Ukristo na Uislamu ni Dini mbili zisizofanana kabisa

Ukristo na Uislamu ni Dini mbili zisizofanana kabisa

  • Musannaf Abd Razak cha Imam Abd Razak Al Sanani
  • Musannaf Ibn Abi Shaybah cha Imam Abu Bakr Ibn Abd Allah Ibn Muhammad Ibn Abi Shaybah aliezaliwa .
  • Sahih Ibn Hibban cha Abu Hatim Muhammad Ibn Hibban .
  • Sunan Ad Darimi cha Imam Muhammad Abd Rahman Ad Darimi As Samarqand
  • Sahih Ibn Huzaymah cha Imam Muhammad Ibn Ishaq Ibn Khuzaymah
  • Sunan Ad Daraqutni cha Imam Abu Hasan Ali Ibn Umar Al Daraqutni
  • Mustadrak Al Sahihain/Mustadrak Al Hakim cha Imam Muhammad Ibn Abd Allah Al Hakim
  • Sunan Al Bayhaqi/Sunan Al Kubra cha Imam Abu Bakr Ahmad Ibn Husayn Al Bayhaqi
  • Sharh Al Sunan na Masabih Al Sunan vya Imam Abu Muhammad Al Husayn Al Baghawi
  • Riyadh as Salihin cha Imam Abu Zakariyah Muhyiddin Sharaf An Nawawi
  • Al Jami’i cha Imam Ismai’l Ibn Umar Ibn Kathir.
Hivi havichambui fani za hadithi bali vimekusanya hadithi.

Tafuta vitabu vya kuanzia kama vile Mustwalahul Hadithi cha Sheikh Uthaymiin, tafuta Mandhumat al Bayquniyyah, Tafuta Risala al-Birkiwi hiivi kama msingi na viko viko, hizo miuswanafat na Sunan, hivyo hukhti fani kama fani ya Hadithi.

Umethibitsha mwenyewe ya kuwa huna dani ya hadithi. Fathu al-bari ya Ibn Hajar ni sherehe ya Sahihul al Bukhari.
 
Nimecheka sana, inaonekana huna elimu ya Hadithi zaidi ya kutaja mgawanyo wa hadithi tena pasi na kuzingatia misingi.

Zipo hadithi ambazo zilionekana ni sahihi lakini zina shida bali dhaifu kabisa, na hii ni baada ya kupembuliwa upya. Tafuta kitabu cha Sheikh Albaniy kiitwacho 'SIlsila Ahadithi Dhaif' kadhalika tafuta kitabu cha Sheikh Muqbil kiitwacho 'Hadith al-Mu'ala dhwahiha as-Swaiha'.

Kingine hakuna "Hadithi Maqtu'". Kanukuu vizuri hili neno.

Nakupa kazi tuwekee hadithi mbili tu ambazo si sahihi toka kwenye Sahihi Bukhar, maana kuna utafauti katika kusihi hadithi na kutokuwa sahihi kabisa. Maana hata Hadithi Sahihi nazo zimegawanyika.
Vitabu vyote ulivyotaja Ninavyo na sio kuwa navyo tu navisoma..

Umesema Nikuwekee Hadithi ambazo sio sahihi kwenye Sahihi Bukhari naomba nikupe Tano..

kwanza nikukumbushe Bwana Kisai..

Ili Hadithi iwe sahihi,Imam Al Shafi'i anasema kuhusiana na Hadith ambayo si Mutawattir kukubalika usahihi wake inabidi: ‘Mpokeaji wake awe ni mwenye kuaminika katika dini yake, awe anajulikana kua hasemi uongo katika kunukuu kwake, awe mwenye kufahamu anachokinukuu, awe mwenye kufahamu kwa kiasi gani mabadiliko ya maneno anayoyanuu yanaweza kubadilisha maana ya anachokinukuu, kimaana na kimaneno’.

Lakini kwa Hadithi kadhaa Ndani ya Bukhari Msimuliaji maarufu ni Abu Huraira ambaye Amesema Uongo mara kadhaa..

Uongo wa Kwanza Alisema kwamba alisali swala ya uoga na ilhali swala hiyo ilifanyika mahala panapoitwa Nakhl katika mwaka wa 5 wa utume ; Abu Huraira alikuwa hajasilimu kwa sababu alisilimu mwaka wa 7 wakati ilipotekwa ngome kuu ya Mayahudi Khaibar [kama Km 80 kaskazini mwa Madina]...

Hadithi inayothibitisha Uongo wake ni hadithi no 4137..
Screenshot_20240408_193213_Adobe Acrobat.jpg


Sasa Tunaanza makosa machache sitataka ypte kwenye Bukhari maana ni mengi..

Sahihi Bukhari Juzzu ya 4 Hadithi no 3330..
Kuhusu Kuoza kwa Nyama..

Nyama Inaoza kwa sababu ya Waisrael
Screenshot_20240408_190700_Adobe Acrobat.jpg


Abu Huraira alisimulia Hadithi na akainasibisha na Mtume kasema ila alipobanwa sana alisema ni mawazo yake mwenyewe na sio mtume...
So kama ukiona anatumia Neno mtume alisema..
Ila baadae walipombana akasema ni maneno yake mwenyewe..

Juzzu ya 7 Hadithi no 5355
Screenshot_20240408_191123_Adobe Acrobat.jpg


Aya zilizokuwepo zamani kwenye Quran Kisha Zikaondolewa..
Sahihi Bukhari hadithi 4090, na Hadithi no 6830..

Mkuu ziko nyinhi sana Hizo ni chache
 
Hivi havichambui fani za hadithi bali vimekusanya hadithi.

Tafuta vitabu vya kuanzia kama vile Mustwalahul Hadithi cha Sheikh Uthaymiin, tafuta Mandhumat al Bayquniyyah, Tafuta Risala al-Birkiwi hiivi kama msingi na viko viko, hizo miuswanafat na Sunan, hivyo hukhti fani kama fani ya Hadithi.

Umethibitsha mwenyewe ya kuwa huna dani ya hadithi. Fathu al-bari ya Ibn Hajar ni sherehe ya Sahihul al Bukhari.
Mkuu hadithi nimeshasoma na najua na japo siwezi kujiita Mwanazuoni au Muhadithina na hapo nimekuonyesha Uchambuzi wa Hizo hadithi zilizokusanywa Na hata ukisoma Bulughul Maram..
Kwa wale wanaoanza kujifunza kuchambua Imechambua vizuri hadithi..

Na hata Hapa nipo nasoma Musnad Ya Iman Hanbal..
Karibu Mkuu..
Screenshot_20240408_194031_My Files.jpg

Screenshot_20240408_194210_Adobe Acrobat.jpg
 
Vitabu vyote ulivyotaja Ninavyo na sio kuwa navyo tu navisoma..

Sasa kama unavyo unashindwaje kuviweka hivyo ambavyo vinaelezea fani ya Hadithi, na wewe unatuwekea vilivyo kusanya Hadithi ?
Umesema Nikuwekee Hadithi ambazo sio sahihi kwenye Sahihi Bukhari naomba nikupe Tano..

kwanza nikukumbushe Bwana Kisai..

Ili Hadithi iwe sahihi,Imam Al Shafi'i anasema kuhusiana na Hadith ambayo si Mutawattir kukubalika usahihi wake inabidi: ‘Mpokeaji wake awe ni mwenye kuaminika katika dini yake, awe anajulikana kua hasemi uongo katika kunukuu kwake, awe mwenye kufahamu anachokinukuu, awe mwenye kufahamu kwa kiasi gani mabadiliko ya maneno anayoyanuu yanaweza kubadilisha maana ya anachokinukuu, kimaana na kimaneno’.

Kuna Hadithi ambazo rawi wake ni Thika, yaani wakweli, waadilifu, sachamungu pia. Soma maana ya Hadithi Hassan.
Lakini kwa Hadithi kadhaa Ndani ya Bukhari Msimuliaji maarufu ni Abu Huraira ambaye Amesema Uongo mara kadhaa..

Uongo wa Kwanza Alisema kwamba alisali swala ya uoga na ilhali swala hiyo ilifanyika mahala panapoitwa Nakhl katika mwaka wa 5 wa utume ; Abu Huraira alikuwa hajasilimu kwa sababu alisilimu mwaka wa 7 wakati ilipotekwa ngome kuu ya Mayahudi Khaibar [kama Km 80 kaskazini mwa Madina]...

Hadithi inayothibitisha Uongo wake ni hadithi no 4137..

Mpaka hapa wewe ndio hujui kuzichzmbua Hadithi. Maswahaba wote ni waadilifu na hawasemi uongo. Nani amekwambia hadithi inatiwa udhaifu kwa mtindo huu ? Nakuuliza swali kwani mtume ameswali sala ya Khofu mara ngapi ? Mpaka ukatae ya kuwa Abuu Huraira hajaswali swala ya Khofu ?

Hapa bado hujakosoa hii Hadithi.

Kingine katika Hadithi kuna fani inayo jishughulisha na Riwaya yaani matini ya Hadithi na Diraya inayo jishughulisha na Sanadi. Katika ukosoaji wa HADITHI, hapo ulitakiwa kwanza uanze kuichambua sanadi ya wapokezi, kisha uje uangalie je Mtume alisali mara ngapi sala ya Khofu ?
 
Mkuu hadithi nimeshasoma na najua na japo siwezi kujiita Mwanazuoni au Muhadithina na hapo nimekuonyesha Uchambuzi wa Hizo hadithi zilizokusanywa Na hata ukisoma Bulughul Maram..
Kwa wale wanaoanza kujifunza kuchambua Imechambua vizuri hadithi..

Na hata Hapa nipo nasoma Musnad Ya Iman Hanbal..
Karibu Mkuu..

Bulughu al Maraam haichambui hadithi kama fani au kwa mtindo wa fani, bali imekusanya hadithi za hukmu za kisheria. Bado fani ya Hadithi hujaisoma bali huenda una vitabu vya Hadithi.

Kingine namna yako ya Uchambuzi wa hadithi haiko sawa, hap onapo kumezidi kuonyesha ni kwa namna gani huijui hiyo fani. Kuna hadithi nyingi ambazo maswahaba wamesingiziwa kadhalika. Kwahiyo ili sasa tuseme wewe umeichambua hadithi na kujua ni sahihi kabla ya kumuelekezea swahaba, lazima kwanza uangalie sanadi ya wapokezi husika. Ili tujue je ni kweli Abuu Huraira hayo maneno alimsikia Mtume ?

Kwahiyo ili uchambuzi wako uwe na mashiko kwanza, lazima uje kutelezea wapokezi wa hiyo hadithi mpaka kwa Abuu Huraira kisha mpaka kwa Mtume, kinyume chake ni makosa kumuita swahaba Muongo kwa mtindo huo.

Sasa nasubiri utuletee kwanza uchambuzi wa wapokezi na utupe sifa zao.

Namna hii huwa wanaitumia sana MASHIA kuwatusi maswahaba, huku elimu ya Rijali wa hadithi hawana.
 
Vitabu vyote ulivyotaja Ninavyo na sio kuwa navyo tu navisoma..

Umesema Nikuwekee Hadithi ambazo sio sahihi kwenye Sahihi Bukhari naomba nikupe Tano..

kwanza nikukumbushe Bwana Kisai..

Ili Hadithi iwe sahihi,Imam Al Shafi'i anasema kuhusiana na Hadith ambayo si Mutawattir kukubalika usahihi wake inabidi: ‘Mpokeaji wake awe ni mwenye kuaminika katika dini yake, awe anajulikana kua hasemi uongo katika kunukuu kwake, awe mwenye kufahamu anachokinukuu, awe mwenye kufahamu kwa kiasi gani mabadiliko ya maneno anayoyanuu yanaweza kubadilisha maana ya anachokinukuu, kimaana na kimaneno’.

Lakini kwa Hadithi kadhaa Ndani ya Bukhari Msimuliaji maarufu ni Abu Huraira ambaye Amesema Uongo mara kadhaa..

Uongo wa Kwanza Alisema kwamba alisali swala ya uoga na ilhali swala hiyo ilifanyika mahala panapoitwa Nakhl katika mwaka wa 5 wa utume ; Abu Huraira alikuwa hajasilimu kwa sababu alisilimu mwaka wa 7 wakati ilipotekwa ngome kuu ya Mayahudi Khaibar [kama Km 80 kaskazini mwa Madina]...

Hadithi inayothibitisha Uongo wake ni hadithi no 4137..
View attachment 2958131

Sasa Tunaanza makosa machache sitataka ypte kwenye Bukhari maana ni mengi..

Sahihi Bukhari Juzzu ya 4 Hadithi no 3330..
Kuhusu Kuoza kwa Nyama..

Nyama Inaoza kwa sababu ya Waisrael
View attachment 2958100

Abu Huraira alisimulia Hadithi na akainasibisha na Mtume kasema ila alipobanwa sana alisema ni mawazo yake mwenyewe na sio mtume...
So kama ukiona anatumia Neno mtume alisema..
Ila baadae walipombana akasema ni maneno yake mwenyewe..

Juzzu ya 7 Hadithi no 5355
View attachment 2958105

Aya zilizokuwepo zamani kwenye Quran Kisha Zikaondolewa..
Sahihi Bukhari hadithi 4090, na Hadithi no 6830..

Mkuu ziko nyinhi sana Hizo ni chache

Ngoja nikusaidie kitu kimoja, kwanza huu ulioweka sio uchambuzi wa kihadithi. Ili uchambuzi wako uwe sahihi, lazima kwanza uanze kuchambua wapokezi wa hiyo hadithi, hii sio habari za pauka pakawa, yaani from no where.

Sababu Imamu Bukhari ana sanadi rudi uje kuzichambua hizo sanadi na kama huwezi kufanya rudi katika vitabu vya Takhriji za Hadithi. Yaani tunataka kwanza tujue kweli masimulizi hayo ameyasimulia Swahaba Mtukufu Abuu Huraira ?
 
Nani aliwaambia ya kuwa amri kumi za Mungu ni nguzo za Ukristo ?

Shida yenu Ukristo ni dini isiyo kuwa na misingi yenyewe haikamiliki mpaka itumie maandiko yasiyo wahusu. Mfano wa kumbukumbu la Taurati. Taurati haikuletwa kwa Wakristo sababu Mpaka Yesu anaondoka hapakuwa na Ukristo duniani.
Shida yenu waislamu mnalazmisha mambo yenu na sisi tuyafuate.... Quran haina Amri 10 alizopewa Musa, amri 10 za Mungu ni nguzo za maadili katika ukristo... Usizini, usiibe, usiue, mpende baba yako na mama yako, na zote nyinginezo
Swali langu linataka uthibitisho ya kuwa alikuwa kweli ni mwanafunzi wa Yesu ? Katika wale wanafunzi 12 wa Yesu Matayo alikuwa ni miongoni mwao ?
Ndio, katika Injili nne za Biblia (Mathayo, Marko, Luka, na Yohana), Mathayo anatajwa kama mmoja wa wanafunzi kumi na wawili wa Yesu.
 
Naam vitabu vyote vinne yaani Taurati, Zaburi, Injili na Qur'an vyote vimeshushwa toka mbinguni. Maandiko ya manabii yalikuwepo hata Muhammad hajazaliwa ?

Unataka kusema Qur'an ilikuwepo kwa manabii wengine ? Umekisoma ulichokiandika ?

Swali zuri, habari za Musa, Ibrahimu, Yesu kwa Muhammad zilitoka kwa Allah kwa kumfunulia mja wake.
Vimeshushwaje bwana wakati vilikuwepo toka kitambo.... Yani yesu mwenye aliishita Torati, alafu miaka buku 7 baadae anakuja mtu na kusema alishushiwa torati na nyie mnaamini

Ni sawasawa atokee mtu leo hii asema ameshushiwa katiba ya Tanzania, alafu ukisoma hiyo katiba yake iwe inafanana na katiba iliyokuwepo mwanzo... Je kashushiwa kweli au kakopi
 
Wewe dogo unajifanya mjuaji sana wa haya mambo wakati ukweli huujui. Na unapenda ligi za kidini ukitetea ukristo wako wakati huna elimu and so unakosa moral authority to establish this type of discussions.

Naomba nikujibu point yako ya kwanza ya Ibrahim.
Kiarabu kina wenyewe sio mnatafsiri mnavyotaka nyinyi. Hiyo aya ya Surat An'aam (6:74) Quran imetumia neno Abi kudenote baba (kama ambavyo wewe umetafsiri)......lakini katika ufasaha wa lugha, Abi haitumiki tu kudenote baba mzazi. Hata baba mdogo/mkubwa inatumika pia yaani uncles au mababu zako waliotangulia (ancestors). Nitakupa ushahidi juu ya hili:-
1. Ukisoma Quran 2:133 wakati Yaqub (Jacob) umemjia umauti akawauliza wanawe watamwabudu nani baada ya kufa kwake? Wakamjibu tutamwabudu Mungu wa baba zako Ibrahim, Ismael na Isihaka. Hapa Ismael naye kaitwa Abi wakati si baba yake mzazi.
2. Kwanza baba yake Ibrahim hakuwa mwabudu sanamu. Ukisoma Quran 14:41 Ibra anaomba yeye na baba yake na waumini wengine waingizwe peponi. So hii ni evidence aliyetajwa pale 6:74 si baba yake mzazi.

Baba yake Ibrahim kwa mujibu wa Uislam anaitwa Tarah, kasome kitabu cha Ibn Katheer, kinaitwa Al bidaya wa Nahaya volume 1 page 139.
Pia nenda usome Tafsiri ya Quran ya Tabari by Ibn Jarir volume 7 page 158 na Historia ya Tabari volume 1 pg 119.

Dogo, ukija huku ujipange sio unakurupuka kama mlevi wa wanzuki. Hivi hujiulizi, yaani makosa uje kiyaona wewe leo wa karne hii ya dot com, huko nyuma hakukuwa na watu wanatafakari mambo haya? Hawakupata majibu?
Ni bora uulize kuliko kuconclude usichokijua.
WHEN YOU ARE NOT SURE, GUESS POSITIVELY.
Sean.
Dogo hawa watu unaowazungumzia humu kwenye Quran sio wanaozungumziwa kwenye Biblia... Historia za hawa watu ni tofauti... Ibrahim wa Quran na Abrahamu wa Biblia ni watu tofauti kimatukio
 
Mwanafunzi gani wa Yesu aliandika injili? Hakuna ushahidi wowote unaoonesha Marco, Luka wala Peter waliandika injili. Hivyo vyote havijulikani alindika nani. Sasa mandishi ya watu kwa utashi wao na uzoefu wao katika dini yanakuwaje neno la Mungu?
Yaani maandishi ya Paulo yawe neno la Mungu? Kwanini Yesu mwenyewe hakuacha maneno yake yawe neno la kuishi angalu tungeyaita neno la Mungu.
Wewe umesoma Biblia au Quran... Aliyesoma Biblia hawezi kubisha kuwa Mathayo, Luka, Yohana waliandika Injili... Sisi Biblia haikushushwa kama nyie na Quran, sisi biblia iliandikwa kwa mujibu wa historia na matukio yaliyotokea
 
Labda hii watu hawajui. Leo si tunazungumzia dini zetu, let's go.

Kuna tofauti ya watu walioandikwa kwenye Biblia na Koran, hilo kwanza ulijue. Ibrahim unayemsoma kwenye Biblia si Ibrahim unayemsoma kwenye Koran.

Ibrahim wa kwenye Biblia baba yake anaitwa Terah ila wa kwenye Koran anaitwa Azar. Kasome Quran 6:74.

Kwenye Biblia wana Yesu, kwenye Koran wana Issa. Huyu Issa hakusulubiwa msalabani, ila Yesu alisulubiwa. Ndugu zangu, hawa ni watu wawili tofauti.

Kuna MUNGU (Almighty GOD) kwenye Biblia na kuna Allah kwenye Koran

So watu wa huku ni tofauti na wa kule. Kwa Biblia, Ishmael anajulikana kama mtoto wa kijakazi, ila kwa Kuran ni tofauti.

So mkikaa na kuzungumza, cha kwanza jueni mnawazungumzia watu wa sehemu tofautitifauti.

Mfalme Suleiman wa Bible alikuwa holy na baadaye akaanguka dhambini ila wa kwenye Kuran alikuwa anaongea mpaka na majini. So mkiwa mnawasoma watu wa kwenye Bible, msije kufikiri ni watu walewale wa kwenye Kuran, sio hivyo.

Musa wa kwenye Biblia alipewa Amri 10 za MUNGU, Musa wa kwenye Koran hakupewa amri 10 zozote.

Biblia inamtambua Samson kama jamaa aliyebarikiwa nguvu na uwezo wa kupambana na udhaifu wake ni kukata nywele zake, ila hakuna kisa cha namna hiyo kwenye Quran.

Biblia imeorodhesha mitume na manabii wengi wakitoka katika chimbuko la wayahudi, wakati Quran haiwazungumzii wayahudi katika chimbuko la unabii.

Ndio maana ukimsoma mtu wa huku, unaona tofauti kubwa na mtu wa kule.

Kuran imemtambua Adam kama mtume, ila kwa Biblia imemtambua kama mtu wa kawaida tu, mtu aliyeumbwa mwanzoni kabisa.

So mlifahamu hilo, sio mnakaa kwenye vijiwe vya kahawa mnabishana weeee meaningwhile watu mnaowazungumzia ni tofauti.

Historia ya Matukio ikitofautiana basi jua kabisa hao ni watu tofauti kabisa.

Hivyo ni vyema kila mtu abaki na anachokiamini, muda au siku ya kiama ndio ukweli utadhihirika nani alikuwa sahihi na nani alikuwa muongo.
Kiama ndiyo kitu gani?
 
Sasa kama unavyo unashindwaje kuviweka hivyo ambavyo vinaelezea fani ya Hadithi, na wewe unatuwekea vilivyo kusanya Hadithi ?


Kuna Hadithi ambazo rawi wake ni Thika, yaani wakweli, waadilifu, sachamungu pia. Soma maana ya Hadithi Hassan.


Mpaka hapa wewe ndio hujui kuzichzmbua Hadithi. Maswahaba wote ni waadilifu na hawasemi uongo. Nani amekwambia hadithi inatiwa udhaifu kwa mtindo huu ? Nakuuliza swali kwani mtume ameswali sala ya Khofu mara ngapi ? Mpaka ukatae ya kuwa Abuu Huraira hajaswali swala ya Khofu ?

Hapa bado hujakosoa hii Hadithi.

Kingine katika Hadithi kuna fani inayo jishughulisha na Riwaya yaani matini ya Hadithi na Diraya inayo jishughulisha na Sanadi. Katika ukosoaji wa HADITHI, hapo ulitakiwa kwanza uanze kuichambua sanadi ya wapokezi, kisha uje uangalie je Mtume alisali mara ngapi sala ya Khofu ?
Sikuona Faida ya Kuichambua kwa kina hadithi hiyo..

Ila kwa sanadi haina shida shida yangu ni matini zake hizo hadithi..

Huwezi kuIpa Hadithi usahihi kwa sanadi pake yake..
Ikiwa ina matini ya Uongo..

Nimekupa hadithi nyingi umeshikilia Moja kwa kuwa umeshikilia hiyo Moja sasa ngoja tuichambue matini zake..

Kwanza Umesema kuwa Mtume alifanya Sala ya hofu kwa vita vingi lakini kwa bahati mbaya ama nzuri hadithi kwenye matini yake imetaja hadi Vita iliyofanyika..Sijui kama unasoma kujibu au unasoma kilichoandikwa..

Screenshot_20240408_193213_Adobe Acrobat.jpg

Narudia Tena swala hiyo ilifanyika mahala panapoitwa Nakhl katika mwaka wa 5 wa utume ; Abu Huraira alikuwa hajasilimu kwa sababu alisilimu mwaka wa 7 wakati ilipotekwa ngome kuu ya Mayahudi Khaibar [kama Km 80 kaskazini mwa Madina]. Bado unabisha???

Haya tuache hapo twende kwenye Kumzulia Mtume, abu huraira kamzushia Mtume kasema kitu ilihali mtume hakusema Unataka muislam aisifie hiyo hadithi..

Au aseme kile Mnachojifunga nacho kuwa maswahaba wote ni wema???

Mwanzoni kwenye hadithi hii alisema kuwa Mtume alisema baada ya watu kumbana sana akasema ni maneno yake!..

Bado unataka Huyo mtu Nimuamini je vipi kadanganya kama hicho kasema watu wakashtuka je vingapi ambavyo hawakushtuka??

Screenshot_20240408_191123_Adobe Acrobat.jpg

Najua sunni mnafundishwa kuheshimu maswahaba nafahamu nilikuwa huko ila Usiwape hadhi ya Utume kama Shia wanavomfanya Ally..

Nataka Tuzungumzie matini ya Hadithi na sio Sanad kwa sababu naamini Bukhari ana sanad isiyo na shaka je hadithi zake (Kimatini "Kiriwaya")

Najua Kigezo unachotaka ni tuxungumzie kulingana na maumbile ya Matn na Isnad ya Hadith, kwamba hadithi ni Munkar au Mudraj..

Najua kwamba Hadithi nyingi za Sahih al bukhar Zina isnad nzuri kabisa na zenye mnyororo usiokatika mpaka kwa mtume..

Ila swali matini yake inaLeta maana na sio Mudraj..
 
Ngoja nikusaidie kitu kimoja, kwanza huu ulioweka sio uchambuzi wa kihadithi. Ili uchambuzi wako uwe sahihi, lazima kwanza uanze kuchambua wapokezi wa hiyo hadithi, hii sio habari za pauka pakawa, yaani from no where.

Sababu Imamu Bukhari ana sanadi rudi uje kuzichambua hizo sanadi na kama huwezi kufanya rudi katika vitabu vya Takhriji za Hadithi. Yaani tunataka kwanza tujue kweli masimulizi hayo ameyasimulia Swahaba Mtukufu Abuu Huraira ?
Hakuna mahali nimesema nimechambua ila umeniomba Hadithi Ambazo haziko.sahihi na ziko.kwenye Usahihi...

Na nimekupa Ila bado mpaka sasa hivi hujaniprove wrong kuwa hadithi hizo ni sahihi au sio sahihi?
UMeomba hadithi nimekupa sasa hivi umeanza sasa kuleta blah blah za Bukhar hana sanad nani kasema buhari ana sanadi..

Bukhar ni Mujitahidi tu na hata Level ya Taqlid hajafika..kwa hiyo atabaki kuwa Imam wa Hadithi tu..
 
Wazo hili lingekosekana hapa ningepotea JF milele.

Hata hivyo hakuna kiumbe kilichojileta duniani kwa ridhaa yake chenyewe bila ya kuumbwa.

Je kabla ya kuumbwa kilikuwa kinaishi wapi na baada ya maisha duniani kitarudi wapi?

Tafakari na chukua hatua, haki hekima kidini [emoji375][emoji375]
Inawezekana huyo aliyeumba kila kitu yupo kweli..... lakini sio huyu wa kwenye hekaya za Bibilia na Quran na scriptures za dini nyingine
We know nothing about “god”
Nadharia yako ya hakuna kinachojiumba chenyewe inatengeneza infinity..... nani kamuumba Mungu, na aliye muumba Mungu kaumbwa na nani?
 
Shida yenu waislamu mnalazmisha mambo yenu na sisi tuyafuate.... Quran haina Amri 10 alizopewa Musa, amri 10 za Mungu ni nguzo za maadili katika ukristo... Usizini, usiibe, usiue, mpende baba yako na mama yako, na zote nyinginezo

Ndio maana nikasema hivi UKRISTO ni dini ambayo Haina misingi, inatumia mafundisho ya mitume wengine kuendesha dini yao. Hili liweke akilini, Mtume Musa alitumwa kwa watu wa Israeli, kadhalika Yesu. Yesu ameondoka hakuacha Ukristo.

Qur'an inazo amri tena kwa ufafanuzi mzuri na hukumu zake.
Ndio, katika Injili nne za Biblia (Mathayo, Marko, Luka, na Yohana), Mathayo anatajwa kama mmoja wa wanafunzi kumi na wawili wa Yesu.

Sasa ndio uthibitishe ya kuwa kweli alikuwa ni katika wale wanafunzi 12 wa Yesu.
 
Vimeshushwaje bwana wakati vilikuwepo toka kitambo.... Yani yesu mwenye aliishita Torati, alafu miaka buku 7 baadae anakuja mtu na kusema alishushiwa torati na nyie mnaamini

Ni sawasawa atokee mtu leo hii asema ameshushiwa katiba ya Tanzania, alafu ukisoma hiyo katiba yake iwe inafanana na katiba iliyokuwepo mwanzo... Je kashushiwa kweli au kakopi

Tuwekee ushahidi wa kuwa Yesu aliishika Taurati. Toa mfano ambao ni hai, nani aje aseme ameshshiwa Taurati na Taurati ili shapita tayari ?

Maana ya kushushwa ni kwa maana mitume husika wanapewa au wanafunuliwa ujumbe toka Mbinguni.

Kufanana sio hoja, Qur'an haifanani na vitabu, ila ina habari kuhusu vitabu vya zamani katika hali ya kuthibitisha ukweli wa Qur'an na kujibu hoja za wapingaji.

Ndio maana katika sababu ambazo ziliwafanya watu wamkubali Mtume ni kuwaelezea habari za kale, na wakastaajabu na kumsadikisha.
 
Sikuona Faida ya Kuichambua kwa kina hadithi hiyo..

Ila kwa sanadi haina shida shida yangu ni matini zake hizo hadithi..

Huwezi kuIpa Hadithi usahihi kwa sanadi pake yake..
Ikiwa ina matini ya Uongo..

Nimekupa hadithi nyingi umeshikilia Moja kwa kuwa umeshikilia hiyo Moja sasa ngoja tuichambue matini zake..

Kwanza Umesema kuwa Mtume alifanya Sala ya hofu kwa vita vingi lakini kwa bahati mbaya ama nzuri hadithi kwenye matini yake imetaja hadi Vita iliyofanyika..Sijui kama unasoma kujibu au unasoma kilichoandikwa..

View attachment 2958239
Narudia Tena swala hiyo ilifanyika mahala panapoitwa Nakhl katika mwaka wa 5 wa utume ; Abu Huraira alikuwa hajasilimu kwa sababu alisilimu mwaka wa 7 wakati ilipotekwa ngome kuu ya Mayahudi Khaibar [kama Km 80 kaskazini mwa Madina]. Bado unabisha???

Haya tuache hapo twende kwenye Kumzulia Mtume, abu huraira kamzushia Mtume kasema kitu ilihali mtume hakusema Unataka muislam aisifie hiyo hadithi..

Au aseme kile Mnachojifunga nacho kuwa maswahaba wote ni wema???

Mwanzoni kwenye hadithi hii alisema kuwa Mtume alisema baada ya watu kumbana sana akasema ni maneno yake!..

Bado unataka Huyo mtu Nimuamini je vipi kadanganya kama hicho kasema watu wakashtuka je vingapi ambavyo hawakushtuka??

View attachment 2958244
Najua sunni mnafundishwa kuheshimu maswahaba nafahamu nilikuwa huko ila Usiwape hadhi ya Utume kama Shia wanavomfanya Ally..

Nataka Tuzungumzie matini ya Hadithi na sio Sanad kwa sababu naamini Bukhari ana sanad isiyo na shaka je hadithi zake (Kimatini "Kiriwaya")

Najua Kigezo unachotaka ni tuxungumzie kulingana na maumbile ya Matn na Isnad ya Hadith, kwamba hadithi ni Munkar au Mudraj..

Najua kwamba Hadithi nyingi za Sahih al bukhar Zina isnad nzuri kabisa na zenye mnyororo usiokatika mpaka kwa mtume..

Ila swali matini yake inaLeta maana na sio Mudraj..
Sasa huwezi kumsema swahaba kuwa ni muongo muda ambao hujaiweka wazi sanadi.

Uchambuzi huanzia katika Sanadi kwanza kisha unaingia katika matini kwa kurejea wanazuoni wa zamani wameizungumzia vipi hadithi husika.

Kwahiyo wewe utakuwa muongo na ni mzushi.
 
Hakuna mahali nimesema nimechambua ila umeniomba Hadithi Ambazo haziko.sahihi na ziko.kwenye Usahihi...

Na nimekupa Ila bado mpaka sasa hivi hujaniprove wrong kuwa hadithi hizo ni sahihi au sio sahihi?
UMeomba hadithi nimekupa sasa hivi umeanza sasa kuleta blah blah za Bukhar hana sanad nani kasema buhari ana sanadi..

Bukhar ni Mujitahidi tu na hata Level ya Taqlid hajafika..kwa hiyo atabaki kuwa Imam wa Hadithi tu..

Sio lazima useme kwamba umechambua, ila ulichokofanya ni uchambuzi wa uongo ambao haujakaa kielimu.

Sio jukumu langu kukuonyesha ya kuwa ni sahihi au dhaifu, bali nakukosoa wewe kutumia njia ambayo sio sahihi kudai swahaba Abuu Huraira kuwa ni muongo.

Naam nimeomba hadithi, ambayo kwa misingi ya elimu ya Hadithi bado hujaonyesha udhaifu au kutokuwa sahihi kwa hadithi hiyo, zaidi ya kuonyesha huna elimu ya Hadithi.

Wapi nimeandika ya kuwa Bukhari Hana sanadi ? Nimesema anazo sanadi, huwezi kudhoofisha hadithi bila kuwaangalia rawi wa hadithi husika.

Lakini vile vile unaweza kudhoofisha hadithi ikienda kinyume na itikadi sahihi ya Uislamu au ikienda kinyume na Qur'an. Sababu maswahaba wote ni waadilifu, unaweza kuhitimisha ya kuwa swahaba Abuu Huraira hawezi kusema maneno kinyume na mafundisho ya Mtume au kinyume na Qur'an.

Unajua maana ya Taqlid jifunze kutumia haya maneno vizuri.
 
Sasa huwezi kumsema swahaba kuwa ni muongo muda ambao hujaiweka wazi sanadi.

Uchambuzi huanzia katika Sanadi kwanza kisha unaingia katika matini kwa kurejea wanazuoni wa zamani wameizungumzia vipi hadithi husika.

Kwahiyo wewe utakuwa muongo na ni mzushi.
MKuu unazunguka ila Sijaona Kuhusu Jibu kuhusu Hadithi nilizokupa...maana Ziko wazi kabisa..
zijibu kwanza Hadithi hizo..

Maana nimeshakujibu Sanadi zao Hazina shaka ila matini ndo yana mashaka sasa hebu zijibu hizo matini acha Kuzunguka..

Je, Abu hurairah aliposema Mtume amesema na baadae watu walipomzonga kumuuliza Akiri mtu kasema na akabadilisha na kussma kassma yeye sio mtume hakudanganya?

Je, Abu hurarah aliposema aliswali swala ya Hofu na mtume mwaka wa 5 wa utume wakati Abu Huraira alikuwa hajasilimu kwa sababu alisilimu mwaka wa 7 wakati ilipotekwa ngome kuu ya Mayahudi Khaibar hakusema Uongo???

Au unaogopa Kusema Abu huraira Alisema uongo kwa sababu ndo anaongoza kwa isnad za Hadithi nyingi zaidi?
 
Sio lazima useme kwamba umechambua, ila ulichokofanya ni uchambuzi wa uongo ambao haujakaa kielimu.

Sio jukumu langu kukuonyesha ya kuwa ni sahihi au dhaifu, bali nakukosoa wewe kutumia njia ambayo sio sahihi kudai swahaba Abuu Huraira kuwa ni muongo.

Naam nimeomba hadithi, ambayo kwa misingi ya elimu ya Hadithi bado hujaonyesha udhaifu au kutokuwa sahihi kwa hadithi hiyo, zaidi ya kuonyesha huna elimu ya Hadithi.

Wapi nimeandika ya kuwa Bukhari Hana sanadi ? Nimesema anazo sanadi, huwezi kudhoofisha hadithi bila kuwaangalia rawi wa hadithi husika.

Lakini vile vile unaweza kudhoofisha hadithi ikienda kinyume na itikadi sahihi ya Uislamu au ikienda kinyume na Qur'an. Sababu maswahaba wote ni waadilifu, unaweza kuhitimisha ya kuwa swahaba Abuu Huraira hawezi kusema maneno kinyume na mafundisho ya Mtume au kinyume na Qur'an.

Unajua maana ya Taqlid jifunze kutumia haya maneno vizuri.
Kwanza siwezi kuzungumza maneno nisiyoyajua maana yake..

Pili Hadithi zote zinazosema Quran Imepunguzwa Aya Unaona ni sawa?

Hadithi zinazosema Quran Kulikuwa na Aya zingine ambazo Zilikuwepo na sasa hazipo zipo sawa?

Twende Kwenye Matini ya Hadithi hizo acha mbwembwe..

Nimekuambia katika Sanadi sheria Inafunga kusema kuwa Abu huraira Hadithi yake sio sahihi ila kwa matini yanatia shaka

ila Kuhusiana na utaalamu wa Hadith basi Imam Abu Ahmad Al Hasan bn Abd Rahman Ibn Khalal Al Farsy Al Ramhurmuzi ambae ni mtaalamu mkubwa wa mfumo wa makundi ya I’lm ya Hadith anasema kua ‘Abd Ar Rahman Ibn Al Mahdi amesema kua:

Wanahadith wako aina tatu: Aina ya kwanza ni wale ambao wenye kumbukumbu nzuri na wenye uangalifu, hawa hua hamna kutokukubaliana juu yao, wa pili ni wale ambao wanafanya makosa lakini Hadith zao ni Sahih na za uhakika, hawa hua haziachwi Hadith zao, na wa tatu ni wale ambao wanafanya makosa mengi sana katika Hadith zao na hawa Hadith zao hukataliwa (matrook).’

na Unataka Kujua maana ya Taqlid 😅😅..


MAANA YA TAQLID maana yake ni kufuata ushauri wa kisharia kutoka kwa mtu (ambae ushauri wake si uthibitisho katika Sharia’h ya kiislam) bila kutaka uthibitisho kutoka kwa mtu umfuatae. (Maana hiyo imetolewa kwenye Al-Mustasfa min usul al-Fiqh, Imam Al Ghazal)

Hii ina maana kua mtu afanyae Taqlid ambae kwa kilugha huitwa Muqallid hachukui ushauri wa yule aliefanya Ijtihad kua ni chanzo cha Sharia’h za Kiislam, kwani chanzo cha Sharia’h za kiislam ni Qur’an na Sunnah.

Sababu inayomfanya Muqallid kumfuata Mujtahid ni kuamini kua Mujtahid ana elimu na uwezo wa kuchambua Qur’an na Hadith ambao yeye Muqalid hua hana. Taqlid hufanywa katika mambo ya Fiqh.

Na Usisahau Fiqh imetokana Na Sunna na Quran Na Hadithi huwezi kuiacha


Bado narudia Tena Jibu maswali acha kukwepa Maswali
 
Back
Top Bottom