Ukweli Mchungu: Rais Samia hupendwi na Wananchi wengi

Ukweli Mchungu: Rais Samia hupendwi na Wananchi wengi

Bandari day 22 July
 

Attachments

  • IMG-20230716-WA0840.jpg
    IMG-20230716-WA0840.jpg
    320.9 KB · Views: 1
Gharama ya kufanya uchaguzi baada ya kifo Cha Magu Si kubwa kuliko HASARA Sa100 anayoingiza Taifa Kwa sasa.

Na Bado miaka 3.
 
Sio kweli kuwa mama hapendwi na
wananchi, ni rais ambaye ameleta utulivu na amani kwenye mioyo ya wananchi wengi. Ila kwenye hili la bandari kazidiwa akili na genge la wanyanganyi, inawezekana yuko Kama picha kuna rais wa nchi hii yuko nyuma ya pazia kashika rimoti yeye kawekwa kama geresha.
 
Mimi kwa upande wangu ngoja ninyamaze tu maan, kuna wengne humu had huw wanatukana ila wanapeta tu

Ila sisi wengne na Damu zetu za Kunguni 😂😁 unawez shangaa Nimelitoa neno humu kesho Nikajikuta Lokapu... Ila niishie tu kusema kwamba 2025 Mabadiliko yafanyike.
 
Tunampenda,Muacheni mama afanye kazi,haitakaa itokee Rais apendwe na Wananchi wote

Watz hamueleweki, Magufuli alipokua hai alipigwa maneno ya kila aina,kaondoka mnaibuka kumkumbuka,Watz wanatakiwa wapelekwe mpera mpera tu
 
Utampendaje mtu ambaye hajachaguliwa na wananchi?yeye amepata urais kwa njia haramu,hivyo hawezi kupendwa.kingine ambacho ni kikubwa zaidi ni ulegelege wa kusimamia rasilimali za nchi.yeye kila kitu ni kusaini tu hata vitu vya hovyo kabisa.mfano mkataba wa uuzwaji wa bandari
 
Utampendaje mtu ambaye hajachaguliwa na wananchi?yeye amepata urais kwa njia haramu,hivyo hawezi kupendwa.kingine ambacho ni kikubwa zaidi ni ulegelege wa kusimamia rasilimali za nchi.yeye kila kitu ni kusaini tu hata vitu vya hovyo kabisa.mfano mkataba wa uuzwaji wa bandari
Ameingia kihalali mkuu, hajajiingiza kwa nguvu uongozini....
 
Chawa hawapendi taarifa kama hizi. Watakushukia kama mwewe!!

Kimsingi hali imekuwa mbaya mno kuliko wakati wowote. Sasa hivi hata kwenye TV watu hawataki kabisa kusikia hotuba ya mama.

Kwangu mimi Rais Samia ni kiongozi mzuri sana na ninampenda. Tumeona mengi anatenda vizuri. Lakini uungwana ni pamoja na kuujua ukweli na kuufanyia kazi.

Chawa wamesababisha fedheha kwa kiongozi wetu. Njia pekee na muhimu mama awapige chini hawa chawa na wasaidizi wanaomzubaisha ili waibe
Too late!!
 
Wanaomchukia Rais SSH ni wale waliozoea zile bata za awamu ya tano. Wale waliokuwa wanaongea lugha yao ya asili katika vikao vya halmashauri hapa nchini.

Walizoea kujiona wao ndio watawala wa milele kwa kutegemea wingi wa watu wa kabila lao. Kifo cha kabla cha mpendwa JPM kikawafanya wakaanza kujihisi kama yatima aliyepoteza wazazi wote wawili.

Hizi nongwa zote wanazoendeleza sababu ni kuhisi mirija yao kukatwa. Na Samia amekua akitumia akili sana kuhakikisha daraja la busisi linamalizika kwa wakati na amezianzisha siasa za uchifu huko kanda ya ziwa makusudi kabisa ili kuwaonyesha hao waungwana kwamba hawajapoteza kila kitu.

Ni aina fulani ya kuwapa faraja hivyo hizi nongwa zote zinazoendelea chanzo chake ni hiyo vita ya siri inayoanzia kwa wale wafuasi wa hayati JPM.

Wanatamani sana wamlaumu Mungu lakini mioyo yao inafahamu kuwa hiyo ni dhambi kubwa.
Mkuu awamu ya 5 kulikuwa na Bata? Au umesahau ile kauli mbiu ya Hapa kazi tu! Nakumbusha tu mkuu si kwa ubaya
 
Mm nafikiri utafiti uwe hivi
Mama anapendwa na wenyehela/matajiri kuliko masikini,masikini wanabanwa huku matajiri wakivinjari mijini. ..ile enzi ya unanijua mm nani imerejea kwa kasi kubwa sn
 
Matatizo ya Chadema ni hallucination. Nani kasema rais hapendwi? Watu wanasema rais hajachafuliwa na wananchi.
Kama Kamala Harris. Ni vice president,lakini watu hawataki kuambiwa eti anaweza kuwa rais.
 
Kuna sehemu wananchi umewakosea. Tafakari!

Toka uanze kazi ni mikoa 2 tu sijatembelea nayo ni Kagera na Kigoma. Mikoa mingine yote nimefika na kujaribu kufanya utafiti wa kawaida.

Hali ni mbaya, Siandiki kwa ubaya lakini ndiyo Hali halisi. Wengi wanakuongelea kwenye mtazamo hasi. Hata kwenye mikutano yako ya hadhara, wasaidizi wako wanatumia nguvu kubwa Sana kushawishi watu wajitokeze. Hii si ishara nzuri kwa kiongozi hasa wa level yako.

Niandikaye hapa ni mmoja wa watu tunaopita vijiweni Hadi vijijini. Tunakutana na watu wa kila aina na makundi tofauti na tunabadilishana mawazo. Na huwa hatuachi kuzungumzia viongozi wetu na msitakabali wa nchi yetu. Kwani Tanzania ndiyo mama yetu wa uraia.

Hali ni mbaya. Hali ni mbayaaaa!
Ndugu zetu walio vijijini wengine hata kisomo ni cha Chini lakini kila tukizungumza kwenye simu wanatuuliza " eti tunasikia hata bandari imeenda alijojo" 😭 huwa nasikitika wakiniuliza hivi lakini najiuliza Hadi huko wanajua? Nagundua teknolojia imerahisisha usambaaji wa taarifa.

Sasa wale wanakuzunguka always watakuambia unakubalika lakini kamwe usiwaamini. Wanatumia nguvu kubwa kuwa corrupt mind lakini pamoja na hilo wakitoka wanakuponda mno wananchi.
Sasa hivi waziri mmoja wa afya ametangaza kuanza kwa clinic binafsi katika hospitali za umma. Mapokeo ya hili ni hasi kwa wananchi na joto la jiwe wameanza kulionja. Wanakwenda hospital wanacheleweshwa makusudi ili ifike saa 10 huduma binafsi zianze. Hali ni mbaya.

Kwenye hotuba zako, tofauti na mtangulizi wako, wewe siku hizi hata ukiwa una schedule ya kuhutubia wananchi wengi hawajiandai kusubiri kwa hamu hotuba ya kiongozi wao na hata kujazana kwenye kumbi za starehe kama ilivyokuwa kwa mtangulizi wako. Nimejaribu kuandika kile nakiona mtaani lakini.

Muda Bado upo kidogo kuelekea 2025 ukiamua kubadilika unaweza, ukiamua kupuuza haya ni Sawa tu.
Lakini kama Hali itakwenda hivi Hadi 2025 mtaleta machafuko baada ya uchaguzi. Hatupendi hayo.

Jamhuri ya muungano wa Tanzania🇹🇿
"Raslimali za nchi ziheshimiwe kwa manufaa ya wote"
Jana niliposti hoja kama hii:


Huyu mama kazi imemshinda. Hata jana kasema mwenyewe kaelemewa na majukumu. Nafasi imempywaya. Hili sakata la bandari ndiyo limedhihirisha kuwa "litmus test" yake. Hawezi kuendelea kuongoza nchi.
 
Back
Top Bottom