Ukweli hausemwi. Kilimo cha Parachichi ni kigumu sana na pesa yake ni ndogo

Ukweli hausemwi. Kilimo cha Parachichi ni kigumu sana na pesa yake ni ndogo

Tuliwaonya Rungwe walipokua wanakata migomba ili kuanzisha kilimo cha parachichi. Binafsi niliwaambia waww makini, wasikimbilie wote huko , kwani kwa wingi wanaoenda nao itapelekea zao hilo lipatikane kwa wingi na hivyo kushuka thamani.
Zaidi kwa kuwa hawana access na soko, wao wanajikuta wanalima ili kujazilizia demands za yule mzungu mwenye access na soko, na wakishakuwa wenggi wataishia kumfaidisha huku wao wakudumaa
Kama ulimsoma Napolean Hill ktk kitabu chake How to be rich.
Yeye anasema, ukiona umeanguka kwenye biashara basi fanya mara mbili yake.
Wale wasiojua structure of the markert and how it operate watajitoa taratibu na kubaki wajasilia mali halisi.
Mimi chuoni nilijifunza kwamba kila kitu kina utitiri hivyo ni wewe kushindindana na utitiri, na tatizo sio kuzalisha bali kuzalisha bidhaa bora na kuuza.
Marketing and selling is everything in business and entrepreneurship.
Ukishindwa kuuza wewe unakosa sifa za mjasiliamsli.
AVOCADO ni industrial crop sasa iweje ioze wakati ni bidhaa ya kiviwanda?
Sisi kama vijana tunatakiwa to innovate different products tuache ujinga wa kusubiri wazungu,wahindi, warabu na wachina kufikiri kwa niaba yetu.
I have alternative for my Avocado.
Bahati mbaya sijaanza kuuza zangu kushuhudia zinavyooza kwa kukosa wateja, ila parachichi zangu hazitaoza.
Ukichunguza uzalishaji wa Avocado ni subsistence agriculture, yaani ni tushamba twa kuokoteza ispokuwa Rungwe Company.
Sasa iweje unishawishi eti Avocado zimezalishwa sana wakati vishamba ni vya kuokoteza?
Avocado agriculture bado sans sana ktk ukubw, yani bado inaachwa na machungwa,chai, nduzi, miwa nk.
Mimi natamani nione mkulima mmoja walau minimum awe na heka 10.
Tujiuliza kikijengwa kiwanda kikubwa kitapata AVOCADO mda wote?
 
Ukitumia akili kwenye jambo lolote unalofanya utakwepa mishale kama hii. Nimesoma na kufuatilia sana parachichi kwa China na nimekubali ni biashara ngumu sana.
1. Soko lake kubwa hasa hizo Hass ni China ambapo wao soko lao linapanda na kushuka kutokana na supply wanayopata kutoka Mexico, Kenya, Australia na zaidi ya nusu kutoka Peru. Ikitokea ni msimu wa Peru huko kwingineko bei inashuka sana, muda wa kupiga hela ni pale nchi nyingine zinapokuwa sio msimu.
China iko busy kujitosheleza kwenye parachichi kwahiyo soko litazidi kupungua, na uzuri wa China ni nchi kubwa yenye usawa wa bahari tofauti sana kila eneo hivyo kila upande unaweza zalisha kwa msimu wake na zikawa sokoni mwaka mzima.

2. Teknolojia hatuna. Unavuna parachichi unapakia kwenye fuso utamuuzia nani uko nje? Hamna cold rooms, hamna grading, hakuna refrigerated trucks, hamna kupima quality, water content, protein, texture, ile nyama ya ndani, mbolea haipimwi, ardhi wanatifua tu hata hawajui ardhi gani ina nini na inakosa nini. Tunaenda kienyeji.

3. Serikali inasubiri kutoza ushuru na kodi, yenyewe hata haijui hiyo biashara na kilimo chake inafanyikaje. Hakuna support kabisa sababu parachichi zikiachwa nchi haitokufa njaa.

4. Ni zao lenye usumbufu na linataka mtaji mkubwa. Wakati huo haliuziki ndani, ukikosa soko la nje ukauza ndani unakula hasara kutokana na gharama kubwa za uendeshaji.

5. Ni zao gumu sana kuuzwa, yani hawa walanguzi wetu wakienda nje uko wanapigwa za uso kirahisi sana. Unatafuta certifications za ubora na kila kitu unapeleka msimu huu, msimu ujao unaweka mtaji wote then Wachina wanapima wanakuta water content kubwa kisa mvua zilizidi uko Niombe. Zinamwagwa, huyo mfanyabiashara atarudi?
Mwaka juzi Wakenya walizuiwa na TFDA ya China kwamba kuna mlipuko wa fruit flies parachichi zao zinaenda na mayai yake. Wakaambiwa ukitaka kuuza menya uuze ile nyama ya ndani. Sasa process ya kumenya na kuuza nyama ya ndani alafu hiyo nyama isiwe nyeusi hata kidogo sio kazi ya kitoto.

Haya yote nimeyajua nikiwa sina mpango wa kulima, ningetaka kulima ningejua mengi zaidi. Sasa mkulima yeye akisikia kwenye redio anaamka na kufyeka eneo atengeneze shamba. Content creators ile ndio kazi yao, kuongea. Usikubali kushikwa masikio
Mkuu
umenena yaliyo kweli kabisaa
kuna mwekezaji alikuja RUNGWE watu walikata mpaka kahawa wakaotesha parachichi
mwaka huu, wakulima wa parachichi mbeya wanalia,,mpaka serekali ya wilaya inawaomba wanunuzi waende.....wakajitokeza wakulima wakachangishana wakapeleka parachichi Njombe na FUSO KADHAA, wamefikisha wakapokelewa,,,ukaguzi umefanyika parachichi zikawa rejected zote tena wakaingia garama tena ya kwenda kutupa

Hiki kilimo kwa NJOMBE waliopiga pesa ni wale waliowahi wakauza MBEGU na wanaosoma ramani TU

Inahitajika ELIMU, mtaji wa kutosha na MUDA otherwise bora tufuge SAMAKI TU wanasema zinalipa
 
Nchi za wenzetu zinajali sana walaji.

Tanzania ni nchi ambayo haijali walaji ndio maana Matunda huanguliwa na kupakiwa kwenye mafuso

Nchi zingine mf Marekani nimewahi fatilia youtube kila bidhaa lazima ipite kiwandani kusafishwa na kuwa packed kuanzia machungwa hadi vitunguu lazima viwe packed.

Huku kwetu nenda pale Mahakama ya Ndizi Mabibo utaweza acha kula ndizi

Nenda Temeke, Tegeta Nyuki hakika huwezi kula.

Madawa mengi sana hutumika muda mfupi kabla ya kuvuna, nina Nyanya nimekaa nazo Mwezi na siku 2 haziozi hadi nikazitupa hazina funza wala nini
Hiyo ipo, lakini kwenye hivi vitu aisee kuna mbegu za aina nyingi sana. Wiki iliyopita nimeanzisha mradi wa bustani bamia, karoti, nyanya, nyanya chungu, spinachi, mchicha, chaina, matango, tikiti maji, sukuma wiki, pilipili.

Wakati naenda mjini kununua mbegu huko ndiko nilishangaa kukutana na mbegu za maajabu, aisee kuna bamia tangu nizaliwe sijawahi kuziona, ni kubwa kama tango. Wakati wa kununua mbegu za nyanya yule mzee kanipa za aina tatu hivi ila moja wapo kaniambia hiyo mbegu nyanya zake hukaa hata miezi miwili bila kuharibika baadae huwa ni kama zinanyauka vile. Na kuna mbegu zingine za nyanya japo sikuweza kuinua kutokana na bei yake kuwa juu kaniambia hii mbegu ukipanda unauwezo wa kuvuna nyanya zaidi ya miezi mitano
 
Hivi kuna kilimo ambacho hakina changamoto, ukienda kulima mahindi unakutana na hali ya hewa na soko, ukienda kulima mpunga utasikia mwaka huu mvua zimekata, kilimo cha kitanzania ni cha uwendawazimu uelewe hilo
Mahindi ni kilimo cha muda mfupi na una alternative, ni tofauti na Parachichi

Ardhi ya Tanzania ni nzuri sana kwa kilimo cha mazao mengi, tatizo la Tanzania ni KUKOSA MTAJI HASA NA KUTOKUWA NA TEKNOLOJIA YA KILIMO.
 
Kwa hiyo kahawa, mahindi, mpunga na viazi ni mazao ya chakula, sio mazao ya biashara, yani hayauziki!

Na parachichi ni zao la biashara, sio zao la chakula, kwa hiyo parachichi haliliki!

Unajua wale walimu wa primary wale walitukaririsha madudu mengi vichwani, tulikuwa hatujielewi na wao hawajielewi masikini ya Mungu!
Kila zao ni la biashara, ila si kila zao ni la chakula kama tumbaku.
 
Nimefanya kilimo cha parachichi kwa miaka nane sasa, nilichokiona ni haya;

1. Kilimo kina mzunguko wake ni mdogo parachichi huzaa kidogo kidogo kadri miaka inavyoenda, unatumia million 10 unapata million mbili.
2. Bei hazijadiliki anayeamua ni mnunuzi unless uwe na mtaji mkubwa ambayo unakuruhusu ku export mwenyewe, na uwe na uwezo wa kuwa na cold room Ili zikikomaa uchume uzihifadhi kama bei hueilewi kwa kipindi hicho (hii mitaji watanzania wengi hatuna). 3. Management ya parachichi ni ngumu sana linahitaji maji kidogo (hapa unaweza manage kumwagilia) linahitaji mbolea za chumvi na mbolea za majani, sumu. Kila nk kwa kiasi kidogo, linahitaji muda Kwa wingi, upatikanaji wa Samadi ni mtihani sana (wengi wamejikuta parachichi zimedumaa na wengine wanazalisha reject kwa wingi) kisa tu wameshindwa kuwa na Samadi, udhibiti wa nyasi (ukweli ni kuwa Ili miti iwe Bora unahitaji kulima badala ya kufyeka nyasi)

Nimefanya observation shambani kwangu panapolimwa pana matokeo kuliko panapofyekwa, distance kati ya mti na mti inamua sana miti iliyokaribu inasumbua sana na mingi huwa haizai vizuri. Hizi issue zimefanya watu tukimbie mashamba yetu, hata kiwango cha pesa kinachotajwa wengi hawapati ni figure za uwongo Ili kujifariji, njoo na hoja zako kupinga zangu hapo juu, zangu ni hizo.

Nashauri kama una pesa zako kidogo lima mazao ya chakula tu viazi, mpunga, mahindi nk hivi vinalipa. Huku pesa ipo na kama location ulipo ni nzuri lima mazao yanayohifadhika like kahawa, miaka miwili inazaa, management yake rahisi. Nalima kahawa makete pia ni mwaka wa tatu tayari nimeanza kuvuna.

NB: Mazao ya chakula ndio kila kitu hizi nyingine tabu umezitafuta.


Kukurupukia hizi mambo shida sana, pole.
 
Watanzania twapenda kurupuka na wazee wa fursa
Wazee wa fursa ni wahuni sana. Wanalimia kwenye daftari na kupeleka taarifa za uongo Instagram na Facebook.

Miaka michache iliyopita walieneza taarifa za uongo kwamba ekari moja ya matikiti mtu anaweza kupata milioni 20 kwa mtaji wa shilingi 2M-3M.

Watu wakakuripuka, wakaangukia pua.
 
Katika Mazao yote Ya Matunda yanayolimwa Tanzania, Wakulima wa Machungwa wanapiga hela kama Mkulima atakua Mtulivu, kilimo hiki Hakina siasa, Mtu mwenye heka Moja ya michungwa aina ya Valencia imbayo imechanganya kuzaa, kupata kuanzia milioni 6 ni mambo la kawaida, tunachoomba Mungu siasa isije ikaingia huku ,Tukaanza kuundiwa bodi,
Watu wanauza mpaka Tsh 100 kwa chungwa Moja bei ya Shamba kama unakua na Uvumilivu na unauza huku unaringa
Mkuu tusaidie location ya huko uliko ili na sisi tuhame huku kwenye parachuchi
 
Migomba ilifyekwa mno, misitu ikachomwa moto na kuvunwa hovyo ili wapande maparachichi.

Kwa maana waliopanda mwaka juzi saivi wanalia tu,parachichi liliwafaidisha wale watu wa mwanzo kabisa miaka ya 2011 kidogo mpaka mwaka juzi.
Bila shaka ulikusudia kuandika 2021??
 
Je ukikomaa na soko la ndani tu je hailipi kweli kama wadau wanavyosema?
Mwaka huu nina project ya heka 20 na watu wana toa tahadhari nami siwezi puuza.
Mkuu soko la ndani limetawaliwa na wahuni na linaendeshwa kihuni, hivyo utapata hasara tu. Walanguzi kipimo chao ni kiroba cha kilo 25 unalipwa efu 3 au 5. Hutaki baki nayo.
 
Back
Top Bottom