Ukweli hausemwi. Kilimo cha Parachichi ni kigumu sana na pesa yake ni ndogo

Ukweli hausemwi. Kilimo cha Parachichi ni kigumu sana na pesa yake ni ndogo

Katika Mazao yote Ya Matunda yanayolimwa Tanzania, Wakulima wa Machungwa wanapiga hela kama Mkulima atakua Mtulivu, kilimo hiki Hakina siasa, Mtu mwenye heka Moja ya michungwa aina ya Valencia imbayo imechanganya kuzaa, kupata kuanzia milioni 6 ni mambo la kawaida, tunachoomba Mungu siasa isije ikaingia huku ,Tukaanza kuundiwa bodi,
Watu wanauza mpaka Tsh 100 kwa chungwa Moja bei ya Shamba kama unakua na Uvumilivu na unauza huku unaringa
Soko la uhakika ni la ndani tu
 
Nashauri kama una pesa zako kidogo lima mazao ya chakula tu viazi, mpunga, mahindi nk hivi vinalipa. Huku pesa ipo na kama location ulipo ni nzuri lima mazao yanayohifadhika like kahawa, miaka miwili inazaa, management yake rahisi. Nalima kahawa makete pia ni mwaka wa tatu tayari nimeanza kuvuna.

Kwa hiyo kahawa, mahindi, mpunga na viazi ni mazao ya chakula, sio mazao ya biashara, yani hayauziki!

Na parachichi ni zao la biashara, sio zao la chakula, kwa hiyo parachichi haliliki!

Unajua wale walimu wa primary wale walitukaririsha madudu mengi vichwani, tulikuwa hatujielewi na wao hawajielewi masikini ya Mungu!
 
Parachichi unazolima ni hizi za biashara?? mfano; Hass avocados, Fuerte avocados Au ni nyingine..maana hizo ni rahisi kufanya biashara maana zinaenda nje japo kuna parameters zake zinahitaji ufuatiliaji wa umakini.
Ila kama unalima parachichi kwa kulenga soko la hapa hapa ndani aiseeh ni hasara.
Hizo za biashara ulime kiutaalamu ukifuata international standards na kuzikatikia certificates kabisa kama GlobalGap certifices e.t.c mbona makampuni yatakufata menyew.
 
Katika Mazao yote Ya Matunda yanayolimwa Tanzania, Wakulima wa Machungwa wanapiga hela kama Mkulima atakua Mtulivu, kilimo hiki Hakina siasa, Mtu mwenye heka Moja ya michungwa aina ya Valencia imbayo imechanganya kuzaa, kupata kuanzia milioni 6 ni mambo la kawaida, tunachoomba Mungu siasa isije ikaingia huku ,Tukaanza kuundiwa bodi,
Watu wanauza mpaka Tsh 100 kwa chungwa Moja bei ya Shamba kama unakua na Uvumilivu na unauza huku unaringa
Mkuu unaweza ni connect na mkulima wa machungwa wa aina hiyo ya valencia?
 
Ukitumia akili kwenye jambo lolote unalofanya utakwepa mishale kama hii. Nimesoma na kufuatilia sana parachichi kwa China na nimekubali ni biashara ngumu sana.
1. Soko lake kubwa hasa hizo Hass ni China ambapo wao soko lao linapanda na kushuka kutokana na supply wanayopata kutoka Mexico, Kenya, Australia na zaidi ya nusu kutoka Peru. Ikitokea ni msimu wa Peru huko kwingineko bei inashuka sana, muda wa kupiga hela ni pale nchi nyingine zinapokuwa sio msimu.
China iko busy kujitosheleza kwenye parachichi kwahiyo soko litazidi kupungua, na uzuri wa China ni nchi kubwa yenye usawa wa bahari tofauti sana kila eneo hivyo kila upande unaweza zalisha kwa msimu wake na zikawa sokoni mwaka mzima.

2. Teknolojia hatuna. Unavuna parachichi unapakia kwenye fuso utamuuzia nani uko nje? Hamna cold rooms, hamna grading, hakuna refrigerated trucks, hamna kupima quality, water content, protein, texture, ile nyama ya ndani, mbolea haipimwi, ardhi wanatifua tu hata hawajui ardhi gani ina nini na inakosa nini. Tunaenda kienyeji.

3. Serikali inasubiri kutoza ushuru na kodi, yenyewe hata haijui hiyo biashara na kilimo chake inafanyikaje. Hakuna support kabisa sababu parachichi zikiachwa nchi haitokufa njaa.

4. Ni zao lenye usumbufu na linataka mtaji mkubwa. Wakati huo haliuziki ndani, ukikosa soko la nje ukauza ndani unakula hasara kutokana na gharama kubwa za uendeshaji.

5. Ni zao gumu sana kuuzwa, yani hawa walanguzi wetu wakienda nje uko wanapigwa za uso kirahisi sana. Unatafuta certifications za ubora na kila kitu unapeleka msimu huu, msimu ujao unaweka mtaji wote then Wachina wanapima wanakuta water content kubwa kisa mvua zilizidi uko Niombe. Zinamwagwa, huyo mfanyabiashara atarudi?
Mwaka juzi Wakenya walizuiwa na TFDA ya China kwamba kuna mlipuko wa fruit flies parachichi zao zinaenda na mayai yake. Wakaambiwa ukitaka kuuza menya uuze ile nyama ya ndani. Sasa process ya kumenya na kuuza nyama ya ndani alafu hiyo nyama isiwe nyeusi hata kidogo sio kazi ya kitoto.

Haya yote nimeyajua nikiwa sina mpango wa kulima, ningetaka kulima ningejua mengi zaidi. Sasa mkulima yeye akisikia kwenye redio anaamka na kufyeka eneo atengeneze shamba. Content creators ile ndio kazi yao, kuongea. Usikubali kushikwa masikio
Mkuu safi sana umezungumza vizur sana..hii biashara ya mazao unaijua vizur na nimfatiliaji.
 
Kilimo kina wenyewe. Ukitaka kufanikiwa kwenye Kilimo basi fanya partnership na mkulima mzoefu wewe ongeza mtaji wa mbolea kukodi mashamba zaidi na pembejeo kwa ujumla.wake alafu huyo mtaalamu mzoefu mwache aendeshe shamba hapo ndio utaona utamu wa kilimo, ila hiki kilimo chenu cha kupost picha whatsapp na twitter sehemu kubwa ni uongo uongo tu wa kwenye picha kwa groung ni different story.
 
Mbona bado Parachichi linahitaji hata huku nchini. Binafsi nimepanda huku Rungwe na kule Kilolo Iringa. Mengi umesema kweli hususan kwenye gharama za kulihudumia. Kuhusu soko, linacheza kwa kulingana na mwaka/msimu na soko la Dunia. Binafsi nimeyatrain maparachichi yangu so huwa naona mwezi wa 9 hadi 11 (OFF SEASON) ambapo duniani hakuna Parachichi so soko huwa la uhakika na ninapiga Bingo hapo. Kikubwa uwe na source ya maji ya uhakika tu mkuu.
Mkuu nilijiuliza hilo swali kwamba lazima parachichi zizae kwa pamoja mbona viumbe vingine vinazaliwa siku moja ila vina mature tofauti. Naomba hoo elimu ya kuzifundisha zizae mda naotaka.
Zangu ndio zipo hatua ya maua ya pili.
Nalimia njombe ba huku changamoto kubwa ni barafu na jua.
Je ukikomaa na soko la ndani tu je hailipi kweli kama wadau wanavyosema?
Mwaka huu nina project ya heka 20 na watu wana toa tahadhari nami siwezi puuza.
 
Kwa hiyo kahawa, mahindi, mpunga na viazi ni mazao ya chakula, sio mazao ya biashara, yani hayauziki!

Na parachichi ni zao la biashara, sio zao la chakula, kwa hiyo parachichi haliliki!

Unajua wale walimu wa primary wale walitukaririsha madudu mengi vichwani, tulikuwa hatujielewi na wao hawajielewi masikini ya Mungu!
According to code of conduct from college desa, it state that " teach the syllabus, don't teach your ideas!".
Walaumu wakuza mitaala.
 
Back
Top Bottom