Ukweli hausemwi. Kilimo cha Parachichi ni kigumu sana na pesa yake ni ndogo

Ukweli hausemwi. Kilimo cha Parachichi ni kigumu sana na pesa yake ni ndogo

Nimefanya kilimo cha parachichi kwa miaka nane sasa, nilichokiona ni haya;

1. Kilimo kina mzunguko wake ni mdogo parachichi huzaa kidogo kidogo kadri miaka inavyoenda, unatumia million 10 unapata million mbili.
2. Bei hazijadiliki anayeamua ni mnunuzi unless uwe na mtaji mkubwa ambayo unakuruhusu ku export mwenyewe, na uwe na uwezo wa kuwa na cold room Ili zikikomaa uchume uzihifadhi kama bei hueilewi kwa kipindi hicho (hii mitaji watanzania wengi hatuna). 3. Management ya parachichi ni ngumu sana linahitaji maji kidogo (hapa unaweza manage kumwagilia) linahitaji mbolea za chumvi na mbolea za majani, sumu. Kila nk kwa kiasi kidogo, linahitaji muda Kwa wingi, upatikanaji wa Samadi ni mtihani sana (wengi wamejikuta parachichi zimedumaa na wengine wanazalisha reject kwa wingi) kisa tu wameshindwa kuwa na Samadi, udhibiti wa nyasi (ukweli ni kuwa Ili miti iwe Bora unahitaji kulima badala ya kufyeka nyasi)

Nimefanya observation shambani kwangu panapolimwa pana matokeo kuliko panapofyekwa, distance kati ya mti na mti inamua sana miti iliyokaribu inasumbua sana na mingi huwa haizai vizuri. Hizi issue zimefanya watu tukimbie mashamba yetu, hata kiwango cha pesa kinachotajwa wengi hawapati ni figure za uwongo Ili kujifariji, njoo na hoja zako kupinga zangu hapo juu, zangu ni hizo.

Nashauri kama una pesa zako kidogo lima mazao ya chakula tu viazi, mpunga, mahindi nk hivi vinalipa. Huku pesa ipo na kama location ulipo ni nzuri lima mazao yanayohifadhika like kahawa, miaka miwili inazaa, management yake rahisi. Nalima kahawa makete pia ni mwaka wa tatu tayari nimeanza kuvuna.

NB: Mazao ya chakula ndio kila kitu hizi nyingine tabu umezitafuta.
Ni hakilipi kwa Tanzania pekee au Dunia nzima? Shida iko hapo, Ukifuatilia Wakenya wanakimbizana na Parachichi balaa.
 
Amna kilimo rahisi mkuu,ukishaamua kuwa mkulima we kuwa chizi kilimo,lima mazao mengi tofauti tofauti,lima katani,lima korosho,lima parachichi,lima machungwa utatoboa tu moja likizingua lingine linakulipa maisha yanasonga.

Kilimo ni dynamic just imagine unazalisha kitu usicho kuwa na uwezo wa kuconsume in any how...sasa si kamali hiyo
 
Nimefanya kilimo cha parachichi kwa miaka nane sasa, nilichokiona ni haya;

1. Kilimo kina mzunguko wake ni mdogo parachichi huzaa kidogo kidogo kadri miaka inavyoenda, unatumia million 10 unapata million mbili.
2. Bei hazijadiliki anayeamua ni mnunuzi unless uwe na mtaji mkubwa ambayo unakuruhusu ku export mwenyewe, na uwe na uwezo wa kuwa na cold room Ili zikikomaa uchume uzihifadhi kama bei hueilewi kwa kipindi hicho (hii mitaji watanzania wengi hatuna). 3. Management ya parachichi ni ngumu sana linahitaji maji kidogo (hapa unaweza manage kumwagilia) linahitaji mbolea za chumvi na mbolea za majani, sumu. Kila nk kwa kiasi kidogo, linahitaji muda Kwa wingi, upatikanaji wa Samadi ni mtihani sana (wengi wamejikuta parachichi zimedumaa na wengine wanazalisha reject kwa wingi) kisa tu wameshindwa kuwa na Samadi, udhibiti wa nyasi (ukweli ni kuwa Ili miti iwe Bora unahitaji kulima badala ya kufyeka nyasi)

Nimefanya observation shambani kwangu panapolimwa pana matokeo kuliko panapofyekwa, distance kati ya mti na mti inamua sana miti iliyokaribu inasumbua sana na mingi huwa haizai vizuri. Hizi issue zimefanya watu tukimbie mashamba yetu, hata kiwango cha pesa kinachotajwa wengi hawapati ni figure za uwongo Ili kujifariji, njoo na hoja zako kupinga zangu hapo juu, zangu ni hizo.

Nashauri kama una pesa zako kidogo lima mazao ya chakula tu viazi, mpunga, mahindi nk hivi vinalipa. Huku pesa ipo na kama location ulipo ni nzuri lima mazao yanayohifadhika like kahawa, miaka miwili inazaa, management yake rahisi. Nalima kahawa makete pia ni mwaka wa tatu tayari nimeanza kuvuna.

NB: Mazao ya chakula ndio kila kitu hizi nyingine tabu umezitafuta.
Binafsi huwa sina imani sana na mazao yanayotegemea mnunuzi mmoja tena wa nnje ya nchi,mazao ya chakula soko lake liko huru sana, ni nguvuzako tu mwenyewe.
 
Binafsi huwa sina imani sana na mazao yanayotegemea mnunuzi mmoja tena wa nnje ya nchi,mazao ya chakula soko lake liko huru sana, ni nguvuzako tu mwenyewe.
Mbona bado Parachichi linahitaji hata huku nchini. Binafsi nimepanda huku Rungwe na kule Kilolo Iringa. Mengi umesema kweli hususan kwenye gharama za kulihudumia. Kuhusu soko, linacheza kwa kulingana na mwaka/msimu na soko la Dunia. Binafsi nimeyatrain maparachichi yangu so huwa naona mwezi wa 9 hadi 11 (OFF SEASON) ambapo duniani hakuna Parachichi so soko huwa la uhakika na ninapiga Bingo hapo. Kikubwa uwe na source ya maji ya uhakika tu mkuu.
 
Ukitumia akili kwenye jambo lolote unalofanya utakwepa mishale kama hii. Nimesoma na kufuatilia sana parachichi kwa China na nimekubali ni biashara ngumu sana.
1. Soko lake kubwa hasa hizo Hass ni China ambapo wao soko lao linapanda na kushuka kutokana na supply wanayopata kutoka Mexico, Kenya, Australia na zaidi ya nusu kutoka Peru. Ikitokea ni msimu wa Peru huko kwingineko bei inashuka sana, muda wa kupiga hela ni pale nchi nyingine zinapokuwa sio msimu.
China iko busy kujitosheleza kwenye parachichi kwahiyo soko litazidi kupungua, na uzuri wa China ni nchi kubwa yenye usawa wa bahari tofauti sana kila eneo hivyo kila upande unaweza zalisha kwa msimu wake na zikawa sokoni mwaka mzima.

2. Teknolojia hatuna. Unavuna parachichi unapakia kwenye fuso utamuuzia nani uko nje? Hamna cold rooms, hamna grading, hakuna refrigerated trucks, hamna kupima quality, water content, protein, texture, ile nyama ya ndani, mbolea haipimwi, ardhi wanatifua tu hata hawajui ardhi gani ina nini na inakosa nini. Tunaenda kienyeji.

3. Serikali inasubiri kutoza ushuru na kodi, yenyewe hata haijui hiyo biashara na kilimo chake inafanyikaje. Hakuna support kabisa sababu parachichi zikiachwa nchi haitokufa njaa.

4. Ni zao lenye usumbufu na linataka mtaji mkubwa. Wakati huo haliuziki ndani, ukikosa soko la nje ukauza ndani unakula hasara kutokana na gharama kubwa za uendeshaji.

5. Ni zao gumu sana kuuzwa, yani hawa walanguzi wetu wakienda nje uko wanapigwa za uso kirahisi sana. Unatafuta certifications za ubora na kila kitu unapeleka msimu huu, msimu ujao unaweka mtaji wote then Wachina wanapima wanakuta water content kubwa kisa mvua zilizidi uko Niombe. Zinamwagwa, huyo mfanyabiashara atarudi?
Mwaka juzi Wakenya walizuiwa na TFDA ya China kwamba kuna mlipuko wa fruit flies parachichi zao zinaenda na mayai yake. Wakaambiwa ukitaka kuuza menya uuze ile nyama ya ndani. Sasa process ya kumenya na kuuza nyama ya ndani alafu hiyo nyama isiwe nyeusi hata kidogo sio kazi ya kitoto.

Haya yote nimeyajua nikiwa sina mpango wa kulima, ningetaka kulima ningejua mengi zaidi. Sasa mkulima yeye akisikia kwenye redio anaamka na kufyeka eneo atengeneze shamba. Content creators ile ndio kazi yao, kuongea. Usikubali kushikwa masikio
Nchi za wenzetu zinajali sana walaji.

Tanzania ni nchi ambayo haijali walaji ndio maana Matunda huanguliwa na kupakiwa kwenye mafuso

Nchi zingine mf Marekani nimewahi fatilia youtube kila bidhaa lazima ipite kiwandani kusafishwa na kuwa packed kuanzia machungwa hadi vitunguu lazima viwe packed.

Huku kwetu nenda pale Mahakama ya Ndizi Mabibo utaweza acha kula ndizi

Nenda Temeke, Tegeta Nyuki hakika huwezi kula.

Madawa mengi sana hutumika muda mfupi kabla ya kuvuna, nina Nyanya nimekaa nazo Mwezi na siku 2 haziozi hadi nikazitupa hazina funza wala nini
 
Nadhani ni mwaka juzi, wilaya ya Rungwe walipatapata kidogo kilo ilikua bei.

Ila mwaka huu ni kulia na kisaga meno, unaambiwa parachichi linauzwa kwa viroba na sio kilo tena.

Parachichi sio kilimo cha kukimbilia saivi, wengi walifyeka mapori walime parachichi ila ndo ivo wamepigwa za uso.
Theories za supply na demand ndizo zimeyumbisha hiyo biashara kwa kiasi kikubwa,
The higher the supply the lower the demand
 
Nadhani ni mwaka juzi, wilaya ya Rungwe walipatapata kidogo kilo ilikua bei.

Ila mwaka huu ni kulia na kisaga meno, unaambiwa parachichi linauzwa kwa viroba na sio kilo tena.

Parachichi sio kilimo cha kukimbilia saivi, wengi walifyeka mapori walime parachichi ila ndo ivo wamepigwa za uso.
Tuliwaonya Rungwe walipokua wanakata migomba ili kuanzisha kilimo cha parachichi. Binafsi niliwaambia waww makini, wasikimbilie wote huko , kwani kwa wingi wanaoenda nao itapelekea zao hilo lipatikane kwa wingi na hivyo kushuka thamani.
Zaidi kwa kuwa hawana access na soko, wao wanajikuta wanalima ili kujazilizia demands za yule mzungu mwenye access na soko, na wakishakuwa wenggi wataishia kumfaidisha huku wao wakudumaa
 
Tuliwaonya Rungwe walipokua wanakata migomba ili kuanzisha kilimo cha parachichi. Binafsi niliwaambia waww makini, wasikimbilie wote huko , kwani kwa wingi wanaoenda nao itapelekea zao hilo lipatikane kwa wingi na hivyo kushuka thamani.
Zaidi kwa kuwa hawana access na soko, wao wanajikuta wanalima ili kujazilizia demands za yule mzungu mwenye access na soko, na wakishakuwa wenggi wataishia kumfaidisha huku wao wakudumaa
Migomba ilifyekwa mno, misitu ikachomwa moto na kuvunwa hovyo ili wapande maparachichi.

Kwa maana waliopanda mwaka juzi saivi wanalia tu,parachichi liliwafaidisha wale watu wa mwanzo kabisa miaka ya 2011 kidogo mpaka mwaka juzi.
 
Back
Top Bottom