Ukoo wetu wote ni masikini. Naombeni ushauri Nawezaje kukata huu mnyororo wa umaskini?

Utaondoka kwenye mnyororo huo kwa kufanya maamuzi katika mambo yako. Mtaji wa fedha kwako ni changamoto ila tambua, MUDA, UJUZI, NGUVU pia unaweza tumia kujipatia kipato.

Kikubwa kua na plan ndogo. Jifunze kuingiza shillingi mia 200 baada ya mida ifike 400, endelea ikuza na kuikuza.
 
Kama ushauri wangu utakuwa na maana uchukue, kama hauna maana tupa kapuni!

✓ jitenge na mnyororo wa ukoo wenu kiroho, hapa mtafute sheikh akupigie dua, anakutenganisha! Ukoo wako unaanza rasmi kuanzia kwako! Make issue kama hii hurithishwa (sometimes) ungelikuwa Mwanza ningelikupa address ya sheikh!

✓Au, tafuta mtaji! Anza biashara yako hata kama ni ya kawaida tu, kisha njoo Kawe uchukue mafuta ya Arise and Shine! (Nimeshuhudia wengi wente situation kama yako, wengine nimekuwa majirani nao), kama huamini uko, tafuta mafuta ya masheikh sanasana ya Qudra! tumia!

✓ukifanya biashara sahau kabisa kuwa mimi nina degree, hutoendelea kamwe, ikiwezekana kaishi mkoa mwingine mbali na huo ulikosomea chuo ili kuwa huru kufanya biashara zako!
 
Sawa, nashukuru mkuu
 
Nimekuelewa viziri mkuu.

Mimi nipo tanga
 
Umasikini mbaya sana, fanya kazi zenye risk kubwa utatoboa vinginevyo utabaki kuwa mtu wa simulizi tu za maisha ya watu
 
Vunja hiyo roho kwa maombi.
Fanya ukipendacho kwa bidii..achana na maneno ya kukukatisha tamaa.
Kila la kheri
 
Habari na Amani ya Mungu iwe juu yako;
wengi wamesema mengi lakini sio wote wamegusa sababu hasa ni nini na nn chakufanya.

nitakueleza ukweli ingawa sio wote watanielewa na kukubali kwasababu asiyejua na hajui hajui kama hajui mpaka atakapojua ( samahani kwa lugha ngumu)

Maisha ni rohoni na yanadhihirka (yanatokea) mwilini. namaanisha kila kitu kinaanza katika ulimwengu wa roho kwanza kabla hujaona yakitukia katika ulimwengu tunao ouna. Ulimwengu wa roho una miaka mingi mno kuliko maisha tunayo ishi, pia unasiri za kutosha.
kabla chochote hakijafanyika kinaaza rohoni kwanza, mfano unaposema kwenu wote ni masikini na mnapitia mambo magumu... hiyo ni tendo liko katika ulimwengu wa roho. hata mmoja wenu akijitahidi anaweza enda juu kidogo na akaanguka chini kwa nguvu sana.

kinachosababisha ni nguvu ya giza/ shetani/ kupitia ama uchawi ama mizimu ambayo wamefanya maagano fulani na kuweka mipaka fulanifulani. Ukifuatilia ukoo wenu utagundua, kwamba wazee walitumikia na kujihusisha na miungu na waliweka maagano fulanifulani, wakitoa sadaka na matambiko.na waliishi maisha fulani ambapo inawalazimisha ukoo wote waishi maisha hayohayo. waliweka madhabahu pia, ama kwenye miti ama milima ama sehemu nyinginezo.

Namna ya kutoka katika mnyororo huo ni kuvunja maagano na kuangusha hizo madhabahu, vingenevyo hamna namna. Kulipa sadaka ambazo zilitolewa ni kwa kutoa sadaka kubwa zaidi ya zile zilitolea. Habari njema ni kwamba DAMU YA YESU ni SADAKA iliyo kubwa kuliko sadaka zote na popote na kwa wakati wowote. kwa hiyo njia pekee ya kupoke auponyaji wako ni kukutana na YESU atakutoa wewe na ndugu zako na ukoo wako.

inasomeka kama ni rahisi, ni kweli - rahisi lakini ina gharama ya IMANI na UVUMILIVU kwa maana ya muda na BIDII, UTII na SHAUKU.

nakazi tu kwamba, hata kama utaweka juhudi kaktka mikakati ye yote ile, huwezi toboa mpaka utengeneze hapo kwanza. haimaanishi uache fanya kazi kabisa ila elekeza nguvu kufunguluwa kwanza, baada ya hapo utafanikiwa

naamini nimesaidia kwa sehemu;
 
Maasai. Lakini imagine sina hata mbuzi
toka umasaini acha mila zote jichanganye mikoa mingine ishi kichanganyikeni usitafte ndugu hata mmoja katafte pesa mpk malengo yatimie oa endeleza pesa hakikisha ndugu hao wakutafte wewe sio wewe uwatafte vingnevyo unatafta kurejea km wao.
 
Nimekuelewa vuzuri mkuu. Nimeokoka na ninasali Pentecost. Naomba muongozo wa kuvunja maagano na kuangusha hizo madhabahu. Ahsante
 
toka umasaini acha mila zote jichanganye mikoa mingine ishi kichanganyikeni usitafte ndugu hata mmoja katafte pesa mpk malengo yatimie oa endeleza pesa hakikisha ndugu hao wakutafte wewe sio wewe uwatafte vingnevyo unatafta kurejea km wao.
Ahsante sana mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…