Ukweli ni kwamba tuna tatizo kubwa sana la uongozi wenye uwezo

Ukweli ni kwamba tuna tatizo kubwa sana la uongozi wenye uwezo

kajekudya

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2015
Posts
2,466
Reaction score
4,916
Duniani kote hatua kubwa za kimaendeleo zinaathiriwa kwa kiasi kikubwa na viongozi wa kisiasa. Hawa ndio hutoa maamuzi ya mwisho kuhusu mstakabali wa Taifa. Hivyo tutake tustake lazima viongozi wetu wakuu wa kisiasa wawe akili kubwa, na wawe weledi.

Anzia Marekani, njoo Uingereza, pita hapo ujerumani, fika Russia, pita hapo china weka kituo Singapore au indonesia, basi fika hata Vietnam. Utakutana na kiongozi aliyeweka msingi wa maendeleo na lazima alikuwa ni akili kubwa na mweledi.

Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alianda kundi kubwa la vijana ambao walipata kila kitu na wangeweza kuwa msaada mkubwa sana, vijana ambao wengi wao walikuwa akili kubwa. Bahati mbaya karibia wote walimgeuka, labda Kama Salim Ahmed Salim ambaye bahati mbaya hakufika pale.

Sasa kwa wale wenzagu na mimi mliobahatika kupitia mfumo rasmi wa shule kuanzia vidudu hadi chuo kikuu. Hivi mnawakumbuka watu waliokuwa wanajishughulisha na siasa mashuleni hadi vyuo vikuu?

Ukweli ni kwamba walio wengi ni wale akili ndogo, wale akili kubwa mlikiwa busy kutafuta "division one" au GPA kubwa ili mbakizwe chuoni au muajiriwe chapu mkiingia mtaani. Wakati huo akili ndogo walikuwa busy kwenye korido za chama kutafuta connections, mwisho wakawa UVCCM, wakaingia kwenye data base Cha Chama.

Sasa Hawa ndio wenye chama, ndio wanaosemwa wanakijua chama, siyo wakuja, wao ndio watagombea ubunge, watakuwa mawaziri, wenye bahati wataukwa Urais, kwani elimu yake ikoje? Watateuliwa kuwa wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri, hawa ndio Sasa wanafanya maamuzi makubwa yanayohusu Nchi hii.

Huku pembeni wanapata ulinzi maridhawa kabisa kutoka kwa ndugu zao wale aliowasema Simbachawene kuwa wanadumu sana huko malindoni.Nyinyi na akiri zenu kubwa mnaishi kuambulia viteuzi vya hapa na hapa na kupiga vi dili vya hapa na hapa lakini akili zenu hamna sehemu mnaweza
kuzitumia kwa manufaa ya Taifa.

Mpo mnatekela maono ya akili zile zilizopata division 4, 3 Bila kusahau gentleman, mkijitahidi mnaishi kupendekeza tu, mara moja moja mnachomoza kwenye ngazi za juu Ila kwakuwa ngazi zote za kisiasa lazima zipate baraka za chama na kwakuwa 90% ndani ya chama ni wale niliowasema basi mnaishi kupigwa vita. Ndiyo, miamba iliyowekeza kwenye korido za Rumumba na siyo kwenye maarifa ndiyo imeshika hatamu.

Niwahakikishie ndugu zanguni tutaendelea kuongoza na Hawa watu wa aina hiyo kwa miaka mingi ijayo kwakuwa they are the only type available at disposal.
 
Uwezo wa viongozi wa nchi husika ni taswira ya uwezo wa jamii katika nchi hiyo. Sehemu yanye jamii ya ovyo itakuwa na uongozi unao akisi hali ya kijamii na kinyume chake
 
Tatizo letu kubwa zaidi ni Katiba
Tatizo kubwa ni nchi Haina watu kabisa, Haina watu wa kuwa viongozi na Haina watu wakuwa raia.

Kwa yanayotokea kungekua na watu makini na sahihi yasingetokea na raia wakaendelea kutazama tu.

Tutafute watu kwenye nchi hii mengine yote tunayo.
 
Mwezi wa 4 ndio unakwenda kuisha hivyo SGR iliyotajwa kuanza majaribio Dr-Moro inapotezewa kimya kimya.

Kweli watanzania ni rahisi kuwahamishia magoli , yaani watu wameacha kujadili masuala ya msingi wanapotezwa dira na genge la CCM walioamamua kujiita chama cha umoja.
 
Kuanzia sasa tuwalee watoto wetu kiuongozi uongozi.

Mimi nilishashtuka kwamba natakiwa nijikuze kismart zaidi kwwmba hata leo nikipata shavu la teuzi yoyote basi jamii inayonizunguka iseme kwamba jamaa anafaa kuwa kiongozi.

Kiongozi awe muungwana.
Awe muaminifu hana tabia ya wizi wala kutapeli.

Kiongozi awe na uwezo mkubwa wa kujenga hoja.

Awe na uwezo mkubwa wa kufikiri.
Asome vitabu mbalimbali vya falsafa na historia.

Awe mahiri katika kujibu maswali.
Awe na hekima za hali ya juu.
Asiwe mtu wa kujikuzakuza na kujiona yeye ndio yeye.

Asiwe malaya malaya wa wazi(kama anafanya sirini atajua mwenyewe na mungu wake hiyo dhambi). Kiongozi awahwshimu watu wakubwa.

Kiongozi lazima uwe expert kwenye fani yako uliyosomea kwamba katika fani yako hakudanganyi mtu.

Kiongozi ujue mambo mengi nje ya fani yako.

Kiongozi uwe na diplomasia nzuri ya kutatua matatizo bila kuleta shida zaidi.

Kiongozi inabidi uwe na huruma na wananchi na sio tumbo lako.

Zipo sifa nyingi sana za kiongozi.

Tanzania tunakosa wwtu wenye sifa hizo kwa sababu jamii ya watanzania bado haijwanza kulea watoto katika misingi ya sifa hizo tokea utotoni,matokeo yake tunapata wale wale ambao tumewatengeneza.
 
when you talk or blame about leadership you shouldn't exclude from it,coz utendaji mbovu ni matokeo msingi ya anaeongozwa kuwa ni dhaifu haijawahi kutokea duniani mtu mwenye chachu ya mabadiliko kushiundwa kubadilisha

change yourself change system
 
Mh. siku hizi haulambi asali? Btw naunga mkono hoja, tunaongozwa na akili ndogo, na hata hao tuliowahi kudhani ni akili kubwa walikosa kitu kinachoitwa "obsession" ya maendeleo, yatokee yasitokee ni sawa kwao.

Anyway, jamii yetu kwa ujumla ina tatizo, tunahitaji mabadiliko ya kijamii kwanza.
 
Kuanzia sasa tuwalee watoto wetu kiuongozi uongozi.

Mimi nilishashtuka kwamba natakiwa nijikuze kismart zaidi kwwmba hata leo nikipata shavu la teuzi yoyote basi jamii inayonizunguka iseme kwamba jamaa anafaa kuwa kiongozi...
Kabisa mkuu vinginevyo wataendelea kiongoza maana wao ndiyo wanajihusisha na siasa
 
Mh. siku hizi haulambi asali? Btw naunga mkono hoja, tunaongozwa na akili ndogo, na hata hao tuliowahi kudhani ni akili kubwa walikosa kitu kinachoitwa "obsession" ya maendeleo, yatokee yasitokee ni sawa kwao.

Anyway, jamii yetu kwa ujumla ina tatizo, tunahitaji mabadiliko ya kijamii kwanza
Boss 😂😂😂😂😂wangu unajua kabisa sijawahi kulamba asali. Mimi siku zote ni mgagagaikoko
 
Kabisa mkuu vinginevyo wataendelea kiongoza maana wao ndiyo wanajihusisha na siasa
Hapa tz wanaoshika nafasi mbalimbali za uongozi wengi wao uwezo ni mdogo sio kwenye tabia,wala uaminifu,wala uwezo wa kuelewa mambo.

Sisi vijana tusome sana kwa sababu madaraka hapewi mjinga,tusome sana ulimwengu na kufuatilia bila ushabiki yanayoendelea duniani kila siku.

Tukifanya hivi tutajua ulimwengu unaendaje
 
Hapa tz wanaoshika nafasi mbalimbali za uongozi wengi wao uwezo ni mdogo sio kwenye tabia,wala uaminifu,wala uwezo wa kuelewa mambo.

Sisi vijana tusome sana kwa sababu madaraka hapewi mjinga,tusome sana ulimwengu na kufuatilia bila ushabiki yanayoendelea duniani kila siku.

Tukifanya hivi tutajua ulimwengu unaendaje
Mkuu muanza na kujihusisha na siasa kuanzia chini miingie kwenye database ya vyama ili mtambulike mpate connections, mpate magod father na mjue figisu na chocho zote. Vinginevyo mtaishia kuambiwa hamkijui chama, hamjawahi kuongoza hata mtaa😄😄😄😄😄
 
Mkuu muanza na kujihusisha na siasa kuanzia chini miingie kwenye database ya vyama ili mtambulike mpate connections, mpate magod father na mjue figisu na chocho zote. Vinginevyo mtaishia kuambiwa hamkijui chama, hamjawahi kuongoza hata mtaa😄😄😄😄😄
Hili nalo ni muhimu sana mkuu.

Ila mimi naamini hakuna figisu mpya,ishu ni kufuatilia saana siasa hata kama haupo humo,ishu ni kuwa na marafiki wanasiasa utapata ABC
 
when you talk or blame about leadership you shouldn't exclude from it,coz utendaji mbovu ni matokeo msingi ya anaeongozwa kuwa ni dhaifu haijawahi kutokea duniani mtu mwenye chachu ya mabadiliko kushiundwa kubadilisha

change yourself change system
Mkuu siyo Africa, the only way ya kubadilisha mambo Africa ni through siasa. Wanasiasa Africa wakiwa madarakani ni Alfa na Omega. Hata ungekuwa na mawazo mazuri kiasi gani Kama hayapo kwa maslahi yao hutoboi mkui
 
Back
Top Bottom