Ukweli kuhusu Wakatoliki kutokuabudu sanamu zilizopo makanisani

Ukweli kuhusu Wakatoliki kutokuabudu sanamu zilizopo makanisani

Kivipi mkuu funguka tujue maarifa gani hayo.
Wewe kama ni msomaji wa biblia unatakiwa ujue huo mstari,Mungu anasema watu wake wanapotea kwa kukosa maarifa.Pia biblia inasema chanzo cha maarifa ni kumcha Mungu,kwa hiyo ili uwe salama unatakiwa umche Mungu.
Na kumcha Mungu kuna vitu vingi vina ambatana na hilo,namshukuru Mungu nilichojifunza wakristo wengi wasiokuwa na bidii ya kumtafuta Mungu na kumjua yeye pamoja na njia zake watapotea.Kuna kundi kubwa hata sasa limeshapotea linahitaji neema ya Mungu.Wengi wameng'ang'ania dini za wazazi wao bila kujua kwa nini wazazi wao wako huko,kila mtu anajukumu la kuiponya nafsi yake.Ni kweli kwa kupigwa kwake Yesu sisi tumepona,lakini kuna kitu unatakiwa ufanye.
Wakristo wengi hawasomi biblia,neno la Mungu halimo moyoni mwao kwa wingi,hivyo wengi wanaishi maisha ya kuwapendezesha wanadamu na si Mungu.Mtu kudanganya haoni shida,mtu kutukana haoni shida,wadada kuvaa mavazi ya utupu hawaoni shida,roho za uzinzi zinatenda kazi sasa kwa kasi kuliko ila watu hawajui.Watu wengi wanaanguka katika uzinzi,hata watumishi wa Mungu wanaanguka,shetani si wa kuchezea ukimpa nafasi anakuharibu.Mbaya zaidi wengi tunafanya mambo lakini hatujui athari zake katika ulimwengu wa roho.
Kwenda kanisani hakumfanyi mtu aingie mbinguni,kuwa kiongozi wa dini au mtumishi wa Mungu siyo tiketi ya kuingia mbinguni kama njia zako si njema machoni pa Mungu.Wengi wataangamia,ni bora leo ukampokea Yesu ili ufanyike upya.
Wengi kwa kutaka kutokupoteza personality zao wata angamia,Yesu alisema mtu akitaka kunifuata kwanza "aikane nafsi yake,kisha jitwike msalaba wake anifuate".Kuikana nafsi si jambo dogo kama watu wanvyodhania,mtumwa huwa akatai.Ukiwa mtumwa wa kristo maana yake unatakiwa kufanya kila unacho agizwa na Bwana,this is not the case with this generation.
Tofautisha utaratibu wa dini yako au kanisa lako na utaratibu wa Mungu usichanganye hivi vitu viwili.SOMA BIBLIA utajua Mungu anataka uishi vipi,watu wanawatii viongozi wao hata kama wanayowambia wafanye yako kinyume na neno la Mungu na hii inatokana na waamini hawayajui maandiko kwa hiyo inakuwa rahisi kupotoshwa.
 
Mimi ni mkatoliki nisiyeunga mkono uwepo wa masanamu kanisani... Na ijumaa kuu huwa sijiangaishi kubusu msalaba. Sisali rozari kwakuwa naamini bikira Maria hawezi kusikia sala zangu...

Ntabakia mkatoliki kwa msimamo wangu.
Nikweli Mangi. We ni kama Mimi nilishaacha kusali sala maria na kuungama kwa Padri nimebaki na sala ya Baba yetu tu.
 
Tusitumie maandiko ya biblia vibaya,nyoka alitengenezwa na Mussa kwanza Mungu mwenyewe alimwambia amtengeneze,je wewe hiyo sanamu uliyo nayo Mungu amekwambia utengeneze?Nyoka wa shaba aliyetengenezwa na Mussa, waliokuwa wameumwa na nyoka walipomtazama walipokea,uponyaji,je hiyo sanamu yako inaleta uponyaji gani?
Kama nilivyosema watu wengi mmepotea kwa sababu mnajua kusoma post za JF,na magazeti ya udaku ila hamna muda wa kusoma biblia zenu.Mwenye masikio na asikie.
 
Nikweli Mangi. We ni kama Mimi nilishaacha kusali sala maria na kuungama kwa Padri nimebaki na sala ya Baba yetu tu.
Mkuu huo ni mwanzo wa kufunguka,endela kusoma biblia utajua mengi na baadaye uta....Mungu wa mbinguni akusaidie.
 
a45092dc64adab9038f8c244e54e52ce.jpg
f1549b3d360ce3adb88f091034009b60.jpg
591ca127ec29def76ff16f860d4398f9.jpg

Hii kitu sitaweza kuiinamia kabisa
7aa9a8c59125d929c5f991394581e552.jpg

Ona hapa
e14f795fa65902fdbe3af509de4bd9f8.jpg

Huyu naye ni binaadam kama mm, naongozwa na Bibie tu
7ea89ef8ab65b49b282a2109ec815fcd.jpg
101f45bed4393ccce6b7837506d75c26.jpg

Labda hiyo ya ndani tu
.... Mtazamo wangu tu...
Samahani kwa ku-copy hiyo post.....!ila ndg ulazimishwi na wala kutokuwepo kwako kwenye kanisa hili hakuathiri chochote....!

Endelea na mambo yako unayoyaamini na waache Wakatoliki waendelee na mambo wanayoyaamini....!

Mungu pekee ndio anayehukumu na wala sio nyie Wasabato/Protestant
 
Tunataka dini inayakayomsaidia muumini kuacha dhambi zake, maana lengo la dini ni kumtafuta Mungu na kuacha dhambi
Sidhani kama roman inatoa hilo suluhisho
 
Samahani kwa ku-copy hiyo post.....!ila ndg ulazimishwi na wala kutokuwepo kwako kwenye kanisa hili hakuathiri chochote....!

Endelea na mambo yako unayoyaamini na waache Wakatoliki waendelee na mambo wanayoyaamini....!

Mungu pekee ndio anayehukumu na wala sio nyie Wasabato/Protestant
Mm ni mroma na nitaendelea kua mromani daima
 
Kabla ujapata majibu ebu weka apa dini&dhehebu lako...!sitaki kuumiza akili yangu kwenye hili tuliwahi kulitolea ufafanuzi sana apo nyuma humu ndani JF.....!sasa leo ili tusiumizane akili fuata masharti hayo kwanza.......!nakusubiri.
1.Roman Catholic

2.soma hichi kipengele chini hapa
T"he Catholic Church during the Council of Trent (1545-1563) issued a clear statement concerning images and statues. According to the 25th Session of this General Council:
The images of Christ and of the Virgin Mother of God, and of the saints are to be had and retained particularly in churches, and due honor and veneration are to be given them; not that any divinity or virtue is believed to be in them on account of which they are to be worshipped, or that anything is to be asked of them, or that trust is to be reposed in images, as was of old by the Gentiles, who placed their hopes in idols; but because the honor which is shown them is referred to the prototypes which these images represent; so that we through the images which we kiss...or bend the knee, adore Christ and venerate the saints, whom they represent. [The Canons & Decrees of the Council of Trent (TAN Books, 1978) p. 215-6]
The Church does NOT compel her members to kneel or pray before images. No one is allowed by the Church to pray to images since they have no ears to hear or power to help us. The Church allows for the veneration of images as long as the honor is directed towards Christ and His saints."
halafu haya si maandishi yangu mkuu na ukitaka link nitakupa
 
Mm ni mroma na nitaendelea kua mromani daima
Hilo ndo swala la msingi hawa vijana wanajituma kuandika ujinga wao unawasoma na kuwaangalia tu. Akili zao ndipo zilipoishia... kutukana ndio jadi yao.

Hakuna wa kukutoa kwenye ukatoliki labda uamue mwenyewe... na hulazimiki kubusu msalaba na kusujudia salamu ili uaminike kuwa wewe ni mkatoliki.

Hakuna wa kukufanya lolote kwenye imani. Sio askofu wala Papa. Kwakuwa kanisa ni la Mungu, sio jengo wala kikundi.
 
Wakristo tusisubiri mtu atusimulie kilichoandikwa kwenye Biblia yaani atusomee Neno la Mungu.
sisi wenyewe tuna wajibu huo. kwani hatujui mtu anayetusomea anania gani miyoni mwake

wapo wanaotaka kutuzuga ili tuangamie. Neno la Mungu likisema usiisujudie sanamu wala kuitumikia na iwe hivyo. Msiwaombe wafu, naiwe hivyo. Mtu akitoka atokako na kusema haka kasanamu kana sura mzuri ya mama wa Yohana mbatizaji tukasujudie tu. jua ana lake jambo anataka kukuzuga tu ili atimiza kazi yake ya uwakala. Neno la Mungu na likae kwa wingi ndani yenu ili liwe NURU ya kujua KWELI ya MUNGU na sio kweli ya dhehebu fulani. Bwana Yesu yeye ndio KWELI na alisema "tazameni Ufalme wa Mungu u ndani yenu mkielewa na kushika NENO langu"
ukitegemea dhehebu likusomee Neno la Mungu SHAULA LAKO.
 
Hilo ndo swala la msingi hawa vijana wanajituma kuandika ujinga wao unawasoma na kuwaangalia tu. Akili zao ndipo zilipoishia... kutukana ndio jadi yao.

Hakuna wa kukutoa kwenye ukatoliki labda uamue mwenyewe... na hulazimiki kubusu msalaba na kusujudia salamu ili uaminike kuwa wewe ni mkatoliki.

Hakuna wa kukufanya lolote kwenye imani. Sio askofu wala Papa. Kwakuwa kanisa ni la Mungu, sio jengo wala kikundi.
juzi tu hapa papa mwenyewe alikili kuwa lengo la martin Luther king halikuwa kuligawanya kanisa ila ilikuwa kulilekebisha kanisa lakini watu bado hawaamini ukisema tu wanesama wewe upo against Roman
 
hakuna dhehebu nnalolichukia kama waroma...na hayo madude wanayaabudu na kwenda kinyume na amri za Mungu.
imeandikwa usijifanyie sanamu ya kuchonga wala kitu chochote kilicho mfano mbinguni,baharini,nchi kavu etc...na kukiabudu.
lakini hawa ndo kwanza ukiingia unakuta kila kona wamechonga masanamu ya maria mtakatifu...masanamu ya yesu..hivi mliwah kuwaona? nyie ndo kwanza mmekazana na rozari mnabusu na zina sanamu ya yesu..ni wazima nyie?
mnachefua.

Sisi menyewe tunakuchukia maana unaabudu usichokijua
 
hakuna dhehebu nnalolichukia kama waroma...na hayo madude wanayaabudu na kwenda kinyume na amri za Mungu.
imeandikwa usijifanyie sanamu ya kuchonga wala kitu chochote kilicho mfano mbinguni,baharini,nchi kavu etc...na kukiabudu. lakini hawa ndo kwanza ukiingia unakuta kila kona wamechonga masanamu ya maria mtakatifu...masanamu ya yesu..hivi mliwah kuwaona? nyie ndo kwanza mmekazana na rozari mnabusu na zina sanamu ya yesu..ni wazima nyie?
mnachefua.


Hivi wewe una imani gani? Imani inayokuruhusu kuchukia wengine umeitoa wapi? Well inawezekana ni Al Shabab au Boko Haram siwez kujua. lakini kama imani yako ni ya kweli huwezi kuchukia wengine, UPENDO ndiyo amri kuu kuliko zote. Lakini kwa upande mwingine, kama wewe huabudu sanamu na hufanyi wanayofanya wengine ambao unawachukia kuliko kitu kingine, basi wewe endelea tu na unachokiamini maana si utaenda mbinguni, Kwani hao wengine ambao kwa akili yako wao hawako sahihi, wanakuhusu nini? Hawali kwako wala hawakupunguzii chochote, kama ni Mbinguni utaenda ukichekelea na wao wataenda motoni ukiwacheka kwa kurukaruka maana unawachukia sana, inakuhusu nini au inakupunguzia nini? Mwisho, endeleeni kuchukiana sababu ya dini mlizoletewa na wazungu na waarabu huku wao wakiendelea na mambo yao. Na kama wazungu kwao dini wala siyo ishu kiiivo ya kuwafanya wachukiane kama nyie malimbukeni mlioletewa, mpaka mnauana sbb eti ya dini
 
Wanajua kuhukumu wenzao tu, wakat hukumu anatoa MUNGU
Mkuu waumini wa siku hizi wanatumia sana hayo maneno,usinihukumu kwani mwenye kuhukumu pekee ni Mungu.Ni kweli anayehukumu pekee ni Mungu lakini kama huyo Mungu amesema katika kitabu chake (Biblia) kwa mfano wazinzi na walevi hawataingia mbinguni.Kama mlevi akiambiwa aache ulevi vinginevyo akifa katika dhambi atatupwa katika ziwa la moto hapo si mtu anahukumu bali Mungu alishahukumu katika biblia.Kwa hiyo wote wanaosema unanihukumu wengi wao hawaijui biblia inasemaje.Biblia inasema "mtu asiye mwamini Yesu huyo amekwisha kuhukumiwa" kwa hiyo mimi nikikutana na mtu hamwamini Yesu,nikimwambia umekwisha kuhukumiwa siyo mimi ninaye mhukumu bali neno limeshamhukumu.
SOMA biblia utajua mengi,hivyo ni vi technique adui amepanda kwa wakristo ili wajipe moyo hawana makosa wafe katika dhambi waingie na shetani jehanamu.Naamini unajua jehanamu haikuumbwa kwa ajiri ya wanadamu,iliumbwa kwa ajiri ya shetani na malika wake.wanadamu wanaingia huko kwa kuwa wamemuasi Mungu.
 
Back
Top Bottom