Ukweli kuhusu Israel, Waarabu, na Ibrahim

Ukweli kuhusu Israel, Waarabu, na Ibrahim

Nani kasema Musa Pharaoh na Musa ni waarabu.... Acha kukurupuka, rudia soma kisha uelewe, ukichukua point bila kusoma kwa umakini lazima upuyange kama unavyopuyanga sasa
Kichwa chako ni kizito kama asili ya hiyo jina lako. hata mimi sikusema Musa ni Maarabu. Ulikuwa unatulazimisha kuwa Musa klazaliwa katika nchi ya waarabu wakati enzi za Musa Misri ilikuwa lkwa Mafarao weusi tii wa jamii za Kusubi. Nilichosema ni kuwa kama Hajiri ni Mmisri basi hawezi kuwa Muaarabu maana zama hizo misri haikuwa na waarabu.
 
So Israel na Waarabu ni baba mmoja ila mama tofauti. Ibrahim alizaa na Muisrael mwenzake kwa kipindi hicho ilikuwa bado haijaitwa Israel na mtoto wake kuitwa Isaka ila yule aliyezaa na kijakazi ambaye ni Mwarabu anaitwa Ishmael. Tatizo kubwa la vita baina ya Mwarabu na Israel ni hapa.
Naomba kufahamu aliyekaribia kuchinjwa na Ibrahim ili kumtoa sadaka ni nani kati ya hao wawili?
Mara kadhaa nimesikia Masheikh wakisema katika ile sikukuu ya kuchinja kwamba Ismail alinusurika kuchinjwa kwaajili ya sadaka ya baba yake, wakristo wanasema Ismail aliondoka Israel kwenda kwao na Mama yake Hajir akiwa mdogo sana ikimaanisha Ibrahim hakuwa na huyo mtoto wakati akienda kutoa sadaka ya kuchinja. Je ukweli ni upi?
 
Kichwa chako ni kizito kama asili ya hiyo jina lako. hata mimi sikusema Musa ni Maarabu. Ulikuwa unatulazimisha kuwa Musa klazaliwa katika nchi ya waarabu wakati enzi za Musa Misri ilikuwa lkwa Mafarao weusi tii wa jamii za Kusubi. Nilichosema ni kuwa kama Hajiri ni Mmisri basi hawezi kuwa Muaarabu maana zama hizo misri haikuwa na waarabu.
Uarabu kwa ismail unatokana na yeye kwenda kukaa huko kwenye Penisula ya uarabuni na akaoa huko uarabuni na kupitia ismail koo nyingi na kabila nyingi zilitengenezwa na kwa sababu Mungu aliweka agano na Abraham kuwa atakuwa Baba wa mataifa mengi basi Waarabu wao wakaona Taifa lao limetokana na ismail, wakamwita Baba wa waarabu
 
Uarabu kwa ismail unatokana na yeye kwenda kukaa huko kwenye Penisula ya uarabuni na akaoa huko uarabuni na kupitia ismail koo nyingi na kabila nyingi zilitengenezwa na kwa sababu Mungu aliweka agano na Abraham kuwa atakuwa Baba wa mataifa mengi basi Waarabu wao wakaona Taifa lao limetokana na ismail, wakamwita Baba wa waarabu
Sahihi kabisa. uwe unaleta masomo yanayojieleza vizuri kama hapa. big up!
 
Naomba kufahamu aliyekaribia kuchinjwa na Ibrahim ili kumtoa sadaka ni nani kati ya hao wawili?
Mara kadhaa nimesikia Masheikh wakisema katika ile sikukuu ya kuchinja kwamba Ismail alinusurika kuchinjwa kwaajili ya sadaka ya baba yake, wakristo wanasema Ismail aliondoka Israel kwenda kwao na Mama yake Hajir akiwa mdogo sana ikimaanisha Ibrahim hakuwa na huyo mtoto wakati akienda kutoa sadaka ya kuchinja. Je ukweli ni upi?
Kwa mujibu wa kitabu cha Kiyahudi torati ambayo Biblia nayo ikiambatana.... Vinasema kuwa Ibrahim alikuwa na watoto wawili ambao ni Isaka na Ismail. Ismail ni mtoto aliyepatikana nje ya Ndoa baada ya kukaa muda mrefu bila Sara kupata ujauzito, hivyo hajir akachaguliwa na sara hili wapate mtoto. Lakini badae baada ya kilio cha muda mrefu Mungu akawabariki mtoto naye wakamwita Isaka, na Ibrahim akampenda sana huyo mtoto badae Mungu akataka Isaac atolewe sadaka kwa sababu alimtii Mungu ikabidi aende kumtoa Isaka sadaka kwa moyo mmoja, lakini badae akatokea malaika na kumuonesha kondoo kama mbadala... Kutokana na kitendo cha utiifu na imani kwa mungu na kuthubutu kwenda kumtoa Mwanae aliyempenda na aliyempata kwa shida basi Mungu akambariki na kumwambia utakuwa baba wa mataifa mengi na mataifa yatatoka kwako
 
Hajira alikua Mmisri kumbuka accient time Khemet waliishi Blacks soma historia vizuri
hajra alikua Mweusi tii kama hao South Sudan people ambao chimbuko lao ni Kemet na Kush kwa Nubian
waarabu walihamia hapo misri miaka ya juzi AD na sio BC!
mkuu Mhaya pitia madesa vizuri Ismail hajawahi kua Mwarabu ila ni Chotara la Babylon na Kemet na alikua half Black!
 
Mungu akataka Isaac atolewe sadaka kwa sababu alimtii Mungu ikabidi aende kumtoa Isaka sadaka kwa moyo mmoja, lakini badae akatokea malaika na kumuonesha kondoo kama mbadala... Kutokana na kitendo cha utiifu na imani kwa mungu na kuthubutu kwenda kumtoa Mwanae aliyempenda na aliyempata kwa shida basi Mungu akambariki na kumwambia utakuwa baba wa mataifa mengi na mataifa yatatoka kwako
Hapa ndipo nashindwa kumuelewa Mungu, kwanini aliingiwa na tamaa hiyo ya kuua?
 
Mungu akataka Isaac atolewe sadaka kwa sababu alimtii Mungu ikabidi aende kumtoa Isaka sadaka kwa moyo mmoja, lakini badae akatokea malaika na kumuonesha kondoo kama mbadala... Kutokana na kitendo cha utiifu na imani kwa mungu na kuthubutu kwenda kumtoa Mwanae aliyempenda na aliyempata kwa shida basi Mungu akambariki na kumwambia utakuwa baba wa mataifa mengi na mataifa yatatoka kwako
Natamani ningesikia kutoka kwa Shosti FaizaFoxy maana upande wake unazungumza tofauti haumtaji Isihaka unamtaja Ismail
 
Tupeane elimu kidogo, kuna watu wanachanganya mambo. Hapa tufundishane jambo moja. Kitu cha kwanza kabisa watu wanachokichanganya ni kuhusu Ibrahim, wengi wanasema Ibrahim alikuwa Mwarabu, ndugu yangu, nikwambie tu kwamba jamaa hakuwa Mwarabu.
akimbilia mpaka kwenye mlima ule aliopaa Yesu, wataomboleza na kulia, hapo ndipo Yesu atashuka kuimaliza vita hiyo, na huo ndiyo utakuwa mwisho wa kila kitu.
Ibrahim hakuwa mwarabu wala myahudi bali alikuwa mkurudi kutoka Iraq.
 
Hapa ndipo nashindwa kumuelewa Mungu, kwanini aliingiwa na tamaa hiyo ya kuua?
Tamaa ngani... Tamaa ni kwa kitu kisicho chako, sisi sote ni wake... Uwezi kuwa na Tamaa na mali yako.

Pili Isaka kwa sababu alikuwa anapendwa sana na baba yake, hivyo Mungu alitaka kujua je Ibrahim anauwezo wa kupoteza kitu anachokipenda kwa kukitoa kwa Mungu. Lakini Ibrahim akaonesha hali ya juu ya utii na Imani kwa Mungu na akawa radhi kumtoa mwanae ampendaye kama sadaka. Mungu aliona uthubutu, utii na Imani ya Ibrahim akaamua na kumbariki kuwa baba wa mataifa mengi, kwamba kupitia hao watoto wake mataifa mengi yatapatikana

Lilikuwa ni fundisho kwamba unapotoa sadaka au msaada basi toa kitu kwa Imani, husiweke Duku duku kwamba nampa shati langu zuri atapendeza kunizidi. Ukitoa kwa moyo safi basi Mungu nae atakubariki mara dufu kama Ibrahim alivyobarikiwa kuwa na uzao mkubwa wa mataifa mengi
 
Hajira alikua Mmisri kumbuka accient time Khemet waliishi Blacks soma historia vizuri
hajra alikua Mweusi tii kama hao South Sudan people ambao chimbuko lao ni Kemet na Kush kwa Nubian
waarabu walihamia hapo misri miaka ya juzi AD na sio BC!
mkuu Mhaya pitia madesa vizuri Ismail hajawahi kua Mwarabu ila ni Chotara la Babylon na Kemet na alikua half Black!
Sina uthibitisho wa moja kwa moja juu ya hilo... Yani vivid evidence, maana waarabu nao wanasema alikuwa muarabu
 
Tamaa ngani... Tamaa ni kwa kitu kisicho chako, sisi sote ni wake... Uwezi kuwa na Tamaa na mali yako.

Pili Isaka kwa sababu alikuwa anapendwa sana na baba yake, hivyo Mungu alitaka kujua je Ibrahim anauwezo wa kupoteza kitu anachokipenda kwa kukitoa kwa Mungu. Lakini Ibrahim akaonesha hali ya juu ya utii na Imani kwa Mungu na akawa radhi kumtoa mwanae ampendaye kama sadaka. Mungu aliona uthubutu, utii na Imani ya Ibrahim akaamua na kumbariki kuwa baba wa mataifa mengi, kwamba kupitia hao watoto wake mataifa mengi yatapatikana


Lilikuwa ni fundisho kwamba unapotoa sadaka au msaada basi toa kitu kwa Imani, husiweke Duku duku kwamba nampa shati langu zuri atapendeza kunizidi. Ukitoa kwa moyo safi basi Mungu nae atakubariki mara dufu kama Ibrahim alivyobarikiwa kuwa na uzao mkubwa wa mataifa mengi
👏🙏
 
Nipe kifungu cha kuthibitisha hilo
ok sir your wish is my commands..
Go and open Song of solomon 1:5
Screenshot_20231004-151746.png


Suleiman au solomon anasema yeye ni mweusi hapo sasa sema kingne boss.
Nakuja naandaa mafungu kwa ajili ya uzi wako wote nitakupa majibu yake yote ....
 
Kwa sababu chimbuko la uislamu linaanzia kwake
Kaka usipotoshe watu jifunze kwanza uislam uulewe,usiandike vitu usivyovijua ni Bora uachie watu wanaojua utaumbuka.chimbuko la uislam halianzii Kwa Ismael ndugu.
 
Kaka usipotoshe watu jifunze kwanza uislam uulewe,usiandike vitu usivyovijua ni Bora uachie watu wanaojua utaumbuka.chimbuko la uislam halianzii Kwa Ismael ndugu.
Waislamu wenyewe wanakuambia uislamu ulikuwepo tangu enzi za Adamu 😂
 
Tupeane elimu kidogo, kuna watu wanachanganya mambo. Hapa tufundishane jambo moja. Kitu cha kwanza kabisa watu wanachokichanganya ni kuhusu Ibrahim, wengi wanasema Ibrahim alikuwa Mwarabu, ndugu yangu, nikwambie tu kwamba jamaa hakuwa Mwarabu.

Ibrahim baada ya kuzaa na kijakazi ambaye alikuwa Mwarabu, inamaanisha damu yake ilichanganyika na ya Kiarabu na ndiyo maana tunasema Ishmael ni baba wa Waarabu kwa sababu mama yake alikuwa Mwarabu.

Nchi za Kiarabu ambazo zipo kwenye umoja ni hizi, Algeria, Bahrain, Iraq, Jordan, Kuwait, Djibout, Saudi Arabia, Tunisia, United Arab Emirates, Yemen, Somalia, Sudan, Syria, Comoros, Misri, Maurtania, Qatar na Palestina.

Kwa nini Waarabu wanamchukia Israel? Ni kwa sababu si Mwarabu mwenzao. Na hao ndiyo wa kizazi cha Ibrahim. Kwa hiyo kama ulikuwa unahisi Ibrahim alikuwa Mwarabu, futa hiyo akilini mwako.

Hata Iran sio Waarabu, najua wengine mtakuwa hamlijui hili kwa undani. Miongoni mwa nchi za Kiarabu, Iran hayupo kwa sababu yeye si Mwarabu.

So Israel na Waarabu ni baba mmoja ila mama tofauti. Ibrahim alizaa na Muisrael mwenzake kwa kipindi hicho ilikuwa bado haijaitwa Israel na mtoto wake kuitwa Isaka ila yule aliyezaa na kijakazi ambaye ni Mwarabu anaitwa Ishmael. Tatizo kubwa la vita baina ya Mwarabu na Israel ni hapa.

Kama Israel angekuwa Mwarabu, leo usingesikia vita vinavyoendelea huko. Na mara zote Israel anawaambiaga kwamba nchi zote za Uarabuni ni mali ya Israel na ndiyo maana kila anapokwenda kupiga, anachukua ardhi na kutanua nchi yake.

Israel walipewa nchi ndogo sana wakae baada ya kutawanywa na Adolf Hitler, baada ya kuanza kurudi, wakaitaka nchi yao, lakini kwa bahati mbaya waliwaona Waarabu washajigawia ardhi yao. Walichokifanya ni kuanza kupigana nao.

Kama unakumbuka Umoja wa Mataifa uliingilia kati, ulichukizwa na kitendo cha Israel kuwapiga Waarabu, walichokifanya, wakawapelekea Biblia ambayo kwa nyuma kuna ramani ya Israel tangu enzi za Musa. Wakawaonyesha na kuwaambia kwamba nchi zote za Uarabuni ni Israel, tutakapokuwa wengi, tutaendelea kupiga na kuirudisha nchi yetu.

So jua hili. Ibrahim hakuwa Mwarabu. Musa hakuwa Mwarabu. Suleimani mtoto wa Daudi na baba yake huyo hawakuwa Waarabu. Ni Waisrael ambao bado wanaendelea kupigana na Waarabu ili wachukue nchi yao iliyowafanya waondoke Misri.

Uzao wa Ibrahim ndiyo uliomleta Yusufu ambaye akawachukua Waisrael kwenda kuishi Misri. Maisha yalikuwa ya raha sana, watu waliionjoi maisha lakini baada ya mfalme huyo kufa, ndipo akaja mfalme mwingine ambaye sasa hakuwataka Waisrael, akawafanya watumwa wake.

Wakafanyishwa kazi. Baadaye ndipo Musa akazaliwa ndani ya ardhi ya Kiarabu. Akapewa jukumu la kuwatoa Israel kutoka hapo Misri kwenda kwao. Wakati huo ndio ambao nao Waarabu walikuwa wamejinyakulia nchi, tena walikuwa ni watu wakubwa kimuonekano.

Musa akaanza mchakato wa kuwatoa Israel Uarabuni na kuwapelekea Israel. Waliishi Misri kwa miaka 400. Wakaondoka na kwenda Misri, na walitumia miaka 40.

Musa hakuingia Israel, alikufa jangwani na Mungu kumzika. Wale waliofanikiwa kuingia huko Israel ndio walioendelea kuipambania ardhi yao mpaka leo hii.

Hapa kuna jambo moja.

Vita ya Israel na Waarabu itapamba moto hapo baadaye. Itapigwa vita kali sana. Sasa kwa kuwa Israel ataonekana kuwa kiburi na mwenye nguvu sana, dunia nzima itaanza kumcharaza. Huyu Marekani anayeonekana kuwa karibu na Israel naye atamgeuka, kila nchi duniani itamgeuka na kumpiga.

Mwisho wa siku baada ya kuona wanapigwa sana, watakimbilia mpaka kwenye mlima ule aliopaa Yesu, wataomboleza na kulia, hapo ndipo Yesu atashuka kuimaliza vita hiyo, na huo ndiyo utakuwa mwisho wa kila kitu.
Abraham,moses,saul,Daud,solomon hawa wote hawajawahi kuwepo ni hekaya
 
Back
Top Bottom