kwa kukosa maisha ya furaha kutoka kwa wazazi na upande wa ndugu wa Baba tena omba Baba mtoto hasiwe muislamu yani mtoto hawezi kupendwa na ndugu wa Baba na Bibi zake, yani mfano Baba yake amefariki siku kuzika wakitaja wasifu wa marehemu wakifika kipengere cha kutaja idadi ya watoto watatajwa watoto wake aliozaa nje ya ndoa kama anawatoto kumi wa ndoa wanatajwa hao tu, hao wa nje ya ndoa hawa tambuliki.

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
Mtoto anaumia kwa kukosa maisha ya furaha kutoka kwa wazazi na upande wa ndugu wa Baba tena omba Baba mtoto hasiwe muislamu yani mtoto hawezi kupendwa na ndugu wa Baba na Bibi zake, yani mfano Baba yake amefariki siku kuzika wakitaja wasifu wa marehemu wakifika kipengere cha kutaja idadi ya watoto watatajwa watoto wake aliozaa nje ya ndoa kama anawatoto kumi wa ndoa wanatajwa hao tu, hao wa nje ya ndoa hawa tambuliki.

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
Ni upuuzi tu
Uzuri kila mtu atatoa hesabu ya ujinga wake
Starehe zako mwenyewe afu unakuja kutesa watoto
 
-Kwa mujibu wa sheria zetu jukumu la kutunza mtoto ni la baba, ndiyo maana mwanaume akimpa mimba binti Ili amkomboe mtoto ni lazima alipe gharama zote za Matunzo ya mtoto, au amuoe hiyo ni Kwa mujibu wa Tamko la Kimila la serikali that is to say Local customery law declaration order
- na Ili apate Matunzo ya mtoto Mama wa mtoto itabidi ampeleke mwanaume kwenye Mahakama ya watoto, na akipinga kwamba huyo mtoto sio Wake Mahakama itatoa Amri ya kwenda kwenye DNA test, na DNA results zikionesha kuwa ni mtoto wake mwanaume utawajibika kumtunza huyo mtoto hata Kama una mke
-
Nawezaje kumchukua mtoto wangu ambar nina muhidumia lakini mama mtoto hataki kunipa nikae naee??
 
Nawezaje kumchukua mtoto wangu ambar nina muhidumia lakini mama mtoto hataki kunipa nikae naee??



Anajua akikupatia ruzuku ya malezi na matunzo ya mtoto itakata kisha yeye atakula nini?!

Hao ndio hutegesha mimba kuzaa watoto kuwafanya kitega uchumi.

Kama hataki achana nae kama mtoto ni damu yako akikua atakutafuta mwenyewe!
 
UKIZAA NA MUME WA MTU, JUKUMU LA KULEA MTOTO NI LAKO MWENYEWE!

Anaandika, Robert Heriel

Unajizima Data sio!

Ati ooh! Alinidanganya Hana MKE, ooh! Sikujua kama kaoa. Wanaume ni Umbwa Koko!

Kama alikuambia Hana MKE si ungemuambia Ukoe wewe sasa ili uwe Mke wake. Mwambie apeleke posa nyumbani, taratibu za kindoa zifuate, iwe ndoa ya kimila au kiserikali au kidini. Kimila utaratibu ni simple Sana. Ukishaenda kutoa posa ukakubali tayari hiyo ni Ndoa.

Binti yangu epuka kujizima data. Mabinti WA siku hizi wengi ni wale wa liwalo na liwe. Wanayachezea Maisha yao kijinga.

Wengi wanajua kabisa Fulani ni mume wa mtu lakini kwa tamaa ya Pesa wanajilengesha Makusudi, na kujibebesha mimba, kisha baadaye wanaanza kusumbua Watu.

Acheni ubinafsi, eleweni kuwa mnawatesa Watoto wenu. Mtoto wako hawezi kulingana kihadhi na mtoto wa kwenye Ndoa. Hawezi kupata thamani kama angezaliwa ndani ya Ndoa. Mtoto wako utakayemzaa badala ya kuwa baraka anakuwa mleta tafrani Duniani.

Kwa nini usitafute Mwanaume wako akakuoa ndipo upate mtoto, uone jinsi ilivyoraha mtoto kulelewa na Baba na Mama. Wewe unazaa na waume za Watu alafu kama chizi ATI unasema ATI alinidanganya hana MKE. Hana MKE ulienda kwao akakutambulisha na Akaja kwenu kutoa Mahari ili useme alikudanganya. Wewe ndiye ulijidanganya.

Jukumu la KULEA MTOTO uliyempata Kwa Mume WA MTU ni jukumu lako ewe Binti yangu.

Hakuna Mwanamke yeyote mwenye Akili, MKE kamili atakayekubali Mume wake akuhudumie wewe au huyo mtoto wako. Na hiyo ipo Naturally ili ujutie Makosa uliyoyafanya, sasa Kwa nini umtese mtoto wako kisa ujinga wako. Ni Bora ukaacha kuzaa na waume za Watu.

ATI ili mtoto wako ahudumiwe ni mpaka vikao, sijui kupelekana Mahakamani, sijui kutukana na mume WA MTU. Kwa nini ujipe Shida? Yaani mpaka Mwanaume apate Pesa ya ziada ndio akupe wewe Pesa ya matumizi ya Mtoto. Lakini mtoto wako hayupo kwenye hesabu za Baba yake kisa Baba anafamilia Kuu anayoiangalia.

Binti yangu, epuka kuzaa na mume WA MTU kama unataka mtoto wako apate mapenzi kamili ya Baba na Mama.

Mke anayomamlaka na Haki zote kumzuia mume wake kutotoa Pesa yoyote nje ya familia. Sio ajabu Wake wakiona Waume zao wanawatoto nje wakapandisha gharama za Maisha ndani ya familia kama kuwapeleka Watoto shule za gharama na matumizi mengi yawe juu kusudi mtoto wako akose kabisa Pesa ya mume wake.

Sarah alimshawishi Ibrahimu kumfukuza Hajiri na mtoto wake waondoke katika nyumba. Ibrahimu Baba wa Imani Kwa mujibu wa Dini ya Uyahudi, uislam na Ukristo akamfukuza Hajiri na mwanaye. Kama Hicho kisa haujapata picha jinsi Hali ilivyo endapo utazaa na Mume WA MTU basi utakuwa unamatatizo.

Acha kuharibu Maisha yako. Acha kuharibu Maisha ya mwanao utakayemzaa. Zaa na Mwanaume wako.

Acha kuvuruga nyumba za Watu. Usiwe Mkosi na janga katika Maisha yako.

Epuka kuolewa MKE mwenza, hakuna kitu kama Hicho. Ni kujidanganya tuu. Ni tamaa zetu wanaume na ubinafsi wetu. Hakunaga mambo ya hivyo. Ni kuharibu Maisha tuu.

Ni Bora uwe mvumilivu na subira. Mpaka mume wako atakapofika ndio ufanye Maisha na kuanzisha familia Naye. Dunia ya sasa sio lelemama.

Ukivunja Kanuni za asili hata ungeunda sheria Kali vipi lazima mambo yazidi kuwa magumu.

Hakunaga msamiati usemao alinidanganya hana MKE. Huo ni Uongo mkubwa. Ulithibitishaje maneno yake.
Mwanaume yeyote kama upo serious naye na unahitaji awe Mumeo sharti umpe Kanuni zako kupima Nia yake. Mwambie afanye hima akuoe.

Elewa kuwa Mwana mpumbavu ni mzigo Kwa Mamaye, na hii inatokana na sababu kuwa Mama ndiye amebeba dhamana ya mtoto.

Nipumzike sasa

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Hakuna Baba anaweza kuona mtoto wake akiteseka! Awe wa nje au wa ndani ya ndoa.
Msiwatishe mabinti waacheni tuzae nao. Mtoto ni blessings
 
Back
Top Bottom