Ukosefu wa maadili unatisha kwa kasi unayoporomoka Tanzania

Ukosefu wa maadili unatisha kwa kasi unayoporomoka Tanzania

Changamoto kubwa inayochangia mmonyoko wa maadili ni umaskini, malezi ya Mzazi mmoja, rushwa za ngono, utandawazi na kukosekana kwa Umoja katika malezi
 
Tatizo la ukosefu wa maadili kwenye jamii ni ubinafsi uliopitiliza wa siku hizi unaotokana na kuingia kwa sera za ubepari katika mataifa yetu. Leo hii mtoto wa kwako ni wa kwako, zamani mtoto alikuwa ni wa jamii nzima. Ukizingua mtaani mzazi au mtu mkubwa yoyote anakupa kichapo na taarifa zikifika home unaongezewa kichapo vilevile, leo hii mtoto akipigwa jirani tena kwa kufanya kosa fulani bhasi ujue kinaumana baina ya mzazi wa mtoto na huyu aliempiga. Wazazi wanalea watoto kama mayai. Mwisho kabisa, tumekuwa tukibeba kila kitu cha mtandaoni bila kuchuja. Utandawazi una mipaka yake lakini sisi tunabeba kila kitu. Kizazi cha 2030s kuendele sikipatii picha itakuwaje.
 
We pambana na maadili yako na to some extent utakavyowalea wanako; hutoweza kamwe kufanya maadili yako 100% yawe ya kila mtu 100% na pia iyo cjui TZ ilikuwa ivi cjui ivi? Jaman utandawazi unayafanya mengi yaonekane ila sio mapya chini ya jua na pia unafki mwingi unafanya watu wengi waonekane watakafitu.
hatuongelei hapa 100% nikipata ja[o nusu percent ni ushindi mkubwa sana.

Kama ulikuwa huelewi, kumtumikia Mwenyezi Mungu ni kuitumikia jamii.

Mficha maradhi, kifo humuumbuwa.

Wewe ni shoga? Kama "ndiyo", tufahamishe ulianza vipi kuwa shoga ili iwasaidie wengine. Au kwa kuwa wewe shoga basi unataka wote wawe mashoga na au waupende ushoga?
 
Mzazi anaweza kuwa drunker Ila mtoto wake akawa sio mtumiaji wa vilevi this is what my parentsdid to me


Kilichopo wamtumikie Mungu tu hapo Maisha ya kiroho ndo kila kitu

Nina 26 yrs
Sinywi pombe
Sivuti sigara Wala bangi
Sifanyi Uzinzi na sijawahi

Namtumikia Mungu Sana na nafurahia Maisha vizuri
Sasa rafiki yangu hapo pombe ni mmomonyoko wa maadili ? Yaani hamuoni raha bila kumnanga mzee pombe popote ilihali yeye hana shida na nyie .

Kaka pombe naomba itoe tafadhali mdogo wangu
 
Mzazi anaweza kuwa drunker Ila mtoto wake akawa sio mtumiaji wa vilevi this is what my parentsdid to me


Kilichopo wamtumikie Mungu tu hapo Maisha ya kiroho ndo kila kitu

Nina 26 yrs
Sinywi pombe
Sivuti sigara Wala bangi
Sifanyi Uzinzi na sijawahi

Namtumikia Mungu Sana na nafurahia Maisha vizuri
Wewe kama mimi kasoro hapo kwenye pombe, japo si mlevi ni mnywaji huwa nakunywa kistaarabu na najua kipimo changu, huwa sinywi kulewa nakunywa for fun na ni mara moja moja sana
 
Hii ni battle kati ya millenials. Baby boomers na gen Z
Silent Gen na Baby Boomers hawahusiki sana hapa, kinachoshangaza Gen X na Millenials ndio wanaoongoza kuvilalamikia vizazi vya sasa, ambao ni Gen Z na Gen Alpha ilihali wao ndio wazazi wao respectively na ndio waliowalea
 
Vitabu vya dini ni muhimu sana, nyinyi wenyewe na watoto zenu wanyimeni vyote msiwanyime maadili mema, na hakuna pakuyapata maadii mema zaidi ya kwenye dini.
Itakua ni kwel kama baada ya dini kuletwa Africa maadili mema yaliongezeka, na kufika sasa tupo karibu kabisa na kilele cha maadili mema, kwasababu waumini wa dini ni wengi mno.
 
Sasa rafiki yangu hapo pombe ni mmomonyoko wa maadili ? Yaani hamuoni raha bila kumnanga mzee pombe popote ilihali yeye hana shida na nyie .

Kaka pombe naomba itoe tafadhali mdogo wangu
Ukitoa maji ,mbele ya maziwa pombe ndio kinywaji cha kale zaidi duniani, mtu kazaliwa 2003 anapigia kelel pombe.
 
Dini ndio msingi wa maadili mema kama ulikua hujui.
Kabla ya hizi dini zote Africa ilikuwa na maadili safi kabisa!


Baada ya hizi dini za kipumbavu kuja muafrica mkristo hawez kuoa muislam na kinyume chake!


Baada ya hizi dini kuja muafrica anakatazwa kula nguruwe.


Dini inamwambia mwafrica kuwa mwafrica mwingine asie muislam ni kafiri

Sent from my Pixel 5 using JamiiForums mobile app
 
Kabla ya hizi dini zote Africa ilikuwa na maadili safi kabisa!


Baada ya hizi dini za kipumbavu kuja muafrica mkristo hawez kuoa muislam na kinyume chake!


Baada ya hizi dini kuja muafrica anakatazwa kula nguruwe.


Dini inamwambia mwafrica kuwa mwafrica mwingine asie muislam ni kafiri

Sent from my Pixel 5 using JamiiForums mobile app
Kabla ya dini Africa mwanaume alikua mwanaume tu ,kulikua hakuna mwanaume mwanamke Africa.
 
Bila ya shaka, wengi wa wale wenye umri iliozido miaka 40 watanielewa.

Tanzania yetu iliyokuwa inasifika ndani na nje ya nchi kwa maadili na nidhamu imeenda "arijjojo", wale waliowahi kucheza na vishada (kites) watanielewa nikisema "arijojo".

Nakumbuka miaka ya nyuma, kuna vijana nilikiuwa nawasiliano nao sana US, wakati huo nami naishi nje ya Tanzania, akanambia kuna rafiki yake anatafuta mchumba nimtafutie, nikamwambia mbona wachumba wapo wengi na vijana siku hizi hakuna anaetaka kutafutiwa, akanambia hujanielewa, hataki mchumba tu, anataka mchumba kutokea Tanzania. Akanielewesha nikamuelewa, nikamuunganisha na watu Dar., Nafurahi kusema akapata mke na mpaka sasa wanazeeka pamoja, watoto zao wameshafikia umri wa kujukuu, kama bado, sina mawasiliano nao ya mara kwa mara.

Hiyo siyo point yangu bali ni mfano tu. Kama hayo yalikuwa mengi sana si kutokea Ulaya tu, hata nchi za jirani walitamani kuoa mwanamke wa Kitanzania, sababu kuu ikiwa ni maadili.

Leo hayo kukutana nayo ni nadra sana, sisemi yamekwisha kabisa, lakini yameporomoka kwa kiwango kikubwa sana. Ni nini kilichotufikisha hapo? Nafahamu wengi sana maisha wanayokutana nayo ndivyo yalivyo, hawatoweza kunielewa kabisa, kwani hawana na cha kulinganisha nayo hayo, sisi wa zamani tunayoyaona kuwa ni maadili mema.

Wewe unayenisoma, maadili mema kwako ni yepi? Tutajie japo moja tu. Inawezekana kabisa nnavyoviona mimi kuwa si maadili mema, kwako ikawa ni ajabu kwanini hilo hayo si maadili mema.

My take; Maadili mema hayafundishwi tu, bali huanzia kwa kuigwa, je ni wazazi ndiyo tulikosea?
Leo hii kumtafutia mtu, wakikwaruzana tu utasikia;

1. Kwanza hukuwa chaguo langu, ni fulani ndo kaniingiza chaka.

2. Pale mitaa ya kwenu nilikuwa namtaka fulani, wewe ukajipendekeza kwa niliyemtuma ukafanikiwa kuniingiza chaka

etc
 
Kabla ya dini Africa mwanaume alikua mwanaume tu ,kulikua hakuna mwanaume mwanamke Africa.
Haya matamaduni ya nje yamekuja kumuharibu muafrica badala ya kumjenga!

Boko Haram wanaua waafrica wenzao kisa dini


Alshabab wanaua ndugu zao kisa dini


Magaido ya msumbiji yanaua ndugu zao kisa dini


Na sijawahi kuona Muislam yoyote duniani akikemea mauaji ya hivi vikundi chini ya dini!



Dini za mwafrica, watu walikuwa wanaomba mvua na ukame unapotea kweli. Leo wamejaa wakina Mwamposa kazi kuuza chumvi na kutembea na wake za watu




Halafu Kuna mpuuzi anaona dini zina mchango.





Sent from my Pixel 5 using JamiiForums mobile app
 
Haya matamaduni ya nje yamekuja kumuharibu muafrica badala ya kumjenga!

Boko Haram wanaua waafrica wenzao kisa dini


Alshabab wanaua ndugu zao kisa dini


Magaido ya msumbiji yanaua ndugu zao kisa dini


Na sijawahi kuona Muislam yoyote duniani akikemea mauaji ya hivi vikundi chini ya dini!



Dini za mwafrica, watu walikuwa wanaomba mvua na ukame unapotea kweli. Leo wamejaa wakina Mwamposa kazi kuuza chumvi na kutembea na wake za watu




Halafu Kuna mpuuzi anaona dini zina mchango.





Sent from my Pixel 5 using JamiiForums mobile app
Yote ya yote ila kina mwamposa mwakapesa 🙌🙌🙌
 
Bila ya shaka, wengi wa wale wenye umri iliozido miaka 40 watanielewa.

Tanzania yetu iliyokuwa inasifika ndani na nje ya nchi kwa maadili na nidhamu imeenda "arijjojo", wale waliowahi kucheza na vishada (kites) watanielewa nikisema "arijojo".

Nakumbuka miaka ya nyuma, kuna vijana nilikiuwa nawasiliano nao sana US, wakati huo nami naishi nje ya Tanzania, akanambia kuna rafiki yake anatafuta mchumba nimtafutie, nikamwambia mbona wachumba wapo wengi na vijana siku hizi hakuna anaetaka kutafutiwa, akanambia hujanielewa, hataki mchumba tu, anataka mchumba kutokea Tanzania. Akanielewesha nikamuelewa, nikamuunganisha na watu Dar., Nafurahi kusema akapata mke na mpaka sasa wanazeeka pamoja, watoto zao wameshafikia umri wa kujukuu, kama bado, sina mawasiliano nao ya mara kwa mara.

Hiyo siyo point yangu bali ni mfano tu. Kama hayo yalikuwa mengi sana si kutokea Ulaya tu, hata nchi za jirani walitamani kuoa mwanamke wa Kitanzania, sababu kuu ikiwa ni maadili.

Leo hayo kukutana nayo ni nadra sana, sisemi yamekwisha kabisa, lakini yameporomoka kwa kiwango kikubwa sana. Ni nini kilichotufikisha hapo? Nafahamu wengi sana maisha wanayokutana nayo ndivyo yalivyo, hawatoweza kunielewa kabisa, kwani hawana na cha kulinganisha nayo hayo, sisi wa zamani tunayoyaona kuwa ni maadili mema.

Wewe unayenisoma, maadili mema kwako ni yepi? Tutajie japo moja tu. Inawezekana kabisa nnavyoviona mimi kuwa si maadili mema, kwako ikawa ni ajabu kwanini hilo hayo si maadili mema.

My take; Maadili mema hayafundishwi tu, bali huanzia kwa kuigwa, je ni wazazi ndiyo tulikosea?
Maadili ni nini??
Maadili gani yameporomoka Tanzania kwa sasa??
Mfano wako pia hauna mashiko.
 
Utandawazi una mchango mkubwa sana katika kuporomoka kwa maadili mema,
Wazazi nao wamekua too busy na kutotafuta hata muda wa kulea watoto wao au kufuatilia mienendo yao,maadili ya Walimu pia yameporomoka,zamani walimu walikua wanaheshimiwa na wanafunzi kuliko walivyokua wakiwaheshimu au kuwaogopa wazazi wao,

Hapa tatizo linaanzia kwenye malezi,So wazazi/Walezi hawana pa kukwepea hizi lawama.
Watu wanaachana na ujima
 
Ulitaka nieneze chuki za upagani?


Kama wewe huna dini unataka wote tusiwe na dini? Kukosa dini ndiyo chanzo kikuuu cha ukosefu wa maadili.

Kama huna dini hayo maadili utajifunza kutokea wapi?
Mbona wenye dini wengi ni wala Rushwa tangu karne na karne, pia huiba uchaguzi na kukandamiza wapinzani.
Haya ni maadili??
 
Tatizo kubwa zaidi la maadili katika nchi hii ni wizi wa pesa za umma na matumizi mabaya fedha za walipa kodi, mengine mengi ni Petty issues tu.
 
Back
Top Bottom