Bwana
Robert Heriel wanaokupinga hawajaelewa Ulichokiandika. Niwasaidie tuu kuwajulisha kuwa Mleta Uzi Hana Nia ya kuwataka wanaume wasilee watoto wa nje la hasha! Bali wanawake wasizae na waume za watu au wanaume ambao hawajawaoa Kwa kutegemea matunzo sawa na watoto wa Ndoa.
Mimi naungana na Robert kuwaasa kinadada kutokufanya mapenzi na wanaume wasio waume zao. Wafahamu ni heri atelekezwe na Manaume aliyemuoa kuliko atelekezwe na mume wa mtu au mwanaume ambaye hajajitambulisha Kwao.
Wanaume tuepuke wanawake wanaotuomba mbegu Kwa ahadi ya kuwa hawatasumbua wake zetu.
Midomo ya Malaya Hudondoza Asali.