Uchaguzi 2020 Ukweli mchungu kwa Lissu, sio kila mtu anaweza kuwa Rais wa JMT

Uchaguzi 2020 Ukweli mchungu kwa Lissu, sio kila mtu anaweza kuwa Rais wa JMT

Kosa lake kubwa lililo mwaribia lissu kuwa Rais wa Tanzania matamshi yake wakati wa mchanga wa dhahabu wa Makenikia , kuunga mkono wazungu wachukue Madini yetu na kusema tusipowapa tutanyolewa kwa chupa , ilo tu linatosha kufuta kwenye ramani ya urais ktk historia ya Maisha yake. kumpa ukuu wa wilaya na ubunge nikosa kubwa tunataka Rais atakae tetea raslimali za nchi yetu . kwa ili tu lissu hafai kuwa Rais wa Tanzania atauza raslimali zetu zote kwa wazungu.

Nonsense!
 
jambo la pili linalo mnyima lissu kuwa Rais watanzania ni kuomba nchi yetu na watanzania wanyimwe Misaada na nchi za magharibi ilo inatosha tu , hata akishinda kutoruhusiwa asiwe rais wa Tanzania kwa ili muelewe wazi hatakuwa rais watanzania nikosa kubwa kwa usalama wa taifa yetu na nchi yetu huyo ni msindikizaji tu. alifanya kosa kubwa na usaliti kwa Nchi yake.
 
Najua kuna mafundi wa kutukana na kupiga lakini huo ndio ukweli uwezi kuisaliti nchi yako harafu ukapewa urais wa nchi ulioisaliti, chadema walikosea wangetafuta wingine tu ila wakitaka kuuza sura ya lissu waendele huo ndio ukweli wenyewe hata ulaya na marekani Msaliti hawezi kupewa urais wa nchi china ndio mbaya zaidi msaliti unajua wanachomfanya.
 
Nampa pole sana mheshimiwa lissu kwa mkasa mkubwa wa kutaka kumuua hakika Mungu ni wema wakat wote alimponya. sifa na utukufu ni wa Mungu. Tatizo la ndugu yangu mdogo wangu lissu alituhukumu watanzania wote kwa dhambi ilivyofanya na watu wachache tusio wajua . nakuomba Tanzania na watanzania tufutiwe Msaada kwa makosa yalio tendwa na watu wachache tukose Misaada kwa dhambi ambazo watanzania hatukuzifanya. huo ni usaliti kwa nchi yako linatosha kumfuta kwenye ramani ya urais hata angekuwa ktk nchi yoyote wasingekubali kuwa rais. ulimi kiungo kidogo matatizo yake ni makubwa ni muhimu kuchunga ulimi maana kuna kesho.
 
Tatizo watu wa Lumumba hawaelewi kuwa urais ni taasisi. Vyombo vya ulinzi na usalama ni sehemu mojawapo ya vyombo vinavyotumiwa na taasisi hiyo. Havihusiki kikatiba ku-influence nani awe kiongozi wa taasisi hiyo. Wanaofanya hivyo ni wananchi kupitia sanduku la kura. Kwa hiyo, yeyote yule anayechaguliwa na watu ndiye anayekuwa rais na vyombo husika sharti vimtii. Kwa hiyo hakuna pingamizi lolote kikatiba kwa TL kuwa rais.
Katiba!
 
Unaweza kuwa na hoja lakini hujatuwekea wazi udhaifu wa Lissu uko wapi? Mbona ni mzalendo tuu?
CCM wametaka kumnunua mara nyingi ili kumnyamzisha lakini alibaki kuwa mpinzani kwa maslahi mapana ya Taifa hili ili aliondolee ndwele ya maumivu ya CCM
Lissu anunuliwe na CCM kwa lipi? Lissu angekuwa hanunuliki angenunuliwa vipi na wazungu?
 
Mbowe mnamsema konyagi

Maalim alimsaliti mzee wa kigamboni kwa Nyerere pia ni mtu wa Oman

Membe kala za gadafi

Lisu kosa lake Nini? Kama hao ni wasafi basi hata Hawa wengine tunaamini ni propaganda.
 
Kwa maslahi hayohayo ya taifa, Lissu hawezi kuwa rais hata kwa siku1
Ndio CCM ilishindwa kumnunua ila mabeberu waliweza tena kwa kujipeleka mwenyewe sokoni..
Ni vile tuu taasisi ya urais imeshuka heshma miongoni mwetu lakini trust me haijashuka heshma kwe mfumo hata chembe.
Una ushahidi wa manunuzi hayo?
Alinunuliwa kwa bei gani?

Lakini zaidia sana waliouza madini yetu kwa mgongo wa uwekezaji ni akina nani?wanatoka chama gani? Na sasa hivi chini ya "mzalendo" hao walioiuza nchi yetu wako wapi?

Na zaidi sana, "mzalendo" alitwambia Kangi Lugola na wenzake waliumiza nchi kwa kutuingiza mkenge wa pigo la zaidi ya trilioni moja, (yaani zaidi ya bilioni 1000) lakini twambie hao wapigaji wamefanywa nini? Na kwa sasa wako wapi?

Siasa za kiafrika hizi zinanawirishwa na ujinga wa wengi, hivyo ni kazi rahisi zaidi kuwa kiongozi wa kisiasa ukiwa Africa kuliko kuwa afisa kilimo/nurse kwenye huu ukanda wa dunia!
 
Kura ni makaratasi tu
Sema tu wewe ni zombi hujitambui. These are your true colours. Noti zote duniani kote ni makaratasi tu. Wakwasi na matajiri wote popote ni kwa sababu ya makaratasi tu. Maendeleo yote kote duniani ni sababu ya makaratasi tu.

Pilikapilika zote Tanzania kote zinafanyika hadi Oktoba 28 kwa ajili ya makaratasi tu. Hayo makaratasi tu yamechapwa kwa gharama kubwa sana. Yana thamani kuliko hiyo gharama ya noti. Yaheshimiwe kwa kuwa yatabeba kitu kikubwa zaidi ya makaratasi tu. Yatabeba matakwa na maamuzi sahihi kwa mustakabali wa taifa letu!
 
Tatizo watu wa Lumumba hawaelewi kuwa urais ni taasisi. Vyombo vya ulinzi na usalama ni sehemu mojawapo ya vyombo vinavyotumiwa na taasisi hiyo. Havihusiki kikatiba ku-influence nani awe kiongozi wa taasisi hiyo. Wanaofanya hivyo ni wananchi kupitia sanduku la kura. Kwa hiyo, yeyote yule anayechaguliwa na watu ndiye anayekuwa rais na vyombo husika sharti vimtii. Kwa hiyo hakuna pingamizi lolote kikatiba kwa TL kuwa rais.
Lumumba hawapendi kusikia hili. Yaani wao wanachojua ni kwamba yale maneno yaliyoko kwenye mkoba aliokabodhiwa jiwe wakati anaenda kuchuka form ya kuomba ridhaa ya kukiwakilisha chama kwa mara ya pili yako sahihi. Yoote ni kutisha watu. Eti Fomu ya kuongoza vyombo vya dora my foot!!
 
T
Unaweza kuwa na hoja lakini hujatuwekea wazi udhaifu wa Lissu uko wapi? Mbona ni mzalendo tuu?
CCM wametaka kumnunua mara nyingi ili kumnyamzisha lakini alibaki kuwa mpinzani kwa maslahi mapana ya Taifa hili ili aliondolee ndwele ya maumivu ya CCM
Tunaomba ushahidi Mkuu wa kutaka kupigwa mnada Lissu na chama tawala.
 
Nipo pamoja nawe kwa afya njema!
Nimefanya uchunguzi wa kina kuhusu wagombea urais hao wawili kwa muda mrefu sasa, nimebaini kuwa Lisu hana SIFA nzuri hapa nchini ukilinganisha Na Mr Membe kwa sababu zifuatazo:

1. Lisu hana utulivu hajui kupanga maneno ya ushawishi, Membe anautulivu mkubwa Na anauwezo wa kupanga lugha ya ushawishi.
2.Wasomi wengi wanamuona Lisu kama ni mtu aliyechanganikiwa kidogo, Membe anaonekana alikwazika tu kidogo kwenye chake cha Zamani
3.Ushirika wa Lisu Na Acacia ndio ulimmaliza Lisu kisiasa, Membe anadosari ndogo sana ya kutelekeza Kiwanda huko kusini.
Lisu anaonekana kwa wenye busara kama mtu hana nidhamu Na mlopokaji mwenye mhemuko usiofaa.Membe anaonekana ni mwenye kujizuia mwenye kiasi.
Lisu anaonekana kwa wazee wengi kama ni msaliti MKUU wa taifa la Tanzania. Membe anatafuta haki yake anayoijua mwenyewe kwa kuwa ni msiri sana kuliko Lisu.
Zaidi unaweza kuongezea nawe pia.
 
Ccm mnatumia mbinu nyingi sana ilitusimsupport LISSU ila ipo hivi mwaka huu lazima mteme NYONGO . Kamwambieni na huyo bwana mabombadia
 
Hahahahaha just hahahahaha ukisikia moja haikai mbili haikai ndo hii sasa
 
Ccm lazima mshikwe vuzi kwanza, akili itawakaa tu
 
Ccm mnatumia mbinu nyingi sana ilitusimsupport LISSU ila ipo hivi mwaka huu lazima mteme NYONGO . Kamwambieni na huyo bwana mabombadia
😂😂😂 Lazima atikiswe hadi akasimulie wajukuu.
 
Back
Top Bottom