Ukweli kuhusu Vita vya Majimaji

Ukweli kuhusu Vita vya Majimaji

Je mtu akibatizwa ama kuslimu anakuwa hana haki ya kubadili jina lake?
Msanii,
Hawa wazalendo hawakumuomba father wa Peramiho aje awabatize.
Father alikwenda pale kuwabatiza akiwaambia kuwa ikiwa watakubali kubatizwa hawatanyongwa.

Father ndiye aliyeeleza kuwa kawabatiza Waislam na kuwapa majina mapya ya Kikristo lakini wenyewe walikuwa tayari wameshakufa.
 
Msanii,
Ninachoeleza ni kuwa hawa wazalendo wengi wao walikuwa Waislam inasemekana 75%.

Baada ya kuhukumiwa kunyongwa wakati wanasubiri kifo ndiyo father kutoka Peramiho akaja kuwabatiza na kuwapa majina mapya ya Kikristo.

Haya ndiyo yaliyotendeka.
Mimi nasomesha yale yaliyotendeka ambayo wengi walikuwa hawayajui.

Ndiyo nikaeleza kuwa Songea Mbano jina lake khasa ni Abdulrauf Songea Mbano.
Mkomanile jina lake ni Khadija.

Haya ndiyo muhimu kwangu na nayaeleza kwa kuwa hayakuwa yanajulikana.
Mohamed,
Naomba nikuulize kitu kimoja hao walionyongwa uislamu wao waliupataje, sababu wengi wao ni masalia ya Wangoni waliotoka South na Wangoni waliotoka kule hawakuwa waislamu wengi walikuwa ni ATR believers, Sasa hawa uislamu wao waliupataje?
 
Vita vya majimaji ni vita vilivyopiganwa na wazee wa kiislam kupinga utawala wa kimabavu wa kijerumani, lakini kwa makusudi vita hivi historia yake imechafuliwa kwa makusudi kuonesha kuwa vilikuwa vita vilivyopiganwa kwa imani za kishirikina.
Ina maana Kinjekitile hakuongopa kuhusu uwepo wa dawa ya maajabu yenye kuzibadili risasi kuwa maji ?... Mohamed Said
 
Ulivyo mdini naona kila kiongozi wa nchii alikua muislamu ila alilazimishwa na mapadri abatizwe apewe jina jipya ili apewe mamlaka.

Unapoteza muda wako na nguvu zako bure..nadhani magonjwa ya uzee yanakunyemelea unajiabisha tu humu wewe mzee.

Tunaendelea kukupuuza.

#MaendeleoHayanaChama
Jiwe ..
Hujafanikiwa kunipuuza.
Huwezi kuwa unaniandikia halafu useme unanipuuza.

Kama una nia ya kunipuuza ni wewe kutoingia kwenye mjadala wangu.
Huko ndiko kupuuza.

Humu nadhani utakuwa unaona kuna watu wakiniandikia huwa siwajibu nakuwa kimya.
 
Viongozi wa kiislam mbona wamepita wengi tu, kwanini mnalalama kuonewa na kukandamizwa na mnasemaga mko wengi hapa nchini!??
Ina maana hao viongozi wa kiislam nao walibariki hilo!?, Achana na hao wa kiserikali si kuna mabaraza pia na viongozi wa kidini, wameshindwa kufanya marudhiano na viongozi wa nchi kuhusu malalamiko yenu??

Shida ni nini mzee wangu!?
Vishu...
Huu Uzi nini maudhui yake?
 
Mohamed,
Naomba nikuulize kitu kimoja hao walionyongwa uislamu wao waliupataje, sababu wengi wao ni masalia ya Wangoni waliotoka South na Wangoni waliotoka kule hawakuwa waislamu wengi walikuwa ni ATR believers, Sasa hawa uislamu wao waliupataje?
Mazigga,
Uislam umeingia Pwani ya Afrika Mashariki zaidi ya miaka 1000 iliyopita na kutokea pwani ukasambaa kote.

Maji Maji imepiganwa kati ya 1905 - 1907.
Jiulize Wangoni waliingia lini nchini.

Uislam haukuwa mgeni katika German Ostafrika.
Ndiyo unakuta Mngoni jina lake Abdulrauf Songea Mbano, Khadija Mkomanile.

Unawakuta Wayao kote huko kusini Waislam ndipo unampata Suleiman Mamba, Hassan bin Omar Makunganya.

Kubwa ni kuwa si Uislam tu utakutananao huko utakuta na Tariqa Quadiriyya na Makhalifa wake hii leo mwaka wa 2022.
 
Ina maana Kinjekitile hakuongopa kuhusu uwepo wa dawa ya maajabu yenye kuzibadili risasi kuwa maji ?... Mohamed Said
Proved,
Mimi hupenda watu wakatumia akili zao wenyewe kujua ukweli.

Mimi ningependa sana kukusikia wewe unasemaje kuhusu suala la maji kugeuka risasi.

Mimi hapa nitakuongezea jambo ili uongee maarifa yako.
Baadhi ya viongozi wa vita walifanyia majaribio dawa hiyo kwa mbwa.

Mbwa alikufa.
Hapa katika mitandao kuna elimu kubwa sana.

Jisomee historia ya Maji Maji kupata ukweli.
 
Proved,
Mimi hupenda watu wakatumia akili zao wenyewe kujua ukweli.

Mimi ningependa sana kukusikia wewe unasemaje kuhusu suala la maji kugeuka risasi.

Mimi hapa nitakuongezea jambo ili uongee maarifa yako.
Baadhi ya viongozi wa vita walifanyia majaribio dawa hiyo kwa mbwa.

Mbwa alikufa.
Hapa katika mitandao kuna elimu kubwa sana.

Jisomee historia ya Maji Maji kupata ukweli.
Mzee Mohamed Said inawezekana pia walihitimisha kuwa inafanya kazi kwa binadamu tu na sio mbwa.

Ila inawezekana upinzani wa Abushiri dhidi ya wajerumani ndio ulichukua msukumo wa kidini zaidi maana ulijikita huko Pangani kuliko Vita ya majimaji ambao ilihusisha uzalendo wa kiasili/tamaduni zaidi kuliko dini.
 
Msanii,
Hawa wazalendo hawakumuomba father wa Peramiho aje awabatize.
Father alikwenda pale kuwabatiza akiwaambia kuwa ikiwa watakubali kubatizwa hawatanyongwa.

Father ndiye aliyeeleza kuwa kawabatiza Waislam na kuwapa majina mapya ya Kikristo lakini wenyewe walikuwa tayari wameshakufa.
Kwa upande mmoja huo ni ukatili wa ajabu kabisa. Kwa upande wa pili ni wazi kulikuwa na hadaa nyingi zenye matumaini yasiyo na nuru kwenye hii issue.

Lakini leo tunaibadilije hiatoria wakati waandishi wake ni hao hao waliotufanyia unyama?
 
Je hawa wapiganaji wa Majimaji ktk picha toka makabila ya Wangindo, Wagoni, Wapogolo n.k zinaakisi uislamu au makabila yao ?

1656873100383.png



Picha machifu wa kiafrika waliohukumiwa adhabu ya kifo kufuatia vuguvugu la kupinga utawala wa Kijerumani almaaruf vita ya Kinjekitile Ngwale kuwaaminisha yakuwa kwa kuongeshwa maji na kuwachanja 'chale' za kufanya risasi kugeuka maji, je imani hii ni ya kiAfrika au ya kiIslamu ?

1656873344911.png



MajiMaji ilichagizwa na wenyeji kulazimishwa kulima zao la Pamba ili litumike kama zao la kulipisha kodi ya kichwa na pamba kusafirishwa kwenda nje kutumika ktk viwanda vya Ujerumani. Je katika imani na utamaduni wa kimapokeo wa dini ya KiIslamu mtawala kukusanya kodi ni haramu? Je mjerumani alilazimisha imani za kilugaluga imani zetu adhimu kabisa za kiAfrika nani alitaka kuzifuta ni wote Wajerumani kupitia Ukristo na UIslamu kupitia Waarabu au kuna mmoja kati ya hao wakuja waliwaacha wazawa waendelee na tamaduni, majina, desturi, matunguli n.k ya kienyeji yaendelee

1656873536041.png


Katika watawala hawa wawili waliowasili toka nchi za mbali kwa majahazi na merikebu ni kweli waliheshimu miungu yetu ya asili ya ZoleLanga Masika, Kinyamkela na majina yetu ya kienyeji ya Chakumwenda bin Msumari au wote walitugilibu kushawishi kwa hadaa au mtutu wa bunduki tufuate yale yote mageni waliyokuja nayo toka huko watokako kwa kuvuka bahari mpaka maeneo ya kwetu?

Picha chini : Askari 'Wamatumbi' wa jeshi la Jerumani ya Afrika Mashariki

1656874428518.png


Source : What Was the Maji Maji Rebellion?

Tujiulize ukoloni mkongwe una tofauti yoyote uwe umetoka bara Ulaya, bara Arabu au Mongolia ? Je mikakati ya kutengeneza dola ya kiJerumani, dola ya kiArabu au kiMongol n.k hata ya sasa ya KiMarekani au kiChina zinautofauti wowote tukasema bora kutwezwa(humiliated) au kulazimishwa majina mageni, tamaduni ngeni, asili ngeni (subjected), uhuru wa ahera huku uhuru wa duniani tumepokwa na wageni wakuja n.k na hivyo tujipige kifua kuwa mkoloni yule ni mbora kuliko huyu ?

 
Waafrika miaka hii baada ya uhuru wamechanganyikiwa kabisa wanaona ufahari kujitambulisha kwa kutumia dini za kitapeli za kigeni kama Uislamu na Ukristo [emoji30][emoji30][emoji30][emoji30]
 
27 / 2/ 1906, Vita vya Majimaji ni vita vilivyopiganwa na wazee wa kiislamu kupinga utawala wa kimabavu wa Kijerumani, lakini kwa makusudi vita hivi historia yake imechafuliwa kwa makusudi kuonesha kuwa vilikuwa vita vilivyopiganwa kwa imani za kishirikina.

Ikumbukwe kuwa kusini mwa Tanzania kuna mkoa unaitwa Lindi, ambapo ndani ya mkoa wa Lindi kuna wilaya inaitwa Kilwa ambapo hapo mwanzo ilikuwa ni dola kamili ya Kiislamu iliyokuwa na utawala kamili na kutumia pesa yake na kuhukumu watu kwa mujibu wa dini ya Kiislam, ambapo kanda yote ya kusini mwa Tanzania walikuwa wanafuata mfumo wa kiislam.

Wajerumani walipoingia walikuta Makadhi na watu wote wakiwa katika imani ya Kiislam huku maisha yakienda bila matatizo yoyote, Wajerumani wakaanza na kufanya mambo ambayo hayakukubalika katika jamii kwa kulazimisha ili malengo yao yafikiwe, maafisa na askari walikuwa wanatembea na rozari na kulazimisha watu kuwa Wakristo kinguvu, baadhi ya maaskari walibaka wanawake wa kiislam ndani ya maboma yao na huko mashambani, hata waislam walipotaka kujua kwanini wake zao au mabinti zao wanabakwa, walijibiwa majibu ya karaha na dharau.

Ndipo chuki ilizidi kuwa juu ya Wajerumani, wazee wa kiislam waliwahimiza vijana wao kujiandaa kwa kujikomboa kutoka katika utawala wa kikafiri, wakisema wakati wa dola ya Kiislamu mambo haya hayakuwepo na iweje leo, ndipo kiongozi wa Wamatumbi aitwae Kinjeketile Ngwale aliwaongoza wapiganaji wa Kimatumbi kupambana na Wajerumani, wakati wote huo ukatili wa Ujerumani ulikuwa unajulikana kote kusini, wakati vita vinaanza na vilianza kwa nguvu kubwa, Wajerumani waliua kila walieona huenda ni adui yao, majeshi ya Ujerumani wakaanzisha kampeni kubwa kukamata kila waliemuona katika majumba ya ibada.

Kumbuka wakati huo nyumba za ibada ilikuwa ni Misikiti na kila wakati wa sala majeshi ya Ujerumani yalivamia misikiti na kumkamata kila waliemkuta humo, ndipo chifu wa Suleymaan Mamba wa kabila la Wamwera akatangaza vita kwa watu wake kuwa kila atakapoonekana Mjerumani akatwe kichwa, nae chifu Abdallah Chami wa kabila la Wangindo nae akatangaza vita rasmi kwa Wajerumani, nae chifu Mataka Ambunje wa kabila la Wayao nae akatangaza vita rasmi na Wajerumani, haikutosha nae Chifu Songea Rauf Mbano wa kabila la Wangoni nae akatangaza vita Wajerumani, na hapo makabila matani makubwa Kanda ya Kusini wakawa wanapigana na Wajerumani, na baadhi ya makabila madogo madogo nayo yakawa yanapigana kuwasaidia ndugu zao dhidi ya Majeshi dhalimu ya Ujerumani.

Makabila hayo ni kama Wandendeule, Wamatengo, Wambunga, Wandamba n.k. Wapiganaji wa vita hivyo mnamo tarehe 5/8/1905 walivamia misheni ya Kanisa Katoliki huko Nachingwea na kufanya shambulio la kustukiza na kuua makumi ya wanajeshi wa Ujerumani na kumuua Askofu Cassian Speis ambae huyu ndio alikuwa Askofu wa kwanza Dar es salaam.

Na mnamo tarehe 14/8/1905 wapiganaji hodari walivamia boma la Mjerumani na kufanya uharibifu mkubwa hali iliyopelekea mapigano makali yalioacha majeruhi na maiti kila upande, wapiganaji wengi walikuwa wanatumia mishale, mikuki, mundu, silaha za jadi na bunduki kadhaaa walitoka baada ya kuwaua majeshi ya Ujerumani, na Mjerumani akitumia bunduki za moto na kupelekea majeshi ya wazalendo kuzidiwa nguvu na Mjerumani kushinda vita hivyo.

Ikumbukwe majeshi ya mjerumani walikuwa wanachoma majumba moto ili kuwakamata wanaume lakini waliokuwa wanaungua mpaka kufa walikuwa ni watoto na wanawake. Nje kidogo ya mji wa Songea kuna kitongoji kinaitwa Mahenge, hapo kuna sehemu ya kumbukumbu ya vita vya Majimaji. Jambo kubwa la mahala hapo ni kaburi kubwa la halaiki ambamo askari zaidi 67 walizikwa kwa pamoja. Na kando ya kaburi hilo la pamoja kuna kaburi la Ally Songea Mbano ambae yeye alizikwa peke yake.

Kwa mara ya kwanza nilitembelea Makumbusho hayo mwishoni mwaka 2007. Baada ya kusaini kitabu cha wageni na kulipa ada ya kituo muhudumu wa kituo hicho alitupa karatasi yenye orodha ya majina ya wale wote walionyongwa na kuzikwa hapo. Ukiitazama orodha hiyo na hasa ukiwa Mwislam jambo moja litakustuwa. Robo tatu ya walionyongwa na kuzikwa hapo ni Waislaam. Linaanza jina lake la Kiiislam, kisha kwenye mabano kuna jina la Kikristo na mwishoni linaishia jina la kiasili, mfano Abdulrahman [Dominic] Mputa Gama.

Muhudumu akatueleza kuwa hawa mashujaa wa vita vya Maji Maji kabla ya kunyongwa alikuwako padri ambae aliwabatiza na kuwapa majina ya Kikristo na baadae kunyongwa, wengi walibatizwa kwa hadaa kuwa wakibatizwa wataachiwa huru, wote katika hao walionyongwa walikuwa ni Waislam. Uzuri ni kwamba katika orodha hiyo kulikuwa na jina na sahihi ya yule padri aliyewabatiza, na kwa mkono wake [huyo padri] aliiyaandika hayo majina. Karatasi yenyewe ilihifadhiwa vizuri kwenye fremu ngumu ya kioo. Tuliomba kwa nguvu zote kupatiwa hiyo karatasi ya majina hata kwa kununua lakini haikuwezekana pamoja na kuwaona wakubwa wa kituo hicho.

Niliporudi kwa mara ya pili mwezi July 2009 nilipata mstuko. Karatasi iliyohifadhiwa kwenye fremu ngumu ya kioo, iliyokuwa na majina ya Kiislaam ya mashujaa wa vita vya Maji Maji, haikuwapo, na badala yake imewekwa karatasi nyingine ambayo ndani ya karatasi hiyo majina ya Kiislaam ya mashujaa hao wa vita vya Maji Maji yameondolewa na kuachwa majina ya ubatizo na yale ya kiasili tu, jina la padri, sahihi yake na wadhifa wake katika Kanisa Katoliki pia vimeondolewa na karatasi yenyewe haikuwa kwenye fremu ya kioo na ilikuwa katika fotokopi tu.

Nilimuuliza muhudumu kulikoni? Akasema, "Songea pana mzee mmoja maarufu sana katika historia ya TANU na historia ya kuasisiwa Bakwata anaitwa kwa kifupi M. S. Mzee huyu ana binti yake ambaye ameolewa na Mzungu wa Kijerumani. Binti huyu na mumewe wa Kijerumani walikuja hapa Songea matembezi. Hivyo kwa shinikizo la huyu mzee M.S. karatasi hiyo alipewa huyu Mzungu kwa ahadi kwamba anaipeleka Ujerumani na atairudisha. Hivyo ndivyo karatasi ile asilia ilivyotoweka.

Kubwa katika karatasi ile ni ule ushahidi wa majina kuwa wote katika wale walionyongwa na kuzikwa hapo ni Waislaam, wengi katika hao walihadaiwa kuachwa huru hivyo wakabatzwa ispokuwa wachahe sana waligoma kama shujaa Ally Songea Mbano. Huyu kwa ushujaa wake wa kupambana na Wajerumani aligoma na akasumbua sana kiasi akanyongwa siku yake na peke yake na ndio sababu akazikwa peke yake.

Ukiingia ndani ya kinyumba cha ghorofa, unaanza kuona picha za mashujaa wa Maji Maji wakiwa wamevaa mavazi ya vita mithili ya mahujaji wanavyovaa Ihraam wakati wa hija. Kinachoongezeka kwao ni vilemba kichwani. Chini ya kila picha kuna jina la aliyekuwa kwenye picha ile. Ukipanda gorofani utaona silaha za kijadi kama mikuki, pinde, ngao n.k. Kinachosisimua zaidi ni mavazi ya vita. Mavazi ya vita ya askari wa Maji Maji wengi walivaa kanzu za Kiislaam na vilemba.

Jambo jingine linalosisimua ni kile ambacho watu wa kituo hicho wameandika "rosary" hili ni jina la Kikristo, hasa la Kikatoliki, ni zile shanga ambazo huning'inia msalaba lakini unapotazama hicho kilichoitwa "rosary" utaona si "rosary," bali ni tasbihi hasa ya Kiislaam yenye kupangika hasa shanga zake, 33, 33,34. Maneno yaliyoandikwa kuelezea "rosary" hizo ambazo ni tasbihi ni;

"Hizi ni rosary ambazo wapiganaji wa Majimaji walikuwa wakitumia KUTAMBIKA kabla ya kwenda vitani kwa kuamini kwamba zitawakinga na risasi. "Ukweli ni kwamba hawa askari wa Maji Maji wengi walikuwa ni Waislaam hivyo hawakuwa WAKITAMBIKA bali walikuwa wakitumia tasbihi hizo kufanya dhikri kwa Allah kabla ya kwenda vitani. Midhali sisi Waislaam hatujawa tayari kuandika historia yetu kama Waislaam wanaotuandikia watapotosha na kupindisha na kutuzulia wanavyotaka.

Hapo gorofani kuna jambo jingine la kusisimua. Kuna magudulia na makopo. Wameandika kuwa, haya ndio makopo ambayo askari wa Maji Maji walikuwa wakiyatumia KUNAWA kabla ya kwenda vitani [kushika udhu na sio kunawa] pia kwa kuamini kuwa maji hayo yatawakinga. Muhudumu alitueleza kuwa kumbukumbu nzuri na za kuaminika ziko Jimbo Kuu la Wakatoliki Peramiho. Tulikwenda jimboni lakini hatufanikiwa kwa sababu za ki-urasimu tu. Tulitakiwa tupate kibali cha Askofu Mkuu. Hatukukipata.

Kwa yale tuliyoyaona na kuyashudia yafuatayo;

Vita vya Maji Maji havikuwa ni vita vya kizalendo, kwamba wazalendo walikuwa wakipigania nchi yao. La. Vilikuwa ni vita vya Waislaam wakipigana na Wakristo wa Kijerumani waliovamia maeneo asilia ya Waislaam kwa lengo la kuuwa Uislam na kusimamisha Kanisa kwani mazingira yote utayoyaona ya mashujaa wa vita vya Maji Maji ni mazingira ya Kiislaam, kingine ni kwamba hukuti mahala yalipo makaburi ya askari wa Kijerumani ila katika miji ya Waislaam kama Kilwa, Bagamoyo n.k.

Kwa nini wauliwe maeneo ya Waislaam tu? Walifuata nini huko? Kuna upotoshaji mkubwa sana wa historia ya vita vya Maji Maji. Vinaoneshwa kama ni vita vya wazalendo wakipigana na wakoloni wa Kijerumani, wakati ukweli si hivyo. Ukweli ni kwamba vita vya Maji Maji vilikuwa ni vita baina ya Waislaam na Wakrito wa Kijerumani, Waafrika Wakristo wa Songea walijiunga na Wakristo wenzao wa Kijerumani dhidi ya Waafrika wenzao wa Kiislam. Wakristo wameitafiti hakika hii na wakaijua kisha wameificha kwa maslahi yao.

Kuna haja ya wasomi wetu wa Kiislaam kufanya juhudi za makusudi za utafiti wa historia yetu ili kukifanya kizazi hiki cha Kiislaam kujitambua zaidi na kujenga ujasiri. Taasisi za Kiislaam na watu binafsi [matajiri] wawawezeshe kiuchumi wasomi hawa kufanya kazi hii. Mwaka 2008 nimetembelea Kilwa Kisiwani, huko nikamkuta Mzungu wa Kifaransa akiandika historia ya Kilwa Kisiwani akiitwa Thiery, ameweka kambi na majenereta ya umeme, solar power na makompyuta. Kazi nyingine kubwa alokuwa akifanya ni kukarabati yale magofu ambayo mengi ni Misikiti na majumba ya mawe ya wafalme wa kale.

Kilwa Kisiwani ni moja kati ya dola kubwa za Kiislaam katika mwambao wa Afrika Mashariki, ndio dola ya mwanzo kuwa na sarafu yake ambayo iliandikwa jina la Allah. Tuliposoma kazi ile ya Yule Thiery Mfaransa tayari alikwisha ipotosha kwa kiasi kikubwa. Sikuwa na la kumfanya. Kizazi cha vijana wa Kiislaam hakitopata historia ya kweli ya Kiislaam kama tutawaacha akina Thiery waandike na hivyo vijana wetu hawatajitambua na hawatokuwa na ujasiri katika Uislam wao.

Maisha yao ya kila siku, hawa wanajua ni nini hasa wamekifanya kwa wazee wetu, kuanzia kwa Chifu Kimweri mpaka Chifu Mkwawa, wanasema etia mejiua, ni nani anaweza kujiua mpaka kukin'goa kichwa chake jamani?!

Majeshi yaliyofanya mauaji dhidi ya wazee ni Major Johannes, Captain Mortz Merker, Luteni Spiegel, Staff Sajent Engalnd na wengineo!

Ewe Allah (S.W.T.), Wazidishie adhabu hao madhalimu wa Kijerumani, Amiiyn!

Ahsateni, Nakutakieni siku njema!
Hamna sehemu yoyote watazidishiwa adhamu wakati hamtaki fanya kazi mmekalia ufisadi na wizi wa mali za uma
 
Kwa upande mmoja huo ni ukatili wa ajabu kabisa. Kwa upande wa pili ni wazi kulikuwa na hadaa nyingi zenye matumaini yasiyo na nuru kwenye hii issue.

Lakini leo tunaibadilije hiatoria wakati waandishi wake ni hao hao waliotufanyia unyama?
Msanii,
Historia tumeshaibadili miaka mingi iliyopita.
Unaona hapa watu wanavyohemkwa kwa kueezwa kuwa Mkwawa aliuwa Muislam.

Wenye kusema hayo ni wao wenyewe waliokuwa na Mkwawa na wameandika na kuonyesha barua alizokuwa akiandika Mkwawa kwa hati za Kiarabu.

Wameeleza urafiki baina ya Mkwawa na Abushiri bin Salim na wameonyesha na bunduki ambayo Abushiri alimpa Mkwawa.

Leo katika historia hii mimi huisomesha kupitia maisha ya Abdulrauf Songea Mbano.
 
Tatizo la kuwa na wasomi ambao hawajaelimika litaendelea kuitafuna sana Africa. Inashangaza kuona mtu anapigania kutambulishwa kwa majina ya 'Slave masters', majina yetu ya asili tunayaona hayana maana, hii ni aibu. Imenikumbusha song of lawino and ocol
Kwahiyo mf. Hilo la Dominic ndo la asili eti eh!
 
Ulivyo mdini naona kila kiongozi wa nchii alikua muislamu ila alilazimishwa na mapadri abatizwe apewe jina jipya ili apewe mamlaka.

Unapoteza muda wako na nguvu zako bure..nadhani magonjwa ya uzee yanakunyemelea unajiabisha tu humu wewe mzee.

Tunaendelea kukupuuza.

#MaendeleoHayanaChama
Mwache afanye au kuandika anachojisikia maana uhuru huo anao,,!! Wewe lete andiko lako hapa la namna yako tulisome pia..
 
Kama walibatizwa wakapewa majina mapya nashindwa kuelewa wanapoyatumia majina hayo kuna kua na shida Gani.
Pia tunaweza kutazama Koo zao sasa hivi ni watu wa dini Gani?
Huenda familia za wahusika ndio waliotaka marekebisho ya majina kwa kuona kwamba yamekosewa na wao wanajua jamaa zao walibatizwa na kupewa majina mapya.
Kama jamaa zao hawajalalamika basi walioandika upya wako sahihi.
Ukitaka kuona shida ya kutumia jina lisilo lako fanya hivi.. mwambie mzazi wako wakike(mama yako) abadilishe pale kwenye jina la baba yako yaani kama wewe unaitwa dindili chuma basi aseme kuanzia leo wewe ni dindili komwe.. alafu huyu komwe awe ni jirani yenu pale mtaani,, baada ya hapo wewe uje urejeshe mrejesho hapa kama Kuna shida au laaa
 
kujitambulisha kwa kutumia dini za kitapeli za kigeni kama Uislamu na Ukristo

Kabisa hawataki kusikia mazingombwe ya Kinjekitile Ngwale jina halisi la Ki-Rufiji likitumika kuwa ndiye aliwahamashisha waafrika kupambana na ukoloni mkongwe ambao hatujali kama ni wa ki-Jerumani, kiKristo, KiArabu, KiIslamu uliokuwa na nia siyo ya kututawala tu bali kufuata asili zetu za majina, mazingaombwe, destruri, mila, elimu na tamaduni zetu ili tufuate za kigeni.

Ni aibu hata wamatumbi wadai kuwa jando ni Uislamu au Uyahudi wakati mababu zetu tendo hilo lilikuwepo kabla ya wageni kutua ktk pwani ya pande hizi za dunia yetu.

Tutakataa kuuita watoto wetu Chausiku na kuwabatiza Kieran na kadhalika kama vile Afrika watoto hawazaliwi usiku au kuwaita Stella badala ya Nyota wakati pia mtoto anaweza zaliwa wakati nyota inaonekana angani.

Hii ni mifano lukuki ya kuiga ya wakuja kama vile matukio, elimu, majina ya mashujaa, viongozi wa kiimani wa kiAfrika hawakuwepo n.k n.k
 
Vita ya majimaji ambao ilihusisha uzalendo wa kiasili/tamaduni zaidi kuliko dini

Yaani najisika fahari hatimaye kuona kuwa mababu walionesha uzalendo wa kiasili / tamaduni kumkabili mkoloni mkongwe aliyekuja kwa vyombo vinavyosafiri katika bahari kubwa.

Wazee hawa hawakupigania kufia imani ya kingeni bali utu na uhuru wao wa kuzaliwa watu huru eneo hili la Afrika.

Propaganda zikawa kuwa ni Uislamu dhidi ya Jerumani au kodi ya kichwa dhidi ya Jerumani.

Hapo jambo kubwa la hadaa kuficha joho au kanzu la ukoloni wa kila aina uwe wa kidini, kibiashara ulitumika katika kuandika historia.

Na mara nyingi mshindi mwenye mabavu yaliyopitiliza ndiyo anaamua historia hiyo iandikwe vipi kwa manufaa mapana ya mkoloni awe ametoka Arabuni, Ulaya, Marekani ya Kaskazini n.k
 
Je hawa wapiganaji wa Majimaji ktk picha toka makabila ya Wangindo, Wagoni, Wapogolo n.k zinaakisi uislamu au makabila yao ?

View attachment 2280151


Picha machifu wa kiafrika waliohukumiwa adhabu ya kifo kufuatia vuguvugu la kupinga utawala wa Kijerumani almaaruf vita ya Kinjekitile Ngwale kuwaaminisha yakuwa kwa kuongeshwa maji na kuwachanja 'chale' za kufanya risasi kugeuka maji, je imani hii ni ya kiAfrika au ya kiIslamu ?

View attachment 2280154


MajiMaji ilichagizwa na wenyeji kulazimishwa kulima zao la Pamba ili litumike kama zao la kulipisha kodi ya kichwa na pamba kusafirishwa kwenda nje kutumika ktk viwanda vya Ujerumani. Je katika imani na utamaduni wa kimapokeo wa dini ya KiIslamu mtawala kukusanya kodi ni haramu? Je mjerumani alilazimisha imani za kilugaluga imani zetu adhimu kabisa za kiAfrika nani alitaka kuzifuta ni wote Wajerumani kupitia Ukristo na UIslamu kupitia Waarabu au kuna mmoja kati ya hao wakuja waliwaacha wazawa waendelee na tamaduni, majina, desturi, matunguli n.k ya kienyeji yaendelee

View attachment 2280156

Katika watawala hawa wawili waliowasili toka nchi za mbali kwa majahazi na merikebu ni kweli waliheshimu miungu yetu ya asili ya ZoleLanga Masika, Kinyamkela na majina yetu ya kienyeji ya Chakumwenda bin Msumari au wote walitugilibu kushawishi kwa hadaa au mtutu wa bunduki tufuate yale yote mageni waliyokuja nayo toka huko watokako kwa kuvuka bahari mpaka maeneo ya kwetu?

Picha chini : Askari 'Wamatumbi' wa jeshi la Jerumani ya Afrika Mashariki

View attachment 2280169

Source : What Was the Maji Maji Rebellion?

Tujiulize ukoloni mkongwe una tofauti yoyote uwe umetoka bara Ulaya, bara Arabu au Mongolia ? Je mikakati ya kutengeneza dola ya kiJerumani, dola ya kiArabu au kiMongol n.k hata ya sasa ya KiMarekani au kiChina zinautofauti wowote tukasema bora kutwezwa(humiliated) au kulazimishwa majina mageni, tamaduni ngeni, asili ngeni (subjected), uhuru wa ahera huku uhuru wa duniani tumepokwa na wageni wakuja n.k na hivyo tujipige kifua kuwa mkoloni yule ni mbora kuliko huyu ?

Utawala wa kijerumani ulikuwa wa moja kwa moja 'direct rule' tena uliambatana na matumizi makubwa ya nguvu na ukatili ndio chanzo hasa cha kuzuka migogoro na watawala wa kijadi.

Waingereza waliona athari wa aina hiyo huko Kenya (baada ya kupambana na Wanandi), Zimbabwe na kwingineko hivyo waliwatumia viongozi hao hao wa kijadi kama daraja la utawala (indirect rule).

Kwa Sasa kusema Marekani, China n.k zina ukoloni huenda ni sahihi au sio sahihi pia, isitoshe hawa wa Sasa tumeingiliana mno kibiashara tofauti na enzi hizo na baadhi ya makampuni na mashirika yao huendesha kazi zao huku Africa na kutoa ajira, kulipa Kodi, japo wanaweza kushawishi siasa ila itategemea na nyie wenyewe.
 
Back
Top Bottom