Ukweli kuhusu Wakatoliki kutokuabudu sanamu zilizopo makanisani

Ukweli kuhusu Wakatoliki kutokuabudu sanamu zilizopo makanisani

Kutafsiri vitu kwa mafungu ni dalili ya uelewa mdogo.
Kuita jumapili ni siku ya jua, kwani kuna siku ya jua na siku za nini?
Sun(sunday)= jua
Saturdays (saturn) = shetani. Huwa naona zote ni tafsiri za waliokosa maarifa.
Madhehebu mengi yamekuwa yakitafuta mapungufu kwenye imani tofauti na kusahau mapungufu yao.
Ni wazi kwamba kila dhehebu lina mapungufu yake. Ila imani ya mtu na matendo yake havitegemei sana dini.

Labdwa kwa wale wanaotafuta wafuasi ili kukuza mfuko wa sadaka.
 
Labda nami niweke neno kdg.. je siku ya sabato ya bwana ni lini? Kama ni jmos au jpili bas naomba aya toka kweny biblia. Pia kama unaweza muuliza huyo mchungaj ingekua heri atupe majibu hayo, lingine... Ni nani aliezipa majina cku tulizonazo? Maana kweny maandiko hazijaandwa jmos au jpili!!
Siku ya bwana ndugu yangu ni siku ya Jumamosi.
 
The Catholic Church played a vital role in the trans-Atlantic slave trade, according to historians and several published thesiis on the topic.

The trans-Atlantic slave trade was introduced by the coming of the Europeans who came with the Bible in the same manner that Arab raiders and traders from the Middle East and North Africa introduced Islam through the Trans-Saharan slave trade, according to AfricaW.com, a premiere informational website available throughout the continent.

“In fact, the Church was the backbone of the slave trade,” the authors wrote. “In other words, most of the slave traders and slave ship captains were very ‘good’ Christians.”

For example, Sir John Hawkins, the first slave-ship captain to bring African slaves to the Americas, was a religious man who insisted that his crew “serve God daily” and “love one another.” His ship, ironically called “The Good Ship Jesus,” left the shores of his native England for Africa in October 1562. Some historians argue that if churches had used their power, the Atlantic slave trade might have never occurred.
Mwandishi amekosa akili na maarifa.

Nilitegemea huyo.mwandishi angekuja na maelezo yanayothibitisha kuwa Kanisa Katoliki lilishiriki kwenye biashara ya utumwa, kumbe hakuna lolote.

Anaishia kumtaja Captain wa meli iliyobeba watumwa kuwa alikuwa mkristo mzuri (huo ukristo mzuri aliupimaje?) Ningeshtuka kama ningesikia kuwa Kanisa Katoliki lilikuwa linamiliki meli za kusafirisha watumwa kwenda sokoni. Au Askofu alikuwa anaendesha meli ya kusafirishia watumwa.

Hivi hata leo hii, tuna majambazi wangapi ambao ni wakatoliki, wasabato, waprotestant au waislam? Huo ujambazi unafanywa na ukatoliki, usabato, uislam wao au wao ndio wanaokuwa majambazi?

Id Amin alikuwa muislam, alikuwa mtawala wa Uganda, aliua watu wengi wasio na hatia. Hiyo inaweza kuhalalisha kusema kuwa Uislam ulitawala Uganda kwa sababu Amin alikuwa muislam? Au hata kusema uislam uliua watu Uganda, kwa sababu kiongozi aliyeua raia alikuwa muislam?

Wafanyabiashara wakubwa wa biashara ya utumwa walikuwa ni waislam. Je, unaweza kusema kuwa ni uislam ndiyo ulikuwa unafamya biashara ya utumwa? Lakini ili biashara ikamilike lazima uwe na muuzaji na mnunuzi. Wanunuzi wakubwa walikuwa wazungu ambao baadhi yao walikuwa ni wakristo, lakini ni wao ndio waliokuwa wakishiriki hiyo biashara, siyo ukristo wao.

Huyo mwandishi bila shaka amenyimwa maarifa na akili.
 
Labda nami niweke neno kdg.. je siku ya sabato ya bwana ni lini? Kama ni jmos au jpili bas naomba aya toka kweny biblia. Pia kama unaweza muuliza huyo mchungaj ingekua heri atupe majibu hayo, lingine... Ni nani aliezipa majina cku tulizonazo? Maana kweny maandiko hazijaandwa jmos au jpili!!
Soma Luka 23 kuanzia fungu la 50, soma Kwa makini ili uelewe siku ya Saba ni ipi na siku ya kwanza ya juma ni ipi Kwa mjibu wa biblia.
 
Mnaabudu sanamu ya Maria na Yesu
Wakati Amri ya Kwanza imekataa hilo swala

Kama hamuoni yatosha mkaamua kuifuta hiyo amri
Huelewi chochote. Waulize wanaofahamu. Huelewi maana ya kuabudu.

Haya maneno huwa yanasemwa na baadhi ya wakristo waliokosa maarifa lakini huwezi kusikia kutoka kwa viongozi wenye elimu ya kutosha ya dini, hata kama siyo wakatoliki. Ila wale wakristo wa kusoma mstari mmoja wa biblia, bila hata kuelewa content, wanatoka na kuanza kupiga kelele kuwa Wakatoliki wanaabudu sanamu.

Wayahudu walipoitazama sanamu ya shaba walikuwa wanaiabudu?

Wayahudi walipokuwa wakisafiri na sanduku la amri za Mungu, walikuwa wanaliabudu?

Waisrael walipoyaweka makerubu kwenye hekalu lao walikuwa wanaabudu?

Wayahudi walipoibeba mifupa ya Yakobo, walikuwa wanaiabudu?
 
Mtu mmoja alikuwa anaoga basi kichaa akapita na kuzichukua nguo zake naye mtu yule akatoka na kumkimbiza huku akiwa uchi .je wadhani wapita njia watasemaje
 
Kanisa katoliki Lina kazi moja tu,kububiri injili na kuwaonesha watu njia ya wokovu
Kazi ya kusema nani anasali lini na wapi tumewaachia wasa

Na mchungaji huyo ndo wewe mwenyewe, muadventista maskini, unayejaribu kujustify umaskini wako kwa kuwapa lawama wakatoliki kuwa kwa wao kuabudu sanamu, Mungu anakulaani wewe unakosa hela ya kula.

Ulishawahi kuona sehemu wakatoliki wameweka sanamu wanaliita Mungu na kuliabudu kama Mungu wao?

Musa alipotengeneza sanamu la nyoka na kuwaambia waisrael atakayemtazama yule nyoka atapona, alikuwa anaabudu sanamu?

Kipi bora, kati ya kutenengeza sanamu linalokukumbusha kuwa kuna mtu(binadam mwenye mwili) aliyeitwa Masihi ambaye pengine alifanana hivyo, na kisha kuamini kuwa mtu huyo aliyefanana na sanamu lako, ni hakika alikuwa mwana wa Mungu, na ukakiri kwa kinywa chako na kufuata mafundisho yake AU kufuata mawazo ya mtu mmoja aliyekwaminisha kwamba Jumapili sio siku sahihi ya kusali na akakufundisha kuwachukia wakatoliki halafu mtu akafa kama utakavyokufa wewe?

Shika imani yako, kama ipo sahihi kuliko ukatoliki si ndo safi wewe uende mbinguni wao waende motoni.
Unapaswa ujifunze kujibu hoja bila mihemko na tuhuma usizokuwa na uhakika. Mbona wachangiaji wote wameelewa isipokuwa wewe tu.
Hayo niliyosema ni mara yako ya kwanza kusikia? Nikisikia wanalisema vibaya kanisa langu nisiseme. Soma majibu yenye busara uelimike. Nasita kukuita kabila fulani!
 
IMG_7619.jpg
 
Nimekuwa namsikiliza mhubiri mmoja nadhani ni msabato. Kila mara anarejea juu ya makanisa, anayosema ni waabudu Sanamu na wanaosali jumapili (akiita siku ya jua) badala ya sabato. Nadhani ni wakati muafaka wa kumjibu. Uongo ukirudiwa mara kwa mara wasikilizaji wanaweza kudhani ndiyo ukweli. Wajuzi wa mafundisho ya RC ni wakati sasa wa kujibu
Mbona hilo limejibiwa zaidi ya x1000! Wewe wapi aisee. Yaani hiyo ajenda yake ilishapitwa na wakati
 
Hata hao wasabato still hata hio jumamosi wanayoifata ni kalenda ya wakatoliki.
Hii kalenda ya SAsa ilianzishwa na Wakatoliki miaka elf 2 iliyopita hata kabla ya uwepo wa usabato duniani ambao ulianzishwa mwaka 1890 na Hellen G White na Mwenzake
 
Labda nami niweke neno kdg.. je siku ya sabato ya bwana ni lini? Kama ni jmos au jpili bas naomba aya toka kweny biblia. Pia kama unaweza muuliza huyo mchungaj ingekua heri atupe majibu hayo, lingine... Ni nani aliezipa majina cku tulizonazo? Maana kweny maandiko hazijaandwa jmos au jpili!!
Wakatoliki ndio walizipa majina hizi siku hazipo kwenye Biblia. Na ndizo hadi kesho utumiwa Dunia nzima kisiasa, kiuchumi na kijamii pia
 
Usipoteze muda kubishana na mjinga. Kiimani unatakiwa kumwombea.

Paulo aliyekuwa kiongozi mkuu wa kulihujumu Kanisa la Kristo alikuja kuwa mtume wa Kristo aliyefanya kazi kubwa sana. Hata huyo unayemsema, usishangae siku nyingine akasimama mbele yako akikuhubira mafundishobya kweli kuliko hayo ya upotofu anayoyatoa sasa.

Ila kama wewe unayumba kwa sababu ya kutolijua neno la Mungu, jibidishe kuyajua maandiko:

Kwa ufupi kabisa, rejea hapa:

1) kwa nini Kristo aliuawa?
JIBU: Kwa sababu ya kutotii sheria.

2) Sheria gani
JIBU: Sheria ya Musa, yaani kumbukumbu la torati.

3) Sheria gani ilikuwa kuu kuliko zote kwenye kumbukumbu la torati?
JIBU: Sheria ya sabato

Yesu kutozingatia mafundisho ya mafarisayo kuhusiana na sabato, ndiyo mwanzo wa chuki za mafarisayo na makuhani dhidi ya Kristo. Tena wakasema wazi kuwa, kama angekuwa mwana wa Mungu angeitii Sabato. Naye akawaambia wazi kuwa yeye ni mkuu kuliko sabato. Yeye ni bwana wa Sabato. Kwa nini uiabudu siku ya Sabato badala ya kumwabudu yeye aliye bwana wa Sabato?

Kwa hiyo Kristo aliuawa kwa kutoitii sheria. Kwa kutoitii sheria za kumbukumbu la torati, ambako sheria kuu ni utii wa sabato. Kwa sababu kutokutii sabato lisingekuwa kosa kubwa la kuhukumiwa kifo na Pilato kiongozi mwakilishi wa mfalme wa Roma, wakamtengenezea kesi ya kubumba ya uchochezi kuwa anawachochea watu wasilipe kodi kwa mfalme Kaizari wa Roma.

Paulo anasema wazi Kristo alihukumiwa kwa sababu ya kutoitii sheria, akayashinda mauti. Baada ya ushindi wa Kristo yaani kuyashinda mauti, sisi tulioshinda na kufufuka na Kristo, tukirudi kuitumikia sheria, basi kifo cha Kristo ni bure.

Mkristo hustahili kuiabudu sabato, au kuiabudu siku, mwabudu Bwana wa Sabato katika kweli na haki.
Umefunga mjadala
 
Mwandishi amekosa akili na maarifa.

Nilitegemea huyo.mwandishi angekuja na maelezo yanayothibitisha kuwa Kanisa Katoliki lilishiriki kwenye biashara ya utumwa, kumbe hakuna lolote.

Anaishia kumtaja Captain wa meli iliyobeba watumwa kuwa alikuwa mkristo mzuri (huo ukristo mzuri aliupimaje?) Ningeshtuka kama ningesikia kuwa Kanisa Katoliki lilikuwa linamiliki meli za kusafirisha watumwa kwenda sokoni. Au Askofu alikuwa anaendesha meli ya kusafirishia watumwa.

Hivi hata leo hii, tuna majambazi wangapi ambao ni wakatoliki, wasabato, waprotestant au waislam? Huo ujambazi unafanywa na ukatoliki, usabato, uislam wao au wao ndio wanaokuwa majambazi?

Id Amin alikuwa muislam, alikuwa mtawala wa Uganda, aliua watu wengi wasio na hatia. Hiyo inaweza kuhalalisha kusema kuwa Uislam ulitawala Uganda kwa sababu Amin alikuwa muislam? Au hata kusema uislam uliua watu Uganda, kwa sababu kiongozi aliyeua raia alikuwa muislam?

Wafanyabiashara wakubwa wa biashara ya utumwa walikuwa ni waislam. Je, unaweza kusema kuwa ni uislam ndiyo ulikuwa unafamya biashara ya utumwa? Lakini ili biashara ikamilike lazima uwe na muuzaji na mnunuzi. Wanunuzi wakubwa walikuwa wazungu ambao baadhi yao walikuwa ni wakristo, lakini ni wao ndio waliokuwa wakishiriki hiyo biashara, siyo ukristo wao.

Huyo mwandishi bila shaka amenyimwa maarifa na akili.

The Major Role The Catholic Church Played in Slavery​

avatar
by Stacy M. Brown, NNPA Newswire Contributor
Mtafute umuulize
 
Mimi hofu yangu ni wale wanaopotoshwa na wakapotea. Yesu aliwahi kusema hata kama una kondoo mia, moja akipotea unaacha 99 na kumtafuta mmoja aliyepotea. Swali la kijiuliza haya makanisa yanayoibuka Kila kukicha wanapata wapi waumini?
Kanisa Katoliki kazi yake kubwa ni kuwapa mafundisho ya kweli ya Kristo, na siyo kubishana na watu wasioelewa. Kama kuna muumini ataamua kutosikiliza mafundisho yaliyo sahihi, hakuna namna ya kufanya.

Kumbuka kuwa hakuna Kanisa lenye hazina kubwa ya historia ya ukristo kama Kanisa Katoliki, labda mtu aamue kutotaka kujifunza na kutafuta majibu kwa mambo asiyoyajua au yanayomtatiza.

Fahamu kuwa hata Biblia hii ambayo makanisa yote yanatumia, ni Kanisa Katoliki ndiyo lililokusanya na kuweka katika muundo huo uliopo sasa. Kristo alipoondoka hakuacha Biblia, hakuacha kitabu, bali aliacha mitume, na akawapa maagizo.

Biblia unayoiona leo, ilikuja kuwa katika muundo unaokaribia na tulio nao leo, kama miaka 300 baada ya Kristo.

Kwa hiyo huko nyuma kote, ukristo ulienezwa kwa njia ya mafundisho ya mitume. Ndiyo maana tunasema imani ya Kanisa Katoliki imejengeka kwenye mapokeo (yaani wakristo wa mwanzo walifanya nini, katika jambo gani) na neno la Mungu ambalo ni biblia.

Wale wanaotegemea tu kilichoandikwa kwenye Biblia pekee, wanakosa mengi. Kwa maana sehemu nyingine ni maagizo tu lakini yasiyo na ufafanuzi au maelekezo ya namna ya kutenda.

Kwa mfano, Kristo alisema hakuna amri iliyokubwa kuliko amri ya upendo. Baada ya hapo unaenda kwenye mapokeo, unaenda kuona ni namna gani wakristo wa mwanzo waliitekeleza amri hii ya upendo.

Kristo alisema, salini. Tunaenda kuangalia kwenye mapokeo, wakristo wa mwanzo walikuwa wanafanya namna gani ibada zao. Hata kama kutakuwa na mabadiliko ya kiasi fulani kutokana na hali ya wakati (kama vile wakati wa kale watu walikuwa wachache sana, sasa hivi tupo wengi sana) lakini msingi wa kufanya ibada ni lazima uwe ni ule ule maana ndivyo walivyofundisha na kutenda mitume na wakristo wa mwanzo.
 
Ukweli unauma, hawatajibu.
Hiyo inajibika kwa wepesi sana. Halafu ni ujinga tu.
Cha kwanza, muulizeni maana ya kuabudu. Kuna mtu unaweza kuona anaongelea kuabudu kumbe hata maana ya kuabudu hajui. Nasema hivi sababu miye sijawahi ona wakatoliki wanaabudu sanamu. Ila nimeona wakiwa wanaziheshimu kama vile vifaa vingine mle kanisani vinavyoheshimiwa. Unajua ikijifanya mtu wa kuongelea imani za wengine wakati huna elimu kamili ya imani husika unakuwa lijinga lipotoshaji!
Kusali Jumapili ni sawa tu mbona hata hizi siku zilitajiwa majina baadaye sana. Inawezwkana siku wao wanayosema ni siku ya saba wakati huo ilikuwa siku ya nne.
Mambo ya kubwatuka bwatuka kwenye imani usiyoifahamu vizuri ni ujinga tu.
La msingi kujua ni moja; hata wabwatuke mininihi yao ipasuke RC ipo maana imejengwa kwa mwamba imara.
 
Si kwamba wakatoliki wanaabudu sanamu, kuabudu sanamu ni kuiabudu sanamu ichukue mahali pa Kristo. Wakatoliki wanamwabudu MUNGU kupitia Yesu Kristo. Zile image za masanamu ndio uwachanganya wasiojua
 
Nimekuwa namsikiliza mhubiri mmoja nadhani ni msabato. Kila mara anarejea juu ya makanisa, anayosema ni waabudu Sanamu na wanaosali jumapili (akiita siku ya jua) badala ya sabato. Nadhani ni wakati muafaka wa kumjibu. Uongo ukirudiwa mara kwa mara wasikilizaji wanaweza kudhani ndiyo ukweli. Wajuzi wa mafundisho ya RC ni wakati sasa wa kujibu
Wakatoliki huwa hatubishani na wajinga
 
Kwaufupi , wasabato ni wagonvi. wanatafuta kwa namna yoyote ile ugomvi wa kidini na roman catholic. Ni namna ya mapokeo ya dini yao walivyo pokea kutoka kwa waanzilishi wa hilo dhehebu
Kwa asilimia kubwa kwa baadhi ya hao wahubiri wa SDA, mafundisho yao ni kulishambulia Kanisa Katoliki kama vile wameambiwa kuwa watafika mbinguni kwa kufanya mashambulizi hayo.

Lakini wapo wasabato wazuri kabisa ambao hawana muda na hayo mafundisho yao yasiyo na msingi wa neno la Mungu.

Kuna wakati kulikuwa na ujenzi wa Kanisa Katoliki, nilishangaa Kanisa la SDA lilituma wawakilishi wao, na wakatoa mchango wa fedha milioni 5. Na kabla ya harambee, walishiriki ibada ya pamoja toka mwanzo hadi mwisho.
 
Tukitumia lunar calendar ambayo Waisraeli wa Zamani waliyoitumia Kwa ajili ya kuhesabu siku na mwezi na mwaka, utakuja kugundua Sabato waliyopumzika haikuwa Jumamosi, inabadilikq kutokana na mwandamo wa mwezi kwa kalenda iliyopo.
Kalenda hii ilianzishwa na Papa Gregory ndo wasabato wanaitumia kujustify kuwa Sabato ni Jumamosi na kutumia Maandiko ya Kardinal Gibbons ila ukweli upo kwenye lunar calendar.
Ukiniambia Wayahudi wa Sasa wanapumzika Jumamosi nitakuambia wale ni Ashkenazim , Kuna uwezekano mkubwa hawana asili ya Kiebrania .
 

Attachments

ROMAN CATHOLIC ITATAWALA DUNIA TENA KAMA ILIVOFANYA KABLA Ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo Na baada so soon .....................itaua mamilioni kama ilivyoua tena karne ya 16, 17 na 18.... time will tell
Hakukuwa na Kanisa Katoliki kabla ya kuzaliwa Yesu. Dini iliyokuwepo kabla ya Yesu ni hii ambayo sasa inaitwa Judaism, hii wakati huo ilitwa dini ya Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakobo.
 
Back
Top Bottom